Rais Samia, Bado hujaona hili ni tatizo tu?

Rais Samia, Bado hujaona hili ni tatizo tu?

Bora hata VP,PM mwenyewe ni kama kaisusa Serikali...mama fukuza Hawa watu kwanza imefika mahala hata makusanyo ya serikali hawashughuliki kuhimiza kama mwanzo,watu wanaiba dawa za serikali hazifiki za kutosha kwenye vituo vya kutolea huduma nk ..Sasa Wana msaada gani hawa
katika watu wa kwanza anaotakiwa kuwapiga chini ni huyo, it is as if anamdharau kwa kuwa ni mwanamke kutokana na mentality ya kidini. Aanze kula pensheni umri ukiwa bado.
 
Ukimsikiliza Ndugai wa leo sio yule wa miezi miwli nyuma kipindi Mama Samia anashika madaraka, huyu wa sasa amerejea kwenye jeuri na kejeri zilezile za utawala wa Magufuli, Anauhakika na anakokwenda. Ukimsikiliza Mwigulu wa sasa, sio yule wa mwanzo wa utawala wa Mama Samia, Mwigulu wa sasa ana jeuri, kibri na dharau iliyovuka mipaka ya siasa za Dar es Salaamu.

Sasa mwangalie na msikilize mpiga filimbi mdini na mkabila aliyekubuhu wa utawala uliopita bwana Josephat Gwajima, huyu si kwamba anampinga tu Rais Mama Samia, Bali amevuka mipaka na kumtuhumu Rais wa nchi kwamba kahongwa pesa na Marekani ili Marekani iuze chanjo nchini. Genge la utawala uliopita wanaamini Samia ni rais wa Mpito sio rais wa "Awamu". Wanaamini rais wa mpito anakoma 2025 na kwamba mipango yao ya kuwania urais haitaharibiwa na urais wa mpito wa Samia.

Awali kabisa tulionya tukitaka Rais mpya Mama Samia aunde serikali yake badala ya kuendeleza serikali ya mtangulizi wake ambayo ilijengwa mfumo hatari na wa kiharamia kwa miaka zaidi ya mtano. Mfumo huo huwezi kuubomboa kwa kubadili mtu mmoja ambae ni rais tu, bali kuivunja serikali nzima na kuunda serikali mpya.

Kwakuwa siasa ya Dar es Salaam ambako kuibuka kwa nguvu na mtu na kuanguka ni jambo lisiloshangaza, Mfumo uliounda serikali iliyopita bado unanguvu kubwa sana ya kimaamuzi, Pengine lilikuwa kosa kubwa sana la karne kwa Mama Samia kuamua kuendesha nchi kwakutumia mfumo wa serikali iliyopita, Huenda ilikuwa kwa nia njema ama kosa la kimahesabu, kwasasa ni vigumu kujinasua, kinyume chake unajikuta umezungwa na ma spinning doctors hata kama una mamlaka kikatiba lakini wenzio wanakukamata kisiasa, michezo kama blackmails ndio inayouteka utawala mpya. Kundi la wahafidhina limefanikiwa kubaki kwenye mfumo,

Juhudi za Rais wa nchi kupambana na corona kwakufuata masharti ya Shirika la Afya dunia, sasa zinapingwa waziwazi na kundi la utawala uliopita ambalo msimamo wao juu ya janga la corona ulikuwa ni wa kijadi zaidi hali iliyopelekea watu wengi kupoteza maisha katika nchi. Kuhusu Chanjo kwa Tanzania inatakiwa serikali isimame wima itoe elimu ya haraka na ya lazima umuhimu na usalama wa chanjo husika.

Jamii iliharibiwa vibaya sana na Rais Magufuli alipotangaza hadharani kuwa chanjo ya corona haifai, Wazungu hawawapendi Watanzania na tuhuma nyingi lukuki, Leo jamii inamwamini Magufuli kuhusu chanjo, sifiriki kwamba Watz wengi watajitokeza kuchanjwa. Badala ya serikali kutangaza tu kuleteta chanjo, iingie mtaani kutoa elimu na kuhamasisha watu wakachanjwa haraka iwezekanavyo.

Mama Samia, vita vya ndani yako ni vikubwa kuliko hivi vya nje ulivyovianzisha, Wenzio wanakusakizia upigane na wapinzani nje huku wanakumaliza ndani, Ya Joyce Banda yanakugonja. Patana na wapinzani ili ushinde vita vyako vya ndani kirahisi. Vita vya nje hutapigana na Chadema tu, utapigana na dunia nzima hata wanaofadhili bajeti yako watakupiga pia na HAUTASHINDA, wewe ni shahidi wa namna Magufuli alivyopitishwa katika magumu alipoamua kutaka kuua upinzani nchini, hakupigana na Chadema tu, alipigana na dunia nzima akaliumiza taifa na akashindwa yeye. Chadema ipo na itaendelea kuwepo.

Idara ya Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya ulinzi, inakuwaje mtu kama GWAJIMA anamtuhumu RAIS @SuluhuSamia kuhongwa PESA na Marekani ili kupigia CHAPUO Chanjo ya COVIDE19? Mko busy kuhujumu vyama vya upinzani na kumbambikia kesi ya Ugaidi @freemanmbowetz na kuacha huyu anayehatarisha usalama wa nchi?

Tatizo kubwa katika nchi hii ni kwamba sayansi inageuzwa kuwa siasa. Hakuna jamii iliyowahi kuendelea kwa kubeza sayansi na maarifa. Hakuna sababu ya kugomea chanjo huku ukiendelea kufa, lakini ieleweke kwamba chanjo zote duniani hata za watoto chini ya miaka 5 zina madhara. Kuna wengine hupata hadi vilema lakini tunaendelea kupeleka watoto clinic kwani tunaamini kwamba madhara kama yako chini ya asilimia 0.01 sio shida sana. Pili hawa vurusi wa Covid kwamjibu wa wataalamu wamagonjwa na tiba wanasema vinabadilika- mutate. Hivyo chanjo zinaendelea kuboreshwa kadri wanavyobadilika.

Tuheshimu sayansi na tusikilize wataalamu wanachosema na tuheshimu taalama za wenzetu, tusisikilize wanasiasa na matapeli wa kiroho aina ya Gwajima.


View attachment 1868346
Ndiyo maana tunasema hicho chama Cha kinafiki, hakuna kiongozi yeyote wa serikali aliye Pinga Kinga ya Covid kuletwa, wote wanasema ije ila kabla haijaanza kutumika wataalamu wetu wajiridhishe Kama kweli ndiyo Kinga kusudiwa, na Hilo ni la muhimu sana, ww usidhani Kinga watakayo pewa Marekani Ina ubora sawa na itakayo kuja Tz, Acha kuchonganisha viongozi na Rais,

Kuhusu alicho sema Gwajima kwamba watu wanapewa Rushwa na Bill.. Yeye direct kwa speach hiyo alimlenga Gaidi, na ukumbuke Gaidi yy alipo Rudi tu kutoka alipo kuwepo ndipo akaanza harakati za kuhimiza chanjo, na juzi mwanza kadiriki kusema iwe lazima, Sasa mtu Kama huyo utamuelewaje?
 
Namuomba Mheshimiwa SAMIA amchukulie hatua za kinidhamu huyu Gwajima.
"Unasema rais anashadadia"!!!!

Huwezi kutumia lugha ya kejeli namna hii kwa rais.
Mdigeuze mada hspa wapuuzi nyie, Gwajima hakusema Rais ana shadadia, Gwajima alimlenga Gaidi, Yule aliye diriki mpaka kusema chanjo iwe lazima kwa kila Mtanzania, yule aliye Rudi toka ughaibuni na kudai kachanja Kumbe Kesha kunjiwa za kwake
 
Mama Samia kuna mchezo Anachezewa, katengenezewa zengwe achukiwe na chadema kwa kumkamata mbowe, katengenezewa zengwe achukiwe na wananchi kwa Tozo za miamala ya simu, halafu mwisho wanampiga ndani ya serikali, kundi la mwendazake lina nguvu bado alipaswa kuliteketeza kabisa
 
Mama ni kama yuko likizoni.

Ngoja akirudi ofisini atafanyia kazi maoni yenu,kuweni na subra.
 
Hivi huyu mcheza porno anapataje watu wengi hivyo wa kwenda kumsikiliza? Dunia kweli haiishi maajabu! Neno la Mungu ndio unakwenda kulipata kwa mtu wa aina hii?
Wakati akiwa mshenga wa kumleta Lowasa chadema hukuwa mcheza porno?

Wakati chadema mnaenda kanisani kwake kila jumapili na kukaa siti za mbele ili kusikiliza ubuyu wa bashite hakuwa mcheza porno?
 
Yericko sasa unanena kwa lugha!

Tulikuonya hukusikia. Na bado,!

Mwenzio malisa sijui kajificha wapi
 
Ww mpuuzi kama walivyowapuuzi wengine! Serikali ya awamu ya 5 unayoiita ya kudharimu huyo mama yako hakuwemo? Acha ujinga wa kuweka kabali/wedge, hutafanikiwa!
Mungu ibariki Tz!
Yericko ni moja ya wapumbavu waliojazana chadema pale!
.
Anaita genge la selikali iliyopita kanakwamba Samia katokea chadema!
 
inawezekana anawaogopa sukuma gang...laiti angenipa urais kwa masaa sita tu ndipo wangejua kwa nini utingo ni mtu muhimu sana wakati wa safari
Sukuma gang ni kina nani?
 
Chanjo kwa Tanzania inatakiwa serikali isimame wima itoe elimu ya haraka na ya lazima umuhimu na usalama wa chanjo husika.
Ile fomu ambayo ilitembea mitandaoni ambayo haikukanushwa ikielekeza mchomwa chanjo akipata madhara baada ya kuchomwa chanjo hasiilamu serikali, ndiyo ilivuruga imani ya walio wengi sana juu ya chanjo hii. Suala la kusema hata wakufanya operation huwa wanasainishwa fomu halina mashiko, kwa sababu tunachomwa sindano za kwinini....lakini hatujawahi kusainishwa fomu za namna hii.

Serikali ikiuhakikishia umma kuwa chanjo ni salama na kuwa ukipata madhara baada ya kuchomwa chanjo serikali itawajibika .....Na ninadhani umma wa watanzania utaunga mkono zoezi.

Kwa hiyo mawazo yanayoibuliwa na watanzania nafikiri yanachagizwa na msimamo wa serikali wa "kutokuiamini "chanjo yenyewe.
 
katika watu wa kwanza anaotakiwa kuwapiga chini ni huyo, it is as if anamdharau kwa kuwa ni mwanamke kutokana na mentality ya kidini. Aanze kula pensheni umri ukiwa bado.
Yani wewe unamfahamu sana PM kuliko Samia ambae amefanya nae kazi zaidi ya miaka 6?
 
Mama Samia kuna mchezo Anachezewa, katengenezewa zengwe achukiwe na chadema kwa kumkamata mbowe, katengenezewa zengwe achukiwe na wananchi kwa Tozo za miamala ya simu, halafu mwisho wanampiga ndani ya serikali, kundi la mwendazake lina nguvu bado alipaswa kuliteketeza kabisa
Acha ujinga dogo!

Kwamba yote hayo uliyoyataja Samia kashtukia tu yamefanyika?

Sasa kwanini asiingilie yeye kama rais?

Unajua chadema wengi hamna akili! Toka kipindi cha JPM tulikuwa tunawambia huo ni mfumo, ambao umeongoza nchi toka Nyerere. Sasa yanapotekea haya mnanaza kumtetea Samia kwamba siyo yeye ila kuna watu wamemzunguka. Pumbavu kabisa
 
Ukimsikiliza Ndugai wa leo sio yule wa miezi miwli nyuma kipindi Mama Samia anashika madaraka, huyu wa sasa amerejea kwenye jeuri na kejeri zilezile za utawala wa Magufuli, Anauhakika na anakokwenda. Ukimsikiliza Mwigulu wa sasa, sio yule wa mwanzo wa utawala wa Mama Samia, Mwigulu wa sasa ana jeuri, kibri na dharau iliyovuka mipaka ya siasa za Dar es Salaamu.

Sasa mwangalie na msikilize mpiga filimbi mdini na mkabila aliyekubuhu wa utawala uliopita bwana Josephat Gwajima, huyu si kwamba anampinga tu Rais Mama Samia, Bali amevuka mipaka na kumtuhumu Rais wa nchi kwamba kahongwa pesa na Marekani ili Marekani iuze chanjo nchini. Genge la utawala uliopita wanaamini Samia ni rais wa Mpito sio rais wa "Awamu". Wanaamini rais wa mpito anakoma 2025 na kwamba mipango yao ya kuwania urais haitaharibiwa na urais wa mpito wa Samia.

Awali kabisa tulionya tukitaka Rais mpya Mama Samia aunde serikali yake badala ya kuendeleza serikali ya mtangulizi wake ambayo ilijengwa mfumo hatari na wa kiharamia kwa miaka zaidi ya mtano. Mfumo huo huwezi kuubomboa kwa kubadili mtu mmoja ambae ni rais tu, bali kuivunja serikali nzima na kuunda serikali mpya.

Kwakuwa siasa ya Dar es Salaam ambako kuibuka kwa nguvu na mtu na kuanguka ni jambo lisiloshangaza, Mfumo uliounda serikali iliyopita bado unanguvu kubwa sana ya kimaamuzi, Pengine lilikuwa kosa kubwa sana la karne kwa Mama Samia kuamua kuendesha nchi kwakutumia mfumo wa serikali iliyopita, Huenda ilikuwa kwa nia njema ama kosa la kimahesabu, kwasasa ni vigumu kujinasua, kinyume chake unajikuta umezungwa na ma spinning doctors hata kama una mamlaka kikatiba lakini wenzio wanakukamata kisiasa, michezo kama blackmails ndio inayouteka utawala mpya. Kundi la wahafidhina limefanikiwa kubaki kwenye mfumo,

Juhudi za Rais wa nchi kupambana na corona kwakufuata masharti ya Shirika la Afya dunia, sasa zinapingwa waziwazi na kundi la utawala uliopita ambalo msimamo wao juu ya janga la corona ulikuwa ni wa kijadi zaidi hali iliyopelekea watu wengi kupoteza maisha katika nchi. Kuhusu Chanjo kwa Tanzania inatakiwa serikali isimame wima itoe elimu ya haraka na ya lazima umuhimu na usalama wa chanjo husika.

Jamii iliharibiwa vibaya sana na Rais Magufuli alipotangaza hadharani kuwa chanjo ya corona haifai, Wazungu hawawapendi Watanzania na tuhuma nyingi lukuki, Leo jamii inamwamini Magufuli kuhusu chanjo, sifiriki kwamba Watz wengi watajitokeza kuchanjwa. Badala ya serikali kutangaza tu kuleteta chanjo, iingie mtaani kutoa elimu na kuhamasisha watu wakachanjwa haraka iwezekanavyo.

Mama Samia, vita vya ndani yako ni vikubwa kuliko hivi vya nje ulivyovianzisha, Wenzio wanakusakizia upigane na wapinzani nje huku wanakumaliza ndani, Ya Joyce Banda yanakugonja. Patana na wapinzani ili ushinde vita vyako vya ndani kirahisi. Vita vya nje hutapigana na Chadema tu, utapigana na dunia nzima hata wanaofadhili bajeti yako watakupiga pia na HAUTASHINDA, wewe ni shahidi wa namna Magufuli alivyopitishwa katika magumu alipoamua kutaka kuua upinzani nchini, hakupigana na Chadema tu, alipigana na dunia nzima akaliumiza taifa na akashindwa yeye. Chadema ipo na itaendelea kuwepo.

Idara ya Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya ulinzi, inakuwaje mtu kama GWAJIMA anamtuhumu RAIS @SuluhuSamia kuhongwa PESA na Marekani ili kupigia CHAPUO Chanjo ya COVIDE19? Mko busy kuhujumu vyama vya upinzani na kumbambikia kesi ya Ugaidi @freemanmbowetz na kuacha huyu anayehatarisha usalama wa nchi?

Tatizo kubwa katika nchi hii ni kwamba sayansi inageuzwa kuwa siasa. Hakuna jamii iliyowahi kuendelea kwa kubeza sayansi na maarifa. Hakuna sababu ya kugomea chanjo huku ukiendelea kufa, lakini ieleweke kwamba chanjo zote duniani hata za watoto chini ya miaka 5 zina madhara. Kuna wengine hupata hadi vilema lakini tunaendelea kupeleka watoto clinic kwani tunaamini kwamba madhara kama yako chini ya asilimia 0.01 sio shida sana. Pili hawa vurusi wa Covid kwamjibu wa wataalamu wamagonjwa na tiba wanasema vinabadilika- mutate. Hivyo chanjo zinaendelea kuboreshwa kadri wanavyobadilika.

Tuheshimu sayansi na tusikilize wataalamu wanachosema na tuheshimu taalama za wenzetu, tusisikilize wanasiasa na matapeli wa kiroho aina ya Gwajima.


View attachment 1868346
Yaan huyu anatoa kebehi kwa Rais halafu bado wanamchekea,
 
Na wewe uwe na akili ,Chanjo sio tiba 100 % bali ina boost kiasi fulani cha Kinga hakuna waliposema ukipata chanjo 2 huugui bali chance ya kuugua unaipunguza.

ewa wangu pale pale maana mahali unfortunately mutation ya kirusi bado inaendelea.I
Kwa hiyo chanjo ni aina mpya ya ARV mpya!? Hizi hela mli"zokula" sijui....mtazilipaje!
 
Huyu ndugu GWAJIMA anashangaza sana.....

Huyu ndugu yetu GWAJIMA anatafakarisha Sana.....yaani anatafakarisha mno.......


Kwa kweli ANASTAAJABISHA....

Manesi na madaktari wetu wako mstari wa mbele katika KUTUUGUZA....sasa wao kwa wao wakishaajishiana WACHOMWE chanjo ,Gwajima ANAWAOMBEA WAFE KWA JINA LA YESU 😲😲😲

Manesi na madaktari wetu wakitushajiisha sisi wananchi tukachomwe CHANJO ,hatimaye Gwajima ANAWAOMBEA WAFE KWA JINA LA YESU 😲😲😲

Kwanini tunavitumia VITAKATIFU VYA MADHABAHU kueneza propaganda za "conspiracy theories"?!!!

MAPAMBANO DHIDI ya UVIKO 19 ni Vita KUBWA....iweje tunaanza kusalitiana katika uwanja wa MAPAMBANO ?!!

Hivi Gwajima hana ndugu aliyempoteza kutokana na huu UGONJWA?!!

Hivi Gwajima hana jirani ,rafiki aliyempoteza kutokana na UVIKO 19?!!

Hivi Gwajima hana mfuasi wake kanisani ambaye ameangushwa na UVIKO 19,na wafuasi wake hawana ndugu walio wahanga?

Hivi Jimboni KAWE hakuna mgonjwa wa UVIKO....hakuna aliyekufa kwa UVIKO ?!!!

Duuuh 😲😲😲

#ShimeTujiandaeTukachanjwe
#NchiKwanza
#TujilindeNaKulindaWengine
#KaziIendelee
 
Namuomba Mheshimiwa SAMIA amchukulie hatua za kinidhamu huyu Gwajima.
"Unasema rais anashadadia"!!!!

Huwezi kutumia lugha ya kejeli namna hii kwa rais.
Ni maajabu kwa vyombo vya dola wasipodili na huyu mpuuzi taperi na gaidi,

Madam president,mtu Kama Gwaji boy ni wakumpoteza mazima,huyu Ni kirusi katika Nchi, huyu wa kufutwa kabisa, anadharau mamlaka
 
Ni kweli kabisa, alifanya kosa la kiufundi kutofunja serikali aunde yake. Wengi tulitarajia hilo. Alidhani urais alioupata alipewa fadhila ilhali alipigiwa kura na alipiga kampeni sana nchi nzima kuliko hata magufuli.

kwa kadri ambavyo anamuona Mbowe na Chadema ni tishio kwake ndiyo ambavyo hawa vijana wakabila na wadini walikubuhu watakavyoendelea kumtia vidole vya macho.

Na hajashtuka kwamba kuendelea kuwashambulia wapinzani anadhani polisi na wanamsaidia, somebody tell her that it is a subotage. Chuki kubwa inaanza kujengeka katika jamii dhidi yake.

Na sasa amekaa kimya polisi kustorm kanisani, jambo ambalo hata jpm hakuwahi kuruhusu likafanyika ijapokuwa aliwaharss sana wapinzani.

Time is a good judge
Adui mkubwa katika serikali ya huyu mama ni Hawa dizaini ya watu Kama Nchemba,Gwajima na wengineo, sio hao wapinzani wapiga kelele tu hawana madhara, mama akicheka na Hawa Sukuma Gang watamkwamisha kweli, wao akili na malengo yao Ni mwaka 2025 Urais waweke mtu wao
 
Back
Top Bottom