Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

Rais Samia anaendelea kudhihirisha kwamba hakuna atakayebaki salama atakayechezea mali za umma. Tumezoea ripoti za CAG kila mwaka zinatoka lakini hakuna hatua za waziwazi zinachukuliwa, kwa mara ya kwanza Rais Samia anachukua hatua za waziwazi.

Rais Samia amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwaeleza Makatibu Wakuu wote wasome ripoti ya CAG na kujibu hoja zote na kuzifanyia kazi huku akiagiza Watendaji wote wabadhirifu na wazembe wachukuliwe hatua za haraka za kisheria mara moja.

SOURCE: TAARIFA KWA UMMA KUTOKA IKULU MUDA HUU.
Kilaza kama wewe huna lolote la maana

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

View attachment 2582469
Safi sanaa mama Bora ujitoe kwenye dhimma ya kuja kuulizwa

Mafisadi ukiwachekea sana wataiba sanaa
 
Kwa nini asimtumbue Masanja Kadogosa?. Yeye Ndo Mtendaji Mkuu wa TRC.
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe? yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe?
Siyo kila hoja iliyoibuliwa na CAG ni ya ukweli hivyo zinahitaji uchunguzi na kutafutiwa majibu au maelezo sahihi!
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

View attachment 2582469
Kazi ndiyo shakwisha hapo.
Tusubiri ripoti nyingine mwakani!
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe? yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe?
Hujui kama hujui. Subiri.
 
Kazi imeanza......

, naamini safari hii hakuna atakaye salimika kama tu amehusika either moja kwa moja or indirect, au kazembea kutimiza wajibu wake au makosa yamefanywa na walio chini yake.
Hujashtuka tu kuwa ni mapicha yale yale?

Hai wengine aweze kuwatengua, ashindwe kushughulikia wengine wakubwa zaidi yao?

Katibu mkuu atamuwajibisha Waziri?

Amejiridhisha kuwa Katibu wakuu hawahusiki? Watajiwajibisha?
 
Joka La Ndumilakuwili Huuma Likivuvia!!!
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe? yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe?
Wewe vipi yaani unataka kama karani kakosea achukuliwe hatua na Rais. Wewe vipi.
 
Rais ana akili huyu, ametanguliza mgambo believe maelekezo yote yanatoka kwake.
Yeye atakua anasema, katibu funga jera huyo.!!
Uongozi ni technical.
Ni ngumu kumloga rais ila katibu mkuu akionekana kumshugulikia mkurugenzi fulani ni kurogana tu na kuwekeana sumu. Serikalini kuna vituko, yaani jitu jizi ila bado linaona lina haki ya kuiba
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe? yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe?
Subiri ujionee matokeo, mama haendi kimapapara kama dikteta yule.
 
Back
Top Bottom