Pre GE2025 Rais Samia awalipua watu kwa shangwe, nderemo na vifijo mitaani baada ya kuwahakikishia kuwepo Madarakani hadi 2030

Pre GE2025 Rais Samia awalipua watu kwa shangwe, nderemo na vifijo mitaani baada ya kuwahakikishia kuwepo Madarakani hadi 2030

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ndugu zangu Watanzania,

Mitaani ni shangwe, nderemo, vifijo , chereko chereko,furaha,hoihoi na tabasamu tupu kwa wananchi mbalimbali. Hii ni baada ya Rais Samia kukata kiu ya mamilioni ya watanzania waliyokuwa nayo mioyoni mwao. Kiu ya kutaka kuona Rais Samia akiendelea na muhula wa pili wa Urais kwa kuchukua ,kujaza na kurejesha Fomu ya Urais.

Shangwe hiyo imekuja baada ya Rais Samia kutamka hadharani kuwa anataka kuacha alama katika uongozi wake atakapokuwa anajiandaa kurejea Nyumbani Kizimkazi na kuja kuwahoji walipofikia kimafanikio na kimaendeleo katika Masuala Mazima ya ushirika na ugani.

Kauli ya kusema kuwa atakapo Kuwa anajiandaa kurejea Kizimkazi miaka hiyo ya mwishoni kuelekea 2030.imemaanisha kuwa Rais wetu Mpendwa amekubali Ombi na Maombi ya Mamilioni ya watanzania wa makundi mbalimbali waliohitaji kuona akiendelea kuwa Rais Wetu.

Ndio maana makundi kama Walimu walikuwa wamemchangia mamilioni ya pesa kwa ajili ya kuchukulia Fomu ya Urais.pia wahandisi nao pia walikuwa wamechanga mamilioni ya pesa kwa ajili ya kumpatia Usafiri wa helikopta atakayo kuwa anaruka nayo angani na kuteka anga lote la Tanzania kikomandoo wakati wa kampeni,huku bendera ya kijani ikipepea angani.

Kwa hakika Rais Samia ameleta furaha kubwa sana hapa Nchini kwa kauli yake hiyo.ikumbukwe ya kuwa mamilioni ya watanzania chaguo lao ni Rais Samia tuu hapo Mwakani. Watu wengi sana walikuwa wamesema kuwa wanahitaji kuona CCM ikimpatia Rais Samia ugombea Urais.jambo ambalo hata hivyo CCM kupitia viongozi wake ilijibu kwa kusema kuwa Ni Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan mpaka 2030.

Kwa hakika Rais Samia ndiye ameshikilia Furaha ya Mamilioni ya watanzania.kama Ingetokea akakataa ombi la watanzania,kwa hakika angewakatisha sana tamaa na kuwavunja moyo mamilioni ya watanzania ambao kwa sasa wamejaa matumaini tele na uhakika wa kutimiza ndoto zao.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Samia ni rais bora Tanzania tunamuhitaji sana hata baada ya 2030 tumuombee uhai tu
 
Maadui wa Taifa letu na asilimia ambayo Dr Samia anapambania
1:Ujinga 90%
2:Maradhi 90%
3:Umasikini 70%
 
Uchaguzi wa 2025 umekwisha anaandaliwa Mrundi Kafulila kuelekea 2030 ni bandika bandua
Kidumu Chama Cha Mapinduzi😀


Eti Kafulila

Hivi nyie mnalipwa na Kafulila kumtangaza mtandaoni, kwa taarifa yako hata katika Top 30 wanao onekana watafaa kugombea urais 2030, Kafulila hayupo kabisa, wala CCM hawamjui kabisa, so acheni kumtangaza kwa kupewa vihela, Kafulila hata uweke CCM 100 wagombea, hawezi pita
 
Eti "Kuripua" acha kuharibu lugha wewe chawa ni " Kulipua".

Halafu labda ailipue nchi kwa ufisadi uliotamalaki huku yeye akiwa anajiita ni chura kiziwi.

Mafisadi na majizi yaliyotajwa kwenye ripoti ya CAG yanapeta huko mitaani na hakuna hatua yoyote wamechukuliwa.

Kagawa bandari na mbuga zetu kwa waarabu huko ndio kulipua nchi kwa shangwe chawa?
View attachment 3066251
Usipende kuropoka ropoka na kubwatuka hovyo hovyo tu.
 
Back
Top Bottom