Rais Samia: Bado ninaisikia sauti ya Hayati Magufuli akiniambia kuhusu miradi na Dodoma kuwa Makao Makuu

Rais Samia: Bado ninaisikia sauti ya Hayati Magufuli akiniambia kuhusu miradi na Dodoma kuwa Makao Makuu

sina picha mkuu lakini nitajitahidi kukuelekeza kwa ufahamu wangu ulivyo juu ya hii barabara,
hii barabara itachepuka pale mtumba(mji wa kiselikali)
inaelekea kaskazini na kusini
kisha inaelekea magharibi had nara
inaungana na barabara kuu inayoelekea singida,
kwa ufupi ring road
inaizunguka dodoma
dodoma mjini inakuwa katikati imezungukwa na ring road,
mtu anaetoka morogoro
kama anaenda mikoa ya singida, tabora au mwanza,
atakuwa hana ulazima wa kupita katikati ya mji
ili kuepusha msongamano wa magari hasa magari makubwa,
akifika mji wa kiselikali kabla hajaingia dodoma mjini
atachepuka kwenye ring road
atatokezea nara
kisha ataendelea na safari yake pasipo kupitia dom town,
Shukrani kwa ufafanuzi mzuri!Maana yake kama gari inatoka Dar kwenda singida,ikifika mtumba inaweza kuchepuka.Kwahiyo inaweza ikachepukia either kaskazini au kusini (kwa maana pande zote zitakuwa zinatoa?)au itakuwa inachepuka upande mmoja tuu...Pia kama unajua naomba nielekezee barabara hizo au hiyo ya mchepuko itapita mitaa gani kabla ya kutokeaa hapo Nara.
 
Ni suala la msingi amalize miradi ya mtangulizi wake kama hayati alivyofanya kwa Jakaya. Ingawa ameonyesha uwezo zaidi pia kwa kuanzisha ya kwake. Hongera Mama Samia.
Mwendazake aliendeleza mradi wa gesi na bandari ya bagamoyo? SGR ilikuwa iende Kigoma...
 
Shukrani kwa ufafanuzi mzuri!Maana yake kama gari inatoka Dar kwenda singida,ikifika mtumba inaweza kuchepuka.Kwahiyo inaweza ikachepukia either kaskazini au kusini (kwa maana pande zote zitakuwa zinatoa?)au itakuwa inachepuka upande mmoja tuu...Pia kama unajua naomba nielekezee barabara hizo au hiyo ya mchepuko itapita mitaa gani kabla ya kutokeaa hapo Nara.
inayoelekea kusini inapita ihumwa
kwenda hadi iyumbu
alafu inaelekea magharibi kuitafuta nara,
huku kaskazin inakatiza mji wa kiselikari
inatokezea mahoma makulu
inaendelea hadi nzasa
kisha makutupora
alafu inaitafuta nara
bila shaka wewe ni
mnyausi
maana hilo jina la kukaya,
 
Tunaweza kubadilisha mwngi kuifanya Dodoma inawiri lakini itaendelea kuwa mbaya kwa sababu ubaya wa Dodoma ni wa asili. Hali ya hewa ni mbaya, hatuwezi kubadilisha. Ardhi yake ni mbaya, tunaweza kurekebisha kiasi lakini hatuwezi kubadilisha.

Lakini pia hata yale ambayo hufanywa na mwanadamu, Dodoma yamefanyika hovyo sana. Dodoma ina barabara finyu katikati ya mji. Yaani Tabora iliyopangwa na wajerumani mwishoni mwa miaka ya 1800, ina barabara pana na ina mpangilio mzuri maradufu ya Dodoma iliyopangwa na CDA miaka ya 1980, yaani Wajerumani wa miaka ya 1800 walikuwa na akili na weledi kuliko wataalam wa CDA wa miaka ya 1980.
Duuuh kuu street ni finyu mkuu??
 
inayoelekea kusini inapita ihumwa
kwenda hadi iyumbu
alafu inaelekea magharibi kuitafuta nara,
huku kaskazin inakatiza mji wa kiselikari
inatokezea mahoma makulu
inaendelea hadi nzasa
kisha makutupora
alafu inaitafuta nara
bila shaka wewe ni
mnyausi
maana hilo jina la kukaya,
Ok asante sana wa kukaya
 
Tunaweza kubadilisha mwngi kuifanya Dodoma inawiri lakini itaendelea kuwa mbaya kwa sababu ubaya wa Dodoma ni wa asili. Hali ya hewa ni mbaya, hatuwezi kubadilisha. Ardhi yake ni mbaya, tunaweza kurekebisha kiasi lakini hatuwezi kubadilisha.

Lakini pia hata yale ambayo hufanywa na mwanadamu, Dodoma yamefanyika hovyo sana. Dodoma ina barabara finyu katikati ya mji. Yaani Tabora iliyopangwa na wajerumani mwishoni mwa miaka ya 1800, ina barabara pana na ina mpangilio mzuri maradufu ya Dodoma iliyopangwa na CDA miaka ya 1980, yaani Wajerumani wa miaka ya 1800 walikuwa na akili na weledi kuliko wataalam wa CDA wa miaka ya 1980.
Kuna baadhi ya watanzania, wanaroho za ajabu na ubaguzi, Dodoma ni sehemu ya Tanzania, hivi kinachomuuma mtu kuisema sehemu ya Tanzania vibaya ni nini? Unaposema Dodoma ni mbaya ulitaka iweje? Unakosoa uumbaji wa Mungu ktk dunia? Unadhani maeneo yote yakifanana tutaenda kufanya utalii wapi? Tunahitaji utofauti ili kuwe na hali ya kushangaa maeneo mengine na kuyatembelea.

Wanadamu tumepewa mahalifa na Mwenyezi Mungu, hivyo Dodoma bado itapendezeshwa tu. Kama Dubai ilivyokuwa na uasili wake wa jangwa lakini sasa inamaeneo yenye uoto wa mimea. Swala la barabara finyu katikati ya mji ndo staili na design ya mji huo. Unataka katikati ya mji kuwe na barabara pana, kwani unapitisha nini zaidi? Ndo maana barabara pana na kubwa zinapita kando ya mji.

Tutajie ambapo wewe unaona palifaa kuwa makao makuu. Make ukileta ukosoaji, tunauwezo wakukosoa hata wewe kule unakodhani panafaa. Hakuna sehemu iliyokamili. Tuache ushamba. Miji yote inauzuri na utofauti wake unaoifanya iwe ya kipekee.
Ati unaanza tu kukashifu mkoa kuwa ni mbaya, hivi wewe ndo mtaalamu wa kujua upi mji mzuri na upi mbaya. Ebu tutajie mji wewe unao ona ni mzuri, nasi tukuoneshe uwazacho sicho.

Penda nchi yako, penda Taifa lako, jivunie kilichopo kwenye nchi yako, Dodoma ni sehemu ya Tanzania. Na ni makao makuu. Makao makuu hayachaguliwi kwa kufuata ukubwa wa mji au sijui huo uzuri unao sema! Ha ha ha!
 
Rais Samia leo akiwa anaweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa barabara za pete(ring road) jijini Dodoma amesema bado sauti ya mtangulizi wake hayati Magufuli anaisikia ikimtaka akamilishe miradi yote aliyoiacha, ikiwemo huo wa ujenzi wa barabara za ring roads zitakazowezesha kuipanga na kuipendezesha jiji la Dodoma.

Rais Samia amesema ameachiwa urithi mzito wa kukamilisha miradi yote na atafanya kama alivyowaahidi watanzania kuwa hakuna hata mradi mmoja utakaoshindwa kukamilika na wananchi wasiwe na wasiwasi.

View attachment 2113829

Mizimu ya chato iko imara
 
Rais Samia leo akiwa anaweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa barabara za pete(ring road) jijini Dodoma amesema bado sauti ya mtangulizi wake hayati Magufuli anaisikia ikimtaka akamilishe miradi yote aliyoiacha, ikiwemo huo wa ujenzi wa barabara za ring roads zitakazowezesha kuipanga na kuipendezesha jiji la Dodoma.

Rais Samia amesema ameachiwa urithi mzito wa kukamilisha miradi yote na atafanya kama alivyowaahidi watanzania kuwa hakuna hata mradi mmoja utakaoshindwa kukamilika na wananchi wasiwe na wasiwasi.

View attachment 2113829
porojo tu
mbona hukusikia akikuambia kuhusu polepole , ndugai na Lukuvi ?
 
Malizia mama yetu
20220210_073029.jpg
20220210_073013.jpg
 
Kabisa mkuu yaani huyu mwamba angeongezea hata miaka mitatu mbele nchi hii tungekuwa nusu ya South japo yeye alienda mbali zaidi eti kama Europe [emoji4]
Tatizo gaidi asingekuwa ndani
 
Back
Top Bottom