Rais Samia awataka Wazanzibari kutunza Mila na Desturi zao. Wamaasai hawahusiki?

Rais Samia awataka Wazanzibari kutunza Mila na Desturi zao. Wamaasai hawahusiki?

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa jamii zinazoishi maeneo yenye vivutio vya Utalii, kuendeleza mila na desturi za maeneo hayo ili kulinda heshima ya mila hizo na kuendelea kuvutia utalii.

Rais Samia ametoa wito huo leo, wakati akifunga mafunzo ya Tamasha la Kizimkazi, ambayo yamehusisha Sanaa, Utalii, Uvuvi, Ufugaji, Kilimo na Ujasiriamali, katika Uwanja wa Mwehe, Makunduchi Visiwani Zanzibar.

Amesema katika baadhi ya maeneo, Wenyeji hususani Vijana wamekuwa wakiiga utamaduni wa Wageni, hali ambayo inapelekea hata Wageni kuona hakuna jipya katika maeneo hayo.

Amesema Utalii ambao nchi inauhitaji, ni Utalii wenye kudumisha tamaduni, mila na desturi za Wenyeji, kwani ndivyo ambavyo huwavutia Wageni kutoka Mataifa mbalimbali kwa ajili ya kushuhudia Mtindomaisha wa Wenyeji.

950BA36A-9A8E-452E-92AB-2B96AF7E0232.jpeg
 
Anataka Mila za Kizimkazi zitunzwe ila anapenda kuona Mila za Wamasai zinapitea, ikumbukwe kabila la masai ndo kabila pekee Tz linalotunza Mila zao toka enzi za mababu na mabibi zetu.
Sijui kwa nini huyu mama amejitenga sana na Wamasai !!!
na sio yeye pekee, hata ndugu yake (Marehemu Raisi Mwinyi) aliwapa Waarabu hiyo Loliondo na hata yule mwandishi Stan Katabalo wakamtoa uhai kiana... hawa watu sijui shida iko wapi na utamaduni wa wamasai... Mungu anawaona sana.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa jamii zinazoishi maeneo yenye vivutio vya Utalii, kuendeleza mila na desturi za maeneo hayo ili kulinda heshima ya mila hizo na kuendelea kuvutia utalii.

Rais Samia ametoa wito huo leo, wakati akifunga mafunzo ya Tamasha la Kizimkazi, ambayo yamehusisha Sanaa, Utalii, Uvuvi, Ufugaji, Kilimo na Ujasiriamali, katika Uwanja wa Mwehe, Makunduchi Visiwani Zanzibar.

Amesema katika baadhi ya maeneo, Wenyeji hususani Vijana wamekuwa wakiiga utamaduni wa Wageni, hali ambayo inapelekea hata Wageni kuona hakuna jipya katika maeneo hayo.

Amesema Utalii ambao nchi inauhitaji, ni Utalii wenye kudumisha tamaduni, mila na desturi za Wenyeji, kwani ndivyo ambavyo huwavutia Wageni kutoka Mataifa mbalimbali kwa ajili ya kushuhudia Mtindomaisha wa Wenyeji.
View attachment 3075149
Just Dah!
 
Uwepo wa masai unawafunika wazanzibari kwenye suala zima la utalii
na sio yeye pekee, hata ndugu yake (Marehemu Raisi Mwinyi) aliwapa Waarabu hiyo Loliondo na hata yule mwandishi Stan Katabalo wakamtoa uhai kiana... hawa watu sijui shida iko wapi na utamaduni wa wamasai... Mungu anawaona sana.
ni mbinu za kimkakati
 
Kizimkazi, zanzibar hakuna wanyama, mbugani wenyeji ni wanyama, binadamu wamevamia
, so yuko sahihi 1000%
 
Anataka Mila za Kizimkazi zitunzwe ila anapenda kuona Mila za Wamasai zinapitea, ikumbukwe kabila la masai ndo kabila pekee Tz linalotunza Mila zao toka enzi za mababu na mabibi zetu.
Sijui kwa nini huyu mama amejitenga sana na Wamasai !!!
Ahsante kwa ☝🏿
===========
 
Uwepo wa masai unawafunika wazanzibari kwenye suala zima la utalii
Maono na maoni fikirishi haya. Unaona mbali, hatahivyo suala hilo hawezi kufanya peke yake.

Swali najiuliza: 'Atakuwa anafanya hivyo na nani?'

....anyways, unayodhania, yanafikirisha.
🤯
 
Maono na maoni fikirishi haya. Unaona mbali, hatahivyo suala hilo hawezi kufanya peke yake.

Swali najiuliza: 'Atakuwa anafanya hivyo na nani?'

....anyways, unayodhania, yanafikirisha.
🤯
Nilikuwa namjibu mdau mmoja hapo juu kauliza kwanini marais wanaotokea zanzibar ndo wanawanyanyasa wamasai na ardhi yao, longido, ngorongoro zimeuzwa chini ya tawala za hao watu wawili, ukitizama kwa mapana wamasai wana nguvu sana kwenye utalii huwezi zungumzia utalii wa Tanzania bara(Tanganyika) bila kutaja wamasai, haya hiyo ngorongoro kutajwa kwenye urithi wa dunia ni kwasababu ndiyo hifadhi pekee binadamu na wanyama pori wanaishi kwa pamoja, hiyo tu inatosha kuifunika zanzibar, kwahiyo ni mkakati tu wa kudhoofisha upande mmoja ili mwingine anufaike na udhoofu huo
 
ukitizama kwa mapana wamasai wana nguvu sana kwenye utalii huwezi zungumzia utalii wa Tanzania bara(Tanganyika)
100% ✓

Yote tisa. Suala la Wamaasai huwa lina nibugudhi, kwa sababu hizo ulizozilezea hapo juu.

Yaani mila na desturi zao ndizo zinazowavutia watalii wa 'Culture'- Culture Tourism.

Kuwaondoa ni kosa, kuwanyima haki ni kosa, lakini hii Genocide wanayofanyiw. ni mbaya zaidi.

Naafik, Wamaasai wana nguvu sana-ni moja ya makabila machache sana Duniani ambayo imedumisha, kuheshim na kuendeleza mila na Desturi zake. Utamaduni huo ukipotea, hakuna cha Mmasai, hakuna cha Utalii wala hakuna cha Hesgima kwa NCHI.
 
100% ✓

Yote tisa. Suala la Wamaasai huwa lina nibugudhi, kwa sababu hizo ulizozilezea hapo juu.

Yaani mila na desturi zao ndizo zinazowavutia watalii wa 'Culture'- Culture Tourism.

Kuwaondoa ni kosa, kuwanyima haki ni kosa, lakini hii Genocide wanayofanyiw. ni mbaya zaidi.

Naafik, Wamaasai wana nguvu sana-ni moja ya makabila machache sana Duniani ambayo imedumisha, kuheshim na kuendeleza mila na Desturi zake. Utamaduni huo ukipotea, hakuna cha Mmasai, hakuna cha Utalii wala hakuna cha Hesgima kwa NCHI.
Na ndo hicho wanakiua hao wazenji kwa makusudi au kwa kutojua watendalo,
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa jamii zinazoishi maeneo yenye vivutio vya Utalii, kuendeleza mila na desturi za maeneo hayo ili kulinda heshima ya mila hizo na kuendelea kuvutia utalii.

Rais Samia ametoa wito huo leo, wakati akifunga mafunzo ya Tamasha la Kizimkazi, ambayo yamehusisha Sanaa, Utalii, Uvuvi, Ufugaji, Kilimo na Ujasiriamali, katika Uwanja wa Mwehe, Makunduchi Visiwani Zanzibar.

Amesema katika baadhi ya maeneo, Wenyeji hususani Vijana wamekuwa wakiiga utamaduni wa Wageni, hali ambayo inapelekea hata Wageni kuona hakuna jipya katika maeneo hayo.

Amesema Utalii ambao nchi inauhitaji, ni Utalii wenye kudumisha tamaduni, mila na desturi za Wenyeji, kwani ndivyo ambavyo huwavutia Wageni kutoka Mataifa mbalimbali kwa ajili ya kushuhudia Mtindomaisha wa Wenyeji.

Ndiyo maana wengine tunaamini mabaya anayotenda Tanganyika ni kwa sababu ya Uzanzibari wake. Hana uchungu na Tanganyika ndiyo maana vijana wetu wanauliwa kama kuku
 
Back
Top Bottom