Kuna rapper mmoja Mmarekani anaitwa Jadakiss, alisema katika moja ya nyimbo zake:-
"If I wasn't on some shit, I'm getting on it".
Alikuwa analalamika kuhusu mambo aliyokuwa anazushiwa. Akasema kwamba, sasa, kwa sababu watu wanamzushia sana, ataanza kufanya kweli hayo anayozushiwa ili lawama anazopewa zisiwe za bure, ziwe za kweli.
Nilivyoifikiria kesi hii ya ugaidi ya Mbowe nikakukmbuka mstari huo wa Jadakiss.
Nikasema, hawa CHADEMA wanaozushiwa ugaidi, hivi wakisema sawa, mnatuzushia ugaidi, sisi si magaidi, lakini kwa sababu mnatuzushia, sasa tunaanza kufanya ugaidi kweli ili kutimiza uzushi wenu.
CHADEMA wakaanza kupiga mabomu ofisi za CCM na nchi ikaingia katika milipuko ya mabomu.
Hao wanaozusha ugaidi watafurahi kuona uzushi wao unatimia?
Maana haya mambo mengine ni kama kunuia kitu kitokee, na hata mazungumzo ya ugaidi tu yanaweza kuanza kufanya watu wafanye kweli.