Rais Samia hapa ulikosea kidogo na sijui ni nani alikujaza Upepo na ukalisema hili

Rais Samia hapa ulikosea kidogo na sijui ni nani alikujaza Upepo na ukalisema hili

Ila mlikuwa mnamnanga samia kuwa ni Rais lelemama, kwamba magufuli alikuwa kidume anawakemea mabeberu,

Sasa Samia anaendesha nchi vile alivyokuwa anaendesha magufuli tunaanza kumlaumu

Hotuba Nimeisikiliza Yapo Ya Mabeberu Amesema Kwa Ukali Wakati Tunawategemea
Whether yuko sahihi au hayuko sahihi, Rais wa Nchi anatakiwa kuzungumza yale anayoyaamini hadharani. Na ndiyo maana SSH ni Rais wa JMT.

Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hasemi anayoyaamini wala kuonesha msimamo wake wazi juu ya yale anayoyaamini kwenye kuongoza nchi yake. JPM allifanya, BWM alifanya, JK alifanya na wengine. Kwa kuzungumza leo amefanya jambo la maana japo wahafidhina na wapinzani wake watamkosoa kwenye yale aliyosema lakini muhimu amesema na hakuna mtu angemsaidia kusema.

That is the President we need.
Nafikiri mnapaswa kumshauri vizuri. Rais asijiingize kwenye malumbano na Mabalozi wa nchi za nje hususani nchi za Magharibi Kama Marekani, ni hatari Sana kwake yeye mwenyewe binafsi na kwa nchi pia. Hao watu Wana mbinu nyingi Sana za kuweza kutudhibiti na kutuhujumu au kumhujumu huyo Rais endapo kama watapenda. Uwezo huo wanao.
 
Kauli yako kuwa Balozi za Kigeni ambazo zilikemea na kutaka Uchunguzi wa Kifo cha Mzee Kibao (ukiilenga hasa Marekani) kuwa zilifanya hivyo bila ya Baraka za Marais wao umeikosea mno Kuisema.

Na ukaenda mbali zaidi kusema kuwa kama kungekuwa na baya basi hao Marais wenye Uwakilishi wao kupitia Balozi zao nchini Tanzania wao wenyewe wangekupigiia.

Yaani Rais Samia pamoja na Urais wako wote huo na hao Wasaidizi wako hujui kuwa Sauti ya Balozi mwakilishi wa nchi ni Sauti ya Rais wa hiyo nchi husika?

Kiufupi ni kwamba huna Watu wazuri wa Masuala ya Kidiplomasia kwani kama ungekuwa nao nina uhakika wasingekuruhusu Kukizungumza hiki Kituko ulichokizungumza leo.

Namalizia kwa Kukushauri tu kwamba ukitaka haya Mataifa ya Kigeni yaache ulichokimaanisha kuwa ni Kihehere chao kwa Kukemea matukio mabaya ya Utekaji na Mauwaji basi nawe hakikisha unaongoza vyema na Kuchukua hatua stahiki kwa haraka.

Na ni matumaini yangu makubwa GENTAMYCINE kuwa baada ya leo Kukerwa nao (haya Mataifa makubwa ukiilenga Marekani) kwa Kukemea matukio mabaya nchini basi hata Wewe (kama Rais) hutotembeza tena Bakuli Kwao kuwaomba Misaada mbalimbali kwakuwa kwa sasa Tanzania ilipofikia chini yako ina uwezo wa Kujitegemea yenyewe Kiuchumi, Kisiasa, Kijamii na tayari imeshaifikia Marekani kwa kila Kitu.

Soma Pia: Rais Samia kwa Mabalozi: Hatupo hapa kuelekezwa nini cha kufanya kwenye nchi yetu
GENTAMYCINE Dkt Samia sijui kimempata kitu gani. Mi nilitegemea angekaa tu kimya maana wenzetu kila kauli wanaenda field, yaani wanaenda chimbo na wanakuwa na mkakati wa kizazi, na vizazi. Nadhani tupo vitani mpaka now na hayo mataifa ya Magharibi in addition na vita tuliyonayo ya dharula ya kifo cha rais aliyekuwa madarakani Dkt Magufuli. Nadhani zile 4R zake angeendelea nazo kimya kimya bila kuleta taharuki na huku mengine akishaghulikia kimya kimya. Kauli tata ni mbaya sana kwa wenzetu wa magharibi kwa sababu maisha yao bila Africa ni magumu sana.
 
Nafikiri mnapaswa kumshauri vizuri. Rais asijiingize kwenye malumbano na Mabalozi wa nchi za nje hususani nchi za Magharibi Kama Marekani, ni hatari Sana kwake yeye mwenyewe binafsi na kwa nchi pia. Hao watu Wana mbinu nyingi Sana za kuweza kutudhibiti na kutuhujumu au kumhujumu huyo Rais endapo kama watapenda. Uwezo huo wanao.
Mkuu with due respect!

Ndiyo maana yeye ni Rais wa JMT, unadhani hajui consequences? gharama ya kuwa Rais wa nchi ndiyo hiyo. Hauwezi kuwa mtu neutral.

Na mimi kama Mtanzania nilitamani nisikie Raia namba moja wa Nchi ana mtazamo gani kuhusu mabalozi wa nje wanapozungumzia mambo yetu wayazungumziaje. Ukiwa na Rais muoga huna Nchi mzee.
 
Kiufupi Mimi binafsi namlaumu sana magu kutuachia bwawa lisilo na samaki zaid ya giant weeds yani akili ni zero kabisa kabisa hakuna kitu kichwani
Kuwa na adabu wewe!! Bwawa umeliacha katikati ya mapaja ya mkeo unakoegelea na kuzama hadi kichwa. Nyoko sana wew. Hotuba ya Amiri Jeshi Mkuu imekutoweni kwenye mstari mmekaa kaa vipanya vilivyonyeshewa na mvua.
 
Leo ndio amenikosha kwa furaha. Hatuwezi kuwa taifa la watu wakujikomba. Akina chief Mangingo endeleeni kulamba miguu. Leo laongea kama Rais wa nchi. Japo yapo siyaelewi ya rasilimali za nchi
 
Mkuu with due respect!

Ndiyo maana yeye ni Rais wa JMT, unadhani hajui consequences? gharama ya kuwa Rais wa nchi ndiyo hiyo. Hauwezi kuwa mtu neutral.

Na mimi kama Mtanzania nilitamani nisikie Raia namba moja wa Nchi ana mtazamo gani kuhusu mabalozi wa nje wanapozungumzia mambo yetu wayazungumziaje. Ukiwa na Rais muoga huna Nchi mzee.
Kwani Sasa hivi ana nchi?

Sitaki kueleza yasiyotakiwa kuelezea hapa hadharani. We have completely nothing. Huwezi kuwa na jeuri ikiwa kila kitu unamtegemea mtu nwingine akusaidie ili uinuke. Wakidhamiria kumdhibiti, itakuwa ni kazi ndogo Sana kwao.
 
Unamuuliza nani? Wew unataka nini? Huyo ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii. Ameshalihutubia taifa hayo mengine yasiyokufurahisha yavumilie kijana.
Usimjaze upepo bure, atahujumiwa. Wazungu Wana mbinu nyingi Sana. Usiwachezee.

Waingereza kwenye kuwadhibiti watu kama hao huwa Wana msemo wao kwamba "There is more than one way of skining a cat."
 
Kauli yako kuwa Balozi za Kigeni ambazo zilikemea na kutaka Uchunguzi wa Kifo cha Mzee Kibao (ukiilenga hasa Marekani) kuwa zilifanya hivyo bila ya Baraka za Marais wao umeikosea mno Kuisema.

Na ukaenda mbali zaidi kusema kuwa kama kungekuwa na baya basi hao Marais wenye Uwakilishi wao kupitia Balozi zao nchini Tanzania wao wenyewe wangekupigiia.

Yaani Rais Samia pamoja na Urais wako wote huo na hao Wasaidizi wako hujui kuwa Sauti ya Balozi mwakilishi wa nchi ni Sauti ya Rais wa hiyo nchi husika?

Kiufupi ni kwamba huna Watu wazuri wa Masuala ya Kidiplomasia kwani kama ungekuwa nao nina uhakika wasingekuruhusu Kukizungumza hiki Kituko ulichokizungumza leo.

Namalizia kwa Kukushauri tu kwamba ukitaka haya Mataifa ya Kigeni yaache ulichokimaanisha kuwa ni Kihehere chao kwa Kukemea matukio mabaya ya Utekaji na Mauwaji basi nawe hakikisha unaongoza vyema na Kuchukua hatua stahiki kwa haraka.

Na ni matumaini yangu makubwa GENTAMYCINE kuwa baada ya leo Kukerwa nao (haya Mataifa makubwa ukiilenga Marekani) kwa Kukemea matukio mabaya nchini basi hata Wewe (kama Rais) hutotembeza tena Bakuli Kwao kuwaomba Misaada mbalimbali kwakuwa kwa sasa Tanzania ilipofikia chini yako ina uwezo wa Kujitegemea yenyewe Kiuchumi, Kisiasa, Kijamii na tayari imeshaifikia Marekani kwa kila Kitu.

Soma Pia: Rais Samia kwa Mabalozi: Hatupo hapa kuelekezwa nini cha kufanya kwenye nchi yetu
Usipotoshe watu. Kama balozi ana neno la Rais wake kwa TRais wetu kuna protokali yake ya kulifikisha serikalini na kuna level yake ya kuwaasiliana nao.

Rais ws nchi yoyote ya nje anaongea na Rais wetu kwa protokali zake.

Tais Samia yupo sahihi 100%.
 
Back
Top Bottom