Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Ndio maana alilaaniwa alichukua nafasi ya Mungu kwa kujiita simba wa Yuda, ni heri angejiita simba wa msimbazi angeepuka laana.
 
Nawaza tu Mtume M angetajwa kuhusiana na huo mfano nadhani mtaani pangeshachafuka mno na wafia dini flani, hakika wakristo ni wastaarabu sana.
Dunia ina amani kutokana na uvumilivu wa imani tulionao wakristo na hilo halina ubishi. Sijapendezwa kabisa na kauli hiyo ya Simba wa Yuda hata kama ni alikuwa mkali kama simba ni bora angeitwa hata simba wa Chato
 
Nimekesha natafuta mabandiko dark..... ya yoga 🤣🤣🤣🤣🤣
====
Kama mazuri vile!!
 
Tusijidanganye.Watumishi si kwamba wana nidhamu ya kweli.Uoga,unafiki na kujipendekeza hasa kwa watu wa CCM ndiyo vimetamalaki.Ni kujilisha upepo tu.Binadamu anatakiwa ajengewe mazingira ya upendo,kujiamini na kuwajibika kwa haki.
Tanzania?
 
Anataka fisi wapangiwe cha kufanya kwenye zizi la kondoo????

Endeleeni kuchutama siku mkizinduka.....
 
Kama ilikuwa inaketa tija safi sana!
.
Sasa yeye ajenge huo mfumo sasa anaotaka wa kutoka moyoni, aujenge ili mambo yaende hicho ndio watu wanataka

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
Mambo yanaenda, wewe huoni!?. Wala hatutaki mambo mengi, tunahitaji tu amani ya moyo.


Jesus is Lord of lords
 
Bora aliye tengeneza nidhamu ya woga kuliko anaesema ule kwA urefu wa kamba

Kifupi mama kashindwa ongoza anatafuta kichaka cha kujificha yeye kaleta nidhamu gani ama ndo kuharibu nidhamu ya woga na kuruhusu upuuzi anaona kafanya Kazi kweli
 
Nawaza tu Mtume M angetajwa kuhusiana na huo mfano nadhani mtaani pangeshachafuka mno na wafia dini flani, hakika wakristo ni wastaarabu sana.
Kasema Simba wa Yuda lakini anaoneakana hafahamu vizuri maana yake Simba wa Yuda.

Ni Kheri kwamba Simba wa Yuda Yesu kristo Anatajwa kila mahali duniani
 
Mimi siyo mtumishi mkuu.Watumishi kama walivyo watu wengine nao wana udhaifu mwingi tu.Na ndiyo binadamu alivyoumbika.Makosa, changamoto.Hayo yote yasitufanye tukawa wanyama kwao.Kupeana nidhamu si lazima upande juu ya paa na kuutangazia umma kwamba unanikomesha Hapo unanitia usugu(unawapa usugu na wenzake) uso lazima.Toa miongozo.Hitaji tija.Hayo mengine ni ziada tu.
 
Dunia ina amani kutokana na uvumilivu wa imani tulionao wakristo na hilo halina ubishi. Sijapendezwa kabisa na kauli hiyo ya Simba wa Yuda hata kama ni alikuwa mkali kama simba ni bora angeitwa hata simba wa Chato
Nadhani mama hajui maana ya "Simba wa Yuda" vinginevyo asingemfananisha na yule mzee. TUMSAMEHE.


JESUS IS SAVIOR!
 
Awamu ile kulikwa na wapigaji sana lakini kwa sababu ya jamaa akiwalinda na wakionekana wanatenda haki
Genge tiifu la Magufuli wote Ni MATAJIRI wa kutisha.

  • Bashite
  • Mnyeti
  • Sabaya
  • Mfugale
  • Dotto James
  • Dotto Biteko
  • Mbunge wa Chato
  • Kijazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…