Rais Samia, imulike Bandari ya Dar nchi inahujumiwa, kaweke Kambi pale Bandarini

Rais Samia, imulike Bandari ya Dar nchi inahujumiwa, kaweke Kambi pale Bandarini

Samia hata akijitahidi kuonesha hataki utani hafananii na kiongozi alie serious, na vile nina wasiwasi nae anaweza kwenda huko bandarini kukagua halafu wajanja bado wakaiba akiwepo, huyu Rais wetu kwakweli sijui namuonaje...

Udadisi kama kuuliza maswali juu ya taratibu mbalimbali ya huko bandarini sijui kama anao uwezo, naona anasubiri wasaidizi wake wamjuze wakati hao wasaidizi ndio wapigaji wenyewe.
Ikiwa tunaamini kila kitu anadanganywa, hata akienda huko bandari atadanganywa tu.
 
Haya nilitegema kabisa. Unajua Magufuli alikuwa mkali lakini hakuwa anatumia elimu na sayansi kwenye kuongoza. Matokeo yake ni kuwa watu walikuwa wanamwogopa mtu mmoja na siyo kuwajibika kwa sababu ya mfumo ulio mzuri. Kiongozi wa namna hii akiondoka ni lazima anaacha ombwe kubwa la uongozi, na watu wanaona kama wamepewa nafasi ya kupumua.
Umeongea kitu kikubwa sana, shida sio ukali na shida sio upole.
Hapondio balaa lilipo, na bahati mbaya wa kutumia akili ili mambo yaende hayupo
 
Chanzo ni nini?

Kwani awamu ipi ilijaa sera za kishenzi za kufukuza wawekezaji?

Awamu ipi tumeshuhudia wawekezaji wakitimkia kwao?

Tuanzie hapo msitake kutusahaulisha.
 
Samia hata akijitahidi kuonesha hataki utani hafananii na kiongozi alie serious, na vile nina wasiwasi nae anaweza kwenda huko bandarini kukagua halafu wajanja bado wakaiba akiwepo, huyu Rais wetu kwakweli sijui namuonaje...

Udadisi kama kuuliza maswali juu ya taratibu mbalimbali ya huko bandarini sijui kama anao uwezo, naona anasubiri wasaidizi wake wamjuze wakati hao wasaidizi ndio wapigaji wenyewe.
Hapo kwenye udadisi ndio ninamashaka makubwa sana.
 
Samia hata akijitahidi kuonesha hataki utani hafananii na kiongozi alie serious, na vile nina wasiwasi nae anaweza kwenda huko bandarini kukagua halafu wajanja bado wakaiba akiwepo, huyu Rais wetu kwakweli sijui namuonaje...

Udadisi kama kuuliza maswali juu ya taratibu mbalimbali ya huko bandarini sijui kama anao uwezo, naona anasubiri wasaidizi wake wamjuze wakati hao wasaidizi ndio wapigaji wenyewe.
Yaani rais ajue taratibu za kila kitengo kila sekta nchini,asitegemee wasaidizi,unafikiri sawasawa!?
 
Kwani tatizo ni nini haswa? Hizo meli wanazichelewesha makusudi kukaa hapo au namna gani?
 
Si tuliambiwa gati zimejengwa mpya na vifaa vya kisasa vya kupakua mizigo, imekuwaje tena!
 
Tatizo ni siasa za nchi hii zinatukwamisha…hv kwanini watanzania tusikabidhi jeshi lituongoze kwa miaka 20….hawa jamaa wamepitia mikiki mingi jeshini wana uzalendo wakupindukia hawana tamaa km za wanasiasa…halafu Putin awe baba wetu wa kiroho
 
Wewe ni kama umechanganyikiwa tu au una utapiamlo wa akili.

Unahitaji PhD kujua kuwa Rais ambae anahamasisha ufisadi katika Serikali yake hawezi tena wakati huohuo kupambana na ufisadi huo?

Yaani unataka Rais ahamasishe ufisadi na kupambana na ufisadi huo kwa wakati mmoja?WTF?!
View attachment 2145904
Umemjibu vizuri sana, natumaini atakuwa amekuelewa vyema kabisa.

Samia hana mpango, na hata uwezo wa kufanya hayo anayolilia huyo mleta mada.

Hivi wale watu waliokuwa wameweka mrija kwenye bomba la mafuta kule Kigamboni walifanywa nini hadi leo?

Naona hata yule binti, mkuu wa wilaya alihamishwa toka eneo hilo!

Samia anajenga 'Oligarch' wake, usitegemee lolote jingine kutoka kwake.
 
Jinsi kamba yako inavokuruhusu ndio kadri unavokula, nikasema lakini mbona mnakula sana, mnavimbiwa, sikweli kwamba hampati kwenye maeneo yenu,mnapata, lakini jipimie,, JIPIMIENI - Rais Samia Suluhu Hassan

Mkuu bandarini nao wanajipimia,,meli zitakuwa zinapakuliwa kwa Connection
 
CCM mliponea chupu enzi za JK lakini kwa mwendo huu sijui mtapona vipi! Litakuja wimbi ambalo hamtaweza kuli manage.

Tatizo hakuna upinzani Tanzania kwa sasa. Kungekuwa na upinzani makini wanachukua nchi hii 2025.
 
Just thinking aloud: unaweza kuwa mpango wa kuaminisha watu kuwa bandari ya Dar imeelemewa hivyo solution ni kujengwa bandari ya Bagamoyo. Tutafakari: Thread kama hizi zinazoweza kufuatiliwa na matamko kutoka kwa viongozi kuwa ''hata kwenye mitandao kelele zinapigwa kuwa bandari ya Dar imeshindwa kuhimili msongamano hivyo bila bandari ya Bagamoyo ni bure''
[emoji437][emoji436]
 
Haya nilitegema kabisa. Unajua Magufuli alikuwa mkali lakini hakuwa anatumia elimu na sayansi kwenye kuongoza. Matokeo yake ni kuwa watu walikuwa wanamwogopa mtu mmoja na siyo kuwajibika kwa sababu ya mfumo ulio mzuri. Kiongozi wa namna hii akiondoka ni lazima anaacha ombwe kubwa la uongozi, na watu wanaona kama wamepewa nafasi ya kupumua.
Ila ilisaidia kwa namna flani
 
Meli za kutoka Dubai kuja DSM huchukua siku 14, Mzigo ukifika Dar Es Salaam bandarini utakaa siku hata 20-28 ukisubiri kupakuliwa.

Meli ikitoka UK au China itatumia siku 28-30 kufika Dar, Mzigo ukifika hapo Bandarini unachukua siku 20-28 zingine kupakuliwa.

Gharama za Usafiri imebidi SHIPLINERS waziongeze kufidia muda mrefu wa kusubiri hapo Bandarini.

Sasa hivi Wafanyabiashara kutoka CONGO DR, RWANDA, MALAWI, ZAMBIA, UGANDA wameanza kukimbilia Bandari ya Mombasa kupitisha mizigo yao.

Mheshimiwa Rais Samia, ukicheka na nyani utavuna Mabua., wananchi vitu vitazidi kupanda bei bila sababu yoyote ya maana.

Nimekuwekea na VIDEO uisikilize kama ushahidi mwingine.

KAZI IENDELEE
Ni wiki kadhaa zilizopita viongozi wa Bandari walikuwa Zambia waki'promote' nchi hiyo itumie bandari yao; hivyo hivyo taarifa zimechapishwa magazetini Uganda wakihimizwa kutumia bandari ya Dar.

Kwa hiyo tuseme hawa viongozi wa bandari wana'promote' bandari isiyokuwa na ufanisi wowote wa kazi? Hawa jamaa wa bandari mizunguko yao hii ni kutafuna hela tu?

Mwisho wa siku tutaambiwa yote yanayotokea bandarini yamesababishwa na Vladimir Putin, na sote tutaelewa yanakotokea matatizo yetu!
 
Back
Top Bottom