Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

HIMARS

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2012
Posts
70,791
Reaction score
98,334
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

20230409_191806.jpg


Pia, soma: Rais Samia Suluhu Hassan afanya uteuzi wake wa kwanza Ikulu. Gerson Msigwa atolewa Ikulu, Dotto James ahamishwa. TPA, TCRA na TRA zapata wakuu wapya
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

109F6D07-CC2A-444E-B6A4-2E9B9A33F52D.jpeg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC). Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (IGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaii Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

IMG_6677.jpeg
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe?

Yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe wakiwemo mawaziri? Kama yupo serious angetakiwa kuwaita mawaziri awaulize, wakati huo wizi ukitokea kwenye wizara zao walikuwa wapi? asiporidhishwa na majibu fukuza.

Haiingii akilini, hawa ambao inawezekana wameshirikiana kwenye wizi, unaagiza wachunguzane, huku ni kudanganyana tu, ndio maana kuna wakati Rais nae anatiliwa shaka.

Alichokifanya Rais hapo ni sawa na kufunika kombe mwanaharamu apite, kuhangaika na dagaa huku mapapa wapo tu ofisini, mimi sioni jipya, kapanua magoli tu hao jamaa wapate visingizio.
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwajibisha waluohusika na uzembe? yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe?
Kwani hizi anazochukua sio hatua? Kumbuka Rais Huwa hana mihemko na hataki kumuonea mtu.

Ukweli ukibainika wote wataondoka.
 
Ndio mamlaka zao za nidhamu/uwajibikaji..so kwa hili Mh Rais yupo sahihi
Vipi kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe na ubadhirifu, mamlaka yao ya uteuzi na nidhamu ni nani?

Hivi unategemea hao wakuu watakuwa tayari kuwatoa sadaka wasaidizi wao watakaobainika kufanya uzembe?

Sababu kwa akili ya kawaida tu, kama wasaidizi wakibainika kusababisha uzembe, swali litakuja, je, wakuu wao walikuwa wapi hadi huo uzembe kutokea?

Alichofanya Rais hapa ni muendelezo wa kulindana, sioni jipya; wakuu watawalinda wasaidizi wao waliofanya uzembe, kama ambavyo Rais nae anawalinda wakuu wao waliosimamia uzembe, mwishowe mbwa mwitu wataendelea kututafuna kila siku.
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe? yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe?
Nchi inachekesha sana
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe? yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe?
Nadhani itamsaidia kukusanya evidence nzuri sana, kupata justification ya kile atakachofanya next (kama atafanya)!
 
Back
Top Bottom