Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Sasa kuogopa kufukuzwa kazi sindio nidhamu inayohitajika. Kama huna hofu ya kupoteza kitu ambacho ni cha maana kwako utakuwaje makini?
Jukwaa hili siku hzi vimejaa vitoto vya darasa la saba F na vi-form 4.0. NO CRITICAL THINKING AT ALL 😄😄
 
Huyu bado hawajui hawa waitwao Watanzania kumbe.
 

"Tunasifiwa kwamba adjustments [maboresho] tuliyoyafanya awamu ya tano kidogo zimekuza heshima ndani ya utumishi wa umma.

“Heshima iliyokuzwa ni ya woga kwa sababu

Asante Rais hii ni kweli. Watu waliacha kutumia weledi na taaluma Yao Kwa kuogopa. Watu waogope wajibu na kazi zao si mtu!
 
Yupo sahihi sana mama .
Hakuna mwananchi anayemkumbuka jiwe kwa mema.
Mkuu watu wanatofautiana mitazamo ndio maana huyu Jiwepamoja na yote ila kazikwa na watu wengi pengine zaidi wanavyozikwa watu wema unaowajua, usitumie nguvu kutaka watu wote wamtizame Jiwe kwa mtazamo wa ubaya muda wote.
 
Magufuri hakuwahi kumtukana Kikwete, Kikwete alitukanwa na Myika kuwa ni rais dhaifu kutokea Tanzania, pamoja na mahalim Self eti ni rais wakuchekacheka tu
 
Hiyo hiyo nidham ya uoga anayoisema ilitusaidia sana raia.., siyo kama kipindi kile mzee wenu watumishi walikuwa wanaweka makoti then inakuwa kaenda kula kutwa nzima., ni ngumu sana kuwaaminisha raja kuwa jamaa alikuwa mbaya kiasi hicho, kila mtu ana mapungufu na hata huyo bibi yenu mapungufu anayo makubwa tu.
 
In reality binadamu wengi hawapendi kazi hasa hzi za kuajiriwa wanafanya tu kwa ajili ya mshahara ili maisha yaende. Hivyo akipata loop hole ya ku-relax nakufanya mambo yake ya ajabu ajabu na kazi haifanyiki kama inavyotakiwa. Hata nchi zilizo endelea wako very strict kwenye kazi kwa kuwa wanajua nature ya binadamu ilivyo na wana mifumo inayo wabana watumishi wa umma hata kwenye private sector pia. Nilitegemea huyu bibi aseme tunaboresha mfumo wa uwajibikaji ili watumishi wa umma wabanwe na mfumo (kanuni na taratibu za utumishi) badala ya kumtegemea kiongozi mkuu wa nchi kwenye kila japo linalohusiana na nidhamu za watumishi wa umma.
 
Asante Rais hii ni kweli. Watu waliacha kutumia weledi na taaluma Yao Kwa kuogopa. Watu waogope wajibu na kazi zao si mtu!
Walikuwa wanaogopa nini sasa kama walikuwa wanafanya kazi zao kwa usahihi?
 
Sasa ni lipi bora nidhamu ya woga au kudharau kabisa. Mwaka juzi Novemba mpaka Februari mwaka jana nilikuwa hospitali nikimuuguza baba yangu. Hakika huduma hospitali ya serikali ilikuwa nzuri mno na wafanyakazi wote madaktari na manesi walikuw wanatoa huduma nzuri. Mwezi uliopita nilifika hapo hospitalini nililala siku nne ilikuwa ni balaa usiambiwe hakuna huduma kabisa na kila unayemgusa awe daktari au nesi majibu utakayopewa utashika adabu. Hivyo hivyo nenda mahakamani ndio hakusemeki leo tunaambiwa huduma zimekuwa nzuri!!! Hamtaweza kufuta mazuri ya JPM
 
Tusijidanganye.Watumishi si kwamba wana nidhamu ya kweli.Uoga,unafiki na kujipendekeza hasa kwa watu wa CCM ndiyo vimetamalaki.Ni kujilisha upepo tu.Binadamu anatakiwa ajengewe mazingira ya upendo,kujiamini na kuwajibika kwa haki.
Mama anataka kujenga utamaduni mpya wa kufanya kazi na mitizamo mipya ya wafanya kazi sasa muhimu ni kuweka mifumo mipya inayotokana na marekebisho ya katiba, sera, sheria na kanuni mpya.
 
Kama ilikuwa na effect nzuri ya mambo kwenda basi jamaa alifanikiwa....wabongo bila vitisho hawaendi.

Ndio maana ata kwemye dini unatishiwa uwepo wa moto...maana bila hivyo hakuna ambaye angekuwa mfuatiliaji wa dini
Ni kweli unafikiri kama sio kuogopa moto nitaanzaje kujinyima kufanya starehe nitavyo hapa duniani au kufanya ibada na kuacha kufanya mambo mengine.
 
Mama anataka kujenga utamaduni mpya wa kufanya kazi na mitizamo mipya ya wafanya kazi sasa muhimu ni kuweka mifumo mipya inayotokana na marekebisho ya katiba, sera, sheria na kanuni mpya.
Utasubili sana huo utamaduni mpya.., kitu ni upigaji tu mwanzo mwisho.
 
Kama ilikuwa na effect nzuri ya mambo kwenda basi jamaa alifanikiwa....wabongo bila vitisho hawaendi.

Ndio maana ata kwemye dini unatishiwa uwepo wa moto...maana bila hivyo hakuna ambaye angekuwa mfuatiliaji wa dini
Ni kweli unafikiri kama sio kuogopa moto nitaanzaje kujinyima kufanya starehe nitavyo hapa duniani au kufanya ibada na kuacha kufanya mambo mengine.
 
Hatimaye Legasi imezikwa rasmi !
 
Mambo yanaenda, wewe huoni!?. Wala hatutaki mambo mengi, tunahitaji tu amani ya moyo.


Jesus is Lord of lords
Amani ya moyo ulijiondolea mwenyewe na sasa umeirudisha mwenyewe, ni suala la kisaikolojia tu hakuna aliyeondoa amani ya mtu ya moyo.
 
Sometimes tunapaswa kuwa wakweli.
Wakati wa Simba wa Yuda:-
(1) Umeme haujawahi kukatikakatika kihuni kihuni kama ilivyo sasa.
(2) Mfuko wa mbolea ulinunuliwa kwa sh. 50,000/- lakini sasa ni sh.120,000/-
(3) Hakukuwa na Ajali nyingi za magari kama ilivyo sasa.
(4) Hakukuwa na visa vingi vya mauaji kama ilivyokuwa miezi michache iliyopita.
(5)Watu wakienda kwenye ofisi za umma walihudumiwa haraka bila ubabaishaji tofauti na inavyoelekea sasa.
(6)Niliwahi kuishi MAKAMBAKO miaka ya 2012/2015, wakati ule ilikuwa ukitembea mitaani kuanzia saa 2 za usiku unapigwa NONDO kichwani, lakini alipoingia Simba wa Yuda NONDO zote zilitoweka ghafla.
Kama mimi ni mwongo, nenda ukawaulize watu wa MAKAMBAKO.
(7) Bei za vitu hazijawahi kupanda kama ilivyo sasa.
Hayo ni machache tu.
Mpaka hapo, utaachaje kumpenda SIMBA WA YUDA?
Utaachaje kumkumbuka SIMBA WA YUDA?
RIP, SIMBA WA YUDA.
Sisi hatutakusahau kamwe hata kama watatengeneza mbinu mbalimbali za kutufanya tukusahau.
RIP, DAD.
 
Tatizo ni mifumo
 
Mdharau biu, hubiuka mwenyewe.

Namwonea huruma sana
Mama Janet na familia yake, kwani kama Mheshimiwa na kidole alichonyoosha kina mantiki yeyote ile kumlenga Hayati basi... hakuona mbiu mwenzake.

Mwenyezi awapatie amani na awaponyeshe na kutoneshwa kwa kidonda cha mpendwa wake na familia yake.

Kama kidole hicho kina mantiki ya kuwaondolea woga wakulima wake(yeye ndie mwenye shamba) basi ataibuka kuvuna magugu. Hakika, kuna ulazimu wakuwa na Kiongozi wa Shamba badala ya Miongozo... yangu macho. Time will tell.

Simba huwa hachezewi sharubu na huo ndio ukweli. Hauwezi kuchezea au kucheza katika himaya ya simba(Kiongozi) na wanawe(wananchi wasio na kiongozi madhubuti) sembuse ndevu zake.

Kweli..."Wamerudi Aiseee" kama vile naona fisi wakinyemelea mifupa ya mzogo(CCM) ambayo simba ameacha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…