Post M-alone
JF-Expert Member
- Aug 18, 2021
- 2,962
- 9,553
Alikuwa wapi kuzungumza hayo mwanzoni?..marehemu anasemwa.
..tena huwa inasisitizwa wanaomdai marehemu wajitokeze.
..Magufuli ameacha deni kubwa la HAKI.
..waliodhulumiwa na Magufuli na serikali yake wanadai haki zao.
..waliopotelewa [ kundi la wasiojulikana] na ndugu zao wakati wa utawala wa Magufuli wanadai kuelezwa ndugu zao wako wapi.
..wapo walioshambuliwa kwa marisasi kwa mfano Tundu Lissu na inaelekea ni kwa " maagizo kutoka juu" wanadai watendewe haki.
..wapo walionyang'anywa fedha zao na mali zao kwa matumizi mabaya ya sheria ya " plea bargain" wanamdai Magufuli.
..waliobambikiwa kesi kwa sababu za kisiasa kutokana na agizo haramu la Magufuli la kuzuia shughuli za vyama vya siasa wanadai haki zao.
..Magufuli alitawala Kidikteta hivyo amefariki huku akiwaacha maelfu ya Watanzania wakimdai HAKI zao.
..Marehemu hasimangwi, ila watu mbalimbali wanaeleza MADENI aliyoacha.
Cc Nguruvi3, Erythrocyte
Mbona Bashite alijivua ukuu wa mkoa akaamua kuingia kwenye kinyang'anyiro cha ubunge, kwani Magu alimuua?
Huo si unafiki, kwa nini msibani Chato aseme yeye na Magu ni kitu kimoja, hivi sasa US anasema Magu hivi Magu vile, vyote ni kumponda jamaa, kama yeye ni kiongozi shupavu, mpigania haki, mwanaharakati angemwambia machoni Magu "mzee unakosea", mbona Kambona alimchana Nyerere? Akatimua mbio ugenini..
Huyu mama ana alama zote za unafiki na uzandiki, na mtu wa namna hii sio mzuri hata kidogo.