Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

Vipi kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe na ubadhirifu, mamlaka yao ya uteuzi ni nani?

Hivi unategemea hao wakuu watakuwa tayari kuwatoa sadaka wasaidizi wao watakaobainika kufanya uzembe?

Kwa akili ya kawaida tu, kama wasaidizi wakibainika kusababisha uzembe, wakuu wao walikuwa wapi hadi huo uzembe kutokea?

Alichofanya Rais hapa ni muendelezo wa kulindana, sioni jipya; wakuu watawalinda wasaidizi wao waliofanya uzembe, kama ambavyo Rais anawalinda wakuu wao waliosimamia uzembe, mwishowe mbwa mwitu wataendelea kututafuna kila siku.
Ni kuwekeana sumu na kuuana kwenda mbele, kurogana na vifo sana. Hakuna fisadi atakayekubali kutolewa kafala.
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe? yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe?
Mkuu hiyo nayo ni hatua pia huwezi.mchukulia mtu hatua bila kuwa n evidences za kutosha. Tukae tusubiri makatibu wakuu ni wataalam kwenye wizara zao so wao wanajua vizuri zaidi kuliko raisi
 
16C63233-1DEA-4DD7-AF83-B41935A25849.jpeg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

View attachment 2582472
Mbuzi wa Kafala wamechacha . Ametafutwa sungura wa kafala Haaa.

Akina Mashimba Ndaki mbuzi wa kafala, Kabudi mbuzi wa Kafala, Lukuvi mbuzi wa kafala. Haaa.
January Makamba Mbuzi wa kufugwa hawezi chinjwa, Makame Mbarawa mbuzi wa kufugwa haitaiweje hawezi kuchinjwa, Napee je Vp kuhusu Ummy Mwalimu,

je kuna inawezekana MKRISTO akawa mbuzi wa kufugwa? haaa, et nani......... mataje
 
Taratibu za uongozi hazipo kama unavyodhani wewe mkuu, yule ni Rais sio Mfalme.
Rais kwa mamlaka yake kisheria, ana uwezo wa kuteua na kutengua walio chini yake, na kama imethibitika walisababisha uzembe uliozaa wizi mpaka aagize wadogo kuchunguzwa, hao wakubwa walio chini yake anawaacha wa kazi gani?
 
Dunia inavisa sana , huyu Rais, kama yeye ni muoga ,siatupishe .

Kwann Urais uwe mtamu Kwa fahari na ulaji ,lkn yeye mwenyewe mzembe na muoga ?.


Kwa kauli hiii inamaana Hawa Mawaziri waloguswa na CAG, wataendelea kudunda tu vizuri
Ungekuwa wewe ungefanyaje? Unazijua kazi na majukumu ya katibu mkuu kwenye wizard?
Duh watz wajuaji sana. Sasa hizi si ndio hatua zenyewe jamani ??? Mlitaka Whitwell wanyongwe bila hata kusikilizwa
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

View attachment 2582469
Sasa hapo katibu mkuu kiongozi yupi asimamie hilo huyu aliyemteua na bado hajaapishwa au yule wa zamani?
 
Tumechoka ... Tumechookaa...
ng'atukenii
 
Back
Top Bottom