Rais Samia: Fedha ambazo zingegharamia Sherehe za miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, zigawanywe sawa

Rais Samia: Fedha ambazo zingegharamia Sherehe za miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, zigawanywe sawa

Watu wameshindwa kitofautisha baina ya usawa na sawa sawa.
Mnamlisha maneno mama, amesema fedha igawanywe kwa usawa na sio sawa sawa, pili swala la kununua meli sidhani kama kuna tatizo, mbona yule mwingine alikuwa ananunua vivuko mara kwa mara!
 
Ccm na Zanzibar ndiyo chanzo kikuu cha Tanganyika kuto kupiga hatua kubwa ya Maendeleo! Haiwezekani watu wako milioni mbili kasoro, halafu wapate haki sawa na watu milioni 60 kasoro!

Kwanza ka nchi kenyewe ni ka visiwa! Kamezungukwa na maji pande zote! Muda wowote ule kanamezwa tu na hayo maji! Halafu wanatudekea dekea hapa! Wajitenge halafu waone kama tutapungukiwa chochote.
Ulikuwa wapi ukashindwa kumshauri Nyerere aungane na Rwanda?
 
Ninachoelewa mtu akiona kitu ni mgizo kwa upande (kinamuumiza + hakina faida) anaubwaga, sasa kinachoshangaza kwa wale wanaosema Zanzibar ni mzigo kwenye Muungano kwani inashindikana nini kuubwaga? UWAMSHO, wao walikuwa wanawaamsha Wazanzibari katika kudai Zanzibar huru, jiungeni nao ili kwa pamoja na ninyi mdai Tanganyika huru. Faqat!
 
Hilo nalo neno. Nijuavyo mimi mambo ya Muungano yanaendeshwa kwa fedha zinazopatikana Tanzania bara ukiacha mikopo toka nje ya nchi. Mathalan, Zanzibar wana mamlaka ya kodi wakati mamlaka ya kodi ya Muungano, yaani TRA huwa haikusanyi kodi huko Zanzibar.

Wazanzibar lazima waelewe kuwa kama hawajadai kuchangia katika Muungano basi wakae kimya kuhusu mgawo wa kitu ambacho hawajachangia.
Screenshot_20210426-153005.jpg

Anza kusoma namba 10 na kuendelea.
 
fedha zilizotengwa kugharamia Sherehe za Muungano, amezibadilishia matumizi na kuagiza zigawanywe sawa kwa bara na Visiwani.
Dooh!

Zigawanywe SAWA?!!!

Watu milioni 1 wapewe kiwango sawa na watu milioni 60 ?!🙄

Hizo fedha zilipatikana kwa kuchanga viwango SAWA baina ya Tanganyika na Zanzibar?

Kwa nini zisirejeshwe zilikopatikana?
 
Nchi 2 huru ziliungana, hiyo theory yenu haileti mantik yoyote kama muliungana kwa bahati mbaya na nchi ndogo vunjeni muungano, hatamu za muungano zote ziko Tanganyika, Wazanzibar wataenda kuungana ata na Comoro ikibidi au watajitegemea
Au iwe wilaya ya mkoa wa Tanga tu
 
Huu Muungano either Tanganyika nao wapate serikali yao ambapo serikali ya Muungano itakufa kifo cha hiari ama tuwe nchi moja na serikali moja. Kwa set up ya ulivyo muungano sasa hauna maisha marefu.
Kabisa.. saivi Tanganyika imekosa mtetezi, ni shamba la bibi
 
Unaelewa nini kuhusu mgawanyo wa mapato ya muungano? Na je unajuaje kuwa hiyo ambayo haivuki bahari kuwa ndio kiasi kinachotakiwa kwa ajili ya watumishi wa serikali ya Muungano waliopo Zanzibar?
View attachment 1765027
Soma hapo kuanzia kipengele namba 10.

Asome vile vile na namba 15 inayo husu masuala ya Mafuta na mali asili - mwishoni mwa mwaka jana si nilimsikia Dk.Shein kama sikosei akisema utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi Baharini karibu na Zanzibar ni suala la Serikali ya mapinduzi Zanzibar na si la muhungano - alitoa impression as if Serikali mbili zimefikia makubaliano kwamba mafuta/gesi itakayo patikana/chimbwa Zanzibar ni mali ya Wazanzibari Serikali ya Muungano haiwahusu!!

Lakini umeme utakao zalishwa Bwawa la Rufiji ni mali ya muungano, Revenue zinakazo kuwa generated na mradi wa ufasirishaji wa crude oil kutoka Uganda kuja Bandari ya Tanga - hizo ni revenue za muungano lazima zigawiwe nusu kwa nusu, nisijue fedha za gesi ya Songo songo zinagawanwaje, dhahabu ya Geita, Almas ya Mwadui,Karafuu ya Zanzibar, Mwani nk.

Binafsi uwa napata wakati mgumu kuelewa kinacho endelea nyuma ya pazia, mengi yaliyo andikwa kwenye makaratasi/kanuni za makubaliano ya muungano wala hayawekewi maanani - miaka 50+ baada ya muungano bado tunazungumzia baadhi ya kero za muungano!!! Sio matatizo bali "KERO" za muungano - hii wapi na wapi??
 
Asome vile vile na namba 15 inayo husu masuala ya Mafuta na mali asili - mwishoni mwa mwaka jana si nilimsikia Dk.Shein kama sikosei akisema utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi Baharini karibu na Zanzibar ni suala la Serikali ya mapinduzi Zanzibar na si la muhungano - alitoa impression as if Serikali mbili zimefikia makubaliano kwamba mafuta/gesi itakayo patikana/chimbwa Zanzibar ni mali ya Wazanzibari Serikali ya Muhungano haiwahusu!!
Hili waliliondoa mapema baada ya kusikia kuna mafuta na gesi. Walichotaka ni kuwa rasilimali zao zisitumike katika muungano. Hapa chini umeeleza vizuri sana
Lakini umeme utakao zalishwa Bwawa la Rufiji ni mali ya muungano, Revenue zinakazo kuwa generated na mradi wa ufasirishaji wa crude oil kutoka Uganda kuja Bandari ya Tanga - hizo ni revenue za muungano lazima zigawiwe nusu kwa nusu, nisijue fedha za gesi ya Songo songo zinagawanywaje, dhahabu ya Geita, Almas ya Mwadui,Karafuu ya Zanzibar, Mwani nk.

Binafsi uwa napata wakati mgumu kuelewa kinacho endelea nyuma ya pazia, mengi yaliyo andikwa kwenye makaratasi/kanuni za makubaliano ya muungano wala hayawekewi maanani - miaka 50+ bado tunazungumzia kero za muungano, sio matatizo bali "KERO" hii wapi na wapi??
Kwakweli inasikitisha sana. Si hayo tu kuna mengi sana
1. Wametaka 21% ajira za muungano. Katika hiyo 21% ajira wanazopata Wazanzibar hazihusu mambo ya muungano. Kwa mfano, Mzanzibar anaajiriwa TAMISEMI, Wizara ya maji, Mawasiliano, Mifugo n.k. kwa sababu zipi

Lakini pia wanataka waajiriwe katika taasisi zisizo za muungano kama TBS wakati kuna ZBS
Kwa Zanzibar 21% ya ajira za muungano ni nyingi kuliko ajira za SMZ.

Licha ya fadhila hizo za ajira bado wanalipwa na JMT ambayo pesa zake zinatoka hazina Dar.
Hakuna ushahidi wowote wa Zanzibar kuchangia muungano kwa miaka takribani 40 sasa.

Kuna masuala ya gharama za muungano. Hapa hutawasikia Wazanzibar wakieleza nini mchango wao
Mathalani, wanachangia nini katika kuendesha wizara ya mambo ya nje! Lakini utawasiki wanataka nafasi sawa za uteuzi katika ubalozi.

Kuna suala la Wabunge! Ikiwa tunasema asilimia 4% ya mapato ya BoT ambayo ni mapato ya rasilimali na kodi za Watanganyika iende Zanzibar, ni vipi basi SMZ haihudumii wawakilishi wanaokuja Dodoma Bungeni?
Wale Wazanzibar wapo Bungeni kwa ajili ya Zanzibar katika mambo yasiyozidi 7. Kwanini Hazina Tanganyika ibebe mzigo wa kuwahudumia ?

Elimu ya Juu: Hili si suala la muungano. Kuna HESLB na ZHESLB . Kwanini basi HSELB ya bara iwape 'msaada; na si mkopo wanafunzi wa Zanzibar kwa wingi zaidi kuliko mkopo unaotolewa na ZHESLB?

Kuna suala la Akaunti ya pamoja ya fedha. Ukiuliza ni ya nini , Wazanzibar watakwambia ni ya kugawana misaada na fedha. Hakuna Mzanzibar atakayekuambia akaunti hiyo ni ya kuchangia na kutoa! hapana! wao ni kutoa tu

Zanzibar ina watu milioni 1.2 na nusu yao wanaishi Tanganyika. Kwa maana kwamba at anytime Zanzibar inakuwa na approx. watu laki 600. Kwa mwendo huu wa kuchota , sidhani kam wanasababu ya kufanya kazi.

Hawana sababu ya kufanya kazi kwasababu kadri mnavyolipa kodi bara, mnavyotumia rasilimali zenu wao wana mtego wa 4% . Sasa piga hesabu ya 4% ya pato la watu milioni 50 wa Tanganyika!

Suluhu hapa ni moja turejee katika rasimu ya Warioba, mambo 7 tu! mengine kila nchi ijishughulishe

Tanganyika inatoa resources nyingi sana kwenda kuhudumia eneo ambalo kwa Tanganyika ni jimbo moja la uchaguzi, huku tukiacha maeneo yanayochangia sana katika Pato la Taifa bila resources. Ni kwa dividend or return gani? Nani wa kumsemea ''Tanganyika'?

Tunabeba lawama za bure kwa fadhila tunazotoa. Je, haitoshi?

Kwasasa ''Changu ni Chetu, chako ni chako'' na hii ifike mwisho.

JokaKuu Pascal Mayalla Ngongo
 
Nguruvi3,

..thank u for tagging me on this thread.

..kwa kweli mimi concern yangu haiko kwenye suala la muungano sasa hivi.

..kinachonifikirisha sasa hivi ni kama ktk utawala wa Mama Samia Suluhu MAUAJI yatakoma au tutaendelea kusumbuliwa na WASIOJULIKANA?

..masuala yote mengine ni secondary, ninachoomba ni Mama Samia Suluhu akomeshe dhuluma na ukatili wa awamu ya 5, arejeshe HAKI kwa kila Mtanzania.
 
Back
Top Bottom