Rais Samia, hili baraza la sasa siyo lako, ni la Magufuli akishauriana na Majaliwa, tengeneza baraza lako!

Ina maana unaunga mkono hizi tozo?
Sio naunga mkono,nimesema sio makini, maana uwezi kusimisha jambo ambalo limeisha tungiwa Sheria na bunge nayeye amesaini, wakati ana watu wakumshauli Kabla hata ya kusainiwa.Samia sio makini hipo siku ataingiza Nchi kwenye machafuko kama atakuwa sio mwangalifu katika maamuzi yake
 

Mkuu samahani Tuwe tuu wakweli...
Hilo la serikali 3 nani Analitaka?
Ni wananchi gani hao unaozungumzia?
Isijekuwa unazungumzia maslahi ya Upinzani ndio unasema ni Wananchi!
Wananchi wanataka maendela maji,Elimu afya,Ajira,Nk Nyie wasomi tena wachache mnalazimisha muonekane ndio sauti ya Wananchi! Wanaotaka Serikali 3!
Hahaha Kweli???
Wananchi wa Kantalamba,Budalabujiga,Muhida,Nyasamba,Wanataka serikali 3???
Masalhi ya wanasiasa hayo
 

Kuvaa barakoa hakuna madhara ya mlo wao, inapofika kwenye eneo la mlo wa ndio wanamvimbia huyo mama. Na kwakuwa mama karithi madaraka basi wanamtisha afuate misingi ya udhalimu.
 
Sio lazima utamtaje JPM ili kujenga hoja yako ya kitoto. Wateuliwa wote wameapishwa na mama, mbele ya camera na kadamnasi.

Tumuombe mama asimame yeye kaka yeye, na atafanikiwa. Akiwaruhusu wasaka tonge karibu yake, amekwisha
Acha uongo,sio mawaziri wote kawaapisha Samia, kawaapisha baadhi aliwabadilisha wizara tu,akina Jafo,Mwalimu,na wa utumishi,sio wote wameapishwa naye, nimesema kama anataka kuunda baraza lake la mawaziri, avunje bunge haitishe uchaguzi mpya.
 
7. Unasema waziri mkuu anaona tu muswada unapita bila kufanya jambo alafu anakuja kuitisha kikao, sawa waziri mkuu ana kosa. Ila ili muswada uwe Sheria ni lazima raisi asaini
Ilipaswa kabla ya raisi kusaini apitie hizo zinazoenda kuwa sheria mpya ili zisiumize wananchi
Kama raisi alisaini na yeye ni sehemu ya tatizo
 
Kuvaa barakoa hakuna madhara ya mlo wao, inapofika kwenye eneo la mlo wa ndio wanamvimbia huyo mama. Na kwakuwa mama karithi madaraka basi wanamtisha afuate misingi ya udhalimu.
Mkuu hakuna wa kumvimbia raisi HAKUNA. Ndio maana alipoingia uliona ametoa karibu kila mtu aliyeona hamfai pale ikulu
Jambo lolote la kitaifa lina baraka zote za raisi
 
Acha uongo,sio mawaziri wote kawaapisha Samia, kawaapisha baadhi aliwabadilisha wizara tu,akina Jafo,Mwalimu,na wa utumishi,sio wote wameapishwa naye, nimesema kama anataka kuunda baraza lake la mawaziri, avunje bunge haitishe uchaguzi mpya.
Lakini pia bado nawaza hilo baraza ambalo watu wanang'ang'ani aunde linakosaje Hawa waliokuwepo? Hawa mawaziri waliokuwepo ndio wenye afadhali zaidi ya hapo atajikuta anawateua akina musukuma, riziwani, shonza, kigwangalla, kibajaji n.k
 
Kiuhalisia huyu mama bado ni makamu wa rais ila kikatiba ndo tunajidanganya hivyo na tambua kaukaimu huo urais. huu ushauri utakuwa na maana siku akichaguliwa kupitia sanduku la kura.

Kwa sasa mwache amalizie Mambo ya magufuli Mungu akimjaalia uzima akashinda 2025 ndo ulifufue hili andiko lako.

Sawa eeeh??

Usisahau kujifukiza corona inaua.
 

Kwa lugha nyingine ni kwamba CCM imejaa mabozongwa!
 
Uandishi uliotukuka na points tupu. Mimi nilishaimba kabisa kuwa Mh. Rais hayuko na wateule wake bali aliazima. Nguo ya kuazima haisitiri ma ta ko. Bado wapo katika maombolezo kwa aliyewateua. Bado wengi wao walimtaka Bwana Yule achukue nafasi yako. Wewe mama unajua yaliyopangwa na yasitimie.
Mama bomoa hiyo nyumba Jenga yako. Nyumba uliyokodi inakuhujumu.

Mama huku mtaani toka uapishwe maji ya kutoka kila siku leo mgawo; umeme ni hautaburiki kwa siku kukatika hata mara 10; Mafuta ya Kula ni mtihani,; Mafuta ya vyombo vya Moto usiombe na sasa funga kazi miamala.
Kuna watu walishapanga 2025 ndiyo wagombea urais hivyo ni lazima uchafuke ili tukutupe.

Watu hao hawako na wewe kimatendo kabisa. Wanayo mitandao yao ya kujadili mbinu za kukudhoofisha.
Mama amka tunakupenda mno.
 
Hapa tunafuata ushauri wa Mwalimu kuwa kumbadili Waziri Mkuu nchi haiwezi kuyumba ila kumbadili rais nchi itayumba
Tudeal kwanza na huyu waziri mkuu aliyeshindwa kutimiza wajibu wake bungeni!
 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara 99 kifungu cha 1 kinasema hivi
 
Mkuu hakuna wa kumvimbia raisi HAKUNA. Ndio maana alipoingia uliona ametoa karibu kila mtu aliyeona hamfai pale ikulu
Jambo lolote la kitaifa lina baraka zote za raisi
Ni kweli, ila sio kwa urais wa kurithi.
 
Kuna kundi analiogopa sana ndani ya chama chake, hili ndilo linamwaribia. Hili kundi lipo kupigania legacy ya bwana wao. Halitakaa limwelewe hata siku moja, anajichosha bure kujaribu kuliridhisha.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Wewe on Nape
 
Pumba tupu
 
Hili Rais alilijua kabisa na alisaini, labda kama alisaini bila kusoma na kuelewa, kitu ambacho ni kosa kubwa pia na inashangaza
 
Reactions: BAK
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…