Rais Samia ingilia kati suala la Mbowe ukubalike zaidi kisiasa; kesi ikitupwa au akishinda itakuharibia taswira yako na ya CCM

Rais Samia ingilia kati suala la Mbowe ukubalike zaidi kisiasa; kesi ikitupwa au akishinda itakuharibia taswira yako na ya CCM

Mbowe mwenyewe hajionei huruma kwahiyo hastaili kuonewa huruma abaki huko alipo,kumchekea nyani shambani ujira wake ni kuvuna mabua.

Unamuonea huruma,unamfutia kesi,akirudi uraiani anakusanya tena wapumbav wenzie waandamane[emoji3525]

Ukitaka uonewe huruma,jionee huruma mwenyewe kwanza kisha waonee huruma na wenzio...
Angemuacha mama afanye kazi ngumu aliyonayo ya kuongoza nchi.

Mkumbuke those first days za mama alifanya huruma nyingi kwa wana CHADEMA na Mbowe wao,aliwafutia makesi, alitengua ile hukumu ya fine na mamilioni ya pesa walirudishiwa

Sasa mama awafanyie nini hawa watu au awanyonyeshe ndo waone wanahurumiwa???[emoji3525][emoji3525][emoji3525]
HARAKATI ZINGINE ZA KI FALA...
 
Very bad advice!
Sahia hata kuwa wa kwanza kuingilia maana Nyerere akisha weka precedent alipomtoa Yule mahabusu mgiriku akiyesema kaiweka serikali ya kifimbo mfukoni...
Au labda una reasoning tofauti- iweke hapa tuichambue...

mwisho, ccm na serikali yao wapambane kwa hoja sio maguvu wanna mitambo ya watoa hoja sasa wanaogopa nini katiba Mpya na tume huru kwa kumshitaki messenger? Fair play uwanjani ndio mpango mzima siku hizi sio maguvu na kukandamiza watu kwa makesi ya kijinga
 
Sahia hata kuwa wa kwanza kuingilia maana Nyerere akisha weka precedent alipomtoa Yule mahabusu mgiriku akiyesema kaiweka serikali ya kifimbo mfukoni...
Au labda una reasoning tofauti- iweke hapa tuichambue...

mwisho, ccm na serikali yao wapambane kwa hoja sio maguvu wanna mitambo ya watoa hoja sasa wanaogopa nini katiba Mpya na tume huru kwa kumshitaki messenger? Fair play uwanjani ndio mpango mzima siku hizi sio maguvu na kukandamiza watu kwa makesi ya kijinga
Kosa ni kosa hata kama mtendaji atakuwa si wa kwanza kulitenda!

Mimi napendelea zaidi mfumo wa haki ndiyo uamue hatia ya Mbowe. Siyo Rais wa nchi.

Leo watu wanataka waziwazi kuwa Rais aingilie kati na kumtoa Mbowe jela na kumfutia kabisa mashitaka.

Ni precedent mbaya sana maana akifanya hivyo, nini kitamfanya asifanye tena hivyo kuhusu mtuhumiwa mwingine yeyote yule huko mbeleni?

Si vizuri hata kidogo Rais kuanza kuingilia mambo ya utoaji haki wakati mfumo wa kufanya hivyo upo.
 
Mtu yeyote mwenye kujua sheria anapoona tu kichwa cha thread hii, atasema sio sahihi, Rais Samia hapaswi kuingilia kati suala la mashitaka ya Mbowe ya Ugaidi kwa kuwa hapaswi kuingilia kati mhimili wa Mahakama. Ni kweli.

Lakini pia, Watanzania wengi sana wanaamini kwa dhati kwamba kesi ya uagaidi dhidi ya Mbowe ina mkono au baraka za Raisi Samia. Labda kweli.

Na wanasheria makini, watakuambia kwamba kesi ya ugaidi dhidi ya Mboewe, pamoja na kelele nyingi sana za Polisi, haina mshiko wa kisheria na kama kweli itasikilizwa kwa haki basi ni rahisi kwesi hiyo kutupwa au Mbowe na washitakiwa wenzake wote kushinda kesi.

Sasa unajiuliza, hivi ilikuwaje Mwanasheria Mkuu wa Serikali asimshauri Rais Samia kwamba kesi kama hii dhidi ya Mbowe haitakuwa na mshindi? Kwanza inaiweka Tanzania katika darubini ya mataifa makubwa ya nje.

Pili inafanya idadi kubwa ya watu kuamini kwamba Mbowe alikamatwa kwa ajili ya makongamano ya Katiba na ugaidi ni kisingizio tu.

Tatu inaonyesha wazi kwa watu wa ndani na nje kwamba CCM wanaogopa Katiba mpya kwa kuwa wanahofia uchaguzi ukifanywa katika mazingira ya kidemokrasia CCM hawatashinda.

Nne Mbowe akifungwa kwa mashitaka kama haya ambayo yapoyapo tu itampa umaarufu zaidi ndani na nje ya nchi, atakuwa Mandela wa Tanzania.

Tano Mbowe akiachiwa Rais Samia na CCM wataonekana wanabambikia wapinzani kesi.

Sasa kama Mwanasheria Mkuu alishindwa kuona haya na kumshauri Rais Samia dhidi ya kesi ya Mbowe, nina mashaka sana na uwezo wake wa kumshauri Rais, au lengo lake la ushauri aliotoa kwa Rais Samia.

Katika mazingira kama haya, ushauri wangu kwa Rais Samia ni kwamba atafute namna ya kuingilia suala hili, bila kuonekana anavunja uhuru wa Mahakama, ili watu wote waone kwamba Mbowe na wenzake waliachiwa na kesi hii kutupwa kwa sababu Raisi Samia alitumia busara katika kuimaliza.

Najua kwa sasa suala hili limemuweka Rais Samia mahali pagumu sana kwa kuwa halikupaswa kufika kote huku, lakini pia akiliacha liendelee mahakamani, matokeo yake yoyote, ya kesi kutupwa nje, au Mbowe na wenzake kufungwa au kuachiwa huru, hayatakuwa mazuri kwake Rais Samia na chama chake CCM
Upo sahihi..
Mbowe amekamatwa kwa maelekezo ya ikulu...kwa hiyo Rais anahusika moja kwa moja.
Na kwasababu yeye ndie alietoa go ahead ya Mbowe kukamatwa, ni yeye ndie wa kuondoa haya mashtaka..kwa namna gani?? Atajua yee mwenyewe.
 
Kosa ni kosa hata kama mtendaji atakuwa si wa kwanza kulitenda!

Mimi napendelea zaidi mfumo wa haki ndiyo uamue hatia ya Mbowe. Siyo Rais wa nchi.

Leo watu wanataka waziwazi kuwa Rais aingilie kati na kumtoa Mbowe jela na kumfutia kabisa mashitaka.

Ni precedent mbaya sana maana akifanya hivyo, nini kitamfanya asifanye tena hivyo kuhusu mtuhumiwa mwingine yeyote yule huko mbeleni?

Si vizuri hata kidogo Rais kuanza kuingilia mambo ya utoaji haki wakati mfumo wa kufanya hivyo upo.
Na zile kesi watu walifunguliwa zikawa Mahakamani na Raisi Magufuli akaagiza watuhumiwa wanaweza kukubaliana na DPP ili walipe faini haikuwa kuingilia uhuru wa Mahakama?

Dont read selectively. Thread imeshasema "Katika mazingira kama haya, ushauri wangu kwa Rais Samia ni kwamba atafute namna ya kuingilia suala hili, bila kuonekana anavunja uhuru wa Mahakama, ili watu wote waone kwamba Mbowe na wenzake waliachiwa na kesi hii kutupwa kwa sababu Raisi Samia alitumia busara katika kuimaliza.

Najua kwa sasa suala hili limemuweka Rais Samia mahali pagumu sana kwa kuwa halikupaswa kufika kote huku,"

Kwa hiyo unachokitataa wewe tayari kimekuwa factored katika thread na sio suala tena la kujadili.

Labda swali la maana ambalo ungeuliza ni "ni vipi Raisi Samia anaweza kuingilia kumaliza hili bila kuingilia uhuru wa Mahakama".

Then ungekuwa una-contribute constructively to the thread, la sivyo unatuambia kitu ambacho tumeshakuambia. Give us suggestions dont expand on challenges that have already been acknowledged in the thread.
 
Yeye ndio raisi na mwenye kuamua nani awe mshauri wake. Lakini ikiwa anafanya mambo kwa kutaka aungwe mkono kugombea tena awamu inayofuata, basi imekula kwake. Raisi Samia anapaswa kufanya mambo bila kujali mambo ya kuungwa mkono na CCM kupitishwa kuwa mgombea uraisi 2025. Ukweli ni kwamba Wapinzani wanaweza kutumia U-Zanzibari wake kumshinda 2025, ikiwa uchaguzi utakuwa huru na wa haki. CCM na washauri wake wanajua hilo. Hivyo ajikatie tu tamaa kuwa mgombea wa CCM wa 2025 ili afanye mambo sio kwa kujipendekeza kwa wana CCM wenye chama upande wa bara ili wamuunge mkono kugombea kwa tiketi ya CCM 2025. Ili awe raisi bora ni lazinma ajifungue minyororo ya kutaka kuwa mgombea uraisi 2025. Akifanya hivyo anaweza kujikuta wananchi wanamuunga mkono kuendelea kuwa rais kuliko hata hao washauri wake wa CCM ambae sidhani kama wana nia njema nae.
Watu mnawaza 2025 wakati mnajua kwa katiba hii rais na mwenyekiti wa ccm ndyo anayeamua nan awe mrithi wake
 
Hoja yako iko bias sana. Assumption yako ni kesi kuondolewa au Mbowe kushinda tu. Kwa nini hauzungumzii pia uwezekano wa Mbowe kupatwa na hatia na kuhukumiwa miaka 20 jela. Rais ataonekna ni shujaa wa kuangamiza magaidi kama Mbowe. Tuache mahakama iamue, ndiyo utawala wa kisheria
Kuna jambo hapa wengi hawajui!!..Mbowe has nothing cha kupoteza kwenye case hii!!..Sasa kama ndivyo Itakua aibu kubwa Kwa serikali kupoteza case hii alafu italeta mtikisiko mkubwa nchini na Duniani kote!!.. Angali jinsi chadema na marafiki zao walivyojipanga kushinda case angalia jinsi case ilivyo kiajabu hata mtu ambae siyo mwanasheria anaweza kusema tayari Mbowe kashinda labda serikali iamue kuingilia Mahakama lakini Kwa jinsi ilivyo ni ngumu sana!!!..
 
Mtu yeyote mwenye kujua sheria anapoona tu kichwa cha thread hii, atasema sio sahihi, Rais Samia hapaswi kuingilia kati suala la mashitaka ya Mbowe ya Ugaidi kwa kuwa hapaswi kuingilia kati mhimili wa Mahakama. Ni kweli.

Lakini pia, Watanzania wengi sana wanaamini kwa dhati kwamba kesi ya uagaidi dhidi ya Mbowe ina mkono au baraka za Raisi Samia. Labda kweli.

Na wanasheria makini, watakuambia kwamba kesi ya ugaidi dhidi ya Mboewe, pamoja na kelele nyingi sana za Polisi, haina mshiko wa kisheria na kama kweli itasikilizwa kwa haki basi ni rahisi kwesi hiyo kutupwa au Mbowe na washitakiwa wenzake wote kushinda kesi.

Sasa unajiuliza, hivi ilikuwaje Mwanasheria Mkuu wa Serikali asimshauri Rais Samia kwamba kesi kama hii dhidi ya Mbowe haitakuwa na mshindi? Kwanza inaiweka Tanzania katika darubini ya mataifa makubwa ya nje.

Pili inafanya idadi kubwa ya watu kuamini kwamba Mbowe alikamatwa kwa ajili ya makongamano ya Katiba na ugaidi ni kisingizio tu.

Tatu inaonyesha wazi kwa watu wa ndani na nje kwamba CCM wanaogopa Katiba mpya kwa kuwa wanahofia uchaguzi ukifanywa katika mazingira ya kidemokrasia CCM hawatashinda.

Nne Mbowe akifungwa kwa mashitaka kama haya ambayo yapoyapo tu itampa umaarufu zaidi ndani na nje ya nchi, atakuwa Mandela wa Tanzania.

Tano Mbowe akiachiwa Rais Samia na CCM wataonekana wanabambikia wapinzani kesi.

Sasa kama Mwanasheria Mkuu alishindwa kuona haya na kumshauri Rais Samia dhidi ya kesi ya Mbowe, nina mashaka sana na uwezo wake wa kumshauri Rais, au lengo lake la ushauri aliotoa kwa Rais Samia.

Katika mazingira kama haya, ushauri wangu kwa Rais Samia ni kwamba atafute namna ya kuingilia suala hili, bila kuonekana anavunja uhuru wa Mahakama, ili watu wote waone kwamba Mbowe na wenzake waliachiwa na kesi hii kutupwa kwa sababu Raisi Samia alitumia busara katika kuimaliza.

Najua kwa sasa suala hili limemuweka Rais Samia mahali pagumu sana kwa kuwa halikupaswa kufika kote huku, lakini pia akiliacha liendelee mahakamani, matokeo yake yoyote, ya kesi kutupwa nje, au Mbowe na wenzake kufungwa au kuachiwa huru, hayatakuwa mazuri kwake Rais Samia na chama chake CCM
Acha poroja mahakama ipo. Ukweli mama samia akitaka mustakabali wake mwema amuachie mara moja sabaya ndio kabambikwa kesi sio mbowe.
 
Kuna rapper mmoja Mmarekani anaitwa Jadakiss, alisema katika moja ya nyimbo zake:-

"If I wasn't on some shit, I'm getting on it".

Alikuwa analalamika kuhusu mambo aliyokuwa anazushiwa. Akasema kwamba, sasa, kwa sababu watu wanamzushia sana, ataanza kufanya kweli hayo anayozushiwa ili lawama anazopewa zisiwe za bure, ziwe za kweli.

Nilivyoifikiria kesi hii ya ugaidi ya Mbowe nikakukmbuka mstari huo wa Jadakiss.

Nikasema, hawa CHADEMA wanaozushiwa ugaidi, hivi wakisema sawa, mnatuzushia ugaidi, sisi si magaidi, lakini kwa sababu mnatuzushia, sasa tunaanza kufanya ugaidi kweli ili kutimiza uzushi wenu.

CHADEMA wakaanza kupiga mabomu ofisi za CCM na nchi ikaingia katika milipuko ya mabomu.

Hao wanaozusha ugaidi watafurahi kuona uzushi wao unatimia?

Maana haya mambo mengine ni kama kunuia kitu kitokee, na hata mazungumzo ya ugaidi tu yanaweza kuanza kufanya watu wafanye kweli.

Mtauliwa kama wale wa kibiti
 
Umeongea point sana, na ndio maana nikasema mtu anaejua sheria ataona kwamba si vema kuingilia kesi iliyoko Mahakamani.

Lakini kuna njia nyingi za busara na hekima kwa raisi kuingilia kesi iliyoko mahakamani, na hilo ndilo ninalomwambia Raisi Samia afanye.

Kwa mfano, suala la kusema watu wenye kesi za uhujumu uchumi mahakamani wanaweza kukubaliana na DPP, ilikuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama, lakini lilifanyika. Sembuse hili?

Kuna ugumu gani kwa Raisi Samia kusema tumefanya mkutano na watu wa upinzani na kwa maslahi ya utaifa wetu tumekubaliana kuiomba ofisi ya DPP kufuta kesi zote za kisiasa nchini ili tuanze ukurasa mpya wa uhusiano kati ya CCM na vyama vya upinzani
Tatizo la washabiki wa wanasiasa wa Nchi hii hilo likifanyika watasema Rais aliwaogopa au walishinda kesi kwa nguvu zao "rejea kesi za Mashekh wa Uamsho na ya Mdude "
 
Kosa ni kosa hata kama mtendaji atakuwa si wa kwanza kulitenda!

Mimi napendelea zaidi mfumo wa haki ndiyo uamue hatia ya Mbowe. Siyo Rais wa nchi.

Leo watu wanataka waziwazi kuwa Rais aingilie kati na kumtoa Mbowe jela na kumfutia kabisa mashitaka.

Ni precedent mbaya sana maana akifanya hivyo, nini kitamfanya asifanye tena hivyo kuhusu mtuhumiwa mwingine yeyote yule huko mbeleni?

Si vizuri hata kidogo Rais kuanza kuingilia mambo ya utoaji haki wakati mfumo wa kufanya hivyo upo.
Hata mimi nakubaliana na wewe kuhusu haki mahakamani, lakini je akipatikana hana hatia, ni nini hatma ya waliomstaki ? Inabidi sasa nchi kama nchi ifikie mahali na kuwafidia wote wale ambao walishtakiwa na baadae mahakama kuona kwamba hawana hatia... pili hizi kesi zinazo wafanya watu wake mahabusi bila dhamana zina-breach haki za watu na due process nzima, sijui majaji wetu hizi sheria huwa wanasomea wapi na kuiacha serikali ifanye inavyotaka katika suala zima la kumaliza hizi kesi haraka...nimesikia wanasema kwamba upelelezi umekamilika , ya nini sasa kuendelea kumshikiria humo ndani na dana dana kibao za procedures tu na kukomoana..,. humu duniani hatuishi milele, tutafute namna ya kupendana sote kama ndugu wa Taifa moja bila chuki, mkwaruzo wala kesi za kuokotezea ushahidi...
 
Kuna jambo hapa wengi hawajui!!..Mbowe has nothing cha kupoteza kwenye case hii!!..Sasa kama ndivyo Itakua aibu kubwa Kwa serikali kupoteza case hii alafu italeta mtikisiko mkubwa nchini na Duniani kote!!.. Angali jinsi chadema na marafiki zao walivyojipanga kushinda case angalia jinsi case ilivyo kiajabu hata mtu ambae siyo mwanasheria anaweza kusema tayari Mbowe kashinda labda serikali iamue kuingilia Mahakama lakini Kwa jinsi ilivyo ni ngumu sana!!!..
Kama kujipanga ndiyo ticket ya uhakika kwa asilimia 100 ya kushinda kesi mahakamani wote waliojipanga wangekuwa wanashinda vyesi vyao. Hivi hujawahi kujiuliza pamoja na wingi wa mawakili wote wa Mbowe kwa nini wanashinikiza aachiwa kabla ya kesi kusikilizwa?. Kuna kitu haukijui. Wao wanaelewa potential risk iliyo mbele ya Mbowe. Usifanye utani na sheria
 
Back
Top Bottom