Rais Samia: Baadhi ya maafisa wa Polisi huiba mafuta ya Serikali kuendeshea vyombo vyao binafsi

Rais Samia: Baadhi ya maafisa wa Polisi huiba mafuta ya Serikali kuendeshea vyombo vyao binafsi

Dawa ni kwa serikali kurudisha allowance kwenye mishahara ili watumishi waweze kugharimia usafiri wa kwenda na kurudi makazini, huenda hao polisi kwenye hiyo mizunguko na magari yao huenda bado wanakuwa wanatekeleza majukumu yao ya kikazi, maana wakati mwingine inakuwa ngumu kujua ni wakati gani polisi yupo kazini au hayuko kazini, labda kama awe amestaafu kazi, ni mtazamo tu lakini.
 
Bila shaka wewe ni polisi, wasilisha hoja yako kunako husika!
Acha Uganga wa kienyeji, hii ni mada iliyoletwa tujadili, pls elekeza maoni kwenye mada, mimi nipo Safi kabisa na ninakula pensheni huku lingusenguse, Ruvuma
 
Acha Uganga wa kienyeji, hii ni mada iliyoletwa tujadili, pls elekeza maoni kwenye mada, mimi nipo Safi kabisa na ninakula pensheni huku lingusenguse, Ruvuma
Kwani ukiwa polisi ni dhambi au unakuwa mchafu na pensheni huwezi kula?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifungua Kikao Kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Makamanda wa Polisi wa Mikoa/ Vikosi katika Shule ya Polisi Tanzania (TPS) Moshi, leo tarehe 30 Agosti, 2022

==

Samia Suluhu Hassan amesema anazo taarifa kuwa baadhi ya maofisa wa polisi kutumia mafuta yanayotolewa na Serikali katika kuendeshea magari yao binafsi yasiyo na uhusiano na kazi za kipolisi. Rais amesema anao ushahidi wa majina ya wahusika pamoja na namba za magari hayo.

Aidha, amelitaka jeshi la polisi kuongeza matumizi ya tehama katika kufanya kazi zake, kuboresha kitengo cha mawasiliano ya ndani na yale yanayohusisha viongozi wakuu wa nchi pamoja na kuepuka matumizi mabaya ya fedha ambayo yamekuwa yanaripotiwa kila mwaka.

Amemtaka CAG kuendelea na kazi nzuri ya ukaguzi anayoifanya pamoja na kumsisitiza aendelee kufichua uovu wa matumizi mabaya ya pesa ndani ya taasisi hii.

Katika kuhakikisha haki inakuwepo, Rais amewataka polisi kuacha tabia ya kubambikia watu kesi pamoja na kuwaweka ndani pasipo kuwa na ushahidi, au ushahidi huo kutokuwa umekamilika. Jambo hili linatia doa taasisi hii pamoja na kuiongezea bajeti Serikali katika kuwatunza mahabusu hawa. Rais amezungumza haya kwa kurejea takwimu za watu walioachiwa baada ya kukosekana kwa ushahidi ambao idadi yao imefikia watu 1840.
Rais asiwaonee tuu mapolisi bali maofisa karibu wote wenye magari ya serikali wanafanya hivyo..

Tatueni hili Kwa kuweka utaratibu mzuri wa matumizi ya mafuta..
 
Kuna wengine nawaona hapa wanamwagilia moyo hapa na Noah yao nahisi ni mafuta ya tozo wanatumia[emoji23][emoji23] kuwakimbiza Wanyantuzu hapa
 
Mi kuna siku boda boda yangu ilikamatwa ilapelekqa kituoni basi dereva akanipigia mi nikatoroka ofsin chapu nikaenda kuta imefungiwa kule msimbazi nyuma kabisa na chain juu basi nikamwita yule dogo akanionyesha askar aliemkamata nikamhoji baada ya hapo dogo akaniambia boda ilikuwa na mafuta full tank kuangalia tyre ya mbele imshabadilishwa na mafuta wameyatoa na side mirow zimefunguliwa na starter imebadilishwa basi pale nikaanza na kazi ingine ya kulipwa maana dogo alivyoipeleka walipomuamuru aliipiga picha ushahidi ukambana tule askari mbona aliniita pembeni tukaelewana maana kama alinishtukia fulani naweza muharibia kibarua
 
Geshi la borish taabu tupu.

Wale jamaa lawama ni yingi mno.

Kabla ya kulivunja inahitajika maombi ya deliverance maana ni kama wana laana flani hivi.
 
Back
Top Bottom