Tetesi: Rais Samia, kama kuna upendeleo huu wa kielimu kwa Wasichana utaliangamiza Taifa

Tetesi: Rais Samia, kama kuna upendeleo huu wa kielimu kwa Wasichana utaliangamiza Taifa

Wakuu naingia kwenye mada moja kwa moja pasipo kuwachosha. Baada ya kushuhudia upendeleo kwa watoto wa kike wanaochaguliwa kuingia kidato cha tano, imenilazimu kutoa angalizo. Kama nchi tunakoelekea sio kuzuri. Kuna baadhi ya watu watachukulia poa lakini upendeleo huu ikiwa utadumu, basi tutarajie kutokea majanga katika nchi yetu.

Kuna waraka nimeuona unatembea social media unaonyesha wanafunzi wa kike kupewa upendeleo maalumu kuingia kidato cha 5. Kwa mfano, kwa tahasusi ya PCB na PCM wasichana watakaochaguliwa kuingia kidato cha 5 ni wenye ufaulu kuanzia alama 7 mpaka 17 wakati kwa wavulana ni kuanzia alama 7 hadi 15! Mbali na tahasusi hizi pia kuna tahasusi nyingine ambazo wasichana wamepewa upendeleo maalumu ili kuwaboost waingie kidato cha 5 kwa ubwete. Waraka huo umetolewa na wizara ya elimu na utaanza kutumika rasmi kuanzia mwaka huu.

Tumekuwa tukishuhudia upendeleo kwa wanawake kwenye siasa kwa kugawiwa nafasi za ubwete kupitia viti maalumu. Sasa naona huu upendeleo umevuka mipaka hadi kwenye elimu. Tunaliangamiza taifa kwa mikono yetu wenyewe, ama kwa makusudi au kwa kutokujua madhara ya baadaye kwa hiki tunachokifanya. Nafikiri upendeleo huu hauwezi kufanyika pasipo Rais wa nchi kushirikishwa na huenda ndiye kaagiza ifanyike hivyo. Lakini amini nawaambia upendeleo wa aina hii una madhara makubwa kuliko unavyoweza kudhani.

Wewe fikiria watoto wa jinsia zote (ke & me) wanafundishwa na mwalimu mmoja kwenye madarasa na mazingira yale yale na mtaala ni mmoja lakini baada ya mitihani watoto wa kike wanapata upendeleo maalumu. Unafikiri watoto wa kiume watajisikiaje au unataka wafanye nini?

Kwa harakaharaka nimegundua madhara yafuatayo yatajitokeza:

1. CHUKI KWA WANAWAKE
Kwa kuwa upendeleo unafanyika waziwazi huku watoto wa kiume (wanaume) wanaona, itafika wakati itajengeka chuki kati ya wanawake na wanaume kuanzia mashuleni hadi makazini kwa wanaume kushindwa kuwapa ushirikiano wanawake. Hata wakati wa kuomba ajira, kwenye usaili wanawake watakuwa wanakaziwa zaidi kwa kuwa walipendelewa kufika hapo walipo. Hii itajenga chuki itakayosambaa na kusababisha mpasuko wa kitaifa.

2. KUSHUKA KWA UFAULU WA WASICHANA
Kwa kuwa watabakia kuwa na akili za kupendelewa, basi hata kwenye masomo watashindwa kufanya jitihada za makusudi na matokeo yake ufaulu wao utazidi kushuka mwaka hadi mwaka. Sasa huu upendeleo utakuwa umewasaidia nini zaidi ya kuwadidimiza?

3. KUONGEZEKA KWA VITENDO VYA KISHOGA
Watoto wa kiume watadhani kuzaliwa wanaume ni makosa au laana. Matokeo yake watatamani wangezaliwa kama wanawake, jambo ambalo lisingewezekana. So, kufuatia kuongezeka vitendo vya kishoga hapa nchini, itakuwa rahisi kurubuniwa kuingia kwenye ushoga, hata ikibidi kubadili jinsia kwa upasuaji ili wawe wanawake wapate upendeleo wa bwerere.

4. KUONGEZEKA UKENGEUFU MIONGONI MWA WANAWAKE
Kuanzia sasa tutarajie kuongezeka mimba za wanafunzi, school dropouts na ujinga mwingine mwingi tu kutoka kwa watoto wa kike kwa kuwa sasa wamepewa nafasi ya kurelax bila kusoma wakisubiri kupendelewa. Na pia tukumbuke tayari wanayo ofa nyingine ya kurejea shule baada ya kujifungua. Tutarajie idadi ya wanafunzi wazazi kuongezeka mara dufu.

5. UNAHARAKATI UCHWARA
Watoto hawa wanaobebwa sasa, wakiwa wakubwa lazima watajiingiza kwenye uanaharakati wa kukandamiza wanaume kwa kisingizio cha kutafuta "haki sawa kwa wote". Watakuwa siku zote, kutwa kucha, wanajikita kwenye uanaharakati na kusahau majukumu yao ya kuwahudumia waume zao na kulea familia. Wataenda mbali zaidi kutaka wanaume nao wafanyiwe upasuaji ili wawasaidie kubeba mimba. Kutakuwa na taifa hapo? Obviously, taifa litasambaratika na kuvunjika vipandevipande!

6. KUONGEZEKA DIGRII ZA CHUPI
Wanafunzi hawa wanaopendelewa kuingia kidato cha 5, kipindi wakifika vyuo vikuu watataka bado waendelee kupendelewa. Hapo ndipo idadi ya digrii za chupi itakapoongezeka. Na kuanzia hapo itakuwa ni mwendo wa kuvua chupi tu hadi kwenye kutafuta ajira na kupanda vyeo huko makazini. Tunajenga taifa la ovyo sana hapo baadaye.

MAONI YANGU
Huu upuuzi unafanyika nchini Tanzania tu. Kama kuna nchi yoyote hapa ulimwenguni inafanya ushirkina huu, niite umbwa mimekaa paleee! Haijawahi kutokea tukawa na upendeleo wa kielimu wa aina hii katika nchi hii. Upendeleo wa kipuuzi kama huu unapaswa kuishia kwenye siasa. Wewe fikiria binti kapendelewa hadi amekuwa daktari. Je, huko mtaani atakuwa anatibu wagonjwa wa upendeleo wenye magonjwa ya upendeleo? Hii ni hatari sana.

Nawasilisha.
Unajua wanaume walioko kwenye nafasi za maamuzi ndio wanachangia anguko la watoto wa Kiume? yenyewe yanadhani sifa ila miaka michache ijayo tutakuwa na Taifa la KIJINGA sana sana wazungu wanaleta Ushoga na ku empower wanawake lengo nikuua uzao lkn majitu yanaona sawa tu
 
Tofauti na hoja ya viti maaluma huna hoja nyingine yoyote ya msingi.

Kuhusu wanawake kupata nafasi za upendeleo katika masomo ni sahihi kwa sababu jamii nyingi hasa za vijijini hazikuthamini masomo kwa mtoto wa kike kwa muda mrefu hivyo serikali inachofanya ni kusahuhisha hiyo injustice ya muda mrefu. Kuna visa vya watoto wa kike wanaambiwa wafeli mitihani ya darasa la saba makusudi ili waolewe.
Wewe ni mwanamke!
 
Hii dunia inapoelekea mwanamme anenda kupata tabu sana. Cha ajabu hayo mambo yanafanyika huku baadhi ya mijanadume ikiwa ndani ya hizo projects.

Siku hizi hata ma bank company ikiwa na wanawake ina possibility kubwa ya kuwa na advantages nyingi tu kwenye suala zima la mikopo.

Hawa mashetani lengo lao ni kuwa hii dunia itawaliwe na wanawake. na kuna mipuuzi kibao bado inaendelea kusapoti hayo mambo utawaona wengi humu wakichangia.
Nikiona mijtu tena miana ume inashobokea women empower nachukia sababu inachangia kuharibu hii Dunia
 
Hujui maana ya gender equality.

Gender equality ni upatikanaji sawa wa haki na fursa kwa jinsia zote. Yani kama mwanamke anataka kuwa Rais kusiwe na sheria zinazozuian au kutatiza yeye kuwa Rais au asinyimwe fursa ya Urais kwa sababu ya jinsia yake.
Your argument is basically a non argument since gender equity is the means aka process of which the goal or outcome is to achieve gender equality. Get your English right next time. My point was gender equality in Western countries and specially in Scandianvia is below what you’d expect despite decades of policies and social engineering efforts to redress the gender imbalance in those societies. End of the day, men will be men, and women will be women.
 
Ndugu Yoda, hii justification yako haina mashiko kwasababu... Kwanza kielimu unazalisha wasomi wa aina gan kama utawapa mbeleko kisa hawakupewa priority kielimu?
Nimefafanua vizuri huko juu kwamba hakuna wanafunzi wa kike wanaochaguliwa kuendelea kidato cha 1, 5 au vyuo wakiwa wamefeli. Kuna tofauti kubwa ya mbeleko na kipaumbele pale ambapo kuna ufinyu wa fursa.
 
Ndugu Yoda, hii justification yako haina mashiko kwasababu... Kwanza kielimu unazalisha wasomi wa aina gan kama utawapa mbeleko kisa hawakupewa priority kielimu?
 
Nikiona mijtu tena miana ume inashobokea women empower nachukia sababu inachangia kuharibu hii Dunia

wengi hua ni wale watumwa wa siasa za kimagharibi, na ndio haohao wanaosapoti mambo ya kishoga
 
Na wewe una amini hakuna zero kweli, hivi unajua kuna watu. Wamekwenda form one hawajui kuandika na kusoma vema, kuhesabu shida lugha ya Malkia ndio zero kabisa. Umeshawahi jiuliza wamepitaje?!

 
kama mwanamke anataka kuwa Rais kusiwe na sheria zinazozuian au kutatiza yeye kuwa Rais au asinyimwe fursa ya Urais kwa sababu ya jinsia yake.
Ni kifungu gani cha katiba kinachozuia hili mkuu? Hii ndio kwanza naisikia kwako.Ufafanuzi tafadhali.
 
Huu upuuzi wa kutunga mitihani ya ku-bet ili wanafunzi wa kike wafaulu ndio unaopelekea wanafunzi kupenya kwenda sekondari wakiwa hawajui KKK. Sijawahi kushuhudia maajabu kama haya katika nchi yoyote hapa Ulimwenguni, kama ipo niite mbwa nimekaa paleeeeee.........
 
children vs career



BTW thanks to distance learning a mum can still get her education while she stays home!
 
Back
Top Bottom