Wanashiba na vipofuWengine utawasubiri wavimbiwe hawavimbiwi.Wanakula polepole,kwa adabu,wanafunga midomo na kuangalia chini.Akiona anataka kuvimbiwa anajipigisha simu,anaenda nje kupunguza uvimbiwaji na kurudi kuendelea kubugia.
Asiye mwizi serikali hii awe wa kwanza kuwashutumu hao vibaka wengine.Mtu akishakuwa kibaka hata umpe nini,ataiba tu.Tabia inakuwa damuni.Mtu anaiba hadi peni au kalenda ya ofisi unatarajia nini hapo?😂😂😂
Kuogopana kutokana na vyeo,ukatili,ushirikina au wanashirikishana.Hapo utampata nani?Watakumaliza mapema kabla haujasema neno.Wanashiba na vipofu
Wametawanyika na kukuacha unachora katuni mchangani.😂😂😂Asiye mwizi serikali hii awe wa kwanza kuwashutumu hao vibaka wengine.
Hii nchi Ina mchwa hatari,Mimi hata hizi control number siziamini,wale wanaozitoa wanashindwa vipi kuongeza control number za kwao.Kuogopana kutokana na vyeo,ukatili,ushirikina au wanashirikishana.Hapo utampata nani?Watakumaliza mapema kabla haujasema neno.
Ndiyo anataka kuwapunguzia ili wawe wanachunga kando ya miti yenye miba.Wanakula kwa urefu wa kamba zao
Acha Uganga wa kienyeji, hii ni mada iliyoletwa tujadili, pls elekeza maoni kwenye mada, mimi nipo Safi kabisa na ninakula pensheni huku lingusenguse, RuvumaBila shaka wewe ni polisi, wasilisha hoja yako kunako husika!
Kwani ukiwa polisi ni dhambi au unakuwa mchafu na pensheni huwezi kula?Acha Uganga wa kienyeji, hii ni mada iliyoletwa tujadili, pls elekeza maoni kwenye mada, mimi nipo Safi kabisa na ninakula pensheni huku lingusenguse, Ruvuma
Rais asiwaonee tuu mapolisi bali maofisa karibu wote wenye magari ya serikali wanafanya hivyo..Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifungua Kikao Kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Makamanda wa Polisi wa Mikoa/ Vikosi katika Shule ya Polisi Tanzania (TPS) Moshi, leo tarehe 30 Agosti, 2022
==
Samia Suluhu Hassan amesema anazo taarifa kuwa baadhi ya maofisa wa polisi kutumia mafuta yanayotolewa na Serikali katika kuendeshea magari yao binafsi yasiyo na uhusiano na kazi za kipolisi. Rais amesema anao ushahidi wa majina ya wahusika pamoja na namba za magari hayo.
Aidha, amelitaka jeshi la polisi kuongeza matumizi ya tehama katika kufanya kazi zake, kuboresha kitengo cha mawasiliano ya ndani na yale yanayohusisha viongozi wakuu wa nchi pamoja na kuepuka matumizi mabaya ya fedha ambayo yamekuwa yanaripotiwa kila mwaka.
Amemtaka CAG kuendelea na kazi nzuri ya ukaguzi anayoifanya pamoja na kumsisitiza aendelee kufichua uovu wa matumizi mabaya ya pesa ndani ya taasisi hii.
Katika kuhakikisha haki inakuwepo, Rais amewataka polisi kuacha tabia ya kubambikia watu kesi pamoja na kuwaweka ndani pasipo kuwa na ushahidi, au ushahidi huo kutokuwa umekamilika. Jambo hili linatia doa taasisi hii pamoja na kuiongezea bajeti Serikali katika kuwatunza mahabusu hawa. Rais amezungumza haya kwa kurejea takwimu za watu walioachiwa baada ya kukosekana kwa ushahidi ambao idadi yao imefikia watu 1840.