Rais Samia awatumbua Wakurugenzi wa Halmashauri wanne kwa ubadhirifu wa Fedha zikiwemo za UVIKO-19

Rais Samia awatumbua Wakurugenzi wa Halmashauri wanne kwa ubadhirifu wa Fedha zikiwemo za UVIKO-19

Usiombe kujikuta uraiani ghafla bin vuuuh!!

Pole sana kwao waliokuwa wakurugenzi , Hongera sana kwa Rais Samia kusimamia maslahi ya Taifa!

Liwe fundisho kwa wengine wenye tabia hizo
Wanarudi kwenye kazi zao kabla ya kuteuliwa, na wanarudi na mishahara yao ya ukurugenzi, watakachokosa mi V8 na marupurupu manono.
Hawa jamaa wakirudi kwenye kazi zao za awali hawapendwi na maboss wao maana wanawazidi mishahara.
 
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa njiani kutoka Mwanza kwenda mkoani Mara, leo Ijumaa ametangaza kutengua uteuzi wa wakurugenzi wanne wa Halmashauri ya Buchosha, Iringa, Mbeya na Singida Mjini baada ya kubainika kutumia vibaya fedha za UVIKO-19.

---

Rais Samia Suluhu Hassan amewatengua Wakurugenzi wa Halmashauri nne kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha na amesema Mkurugenzi wa Geita kama akikutwa na ubadhirifu pia tataenguliwa

Wakurugenzi waliotenguliwa ni Mkurugenzi wa Buchosa, Iringa, Mbeya Mjini na Singida Mjini. Utenguzi umefanyika baada ya Waziri wa OR-TAMISEMI Innocent Bashungwa kusema wanafanya uchunguzi wa haraka kwa wakurugenzi walioripotiwa kufanya ubadhirifu

Halmashauri ya Buchosa ilikuwa chini ya Mkurugenzi Paulo Malala, Mkurugenzi wa Iringa ni Limbe B. Limbe, Mkurugenzi wa Singida Mjini ni Zefrin Kimolo Lubuva, na Mbeya Mjini ni Amede E.A Ngwanidako
Yule wa bunda aliyejenga msingi kwa 60ml anasubiri nini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mama Samia amewatengua wakurugenzi wanne wa halmashauri za Buchosa, singida mjini, Itinga na Mbeya kwa matumizi mabaya ya pesa za Uviko.

Mama Samia nakuunga mkono kwa 100%, kwa kuwa hizi pesa watakaokuja kuzilipa ni wananchi hivyo zinapaswa kutumiwa vizuri ili kuleta maendeleo.

Mfuko wa cement unauzwa 21000 lakini mkurugenzi anaenda kununua kwa 24000. Haya ni matumizi mabaya ya pesa za wananchi na n Bora umeliona hili, japo hapo mwanzo walikuwepo washabiki wakawa wanatetea humu sijui Leo watasemaje.

Mama Samia endelea kuhakikisha kila pesa ya serikali kwenye miradi haipotei.

Lakini pia usiishie kuwatengua tu unaweza kwenda mbali kwa kuwawajibisha zaidi ili kuzuia wengine kujipimia kwa urefu wa kamba zao.




View attachment 2107544
si alisema hatatumbua bali atawapa onyo kwanza imekuwaje hawa amewatengua?
 
DED wa mbeya mjini ametumbua pesa za UVIKO.

Gapo ni nyumbani kwa spika wetu Tulia. Hii imekaaje?

Muwe na weekend njema.
 
Likely huyo Limbe itakuwa ile mada iliyoletwa humu kuhusu kumbaka mtumishi aliyeenda kufuatilia issue yake ya bima.

Nafikiri kama ushahidi upo basi hatua zaidi za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
 
Halmashauri ya Buchosa ilikuwa chini ya Mkurugenzi Paulo Malala, Mkurugenzi wa Iringa ni Limbe B. Limbe, Mkurugenzi wa Singida Mjini ni Zefrin Kimolo Lubuva, na Mbeya Mjini ni Amede E.A Ngwanidako
Ha ha haaa! Wale wa kusema 'hakuna' maamuzi ya hadharani na papo kwa papo, kwani kufanya hivyo ilikuwa kiki, waje hapa tuwaone!

Hii ni kutaka mrejee tukio la mama aliyekuwa anafanya kazi huko kwenye 'hospitali maalumu' kisha akataka kukatisha mazungumzo ya haki.
 
Waandishi wa HABARI nchii hii mpo kimya sana hivi Ile ajali ya msafara wa mkuu wa mkoa mwanza sio alikuwa anapitia hii miradi iliyotafunwa na hao maded ,hao maded ni mafia sana unaweza Kuta waliogopa waandishi watawaumbua kwenye value of money ya kwenye miradi hiyo.
 
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa njiani kutoka Mwanza kwenda mkoani Mara, leo Ijumaa ametangaza kutengua uteuzi wa wakurugenzi wanne wa Halmashauri ya Buchosha, Iringa, Mbeya na Singida Mjini baada ya kubainika kutumia vibaya fedha za UVIKO-19.

---

Rais Samia Suluhu Hassan amewatengua Wakurugenzi wa Halmashauri nne kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha na amesema Mkurugenzi wa Geita kama akikutwa na ubadhirifu pia tataenguliwa

Wakurugenzi waliotenguliwa ni Mkurugenzi wa Buchosa, Iringa, Mbeya Mjini na Singida Mjini. Utenguzi umefanyika baada ya Waziri wa OR-TAMISEMI Innocent Bashungwa kusema wanafanya uchunguzi wa haraka kwa wakurugenzi walioripotiwa kufanya ubadhirifu

Halmashauri ya Buchosa ilikuwa chini ya Mkurugenzi Paulo Malala, Mkurugenzi wa Iringa ni Limbe B. Limbe, Mkurugenzi wa Singida Mjini ni Zefrin Kimolo Lubuva, na Mbeya Mjini ni Amede E.A Ngwanidako
Hivi zaidi ya kufutwa kazi kuna hatua nyingine kama kushtakiwa na kupelekwa mahakamani wanayochukuliwa?
 
Wakafanye shughuli zao za zamani huku wakila mishahara mikubwa.
 
si alisema hatatumbua bali atawapa onyo kwanza imekuwaje hawa amewatengua?
Na siyo onyo!

Bali alisema atawaelekeza mara tatu, baada ya hapo anatumbua..

Sasa sijui imekuwaje tena?
 
Usiombe kujikuta uraiani ghafla bin vuuuh!!

Pole sana kwao waliokuwa wakurugenzi , Hongera sana kwa Rais Samia kusimamia maslahi ya Taifa!

Liwe fundisho kwa wengine wenye tabia hizo
Hao hawaji uraiani ni watumishi wa Umma watapangiwa kazi nyingine
 
Back
Top Bottom