Rais Samia ingilia kati suala la Mbowe ukubalike zaidi kisiasa; kesi ikitupwa au akishinda itakuharibia taswira yako na ya CCM

Rais Samia ingilia kati suala la Mbowe ukubalike zaidi kisiasa; kesi ikitupwa au akishinda itakuharibia taswira yako na ya CCM

Rais hapaswi kuingilia mhimili wa Mahakama.

Lakini, kama kesi serikali ndiyo inashitaki, na rais ndiye kiongozi wa serikali, rais, kwa kushirikiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Mashitaka, anaweza kushauri au kuagiza kesi ifutwe kama kuna sababu za msingi za kufanya hivyo.

Mathalan, rais akipata taarifa za ki intelligentsia kwamba kesi hii Mbowe am3bambikiwq bula ushahidi wala haki, na kabambikiwa na Polisi waliofikiri wanafanya anachitaka rais, wakati rais hataki hivyo, rais anaweza kuwa sawa kuagiza Mkurugenzi wa Mashitaka kufuta kesi na Polisi waliohusika wawajibishwe.

Hilo litapelekea kesi kufutwa na Mkurugenzi wa Mashitaka, bila rais kuingilia Mahakama.
Ni hapo akipata hizo taarifa za ki-intelijensia. Naamini taarifa alizonazo sasa hivi ni kwamba polisi pamoja na ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka wanao ushahidi kamili kama alivyosema IGP. Hizi assumptions za kama kama kama kama hazitakiwi kuwepo tena.
 
Kuna mtu nimemuuliza humu kuwa hivi kweli unadhani Mbowe ni gaidi, bila kutumia akili akajibu haraka kuwa nina mapenzi na Mbowe.

Hivi watu wanadhani Mbowe na Cjadema wakiamua kuwa magaidi watafanya ugaidi kwa nmana ambayo huyu IGP anasema wanafanya na ushahidi tunao? IGH inaonekana anaangalia sana habari za Bokoharam na anatafuta cheap popularity.

Na suala la Mama kuwa makini na maamuzi yake yanayotokana na ushauri anaopewa ni muhimu sana. Sijui ana tatizo gani hapo. NIme speculate kwamba usikute hawa waliomzunguka anawasikiliza sana ili apate kuungwa mkono kuwa mgombea wa CCM 2025. Kama ndivyo atakuwa anapotea sana.
Hivi wewe unawajua waliomzunguka Mama??

Inner circle team ya Mheshimiwa rais unaijua kweli?? I mean kuijua kwa maana ya kuijua!!
 
Hoja yako iko bias sana. Assumption yako ni kesi kuondolewa au Mbowe kushinda tu. Kwa nini hauzungumzii pia uwezekano wa Mbowe kupatwa na hatia na kuhukumiwa miaka 20 jela. Rais ataonekna ni shujaa wa kuangamiza magaidi kama Mbowe. Tuache mahakama iamue, ndiyo utawala wa kisheria
Pole sana na hii chuki yako, ni bure mbowe wamehifadhi tu hiyo kesi ni kiini macho vuguvugu la katiba lipungue wamtoe
 
Mtu ambae hataki kujiingiza kwenye siasa hawezi kutoa ushauri wa kipuuzi hivi. Mbona haukumshauri raisi aingilie kati kesi ya Sabaya au yeye sio mtanzania? Sirro ashasema kwamba police wana uhakika wa kutosha na kile walichomkamatia Mbowe, sasa ww ni nani kumtaka raisi aingilie kuzuia haki isitendeke? Fikiria kwamba kabla mahakama haijathibitisha kupitia ushahidi kuwa fulan kama kosa, hakuna mtu ambae yuko tayar kukubali kwamba alifanya hiki au kile. Sasa raisi akiingilia mahakama ili Mbowe aachiwe, kesho Sabaya na yeye atataka hivyo hivyo maana na yeye ana watu wake wanaoona kuwa ameonewa. So Sabaya akiachiwa na wengine pia watafuatia. Matokeo yake mahakama zetu zitakuwa hazina kazi za kufanya zaidi ya kuwashtaki watu na kuwaachia kiholela olela.
Wafuasi wa vyama vya siasa wanafikiria utawala wa sheria ni kuwaweka ndani wale wanaowachukia tu.........

Ukitazama kwa makini utagundua kuwa wanasiasa wetu pamoja na wafuasi wao hawamaanish kile wanachokipigania bali wana ajenda zao nyuma ya kile wanachokipigania.........

Watu walioshangilia kuwa utawala wa sheria umerudi kwa kukamatwa kwa Sabaya na kuachiliwa kwa Mdude Nyangali ndio hao hao wanaotaka utawala wa sheria uvunjwe ili aachiliwe kiongozi wao.......ndio maana nasema siasa za Tanzania zimekosa weledi bali imebakia mihemko tu........

Ni ngumu sana kuwaelewa wanasiasa wa nchi hii na wafuasi wao.......
 
Kuna rapper mmoja Mmarekani anaitwa Jadakiss, alisema katika moja ya nyimbo zake:-

"If I wasn't on some shit, I'm getting on it".

Alikuwa analalamika kuhusu mambo aliyokuwa anazushiwa. Akasema kwamba, sasa, kwa sababu watu wanamzushia sana, ataanza kufanya kweli hayo anayozushiwa ili lawama anazopewa zisiwe za bure, ziwe za kweli.

Nilivyoifikiria kesi hii ya ugaidi ya Mbowe nikakukmbuka mstari huo wa Jadakiss.

Nikasema, hawa CHADEMA wanaozushiwa ugaidi, hivi wakisema sawa, mnatuzushia ugaidi, sisi si magaidi, lakini kwa sababu mnatuzushia, sasa tunaanza kufanya ugaidi kweli ili kutimiza uzushi wenu.

CHADEMA wakaanza kupiga mabomu ofisi za CCM na nchi ikaingia katika milipuko ya mabomu.

Hao wanaozusha ugaidi watafurahi kuona uzushi wao unatimia?

Maana haya mambo mengine ni kama kunuia kitu kitokee, na hata mazungumzo ya ugaidi tu yanaweza kuanza kufanya watu wafanye kweli.


😄😄😄😄😄😄😄😄😄😄😄😄😄😄😄😄

Eti sasa wanaanza kufanya ugaidi ili iwe kweli. Halafu wakaanza kupiga mabomu ofisi za CCM na nchi ikaingia katika milipuko ya mabomu hahahaahahaha.

Wakati wote huo vyombo vyetu madhubuti vya ulinzi na usalama vimelala?? Jemedari na amir jeshi mkuu Mheshimiwa Mama Samia kipindi hicho atakuwa wapi?? Unajua tunu za taifa la Tanzania wewe???

Amani na upendo!

Jukumu la kwanza kabisa la kiongozi yoyote wa nchi hii ni kuhakikisha amani inatamalaki na katika hilo hakuna kucheka na KIMA.

Sasa hizo hip hop zenu leteni kwenye jamii zetu muone kitakachotokea.

😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Wanaouliza kwa nini Mbowe amekamatwa sasa na si vinginevyo wanasahau kuwa Mbowe, Lema, Meya wa zamani Ubungo Boniface walikamatwa mara baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu kutangazwa na kabla Rais hajaapishwa kwa kuchochea maandamano yasiyo na kikomo kupinga matokeo. Mambosasa alihojiwa na vituo vya ITV na TBC na kutoa madai hayo hayo ya ugaidi.
 
Sahia hata kuwa wa kwanza kuingilia maana Nyerere akisha weka precedent alipomtoa Yule mahabusu mgiriku akiyesema kaiweka serikali ya kifimbo mfukoni...
Au labda una reasoning tofauti- iweke hapa tuichambue...

mwisho, ccm na serikali yao wapambane kwa hoja sio maguvu wanna mitambo ya watoa hoja sasa wanaogopa nini katiba Mpya na tume huru kwa kumshitaki messenger? Fair play uwanjani ndio mpango mzima siku hizi sio maguvu na kukandamiza watu kwa makesi ya kijinga
Haya ni maneno tu. CCM wameogopaje hilo suala la katiba mpya??

Ni CCM kupitia Mheshimiwa Jakaya ndio aliliweka mezani litatuliwe, wapinzani si ndio waliotoka bungeni maana walitaka vikao viendelee tu ili waendelee kula posho. Wao kuona suala linaelekea kumalizika wakaona mchakato wauharibu. Halafu Leo eti CCM wanaogopa katiba mpya
 
Haya ni maneno tu. CCM wameogopaje hilo suala la katiba mpya??

Ni CCM kupitia Mheshimiwa Jakaya ndio aliliweka mezani litatuliwe, wapinzani si ndio waliotoka bungeni maana walitaka vikao viendelee tu ili waendelee kula posho. Wao kuona suala linaelekea kumalizika wakaona mchakato wauharibu. Halafu Leo eti CCM wanaogopa katiba mpya
Ni kweli kwamba fedha zilitumika nyingi , sasa si walimalizie basi? haya malumbano ya nini, kukamatwa kamatwa na mengineyo... wamalizie kilichio baki, kiwe kibaya au kizuri- na tuone mwisho wake. Haya ya kupiga hela, pia ni maneno tu...cha msingi, Katiba iliyokwama ikwamuliwe na tuendelee na mambo mengine.
 
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]

Eti sasa wanaanza kufanya ugaidi ili iwe kweli. Halafu wakaanza kupiga mabomu ofisi za CCM na nchi ikaingia katika milipuko ya mabomu hahahaahahaha.

Wakati wote huo vyombo vyetu madhubuti vya ulinzi na usalama vimelala?? Jemedari na amir jeshi mkuu Mheshimiwa Mama Samia kipindi hicho atakuwa wapi?? Unajua tunu za taifa la Tanzania wewe???

Amani na upendo!

Jukumu la kwanza kabisa la kiongozi yoyote wa nchi hii ni kuhakikisha amani inatamalaki na katika hilo hakuna kucheka na KIMA.

Sasa hizo hip hop zenu leteni kwenye jamii zetu muone kitakachotokea.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Wewe unajua kusoma kwa ufahamu?
 
Ni hapo akipata hizo taarifa za ki-intelijensia. Naamini taarifa alizonazo sasa hivi ni kwamba polisi pamoja na ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka wanao ushahidi kamili kama alivyosema IGP. Hizi assumptions za kama kama kama kama hazitakiwi kuwepo tena.
Kachemka.

Wanaoandamana kwa sababu ya umeme ni wapi huko?

Halafu anajibu swali la Mbowe kirefu, kisha anasema hawezi kujibu swali kwa kuwa kesi iko mahakamani.

Contradiction.
 
Wafuasi wa vyama vya siasa wanafikiria utawala wa sheria ni kuwaweka ndani wale wanaowachukia tu.........

Ukitazama kwa makini utagundua kuwa wanasiasa wetu pamoja na wafuasi wao hawamaanish kile wanachokipigania bali wana ajenda zao nyuma ya kile wanachokipigania.........

Watu walioshangilia kuwa utawala wa sheria umerudi kwa kukamatwa kwa Sabaya na kuachiliwa kwa Mdude Nyangali ndio hao hao wanaotaka utawala wa sheria uvunjwe ili aachiliwe kiongozi wao.......ndio maana nasema siasa za Tanzania zimekosa weledi bali imebakia mihemko tu........

Ni ngumu sana kuwaelewa wanasiasa wa nchi hii na wafuasi wao.......
Wanasiasa wa Tz huwa wanapambana kwa ajili ya matumbo yao na familia zao.
 
Tatizo akitolewa washauri wake wa karibu akina Mdude wanaanza kumrushia matusi Mama, mara ooooh! utanyolewa nywele za sijuhi sehemu gani....hawa wahuni wa chadema wanakiharibu sana chama!

Ila naona kama uchomaji mabweni mashuleni umepungua baada ya Gaidi Mbowe kufungwa, huenda kuna mkono wake kama Polisi walivyodai!!?
Inaonekana wazi unatumia makalio kufikiri!!!
 
Mtu yeyote mwenye kujua sheria anapoona tu kichwa cha thread hii, atasema sio sahihi, Rais Samia hapaswi kuingilia kati suala la mashitaka ya Mbowe ya Ugaidi kwa kuwa hapaswi kuingilia kati mhimili wa Mahakama. Ni kweli.

Lakini pia, Watanzania wengi sana wanaamini kwa dhati kwamba kesi ya uagaidi dhidi ya Mbowe ina mkono au baraka za Raisi Samia. Labda kweli.

Na wanasheria makini, watakuambia kwamba kesi ya ugaidi dhidi ya Mboewe, pamoja na kelele nyingi sana za Polisi, haina mshiko wa kisheria na kama kweli itasikilizwa kwa haki basi ni rahisi kwesi hiyo kutupwa au Mbowe na washitakiwa wenzake wote kushinda kesi.

Sasa unajiuliza, hivi ilikuwaje Mwanasheria Mkuu wa Serikali asimshauri Rais Samia kwamba kesi kama hii dhidi ya Mbowe haitakuwa na mshindi? Kwanza inaiweka Tanzania katika darubini ya mataifa makubwa ya nje.

Pili inafanya idadi kubwa ya watu kuamini kwamba Mbowe alikamatwa kwa ajili ya makongamano ya Katiba na ugaidi ni kisingizio tu.

Tatu inaonyesha wazi kwa watu wa ndani na nje kwamba CCM wanaogopa Katiba mpya kwa kuwa wanahofia uchaguzi ukifanywa katika mazingira ya kidemokrasia CCM hawatashinda.

Nne Mbowe akifungwa kwa mashitaka kama haya ambayo yapoyapo tu itampa umaarufu zaidi ndani na nje ya nchi, atakuwa Mandela wa Tanzania.

Tano Mbowe akiachiwa Rais Samia na CCM wataonekana wanabambikia wapinzani kesi.

Sasa kama Mwanasheria Mkuu alishindwa kuona haya na kumshauri Rais Samia dhidi ya kesi ya Mbowe, nina mashaka sana na uwezo wake wa kumshauri Rais, au lengo lake la ushauri aliotoa kwa Rais Samia.

Katika mazingira kama haya, ushauri wangu kwa Rais Samia ni kwamba atafute namna ya kuingilia suala hili, bila kuonekana anavunja uhuru wa Mahakama, ili watu wote waone kwamba Mbowe na wenzake waliachiwa na kesi hii kutupwa kwa sababu Raisi Samia alitumia busara katika kuimaliza.

Najua kwa sasa suala hili limemuweka Rais Samia mahali pagumu sana kwa kuwa halikupaswa kufika kote huku, lakini pia akiliacha liendelee mahakamani, matokeo yake yoyote, ya kesi kutupwa nje, au Mbowe na wenzake kufungwa au kuachiwa huru, hayatakuwa mazuri kwake Rais Samia na chama chake CCM
Kufungwa ni kumuimarisha mwanasiasa, ingependeze Mbowe afungwe miaka 30 ili apate umaarufu Kama Nelson Mandela.
 
Acha ushabiki, wewe kila kitu watu wanachoandika unaona kina ajenda ya wapinzani? Jaribu kutumia akili yako vizuri na kuona mambo nje ya box la CCM
Ushauri mzuri sana, kama kufungwa Mbowe kutafanya wananchi wapende upinzani na atapoteza Urais chaguzi ifuatayo. Sioni kwa nini kuna kelele. Wamwache awapeleke wapinzani jela ili wapate utawala.
 
nadhani hata kwa wakati huu mali za Mbowe zote zinapaswa zizuiliwe pomja na acount zake.
lazima sheria ya Ugaidi ifuatwe kikamilifu.

Nilishangaa sana alipo fikishwa nakaona Mbowe anaruhusiwa kukumbatiana na jamaa zake!!
mahakamani lazima gaidi alindwe, nilishangaa pale kisutu inakuwaje Gaidi anapewa nafasi ya kukubatiana na watu mahakamani?!! hili halipaswi kujitokeza. ni muhimu vyombo vyetu vyote vikajifunza kutoka mataifa mengine namna ya kudili na watuhumiwa wa Ugaidi.
kamwe vyombo vyetu vya ulinzi na usalama visikubali kuhadaiwa au kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa na mawakili au viongozi wa chadema, lazima sheria ifuatwe kikamilifu kama ilivyo kuwa inafuatwa kwa washitakiwa wengine.
nilishangaa kuwaona watuhumiwa wenzake wa Ugaidi wamefungwa pingu huku Mbowe akiwa hajafungwa pingu, sijafahamu kwa nn,!! kama hakuna ulazima basi wote wasifungwe pingu, sio baadhi wanafungwa wengine hawafungwi!!!
 
Mtu yeyote mwenye kujua sheria anapoona tu kichwa cha thread hii, atasema sio sahihi, Rais Samia hapaswi kuingilia kati suala la mashitaka ya Mbowe ya Ugaidi kwa kuwa hapaswi kuingilia kati mhimili wa Mahakama. Ni kweli.

Lakini pia, Watanzania wengi sana wanaamini kwa dhati kwamba kesi ya uagaidi dhidi ya Mbowe ina mkono au baraka za Raisi Samia. Labda kweli.

Na wanasheria makini, watakuambia kwamba kesi ya ugaidi dhidi ya Mboewe, pamoja na kelele nyingi sana za Polisi, haina mshiko wa kisheria na kama kweli itasikilizwa kwa haki basi ni rahisi kwesi hiyo kutupwa au Mbowe na washitakiwa wenzake wote kushinda kesi.

Sasa unajiuliza, hivi ilikuwaje Mwanasheria Mkuu wa Serikali asimshauri Rais Samia kwamba kesi kama hii dhidi ya Mbowe haitakuwa na mshindi? Kwanza inaiweka Tanzania katika darubini ya mataifa makubwa ya nje.

Pili inafanya idadi kubwa ya watu kuamini kwamba Mbowe alikamatwa kwa ajili ya makongamano ya Katiba na ugaidi ni kisingizio tu.

Tatu inaonyesha wazi kwa watu wa ndani na nje kwamba CCM wanaogopa Katiba mpya kwa kuwa wanahofia uchaguzi ukifanywa katika mazingira ya kidemokrasia CCM hawatashinda.

Nne Mbowe akifungwa kwa mashitaka kama haya ambayo yapoyapo tu itampa umaarufu zaidi ndani na nje ya nchi, atakuwa Mandela wa Tanzania.

Tano Mbowe akiachiwa Rais Samia na CCM wataonekana wanabambikia wapinzani kesi.

Sasa kama Mwanasheria Mkuu alishindwa kuona haya na kumshauri Rais Samia dhidi ya kesi ya Mbowe, nina mashaka sana na uwezo wake wa kumshauri Rais, au lengo lake la ushauri aliotoa kwa Rais Samia.

Katika mazingira kama haya, ushauri wangu kwa Rais Samia ni kwamba atafute namna ya kuingilia suala hili, bila kuonekana anavunja uhuru wa Mahakama, ili watu wote waone kwamba Mbowe na wenzake waliachiwa na kesi hii kutupwa kwa sababu Raisi Samia alitumia busara katika kuimaliza.

Najua kwa sasa suala hili limemuweka Rais Samia mahali pagumu sana kwa kuwa halikupaswa kufika kote huku, lakini pia akiliacha liendelee mahakamani, matokeo yake yoyote, ya kesi kutupwa nje, au Mbowe na wenzake kufungwa au kuachiwa huru, hayatakuwa mazuri kwake Rais Samia na chama chake CCM
Serikali inavyanzo kuliko hili pumba lako
 
Back
Top Bottom