Kuna maswali muhimu ya kujiuliza
Afuate sheria gani? Kavunja sheria gani?
Amheshimu nani? Ni nani kamkosea heshima?
Kwahiyo kesi yake sio ugaidi tena? Bali ni maswala ya sheria na heshima?
Kufuata sheria ni kutovunja sheria. Hivyo kama ameshitakiwa kwa ugaidi, maana yake kavunja sheria ya ugaidi. Na ndiyo maana kesi hiko mahakamani ili mahakama itoe uamuzi. Kuvunja sheria ni kosa.
Nashangaa unapouliza kavunja sheria gani wakati tayari ameshitakiwa kwa sheria alovunja kuhusu ugaidi na yupo mahakamani.
Swala la heshima pamoja na kufuata sheria za nchi, ni vizuri kuheshimu mamlaka za nchi. Ukisoma katika mashitaka yake alifanya njama za kutaka kuhatarisha maisha ya kiongozi alotajwa. Heshima ni muhimu, usipokuwa na heshima unaweza pata wazo la kuondoa uhai wa mtu.
Mama hajasema kesi yake si ya ugaidi. Fahamu kwamba ugaidi ni kuvunja sheria za nchi. Na unapofikia kutokuwa na heshima basi hii itakufanya utende kosa kwani utasukumwa na mihemko ambayo utafanya maamuzi mabaya kama kutaka kudhuru viongozi.
Sheria haiangalii kiongozi wa chama, ni vema mahakama iachiwe uhuru wa kutoa maamuzi yake. Kwa nini hofu ijengwe. Ni watu wangapi Tanzania hii wameshitakiwa, hadi Mawaziri Mramba na Yona wakati huo wa Kikwete walishitakiwa na kupata adhabu. Alie kuwa mkuu wa Wilaya Hai ameshitakiwa na kufungwa miaka 30 na bado ana kesi. Mtu akitenda kosa ana haki ya kushitakiwa bila kuangalia wadhifa wake. Isipokuwa wale walio na kinga tu kwa mujibu wa sheria. Tena hata wao baadae inabidi washitakiwe, hii sheria iondolewe.
Tuache ushabiki, maslahi ya nchi lazima yalindwe. Si kila jambo tulichukulie kisiasa. Umetenda kosa utashitakiwa bila kujali wadhifa wako. Hakuna mtu mwenye uhalali wa kuvunja sheria nchi hii. Sweka ndani wote! Awe wa CCM, awe wa Chadema, Awe CUF hata ACT-Wazalendo na wengineo.