Rais Samia: Kigoma inaenda kuunganisha na gridi ya Taifa

Rais Samia: Kigoma inaenda kuunganisha na gridi ya Taifa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akihutubia wananchi wa Kibondo katika mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Kibondo Mkoani Kigoma, leo tarehe 16 Oktoba, 2022.





Rais Samia akiwa kigoma amesema wanaenda kuzima majenereta huko Kigoma kuwa kuwa Kigoma inaenda kuunganishwa na gridi ya taifa hivyo itapata umeme wa uhakika kwa muda wote. Rais amesema mkoa huo unapakana na nchi kadhaa mabpo ni vizuri kuboresha huduma za nishati kwa kuwa nchi jirani zinaweza kuja kununua umeme kutoka Tanzania.

Katika hatua nyingine Rais amezungumzia miradi ya maji na barabara pamoja na kilimo iliyowekwa katika Mkoa huo. Kuhusu kilimo amesema watu wataanza kufanya kilimo cha umwagiliaji kutokana na uwekezaji utakaowekwa katika sekta hiyo.

Rais Samia yupo Kigoma kwa ziara ya kikazi na amesema ziara hiyo ilicheleweshwa kiasi kutokana na kifo cha malkia wa Uingereza​
 
Ila nimegundua vyama vya upinzani vina nguvu. Huyo Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kigoma alipogusia vyama vya upinzani kutopewa nafasi ya uongozi uwanja ukawa kimya Sana. Nadhani amejifunza kitu
 
Mama anajituma sana katika kuwaletea maendeleo watanzania.

Kila hatua anayo kanyaga ina mafanikio makubwa sana kwa wananchi.

Tunampongeza sana kwa kazi nzuri.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akihutubia wananchi wa Kibondo katika mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Kibondo Mkoani Kigoma, leo tarehe 16 Oktoba, 2022.





Rais Samia akiwa kigoma amesema wanaenda kuzima majenereta huko Kigoma kuwa kuwa Kigoma inaenda kuunganishwa na gridi ya taifa hivyo itapata umeme wa uhakika kwa muda wote. Rais amesema mkoa huo unapakana na nchi kadhaa mabpo ni vizuri kuboresha huduma za nishati kwa kuwa nchi jirani zinaweza kuja kununua umeme kutoka Tanzania.

Katika hatua nyingine Rais amezungumzia miradi ya maji na barabara pamoja na kilimo iliyowekwa katika Mkoa huo. Kuhusu kilimo amesema watu wataanza kufanya kilimo cha umwagiliaji kutokana na uwekezaji utakaowekwa katika sekta hiyo.

Rais Samia yupo Kigoma kwa ziara ya kikazi na amesema ziara hiyo ilicheleweshwa kiasi kutokana na kifo cha malkia wa Uingereza​

ni muda mrefu sana Kigoma ilikua nyuma hivi inamaanisha hizo generator zilikua zikiwekwa mafuta miaka yote tangu uhuru wa nchi
 
Nunueni sola tuu ndugu wananchi, huo umeme wa TANESCO ni upumbavu mtupu, unakatika masaa 18 na bei yake ni bora kulala gizani tuu
 
Kweli waafrica tunajua kupoteza muda kwa mambo yasiyo na maana, siamini kishughuli kama hiki kimechukua masaa matatu, tafadhari tuache huu upuuzi,gharama za sherehe na bei ya magari ya serikali yaliyoingia na msafara wa Raisi na viongozi wengine wa serikali yanaweza hata kuzidi gharama za mradi wao wa maji...hizo V8 ni kama 400milioni na hapo tuu uwanjani kuanzia za wabunge, wakuu wa mikoa na wilaya, msafara wa Raisi, wakurugenzi etc zipo zaidi ya 20, na mradi wa maji wilaya nzima billion 7.....huu ujinga sijui tutaacha lini
 
Back
Top Bottom