Rais Samia kaniangusha na kunisononesha sana ripoti ya CAG 2021-2022

Rais Samia kaniangusha na kunisononesha sana ripoti ya CAG 2021-2022

KWANZA HIVI NDIO VYEO VYAKE

1) Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
2) Mkuu wa nchi na kiongozi namba moja kwa pande zote mbili za Muungano.
3) Amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama.

Hivyo ni vyeo ambavyo vinamruhusu mheshimiwa raisi kuchukua hatua kwa mtu yoyote wa serikalini ambae anafanya kazi yake kinyume na sheria za nchi, aidha kwa yule anaeiibia serikali, anaetoa rushwa, anaepokea au kuchelewesha mipango ya serikali hasa inayohusu maendeleo nk.

Inasikitisha sana mtu mwenye vyeo hivyo anashindwa, au anasita kuwachukulia hatua kali za kuagiza wakamatwe na kufunguliwa mashtaka wale wote waliopatikana na tuhuma za ubadhilifu wa fedha za umma serikalini na badala yake raisi eti anawaomba tu waachie nafasi zao bila kufungwa au kurudisha fedha hizo ili zikatumike katika mambo mengine ya kimaendeleo.

Hata wale aliosema kwamba kila report zinapofika watu hao hao hukutwa na tuhuma zile zile ilitakiwa wakamtwe kwa tuhuma ile ile ya kwanza na kubanwa vizuri walipozipeleka fedha zetu, badala ya kutaka eti washushwe vyeo au kuhamishwa ofisi.

Yani mwizi wa ndala akamatwe na kufungwa huku mwanasheria wa serikali akitafuna kodi zetu kwa kuendesha kesi yake, afu yule anaeiibia serikali mabilioni ya shilingi ahamishwe tu kituo ili akaendelee na utafunaji wa fedha zetu huko katika ofisi nyingine. Ni kwanini asifukuzwe kazi ili nafasi yake ichukuliwe na mtu mungine na ukizingatia kuna watu wengi wana elimu zao mitaani lakini kazi hawana?

Lakini pia sio aishie kufukuzwa tu bali afunguliwe kesi ya uhujumu uchumi na mali zake zote zitaifishwe na kurudishwa katika mikono ya wananchi.

China imeweza kupiga hatua duniani baada ya viongozi wa nchi hiyo kusimamia vyema kodi za wananchi wao kwa kutoa adhabu kali kwa yeyote atakaejaribu kugusa fedha za serikali.
Pia hata Rwanda ipo vizuri baada ya raisi wa nchi hiyo kukitumia vyema cheo chake.

Raisi na amiri jeshi mkuu ukibaki kulalamika, unafikiri mawaziri na viongozi wengine wa kawaida wataweza kuwa na uwezo wa kujiamini kuchukua hatua kweli.

Kama kulalamika umeshalalamika kwa zaidi ya miaka miwili sasa lakini upigaji ni ule ule. Sasa kabla ya kuwaambia watu na hili mkalitizame, tunakuomba na wewe kwanza ujitizame kwamba hiyo ndio njia sahihi ya kuendelea ku deal na mafisadi.

Hebu tumia nguvu zako ulizopewa na katiba yetu kuwachukulia hatua wabadhilifu wa kodi zetu, kabla na sisi hatujaingia barabarani kama wakenya.

Ukicheka na nyani shambani usishangae kuvuna mabua.
CCM ni uozo kuanzia kichwa hadi kwenye unyayo
 
Mifumo ipi mkuu? Kwamba raisi kumsimamisha kazi au kumfukuza kazi mtu alietafuna fedha za umma na kuagiza vyombo vya ulinzi vimkamate na kumhoji na ikiwezekana afikishwe mahakamani nayo inahitaji kubadilisha mfumo?
Muulize ni mfumo gani uliomfikisha mahakamani sabaya na kumkamata na kunyimwa dhamana?
 
Dah! Umejibu vizuri Sana sijui nani kawadanganya CCM pekee ndio tatizo
Kweli mkuu. Kumuamini mwanasiasa yoyote wa chama chochote ni sawa sawa na kuamini kuwa jogoo anaweza kunyonyesha.
 
Tatizo wala si SSH. Bali ni mfumo uliomfikisha hapo. Wengine wanadai Bora JPM lakini Mimi nasema mfumo kwenye Taifa la mamilioni ya watu haubadilishwi na mtu mmoja.
Fanyeni overhaul ya mfumo mzima uliotengenezwa na ccm.
Otherwise mtawalaumu sana wezi na Rais wenu.
Kwa hii mifumo iliyopo hata akija malaika mkuu Gabriel baada ya miezi kadhaa atakuwa mpiga Dili zaidi ya hawa waliopo!
Hii kazi unayotupa sio yetu kabisa, hao wenye madaraka na mamlaka ndio wanaobadilisha mfumo na mara zote wamejikinga kuzuia waendelee na mambo yao. Raisi atambue mamlaka na madaraka yake kwanza, na achukue hatua kama amiri jeshi yeye ndie katiba imempa kinga hao waliopiga pesa anawajua sasa anaweza hata kuamuru wapigwe risasi hadharani.
Sie huku ni kujaza thread JF, hakuna kitu mifumo wala nini kama chawa na yeye katengeneza wake, kama kusifiwa we shahidi sasa ajipime mwenyewe na ajichukulie hatua.
 
Mifumo ipi mkuu? Kwamba raisi kumsimamisha kazi au kumfukuza kazi mtu alietafuna fedha za umma na kuagiza vyombo vya ulinzi vimkamate na kumhoji na ikiwezekana afikishwe mahakamani nayo inahitaji kubadilisha mfumo?
Hapo ndo ipo shida ya mfumo, rais akimsimamisha au kumfuta mtu kazi (sijui kama lipo kisheria) ila wanaoenda kumkamata, kumhoji, na kumshitaki kama hawataki ashindwe basi atashinda na atalipwa pamoja na mafidia mengi atakayogawa kwa wanamfumo waliofuma ushindi. Usipoelewa hivi shauri yako ila ndo mfumo wenyewe sasa.
 
Hatukamati watu kwa tuhuma tuu, sasa ni mpaka uthibitisho!.

P
Itathibitishwaje ikiwa raisi mwenyewe anashauri kuwa watuhumiwa washushwe tu vyeo au wahamishwe ofisi na kupelekwa ofisi nyingine, badala ya kuagiza wasimamishwe wachunguzwe na ikithibitika kuhusika basi hatua zichukuliwe juu yao!

Unategemea kumshusha cheo au kumuamisha ofisi mtuhumiwa ndio njia nzuri ya ku deal nae?

Mkuu soma post yangu namba #29 nimelielezea vizuri.
 
Nchi inaendeshwa kwa kufuata katiba. Rais akiamua kutumia madaraka yake unavyotaka si tutarudi kwenye mambo ya awamu ya 5? Vyombo vya dola ndo vinatakiwa viwakamate wahusika na kuwapeleka mahakamani. Tukisema Mama aanze kutumia ubabe hakutakalika. Tumshukuru sana kwa kuamua kufuata utawala wa kisheria.
Wezi wenyewe jamii ya kina joka la makengeza utaweza kuwakuta na hatia kweli?
 
Hapo ndo ipo shida ya mfumo, rais akimsimamisha au kumfuta mtu kazi (sijui kama lipo kisheria) ila wanaoenda kumkamata, kumhoji, na kumshitaki kama hawataki ashindwe basi atashinda na atalipwa pamoja na mafidia mengi atakayogawa kwa wanamfumo waliofuma ushindi. Usipoelewa hivi shauri yako ila ndo mfumo wenyewe sasa.
Hata wakikutwa na hatia adhabu ya aliyeiba bilioni alipe milioni mbili au jela miaka miwili, hakuna mwenye nia ya dhati ya kupigana na uwizi wa mali ya umma nchi hii
 
Na kuvuna mabua ndio kunakofanyika kwa sasa !! Nchi hii ukiwaambia mimi sikuzowea kufukuzana fukuzana na kufokeana fokeana hapo ujue umewawashia taa ya kijani mijizi ya pesa za umma !!
Nchi imerudi katika mikono ya shamba la bibi.
 
Nimesononeka baada ya kusema hao wapigaji waondolewe sehemu zenye ulaji mwingi wapelekwe sehemu zisizona neema ili wakapate tabu kidogo

Kwanini wasishitakiwe?
 
Acha kuleta porojo. Yaaani unataka ushahidi gani hata kama kuna premafacie evidence?
Hata mimi nimemshangaa anko Pascal Mayalla . Yani anaridhika raisi kushauri watuhumiwa wabadilishiwe ofisi, badala ya kusimamishwa ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zao, na ikithibitika kuwa walihusika wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria za nchi.
 
Muulize ni mfumo gani uliomfikisha mahakamani sabaya na kumkamata na kunyimwa dhamana?
Ndio kuna sehemu nimemjibu kwamba vipi kuhusu Sabaya? Mpaka sasa bado hajarudi kujibu.
 
Nimesononeka baada ya kusema hao wapigaji waondolewe sehemu zenye ulaji mwingi wapelekwe sehemu zisizona neema ili wakapate tabu kidogo

Kwanini wasishitakiwe?
Imagine unamtoa mwizi kwenye nyumba kubwa na kumpeleka kwenye nyumba ndogo ukihisi unamkomoa, wakati zile pesa alizoiba bado anazo ndani, na mwisho wa mwezi anaendelea kupokea mshahara kutoka kwa aliowaibia.
 
Back
Top Bottom