Rais Samia, hata siku moja mwekezaji habembelezwi kuja kuwekeza nchini, tafadhali zingatia yafuatayo watakuja wenyewe

Rais Samia, hata siku moja mwekezaji habembelezwi kuja kuwekeza nchini, tafadhali zingatia yafuatayo watakuja wenyewe

Wakati wawekezaji wanapokuja hapa, unashindwa kujadiliana nao na kuelewana jinsi utakavyonufaika na uwekezaji wao, unawaachia mianya ya kukugonga katika mikataba, halafu wewe unachekelea umepata uwekezaji!
Ikiwa una wawekezaji wale wa kubembeleza waje nchini, ndio unajiwekea mazingira ya kugongwa kwenye mikataba, maana kila kipengele wanakuambia sisi hicho hatutaki, na ukikiweka tunaondoka, na wewe unajichekesha na kusema sawa basi nitakiondoa
 
Hoja makini..ila shida ni huu upuuzi wa kijani..hao wahuni wanachoangalia ni maslahi yao tu.

#MaendeleoHayanaChama
Ndio maana tunasema upinzani wa siasa nchini ulio makini una faida kwa nchi. Siku CCM wakielewa hilo labda itasaidia

Katika upinzani makini huwezi kusema mikataba ya uwekezaji ni siri.
 
Hakuizuii mkuu, ila kunawawezesha kiasi kwamba kina Dangote wanaweza kukuta hawahitaji kuja. Kumbuka, kiwanda cha Dangote kikiwa cha mzawa kuna faida kwamba mzawa hatahitaji ku-repatriate profi (yaani kutoa fedha faida ya kiwanda kwenda nje), bali anakuwa na nafasi kubwa na motivation ya ku-diversify kwenda investment nyingine ndani ya nchi badala ya kupeleka capital kwenda kwao

Sasa suala kubwa ni kwamba, ili Dangote iwe ya Mtanzania badala ya Mnigeria, utamsaidiaje huyu Mtanzania?

Zenawi wa Ethiopia alijaribu, lakini hakuwa makini, kwa sababu jitihada yake ya ku-support investors wa ndani ilisababisha inflation kubwa sana. Ni kama vile useme Nitatoa bilioni 2 za Tanzania kwa watanzania efu mja waanzishe maduka. Matokeo ni kwamba hela ya ndani inakuwa nyingi sana kwenye mzunguko, na nyanya zinapanda bei hadi kufikia shs elfu tano nyanya moja.

Lakini Dangote akija, anakuja na foreign capital ambayo sanasana itafanya shilingi ndio iadimike, kwa sababu inabidi abadilishe dola zake kuwa shilingi ili alipe wafanyakazi, na demand ya shilingi inakuwa kubwa, wakati dollar ipo nje nje inaletwa na kina Dangate. Lakini bado itabdidi uwe makini, maana Dangote akitaka kutoa faida itabidi umpe dola, hawezi kutoa shilingi kwenda Nigeria
Mkuu, nadhani sasa nimeelewa ni wapi tunaposhindwa kuelewana.
Mimi sizungumzii Dangote wa kiTanzania awepo leo hii.
Hii ni process ya muda mrefu ya kwajenga Angote wetu.

Sikumbuki, au sijasikia tu, toka Samia aingie akitamka neno SIDO, wewe umewahi kumsikia?
Umewahi kumsikia akizungumzia sera za serikali yake zinazolenga juhudi hizo?
Ila kila siku nasikia habari za "matrilioni ya wawekezaji' yanayosemekana kayapata kila anapokwenda kwenye ziara zake huko nje.

Acha nisiwe ninaandika mengi humu kwenye mada muhimu kama hii.
 
Ikiwa una wawekezaji wale wa kubembeleza waje nchini, ndio unajiwekea mazingira ya kugongwa kwenye mikataba, maana kila kipengele wanakuambia sisi hicho hatutaki, na ukikiweka tunaondoka, na wewe unajichekesha na kusema sawa basi nitakiondoa
hapa tumeelewana barabara. Ahsante sana.
 
Mkuu, nadhani sasa nimeelewa ni wapi tunaposhindwa kuelewana.
Mimi sizungumzii Dangote wa kiTanzania awepo leo hii.
Hii ni process ya muda mrefu ya kwajenga Angote wetu.

Sikumbuki, au sijasikia tu, toka Samia aingie akitamka neno SIDO, wewe umewahi kumsikia?
Umewahi kumsikia akizungumzia sera za serikali yake zinazolenga juhudi hizo?
Ila kila siku nasikia habari za "matrilioni ya wawekezaji' yanayosemekana kayapata kila anapokwenda kwenye ziara zake huko nje.

Acha nisiwe ninaandika mengi humu kwenye mada muhimu kama hii.
Sawa kabisa, kumbe tuko wote. Acha Dangote wa nche atutengenezee Dangote wa ndani, na kwa sasa tumtengenezee mazingira mazuri Dangote wa nje ili tuje tuwe na Dangote wa ndani.
 
Nakumbk hata aliyekuw MP wa Arusha mjini mhe Lema aliwah sema ushabiki ktk mambo ya msingi ndio kikwazo cha maendeleo nchini,. Yaani tunashindana kama timu za mpira
Unajua huwa naangalia timu za mpira, yaani utakuta mchezaji wa timu moja kama aliokota mprira uliotoka akidhani wao ndio wanarusha, akaambiwa na refa ni timu pinzani wanatakiwa kurusha, unajua huwa hamkabidhi mchezaji wa timu pinzani mpira, anautupia pembeni ili akauokote mwenyewe!
 
Huwa naziona jitihada nyingi za raisi Samia kubembeleza wawekezaji kuja kuwekeza nchini, hadi namuonea huruma kwa sababu naelewa anapigia debe kitu ambacho sio rahisi kufanikiwa. Napenda kumwambia Raisi Samia kwamba wawekezaji hawavutwi au kushawishiwa kwenda kuwekeza kwenye nchi fulani, huwa ni nguvu ya soko (market forces) na mazingira ya uwekezaji katika uchumi huria vitakavyoamua kama wawekezaji watakuja au la.

Raisi Samia unaweza ukaenda Marekani na kwingineko hata kuwatumbuiza wawekezaji kwa taarabu ukipenda, lakini kama Tanzania haina conducive investment environment hawaji ng'o! Uwe unajiuliza, nini kitamfanya mwekezaji aje Tanzania badala ya kwenda nchi nyingine? Namna gani tunaifanya Tanzania kuwa na comparative advantage katika kuvutia wawekezaji? Kumbuka chema chajiuza, kibaya chajitembeza!

Sasa baadhi ya mambo wawekezaji wanayoangalia kuleta investment ni haya hapa, na kwa kweli nimejaribu kutaja karibu yote;
  1. Upatikanaji wa umeme wa uhakika
  2. Upatikanaji wa maji wa uhakika
  3. Soko la uhakika la kile wanachotaka kuwekeza (local na Tanzania as an exporter to regional markets)
  4. Sera za uwekezaji zilizo wazi (policy transparency) na zilizohakikishwa (policy certainty)
  5. Kutokuwepo ukiritimba (red-tape au bureaucracy)
  6. Urahisi wa kuishi Tanzania (residency permits)
  7. Kutokuwepo kwa rushwa (level of corruption in the country)
  8. Uaminifu na uchapakazi wa wafanyakazi (trustworthy and hardworking labor force, sio wadokozi ofisini laptop zikipotea hovyo nk)
  9. Urahisi wa kutoka na kuingia Tanzania (kupata visa, urahisi wa flights kuja nchini nk)
  10. Miundo mbinu ya barabara, airports, majengo ya ofisi nk
  11. Ubora na uhodari (efficiency) na cost za bandari katika kutoa huduma
  12. Kodi rafiki za TRA kwa wawekezaji ambazo zinajulikana kwa kanuni sio za kubambikiana
  13. Sheria za kazi zilizo rafiki (labour laws nchini)
  14. Sheria za utoaji faida (laws and regulations for repatriation of profits)
  15. Usalama katika nchi pamoja na kutokuwapo uhalifu
  16. Utulivu na amani katika siasa za ndani (CCM Vs vyama vya upinzani)
  17. Huduma za afya (matibabu)
  18. Mazingira stareheshe (uzuri wa hoteli na vivutio nk)
Sasa niambie Raisi Samia, kama ungetakiwa kutoa marks kwa kila kipengele hapo juu, ungetoa ngapi? Sasa ukifanyia kazi hayo juu, wala huhitaji kupiga vuvuzela kuita wawekezaji, watakuja wenyewe!

Mfano, ni miaka mingapi wawekezaji wanalia na usumbufu wa residency permits hapa Tanania? Kwa nini hili halijaangaliwa? Kwanza serikali haitoi hata kile kitu kinaitwa permanent residency permit kwa wawekezaji hata wale wakubwa na waliooa Watanzania! Wanasumbuliwa sana na uhamiaji ku-renew permits.

Pili, Watanzania wanajulikana duniani kama wafanyakazi wavivu na wezi! Watu wanaisema nchi yetu vibaya sana katika udokozi ofisini nk. Watu wanaiba hadi stapple pins, sukari, vijiko vya chai vya ofisi! Bosi akisahau laptop mahali imekwenda! Wizi wa mitaani ndio usiseme. Wewe unajua ukiwa uarabuni huko ukasahau kufunga vioo vya gari, bado utaikuta laptop yako na simu kwenye gari, lakini sio hapa kwetu - kwanza wanavunja gari wakiona laptop kwenye gari.

Haya, upatikanaji wa umeme na maji je, ninahitaji kusema hapo kweli? Unamwambia mwekezaji aje kuja kukabiliana na matatizo ya umeme na maji nchi atakuja kufanya nini, kwa sababu anatupenda sana Watanzania au wewe raisi?

Kuna wawekezaji wamelalamika viongozi wa serikali hawapatikaniki, ni rahisi kufanya appointment na kukutana na raisi wa USA kuliko waziri au katibu mkuu Tanzania. Kwa nini? Kwa nini hawa wateule wako wanajifanya miungu watu hard to get? Wawekezaji wanakuambia ilituchukua miezi sita kumwona waziri! Waambie watu wako hawa waache kujifanya miungu watu, wawe na open door policy katika kuhudumia watu, watanzania na wawekezaji.

Vipi urahisi wa kuja au kutoka Tanzania? Achana na sera za visa arrangement reciprocation, yamepitwa na wakati. Kama Marekani wanatusumbua kutupa visa, wewe waambie Wamarekani wakija watapata visa airport kirahisi kabisa. Scrap visa requirements kwa nchi ambazo zina potential za wafanyabiashara kuwekeza nchini. Ifanye Tanzania kuwa the easiest country to fly to, itasaidia kuleta wewekezaji na watalii. Mara nyingi watalii wanazalisha wawekezaji. Kumbuka hilo.

Halafu kumbuka huu ugomvi wenu CCM na vyama vya upinzani una athari kubwa sana katika kuvutia wawekezaji. Hawapendi kusikia sijui Mbowe kafunguliwa kesi za uhaini, Lissu kaomba hifadhi Ubelgiji - unahitaji kuwa concerned na hayo mambo, usiseme hayakuhusu! Wawekezaji siku zote wanapenda strong political opposition kama check na balance dhidi ya chama tawala, hawapendi upinzani dhaifu katika nchi wanazowekeza. Hivyo kuwa na upinzani ulio strong is a good thing for investments - waambie watu wako wa CCM pamoja na viongozi wako wa Bunge. Wasibeze hoja za upinzani Bungeni hasa zenye mshiko, wawekezaji wanasikia!

Una kitu kinaitwa Tanzania Investment Centre, hivi wanafanya kazi gani? Waulize katika hayo hapo juu wana mkakati wowote? Mara ngapi wamekuja kuku-consult kwamba Mheshimiwa raisi hili na hili vinatukwamisha tunaomba uingilie kati? Wapowapo tu wanasubiri mtu agonge hodi waanze kumsumbua badala ya kumsaidia. Wanahitaji kuwa pro-active, waendane na vision yako, sio wakae ofisini wasubiri wewe ukapige debe Marekani ili waje kugongewa hodi.
Yote hayo yameboreshwa na ndio maana unaona wawekezaji wanapishana kila siku Tanzania uongozi wa Rais Samia Suluhu umezalimilia kukuza uwekezaji pia kupitia uwekezaji vijana wapate fursa
 
Sawa kabisa, kumbe tuko wote. Acha Dangote wa nche atutengenezee Dangote wa ndani, na kwa sasa tumtengenezee mazingira mazuri Dangote wa nje ili tuje tuwe na Dangote wa ndani.
Hapana.
Dangote hata siku moja hana nia wala sababu ya kututengenezea mshindani wake. Hili ni jukumu letu, na kuhakikisha kwamba mazingira mazuri kabisa yapo kwa Dangote wetu kupatikana.

Haya "mazingira mazuri" huoni kwamba ni ya faida kwetu wenyewe hasa, zaidi ya hao wanaotoka nje? Ndiyo yawekwe mazingira mazuri ya uwekezaji, hili linamanufaa zaidi kwetu hata zaidi ya hao wa kutoka nje. Sote tunataka umeme mzuri na chee, maji, barabara, reli, n'k..
 
Mkuu 'Synthesizer', ahsante sana kwa mada makini sana hii, nitarudi hapo baadae nikipata nafasi nikusome vizuri zaidi kama nilivyoahidi huko mwanzo.
Ninajua tunakubaliana katika mengi ndani ya mada hii.
 
Hapana.
Dangote hata siku moja hana nia wala sababu ya kututengenezea mshindani wake. Hili ni jukumu letu, na kuhakikisha kwamba mazingira mazuri kabisa yapo kwa Dangote wetu kupatikana.

Haya "mazingira mazuri" huoni kwamba ni ya faida kwetu wenyewe hasa, zaidi ya hao wanaotoka nje? Ndiyo yawekwe mazingira mazuri ya uwekezaji, hili linamanufaa zaidi kwetu hata zaidi ya hao wa kutoka nje. Sote tunataka umeme mzuri na chee, maji, barabara, reli, n'k..
Hahaha! Kweli. Usichukulie literally. Mkuu, angalia nimesema acha Dangote wa nje atutengenezee Dangote wa ndani, na kwa sasa tumtengenezee mazingira mazuri Dangote wa nje ili tuje tuwe na Dangote wa ndani.

Kwa hiyo jukumu la kutengeneza Dangote wa ndani ni letu, Dangote wa nje ana facilitate mazingira, sio kwamba yeye ndio anatungenezea. Anatusaidia pia katika technology transfer kuja nchini. Anao mainjinia na wataalamu alioajiri wazawa, ambao sasa wanaelewa nini kinahusika kutengeneza cement na wanaweza kuwezeshwa kuanzisha viwanda, hata kwa ubia
 
Yote hayo yameboreshwa na ndio maana unaona wawekezaji wanapishana kila siku Tanzania uongozi wa Rais Samia Suluhu umezalimilia kukuza uwekezaji pia kupitia uwekezaji vijana wapate fursa
Hilo ni jibu la kisiasa, tunaloita generic response, ambayo Watanzania ni hodari sana kuyatoa(Wakenya wanaita Kiswahili mingi). Unajibu bila kujibu.

Niambie kipi kimeboreshwa kuhusu visa na residency permits kwanza. Tuanzie hapo, specificities.

Unawaambiaje Wamarekani njooni kuwekeza Tanzania ina amani wakati wanajua Lissu yuko Ubelgiji mkimbizi wa siasa hadi leo, Lema yuko Canada, hutaki mjadala wa Katiba mpya wapinzani wanaopendekeza? Utawadanganya Wamarekani?

Wakikuambia katiba mpya ni positive thing kwa nchi yeyote hata sisi USA tumefanya amendments za katiba mara nyingi, unawajibu hiyo sio priority yangu au sio jambo lilikuwa kwenye ilani ya chama changu kwenye uchaguzi. You must be joking. Watakuona unawapotezea muda.
 
Very deep, bila shaka watakuelewa..

unataka mwekezaji aje huku watu wako maofisi kila kitu rushwa na mambo mengi konakona.

Unataka wawekezaji waje huku work force yako kwa kiasi kikubwa ni unskilled, wavivu, watu wako sio waaminifu wadokozi, wezi wanawaza maisha rahisi

Unataka wawekezaji waje wafokewe na makada wasiojua lolote wala chochote, zaidi ya uchawa, uchawi, na ngono ndio vimewafikisha hapo.

Unataka wawekezaji waje halafu makada wa chama chetu wawalazimishe wawape kazi ndugu zao unskilled, wezi nk, makada walazimishe vikampuni vyao vipate contracts za kazi.

Weka sawa mifumo, tengeneza jamii inayoishi kwa misingi, chama cha makada kikubali dunia imebadirika nacho kibadili mfumo wake wa ujinga ujinga kulea na kukuza vijana wa hovyo...nk nk
 
Huwa naziona jitihada nyingi za raisi Samia kubembeleza wawekezaji kuja kuwekeza nchini, hadi namuonea huruma kwa sababu naelewa anapigia debe kitu ambacho sio rahisi kufanikiwa. Napenda kumwambia Raisi Samia kwamba wawekezaji hawavutwi au kushawishiwa kwenda kuwekeza kwenye nchi fulani, huwa ni nguvu ya soko (market forces) na mazingira ya uwekezaji katika uchumi huria vitakavyoamua kama wawekezaji watakuja au la.

Raisi Samia unaweza ukaenda Marekani na kwingineko hata kuwatumbuiza wawekezaji kwa taarabu ukipenda, lakini kama Tanzania haina conducive investment environment hawaji ng'o! Uwe unajiuliza, nini kitamfanya mwekezaji aje Tanzania badala ya kwenda nchi nyingine? Namna gani tunaifanya Tanzania kuwa na comparative advantage katika kuvutia wawekezaji? Kumbuka chema chajiuza, kibaya chajitembeza!

Sasa baadhi ya mambo wawekezaji wanayoangalia kuleta investment ni haya hapa, na kwa kweli nimejaribu kutaja karibu yote;
  1. Upatikanaji wa umeme wa uhakika
  2. Upatikanaji wa maji wa uhakika
  3. Soko la uhakika la kile wanachotaka kuwekeza (local na Tanzania as an exporter to regional markets)
  4. Sera za uwekezaji zilizo wazi (policy transparency) na zilizohakikishwa (policy certainty)
  5. Kutokuwepo ukiritimba (red-tape au bureaucracy)
  6. Urahisi wa kuishi Tanzania (residency permits)
  7. Kutokuwepo kwa rushwa (level of corruption in the country)
  8. Uaminifu na uchapakazi wa wafanyakazi (trustworthy and hardworking labor force, sio wadokozi ofisini laptop zikipotea hovyo nk)
  9. Urahisi wa kutoka na kuingia Tanzania (kupata visa, urahisi wa flights kuja nchini nk)
  10. Miundo mbinu ya barabara, airports, majengo ya ofisi nk
  11. Ubora na uhodari (efficiency) na cost za bandari katika kutoa huduma
  12. Kodi rafiki za TRA kwa wawekezaji ambazo zinajulikana kwa kanuni sio za kubambikiana
  13. Sheria za kazi zilizo rafiki (labour laws nchini)
  14. Sheria za utoaji faida (laws and regulations for repatriation of profits)
  15. Usalama katika nchi pamoja na kutokuwapo uhalifu
  16. Utulivu na amani katika siasa za ndani (CCM Vs vyama vya upinzani)
  17. Huduma za afya (matibabu)
  18. Mazingira stareheshe (uzuri wa hoteli na vivutio nk)
Sasa niambie Raisi Samia, kama ungetakiwa kutoa marks kwa kila kipengele hapo juu, ungetoa ngapi? Sasa ukifanyia kazi hayo juu, wala huhitaji kupiga vuvuzela kuita wawekezaji, watakuja wenyewe!

Mfano, ni miaka mingapi wawekezaji wanalia na usumbufu wa residency permits hapa Tanania? Kwa nini hili halijaangaliwa? Kwanza serikali haitoi hata kile kitu kinaitwa permanent residency permit kwa wawekezaji hata wale wakubwa na waliooa Watanzania! Wanasumbuliwa sana na uhamiaji ku-renew permits.

Pili, Watanzania wanajulikana duniani kama wafanyakazi wavivu na wezi! Watu wanaisema nchi yetu vibaya sana katika udokozi ofisini nk. Watu wanaiba hadi stapple pins, sukari, vijiko vya chai vya ofisi! Bosi akisahau laptop mahali imekwenda! Wizi wa mitaani ndio usiseme. Wewe unajua ukiwa uarabuni huko ukasahau kufunga vioo vya gari, bado utaikuta laptop yako na simu kwenye gari, lakini sio hapa kwetu - kwanza wanavunja gari wakiona laptop kwenye gari.

Haya, upatikanaji wa umeme na maji je, ninahitaji kusema hapo kweli? Unamwambia mwekezaji aje kuja kukabiliana na matatizo ya umeme na maji nchi atakuja kufanya nini, kwa sababu anatupenda sana Watanzania au wewe raisi?

Kuna wawekezaji wamelalamika viongozi wa serikali hawapatikaniki, ni rahisi kufanya appointment na kukutana na raisi wa USA kuliko waziri au katibu mkuu Tanzania. Kwa nini? Kwa nini hawa wateule wako wanajifanya miungu watu hard to get? Wawekezaji wanakuambia ilituchukua miezi sita kumwona waziri! Waambie watu wako hawa waache kujifanya miungu watu, wawe na open door policy katika kuhudumia watu, watanzania na wawekezaji.

Vipi urahisi wa kuja au kutoka Tanzania? Achana na sera za visa arrangement reciprocation, yamepitwa na wakati. Kama Marekani wanatusumbua kutupa visa, wewe waambie Wamarekani wakija watapata visa airport kirahisi kabisa. Scrap visa requirements kwa nchi ambazo zina potential za wafanyabiashara kuwekeza nchini. Ifanye Tanzania kuwa the easiest country to fly to, itasaidia kuleta wewekezaji na watalii. Mara nyingi watalii wanazalisha wawekezaji. Kumbuka hilo.

Halafu kumbuka huu ugomvi wenu CCM na vyama vya upinzani una athari kubwa sana katika kuvutia wawekezaji. Hawapendi kusikia sijui Mbowe kafunguliwa kesi za uhaini, Lissu kaomba hifadhi Ubelgiji - unahitaji kuwa concerned na hayo mambo, usiseme hayakuhusu! Wawekezaji siku zote wanapenda strong political opposition kama check na balance dhidi ya chama tawala, hawapendi upinzani dhaifu katika nchi wanazowekeza. Hivyo kuwa na upinzani ulio strong is a good thing for investments - waambie watu wako wa CCM pamoja na viongozi wako wa Bunge. Wasibeze hoja za upinzani Bungeni hasa zenye mshiko, wawekezaji wanasikia!

Una kitu kinaitwa Tanzania Investment Centre, hivi wanafanya kazi gani? Waulize katika hayo hapo juu wana mkakati wowote? Mara ngapi wamekuja kuku-consult kwamba Mheshimiwa raisi hili na hili vinatukwamisha tunaomba uingilie kati? Wapowapo tu wanasubiri mtu agonge hodi waanze kumsumbua badala ya kumsaidia. Wanahitaji kuwa pro-active, waendane na vision yako, sio wakae ofisini wasubiri wewe ukapige debe Marekani ili waje kugongewa hodi.
Sema wewe kiazi, sisi mihogo tutaambiwa tuna mizizi. Ukweli mtupu umeandika. Hakuna mtu anayebembelezwa kufanya biashara sehemu fulani. Mwekezaji ni mfanya biashara na si mzee wa kanisa. Anachoangalia ni sehemu yenye maslahi kwa uwezekaji wake. Mengine ni kujidanganya tu.
 
Huwa naziona jitihada nyingi za raisi Samia kubembeleza wawekezaji kuja kuwekeza nchini, hadi namuonea huruma kwa sababu naelewa anapigia debe kitu ambacho sio rahisi kufanikiwa. Napenda kumwambia Raisi Samia kwamba wawekezaji hawavutwi au kushawishiwa kwenda kuwekeza kwenye nchi fulani, huwa ni nguvu ya soko (market forces) na mazingira ya uwekezaji katika uchumi huria vitakavyoamua kama wawekezaji watakuja au la.

Raisi Samia unaweza ukaenda Marekani na kwingineko hata kuwatumbuiza wawekezaji kwa taarabu ukipenda, lakini kama Tanzania haina conducive investment environment hawaji ng'o! Uwe unajiuliza, nini kitamfanya mwekezaji aje Tanzania badala ya kwenda nchi nyingine? Namna gani tunaifanya Tanzania kuwa na comparative advantage katika kuvutia wawekezaji? Kumbuka chema chajiuza, kibaya chajitembeza!

Sasa baadhi ya mambo wawekezaji wanayoangalia kuleta investment ni haya hapa, na kwa kweli nimejaribu kutaja karibu yote;
  1. Upatikanaji wa umeme wa uhakika
  2. Upatikanaji wa maji wa uhakika
  3. Soko la uhakika la kile wanachotaka kuwekeza (local na Tanzania as an exporter to regional markets)
  4. Sera za uwekezaji zilizo wazi (policy transparency) na zilizohakikishwa (policy certainty)
  5. Kutokuwepo ukiritimba (red-tape au bureaucracy)
  6. Urahisi wa kuishi Tanzania (residency permits)
  7. Kutokuwepo kwa rushwa (level of corruption in the country)
  8. Uaminifu na uchapakazi wa wafanyakazi (trustworthy and hardworking labor force, sio wadokozi ofisini laptop zikipotea hovyo nk)
  9. Urahisi wa kutoka na kuingia Tanzania (kupata visa, urahisi wa flights kuja nchini nk)
  10. Miundo mbinu ya barabara, airports, majengo ya ofisi nk
  11. Ubora na uhodari (efficiency) na cost za bandari katika kutoa huduma
  12. Kodi rafiki za TRA kwa wawekezaji ambazo zinajulikana kwa kanuni sio za kubambikiana
  13. Sheria za kazi zilizo rafiki (labour laws nchini)
  14. Sheria za utoaji faida (laws and regulations for repatriation of profits)
  15. Usalama katika nchi pamoja na kutokuwapo uhalifu
  16. Utulivu na amani katika siasa za ndani (CCM Vs vyama vya upinzani)
  17. Huduma za afya (matibabu)
  18. Mazingira stareheshe (uzuri wa hoteli na vivutio nk)
Sasa niambie Raisi Samia, kama ungetakiwa kutoa marks kwa kila kipengele hapo juu, ungetoa ngapi? Sasa ukifanyia kazi hayo juu, wala huhitaji kupiga vuvuzela kuita wawekezaji, watakuja wenyewe!

Mfano, ni miaka mingapi wawekezaji wanalia na usumbufu wa residency permits hapa Tanania? Kwa nini hili halijaangaliwa? Kwanza serikali haitoi hata kile kitu kinaitwa permanent residency permit kwa wawekezaji hata wale wakubwa na waliooa Watanzania! Wanasumbuliwa sana na uhamiaji ku-renew permits.

Pili, Watanzania wanajulikana duniani kama wafanyakazi wavivu na wezi! Watu wanaisema nchi yetu vibaya sana katika udokozi ofisini nk. Watu wanaiba hadi stapple pins, sukari, vijiko vya chai vya ofisi! Bosi akisahau laptop mahali imekwenda! Wizi wa mitaani ndio usiseme. Wewe unajua ukiwa uarabuni huko ukasahau kufunga vioo vya gari, bado utaikuta laptop yako na simu kwenye gari, lakini sio hapa kwetu - kwanza wanavunja gari wakiona laptop kwenye gari.

Haya, upatikanaji wa umeme na maji je, ninahitaji kusema hapo kweli? Unamwambia mwekezaji aje kuja kukabiliana na matatizo ya umeme na maji nchi atakuja kufanya nini, kwa sababu anatupenda sana Watanzania au wewe raisi?

Kuna wawekezaji wamelalamika viongozi wa serikali hawapatikaniki, ni rahisi kufanya appointment na kukutana na raisi wa USA kuliko waziri au katibu mkuu Tanzania. Kwa nini? Kwa nini hawa wateule wako wanajifanya miungu watu hard to get? Wawekezaji wanakuambia ilituchukua miezi sita kumwona waziri! Waambie watu wako hawa waache kujifanya miungu watu, wawe na open door policy katika kuhudumia watu, watanzania na wawekezaji.

Vipi urahisi wa kuja au kutoka Tanzania? Achana na sera za visa arrangement reciprocation, yamepitwa na wakati. Kama Marekani wanatusumbua kutupa visa, wewe waambie Wamarekani wakija watapata visa airport kirahisi kabisa. Scrap visa requirements kwa nchi ambazo zina potential za wafanyabiashara kuwekeza nchini. Ifanye Tanzania kuwa the easiest country to fly to, itasaidia kuleta wewekezaji na watalii. Mara nyingi watalii wanazalisha wawekezaji. Kumbuka hilo.

Halafu kumbuka huu ugomvi wenu CCM na vyama vya upinzani una athari kubwa sana katika kuvutia wawekezaji. Hawapendi kusikia sijui Mbowe kafunguliwa kesi za uhaini, Lissu kaomba hifadhi Ubelgiji - unahitaji kuwa concerned na hayo mambo, usiseme hayakuhusu! Wawekezaji siku zote wanapenda strong political opposition kama check na balance dhidi ya chama tawala, hawapendi upinzani dhaifu katika nchi wanazowekeza. Hivyo kuwa na upinzani ulio strong is a good thing for investments - waambie watu wako wa CCM pamoja na viongozi wako wa Bunge. Wasibeze hoja za upinzani Bungeni hasa zenye mshiko, wawekezaji wanasikia!

Una kitu kinaitwa Tanzania Investment Centre, hivi wanafanya kazi gani? Waulize katika hayo hapo juu wana mkakati wowote? Mara ngapi wamekuja kuku-consult kwamba Mheshimiwa raisi hili na hili vinatukwamisha tunaomba uingilie kati? Wapowapo tu wanasubiri mtu agonge hodi waanze kumsumbua badala ya kumsaidia. Wanahitaji kuwa pro-active, waendane na vision yako, sio wakae ofisini wasubiri wewe ukapige debe Marekani ili waje kugongewa hodi.
Ukiwa huna hayo lazima umbembeleze,sio rahisi kwa hayo Mambo kufanyika kirahisi maana mengi take yanahitaji pesa
 
Very deep, bila shaka watakuelewa..

unataka mwekezaji aje huku watu wako maofisi kila kitu rushwa na mambo mengi konakona.

Unataka wawekezaji waje huku work force yako kwa kiasi kikubwa ni unskilled, wavivu, watu wako sio waaminifu wadokozi, wezi wanawaza maisha rahisi

Unataka wawekezaji waje wafokewe na makada wasiojua lolote wala chochote, zaidi ya uchawa, uchawi, na ngono ndio vimewafikisha hapo.

Unataka wawekezaji waje halafu makada wa chama chetu wawalazimishe wawape kazi ndugu zao unskilled, wezi nk, makada walazimishe vikampuni vyao vipate contracts za kazi.

Weka sawa mifumo, tengeneza jamii inayoishi kwa misingi, chama cha makada kikubali dunia imebadirika nacho kibadili mfumo wake wa ujinga ujinga kulea na kukuza vijana wa hovyo...nk nk
Hii Ni Africa hayo Mambo hayaondoki overnight
 
Uaminifu na uchapakazi wa wafanyakazi (trustworthy and hardworking labor force, sio wadokozi ofisini laptop zikipotea hovyo nk)


Kwa jambo hilo Watz tumelaanika.!!--- tumefanya wizi, udokozi, rushwa, ufisadi, nk katika ngazi zote ni jambo la fahari.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Fikiria unakuta li waziri lina hojiwa kwenye TV, linaanza kuchokonoa pua na vidole.....
Hapo mwekezaji anachoka kabisa....
 
Viongozi wetu wanaotunga sera na kusimamia sijui huwa wanasomea nini vyuoni kama mambo basic tu kama haya hawayaelewei! Inafikirisha sana.
 
Viongozi wetu wanaotunga sera na kusimamia sijui huwa wanasomea nini vyuoni kama mambo basic tu kama haya hawayaelewei! Inafikirisha sana.
Wako bize kuibia umma tu na kuhakikisha ccm ina dumu madarakani
 
Back
Top Bottom