Rais Samia kaniangusha na kunisononesha sana ripoti ya CAG 2021-2022

Rais Samia kaniangusha na kunisononesha sana ripoti ya CAG 2021-2022

Na mimi inanitia shaka kwamba huyu Bi mkubwa kuendelea kulakamika tu kama raia wa kawaida wa mtaani isijekuwa anatupiga changa la jicho kumbe lao ni moja pamoja na hao mafisadi na wabadhirifu wa pesa yetu.

Mama asitake kituaminisha kwamba cheo chake amekipata kwa bahati mbaya, inampasa akitendee haki cheo chake, haiwezekani Wananchi tunalalamikia shida na Ugumu wa maisha ilhali kuna watu wanakwapua billions of Shillings zetu na iishie kuwasema tu kwenye podium na habari iishe kirahisi hivyo!!,

Our beloved Mom, with due respect, you seriously need to take concrete actions in accordance with the laws to pin those swindlers of Our money. Those culprits are tarnishing your political image not only within but also outside the country.
Mawaziri ndo wanaiba fedha halafu anasema mawaziri na makatibu wa kuu mtu saidie
 
Khaaa umevuka mipaka mkuu! Tuliza hasira kidogo! Tukosowe kwa staha!
Its true staha peleka kwa mumeo watu wanakata makodo , matozo gharama za maisha zipo juu halafu kuna wwtu wanaenda kukwapua mahela hayo kiurahisa .hivi unajua watakuwa wameua watanzania wangapi unafikiri
 
Hayo yote alikua akiyaweza jiwe Magufuli japo maamuzi yake mliyaona ni utopolo saiv ndo mtaelewa mwendo mzuri wa kuwaendesha Watanzania
Alishaenda zake! Sasa Mkuu kifanyike kipi wakati Mwendazake hayupo?
 
KWANZA HIVI NDIO VYEO VYAKE

1) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
2) Mkuu wa nchi na kiongozi namba moja kwa pande zote mbili za Muungano.
3) Amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama.

Hivyo ni vyeo ambavyo vinamruhusu mheshimiwa Rais kuchukua hatua kwa mtu yoyote wa serikalini ambae anafanya kazi yake kinyume na sheria za nchi, aidha kwa yule anaeiibia serikali, anaetoa rushwa, anaepokea au kuchelewesha mipango ya serikali hasa inayohusu maendeleo nk.

Inasikitisha sana mtu mwenye vyeo hivyo anashindwa, au anasita kuwachukulia hatua kali za kuagiza wakamatwe na kufunguliwa mashtaka wale wote waliopatikana na tuhuma za ubadhilifu wa fedha za umma serikalini na badala yake Rais eti anawaomba tu waachie nafasi zao bila kufungwa au kurudisha fedha hizo ili zikatumike katika mambo mengine ya kimaendeleo.

Hata wale aliosema kwamba kila report zinapofika watu hao hao hukutwa na tuhuma zile zile ilitakiwa wakamtwe kwa tuhuma ile ile ya kwanza na kubanwa vizuri walipozipeleka fedha zetu, badala ya kutaka eti washushwe vyeo au kuhamishwa ofisi.

Yani mwizi wa ndala akamatwe na kufungwa huku mwanasheria wa serikali akitafuna kodi zetu kwa kuendesha kesi yake, afu yule anayeiibia serikali mabilioni ya shilingi ahamishwe tu kituo ili akaendelee na utafunaji wa fedha zetu huko katika ofisi nyingine. Ni kwanini asifukuzwe kazi ili nafasi yake ichukuliwe na mtu mungine na ukizingatia kuna watu wengi wana elimu zao mitaani lakini kazi hawana?

Lakini pia sio aishie kufukuzwa tu bali afunguliwe kesi ya uhujumu uchumi na mali zake zote zitaifishwe na kurudishwa katika mikono ya wananchi.

China imeweza kupiga hatua duniani baada ya viongozi wa nchi hiyo kusimamia vyema kodi za wananchi wao kwa kutoa adhabu kali kwa yeyote atakaejaribu kugusa fedha za serikali. Pia hata Rwanda ipo vizuri baada ya raisi wa nchi hiyo kukitumia vyema cheo chake.

Rais na amiri jeshi mkuu ukibaki kulalamika, unafikiri mawaziri na viongozi wengine wa kawaida wataweza kuwa na uwezo wa kujiamini kuchukua hatua kweli.

Kama kulalamika umeshalalamika kwa zaidi ya miaka miwili sasa lakini upigaji ni ule ule. Sasa kabla ya kuwaambia watu na hili mkalitizame, tunakuomba na wewe kwanza ujitizame kwamba hiyo ndio njia sahihi ya kuendelea ku deal na mafisadi.

Hebu tumia nguvu zako ulizopewa na katiba yetu kuwachukulia hatua wabadhilifu wa kodi zetu, kabla na sisi hatujaingia barabarani kama wakenya.

Ukicheka na nyani shambani usishangae kuvuna mabua.
Nani kama Mama?
 
Rudi kasome kuanzia uraia, civics, GS, DS, hadi political science.
Wenye nguvu ni wananchi ndani ya nchi Wao ndo wanaamua waongozweje!
Wananchi wa nchi gani???? kwa nyie mliokuwa shule ndio mnavyofundishwa mambo yenu ya kusadikika huku mtaani
 
Kuna shida ya elimu ya utawala wa sheria , hata kama hayo mamlaka Rais anayo haipi jukumu la kutoa amri,Kamata, weka ndani,ndiyo mtu aende mahakamani Rais anatufundisha juu ya Ubutu wa taasisi zetu za haki jinai na uchunguzi,nadhani kuna haja CAG report na PCCB report itungwe sheria kali mtu wa watu wakitajwa kuhusika na wizi wa mali za umma basi siku hiyo watajwe na wawekwe kizuizini kwanza.
 
Wananchi wa nchi gani???? kwa nyie mliokuwa shule ndio mnavyofundishwa mambo yenu ya kusadikika huku mtaani
Kenya baada ya wananchi kuandamana mfululizo bila kujali ukatili wa polisi... Imefikia hatua Ruto kaomba Pause!
Wakumbusheni wananchi umuhimu na ukuu wao kwenye nchi! Msiwakatishe tamaa!
 
Na hao internal auditors ndiyo wanafanya michongo na wakuu wa wa wizara, kurugenzi na taasisi za umma
Sasa hapa Audit inatoa Ukweli? Hakuna anayekubali kufa Njaa. Yaani hakuna Mkate Mgumu mbele ya Chai ya Moto.
 
Back
Top Bottom