Rais Samia kila akisifia mazuri yaliyofanywa na Hayati Magufuli; Nderemo, shangwe na makofi hutawala. Hii ina maana gani?

So sad!
 
Nilishasema policy ya huyu ni Ile Ile,kusifia marehemu akiwa ndani ,kumponda akiwa nje..ni win win situation kwake..ila kwa jinsi wapiga Kura wa tz walivyokuwa hamnazo,they fall for this act every time.
Yaani!
 
Nimeipenda hii!
 
Kwa vile wengi tuna roho mbaya tuna hamu ya kusikia " fulani katumbuliwa, fulani kakamatwa kwa amri ya kiongozi fulani, fulani kafukuzwa kazi jukwaani, fulani kapotezwa nk.

Jamii yenye mifumo imara inayofanya kazi vema haihitaji siasa za sarakasi majukwaani.Yaasii zinafanyakazi zilizopangiwa.

Tuache roho mbaya!!
Tuache hisia eti siku ndio inakuwa yule kapiga sijui nn.

Hivi aliyepiga 1.3 trilioni na CAG akahoji alikuwa nani?

Tuamke!!
 
Ni jambo jema kufurahia mamb mazuri pia tusiwachukie wanaosema mabaya yake pia, maan yote ni sehem ya uongoz husika!!
 
kiujumla bwana yule alikuwa kipenzi cha watanzania waliozoea mchezo mchafu wa wizi wa fedha za umma na ujanja ujanja hakuwahi kumpenda hadi sasa watu hao hawataki kulisikia jina hilo.
 
kiujumla bwana yule alikuwa kipenzi cha watanzania waliozoea mchezo mchafu wa wizi wa fedha za umma na ujanja ujanja hakuwahi kumpenda hadi sasa watu hao hawataki kulisikia jina hilo.
Inavyoonekana Mkuu.
Maana Watanzania wa hali ya kawaida ambao ndo wengi, inaonekana walikuwa wanampenda sana.
Na kadri siku zinavyozidi kusonga, hata wale waliomchukia wanampenda kama ambavyo mwenyewe aliwahi kutabiri enzi za uhai wake.
"NAJUA SIKU MOJA MTANIKUMBUKA, TENA MTANIKUMBUKA KWA MEMA WALA SI KWA MABAYA".
 
Jpm anapendwa na mazuzu na ambayo hayana elimu kabisa. Chunguza utagundua. Na kilichowafulihisha ni Ile ya kutumbua tumbua hivyo walikuwa wakifirahi ili wote wote wawe maskini. Hivyo ni wivu na ushamba wa baadhi ya watanzania. Hakuna msomi anayempenda jpm
 
Msomi mwenye akili timamu asimpende Hayati JPM?!
Nina mashaka na elimu yako..
Umchukie mtu ambaye;
1. Kajenga miundombinu mizuri na ya kisasa
2. Alidhibiti tozo na kodi kandamizi kama zilizopo sasa hivi
3. Alitoa Elimu bure kuanzia msingi hadi sekondari
4. Alidhibiti mfumko wa bei za vitu na gharama za maisha kwa ujumla
5. Alithubutu kutotufungia wakati wa Covid 19
6. Alinunua ndege zaidi ya 12
7. Kajenga meli na vivuko vya kutosha n.k!
Hao wasomi wanaomchukia, ni wapumbavu na wasio na uzalendo wowote na nchi yetu ova.
 
Kila usikiapo kelele nyingi kutoka katika umati mkubwa wa watu haimaanishi kuwa ni shangwe wakati mwingine dalili ya watu kuonyesha kujutia jambo, janga ama dhahama kubwa iliyowakumba.
 
Inatokana na yeye binafsi kujibainisha kwa kauli na vitendo kumpinga jpm. Alianza kwa maneno kuonesha yeye hapendi ukali wala hataki wafanyakazi kua na nidhamu ya woga. Hilo likafurahiwa na wapigaji na wazembe. Pia akamtimua kijana mwanamapinduzi sabaya aliyeaminiwa sana na magufuli na kumfunga jela. Kisha akaanza kuwarudisha kwenye uongozi wale walitumbuliwa na jpm na wale waliyosikika wakimsengenya jpm na kumdharau kwa ubaya mmoja baada ya mwingine. Yote hayo yakawafurahisha fisadi na wazembe kazini. Na kuna mengine mengi.
Matokeo yake kwake yamekua hasi. Wananchi wengi waliyompenda na kumwamini magufuli wakavunjika moyo. Mama akalijua hilo.
Sasa badala ya kumtaja magufuli kwa vijembe dhidi yake anamtaja kwa sifa pale lipo jambo lakumtolea sifa na mambo hayo yako lukuki na kila mahali. Inapobidi kumtaja magufuli wananchi hushangilia sana kwa kumsuta yeye mwenyewe. Ni kama wanampiga na yeye kijembe. Huo ni mtazamo wangu.
 
Umeongea vizuri sana Mkuu. Mi nafikiri Mh. angejitahidi tu kumsifu mtangulizi wake na kujitahidi kufuata nyayo. Hii itamrahisishia kazi ya kujinadi mwaka 2025, kuliko akiendelea kumponda na kumpiga vijembe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…