Rais Samia: Baadhi ya maafisa wa Polisi huiba mafuta ya Serikali kuendeshea vyombo vyao binafsi

Rais Samia: Baadhi ya maafisa wa Polisi huiba mafuta ya Serikali kuendeshea vyombo vyao binafsi

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifungua Kikao Kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Makamanda wa Polisi wa Mikoa/ Vikosi katika Shule ya Polisi Tanzania (TPS) Moshi, leo tarehe 30 Agosti, 2022

==

Samia Suluhu Hassan amesema anazo taarifa kuwa baadhi ya maofisa wa polisi kutumia mafuta yanayotolewa na Serikali katika kuendeshea magari yao binafsi yasiyo na uhusiano na kazi za kipolisi. Rais amesema anao ushahidi wa majina ya wahusika pamoja na namba za magari hayo.

Aidha, amelitaka jeshi la polisi kuongeza matumizi ya tehama katika kufanya kazi zake, kuboresha kitengo cha mawasiliano ya ndani na yale yanayohusisha viongozi wakuu wa nchi pamoja na kuepuka matumizi mabaya ya fedha ambayo yamekuwa yanaripotiwa kila mwaka.

Amemtaka CAG kuendelea na kazi nzuri ya ukaguzi anayoifanya pamoja na kumsisitiza aendelee kufichua uovu wa matumizi mabaya ya pesa ndani ya taasisi hii.

Katika kuhakikisha haki inakuwepo, Rais amewataka polisi kuacha tabia ya kubambikia watu kesi pamoja na kuwaweka ndani pasipo kuwa na ushahidi, au ushahidi huo kutokuwa umekamilika. Jambo hili linatia doa taasisi hii pamoja na kuiongezea bajeti Serikali katika kuwatunza mahabusu hawa. Rais amezungumza haya kwa kurejea takwimu za watu walioachiwa baada ya kukosekana kwa ushahidi ambao idadi yao imefikia watu 1840.
 
Yes my President kwa hili la technology ni muhimu mno, haki nyingi zinapotea au kukandamizwa kwa makusudi na jeshi letu la police, hili jeshi linatakiwa kufanyiwa totally overhaul ili liendane na hali halisi on the ground,mafunzo ya kitechonolojia yatolewe, police wawe na foresinc lab yao sio kutegemea ya mkemia wa serikali, tuwe na IPID ndani ya jeshi hili, na kila kituo cha police kiwe na desk la GBV, na tuwe na special units within our police
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifungua Kikao Kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Makamanda wa Polisi wa Mikoa/ Vikosi katika Shule ya Polisi Tanzania (TPS) Moshi, leo tarehe 30 Agosti, 2022

==

Samia Suluhu Hassan amesema anazo taarifa kuwa baadhi ya maofisa wa polisi kutumia mafuta yanayotolewa na Serikali katika kuendeshea magari yao binafsi yasiyo na uhusiano na kazi za kipolisi. Rais amesema anao ushahidi wa majina ya wahusika pamoja na namba za magari hayo.

Aidha, amelitaka jeshi la polisi kuongeza matumizi ya tehama katika kufanya kazi zake, kuboresha kitengo cha mawasiliano ya ndani na yale yanayohusisha viongozi wakuu wa nchi pamoja na kuepuka matumizi mabaya ya fedha ambayo yamekuwa yanaripotiwa kila mwaka.

Amemtaka CAG kuendelea na kazi nzuri ya ukaguzi anayoifanya pamoja na kumsisitiza aendelee kufichua uovu wa matumizi mabaya ya pesa ndani ya taasisi hii.
Raisi chukua hatua kama taarifa kamiri unazo sasa ukisema hadharani bila kuchukua hatua sie watowa Tozo tutakuelewa je?
 
Raisi chukua hatua kama taarifa kamiri unazo sasa ukisema hadharani bila kuchukua hatua sie watowa Tozo tutakuelewa je?
Katika utawala/uongozi wa sheria hauwezi tu kutamka hadharani huyu au yule ni wezi au kuwatukana.Au kuwaambia watazitolea kwenye matundu...Ni lazima taratibu za kisheria zifuatwe.Ukimtuhumu mtu halafu akakushinda au sheria ikamkosa ndiyo mwanzo wa serikali kumlipa mamilioni.
 
Katika utawala/uongozi wa sheria hauwezi tu kutamka hadharani huyu au yule ni wezi au kuwatukana.Au kuwaambia watazitolea kwenye matundu...Ni lazima taratibu za kisheria zifuatwe.Ukimtuhumu mtu halafu akakushinda au sheria ikamkosa ndiyo mwanzo wa serikali kumlipa mamilioni.
Si raisi ina intelligence ya hali ya juu unashindwa je kujua mhusika halisi wa huo wizi waajibike haraka bila kutuzidishia uchungu sie walipa tozo
 
Si raisi ina intelligence ya hali ya juu unashindwa je kujua mhusika halisi wa huo wizi waajibike haraka bila kutuzidishia uchungu sie walipa tozo
Na ndiyo inapasa wapeleleze vizuri na wawafikishe mahakamani.
NB:Wakati mwingine kauli ya kiongozi huwa ni kuwaweka mguu sawa(waogope na kuchukia uhalifu)kimaadili ili kila mmoja ajitafakari.
 
Yes my President kwa hili la technology ni muhimu mno, haki nyingi zinapotea au kukandamizwa kwa makusudi na jeshi letu la police, hili jeshi linatakiwa kufanyiwa totally overhaul ili liendane na hali halisi on the ground,mafunzo ya kitechonolojia yatolewe, police wawe na foresinc lab yao sio kutegemea ya mkemia wa serikali, tuwe na IPID ndani ya jeshi hili, na kila kituo cha police kiwe na desk la GBV, na tuwe na special units within our police
Bila shaka wewe ni polisi, wasilisha hoja yako kunako husika!
 
Back
Top Bottom