Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Hata kama alikuwepo lakini angefanyaje kwa mfano?

Kwani bwana yule alikuwa akiambilika kwa jambo lolote na kusikia?

Alishasema yeye hapangiwi!
Kwani Samia anapangiwa labda na Kikwete tu ila Ndugai kutoa maoni pinzani tu kamshughulikia.
 
Hata kama alikuwepo lakini angefanyaje kwa mfano?

Kwani bwana yule alikuwa akiambilika kwa jambo lolote na kusikia?

Alishasema yeye hapangiwi!
Aliitwa Baba Haambiliki.
 
Kwani Samia anapangiwa labda na Kikwete tu ila Ndugai kutoa maoni pinzani tu kamshughulikia.
Ndugayi alijisahau akaona kama yupo kwenye vikao vya sukuma gang.
 
Ni sifa kwelikweli, ndio maana ww kila siku uko humu. Kama vipi ondoka ukatolee maoni yako TBC1 maana ww ndio unaijua vizuri Tanzania.
Nani anakusikiliza hayo maoni yako sasa? Kuna watu wana miaka kibao humu Jf ila hawachangii chochote wanaishia kusoma tu sasa wewe unaona kubwabwaja humu ndio bonge la issue cha ajabu maoni yako yanaishia humu humu hayana athari yeyote.
 
Ndugayi alijisahau akaona kama yupo kwenye vikao vya sukuma gang.
Angekuwa Simba wa yuda ndio kafanya hivyo sasa hivi mishipa ya shingo ingekuwa inakutoka kwa kulipigia kelele hilo jambo, tatizo lenu ni wanafki mnapiga kelele tu humu.
 
Kwani Samia anapangiwa labda na Kikwete tu ila Ndugai kutoa maoni pinzani tu kamshughulikia.


Nimekuelewa,

Ni kweli Ndughaii aliongea jambo sahihi kabisa,

Tena hata kwa mujibu wa Katiba inaruhusiwa mwananchi kutoa maoni yake juu ya jambo lolote lile.

Lakini kwenye swala la Ndughaii kuna la kujifunza,

Unajua ukiangalia kwa macho ya rohoni kilichomtokea Ndughaii huenda ni adhabu na malipo ya yale alokuwa akiwafanyia wengine [emoji108]

Madam ametumika tu na Mungu kumuadhibu lakini ile huenda ilikuwa ni matokeo ya vile alivyowafanyia wengine.

Imeandikwa: ajikwezae atashishwa, ajishushae atakwezwa.

Pia Imeandikwa; Mungu humpinga mwenye kiburi.

Unajua kanuni mojawapo ya rohoni iko hivi;

Ukimuonea mtu au humuumiza mtu sababu ya madaraka yako, pesa yako, n.k ujue Mungu atainua mtu mwingine mwenye nguvu au pesa au madaraka zaidi yako akushughulikie ipasavyo [emoji108][emoji108]

Na wakati mwingine Mungu huamua kuingilia kati mwenyewe kwa kutimiza mapenzi yake!

Kwa hiyo tuishi na watu wote kwa wema na haki.

Yani kwa kufanya hivyo Mwenyezi Mungu atamu- establish na kinyume chake mtu huyo muovu huondolewa kwenye kile anachotegemea matharani madaraka, pesa, nguvu n.k

Yani hata kama unataka kumuadhibu mtu muadhibu kwa haki ambayo ipo kisheria na kuzingatia utu pia.
 
Hizo hizo kelele zake ndiyo zinawanyima watawala usingizi kwani kupitia mitandao wanazipata kero za wananchi
Wewe kweli una matatizo, kwa kipimo gani au dalili ipi inayokufanya uhisi hizi kelele zenu humu zinawafanya watawala wakose usingizi?

Hivi kelele za jibwa koko unajua kabisa haling'ati zitakunyima amani? Mi naona mnapiga kelele na kupata stress ila wenyewe huko yakwao yanaenda kama watakavyo sasa kuna kukosa usingizi hapo?
 
Huo upande wa Ndugai ila kwa upande wa rais kwa kile alichofanya tafsiri yake ni matumizi mabaya ya madaraka pia.
 
Wanaomtetea marehemu magufuri ni mashetani wenzie.

Kwa jinsi alivyokuwa na roho mbaya yaani nashangaa kuona Kuna mtu anamtetea!

Yule basi tu lakini ingekuwa huko jehanum tunawasiliana, basi tungepeleka Kuni Ili aongezewe moto.
Hujitambui aisee hakuna Rais aliyeiletea maendeleo makubwa Tanzania Kwa muda mfupi kama Magufuli pia Alidhibiti mfumuko wa bei sasa hivi watanzania wanalia kila kitu kinapanda bei
 
Samia anapitia na kisha anakuja kuwajibu nyodo na yale mnayomkosoa yanabaki vilevile habadili chochote, sasa hapo utasema kuna pressure?

Magufuli aliona hamfanyi kazi kutwa kubwabwaja tu mitandaoni ndio maana akatamani ifungwe, mlipiga sana kelele kuhusu Makonda hadi mkachoka ila Jiwe hamkumpa pressure yeyote hadi mwenyewe huko alipomchoka kipindi nyie mshanyoosha mikono.

Huo ndio ukweli.
 
Angekuwa Simba wa yuda ndio kafanya hivyo sasa hivi mishipa ya shingo ingekuwa inakutoka kwa kulipigia kelele hilo jambo, tatizo lenu ni wanafki mnapiga kelele tu humu.
Simba wa Yuda hana anaye mkubali hapa nchini kisa tabia zake za kukosa utu.
 
Nakumbuka Ndugayi alivyo wanyanyasa wapinzani utadhania hawakuwa na haki ya kuwa pale bungeni.

Alivyokuwa anamchukia Mbowe uradhani lile bunge ni mali yake binafsi.

Alivyo mfuta Lissu ubunge na kumnyima haki zake ni jambo ambalo lilitakiwa kukemewa na kila mtanzania.
 
Una uhakika gani kama mimi sipo kwenye walio timiza wajibu mara baada ya kupigiwa kelele mitandaoni?

Au unajiongopea kuwa mpinzani wa serikali au mkosoaji wa serikali lazima awe nje ya system?
 
Una poteza muda wako, hao wapo kama 15-20 hapa Jamboforums, ni kama ma bots flani, wanarudia talking points hizo hizo za kumtukana marehemu muheshimiwa JPM. Hawajui wanasapoti nini wala wanapinga nini, wao ni JPM tu kama vile aliwatungulia wake zao.
Alikutungulia mke wako tu
 
Huna lolote zaidi ya kutetea legacy ya kulazimisha ya meco
 
Nani anakusikiliza hayo maoni yako sasa? Kuna watu wana miaka kibao humu Jf ila hawachangii chochote wanaishia kusoma tu sasa wewe unaona kubwabwaja humu ndio bonge la issue cha ajabu maoni yako yanaishia humu humu hayana athari yeyote.

Acha kupanick tafadhali, au mpaka serekali itokeze iseme imefanyia kazi madai ya Tindo wa jf?
 
Acha kupanick tafadhali, au mpaka serekali itokeze iseme imefanyia kazi madai ya Tindo wa jf?
Sio lazima uwe wewe moja kwa moja hata ile kwa umoja wenu, mfano sasa mnadai katiba mpya.
 
Huna lolote zaidi ya kutetea legacy ya kulazimisha ya meco
Wewe hiyo chuki yako kwa Magufuli ndio inafanya uone kila mwenye mtazamo tofauti na wako kuhusu Jiwe basi unamuona ni mtetezi wa legacy.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…