Rais Samia: Don't rock the boat. Biashara na uchumi vitayumba

Dua lipi tena!

Kazi ninayofanya ingeniwezesha kupata maendeleo makubwa pasingekuwepo na watu wa aina yenu mnaokwamisha juhudi zetu. Lakini najuwa tutafika tu kwa sababu hamuwezi kuzuia kujikomboa kwetu hata mhangaike vipi.
Nyie ndio aliwapenda sana Magufuli, mlioitikia na kukubali kuitwa wanyonge.
Huo ni uchaguzi wako!
 
Ninyi ndii mmejiaminisha kuwa mtu muwekezaji ni mwenye pesa ya kumwaga na haogopi hasara, na ukimwambia lete pesa anaenda benki kuzichota na kukuletea bila maswali.

Hili somo la uwekezaji , mkuu kwako ni kihindi, nakushauri tu hebu fanya zoezi dogo tu la uwekezaji, fungua frame ya duka.

Pengine utaelewa kwa nini maduka na biashara nyingi zimerudisha leseni za biashara.
 
Mama Samia charanga karata vizuri, tunahitaji mtaji wa tranquility.
Unatoa ushauri kwa mgeni ambaye nchi ikianguka kiuchumi hana hasara yoyote! Atarudi nchini kwake na kuendelea na maisha yake.
 
Scapegoating kama kawa. Wakati ule mkasema maduka yanafunga kisa Magufuli. Leo mnasema maduka yanafunga kisa Samia. Kuna jirani yangu hapa kafunga duka lake. Asingekuwa jirani nnayemfahamu kindakindaki na kufahamu pia kisa cha kufunga pengine nami ningeamini sababu ni Magufuli au Samia.

Tukirudi kwenye mada. Hakuna mazingira yoyote hapa Tanzania yatakayomfanya mwekezaji origino aliyejipanga na anayejua nini anataka kufanya atashindwa kuwekeza. Au kwa nini unadhani wachina wameweza kupenya hadi sehemu za ndani ndani humu Tanzania na kufungua tuviwanda vyao na wanapeta tu? Ni kwa sababu hawana tyme na power plays za wanasiasa. Wana skills, wana capital, wana business plan, wamecalculate risk-to-benefit ratio na wana vibali vyote vya kiserikali vya kufanya biashara. And they are winning!

Ukiona mtu anatanguliza issues zingine tofauti na issue kuu iliyo mezani ujue ana lake jambo. Usipoteze muda na watu wa aina hiyo.
 
Nyie watu wa kwenye madeski ya nadharia, msiojua hata kuuza nyanya kama machinga mna shida sana.
Sijui nikujibu vipi kama kuelewa kwenyewe huelewi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…