Rais Samia kuanza safari ya kikazi nchini DR Congo

Rais Samia kuanza safari ya kikazi nchini DR Congo

Nilichosema mimi mkuu ni kwamba ziara za Rais katika nchi mbalimbali zinapaswa kubase kwenye vipaumbele vyenye tija kwa Taifa.

Kwani Rais anapoenda Congo hatuna ubalozi huko?

Ohhh my Godness!!!Mkuu nimeitumia japani kama mfano tu wala sijamaanisha kuwa ina tija kuliko Burundi. Angalia andiko langu kuna neno "kwa mfano" kabla ya kuitaja Japan.

Sasa umejuaje kuwa alienda Russia kwa sababu ni jirani yake na wala siyo kwa sababu ni kipaumbele chenye tija kwa nchi yake?

Mimi msimamo wangu ni uleule hata kama hutaki kuelewa; kuwa Taifa huwa linaongozwa kwa kuzingatia vipaumbele vyenye tija.Je,Congo Burundi na wengineo wana tija kwetu kuliko Mataifa mengine duniani hadi tuwape kipaumbele cha kuanza kuwatembelea?

Again,nilitumia japan kama mfano tu kama nilivyosema hapo juu.

Hoja yangu ni nyepesi sana ila ngumu sana kwako kuielewa.Mimi sijalazimisha aanze kwenda popote pale ila hoja yangu ya msingi ni kwamba anapaswa aanze kwenda kule ambapo ni kipaumbele chenye tija kwa Taifa letu kwa sababu Taifa huongozwa kwa kuzingatia vipaumbele.
Mkuu hebu niambie unaelewaje hiyo kauli ya kipaumbele chenye tija?

Yaani kwenda kuwabembeleza majirani waendelee kutumia bandari yako na kufanya biashara na wewe sio kipaumbele chenye tija kwa definition yako? Ila kwenda china kuwaomba wafungue kiwanda cha bajaji na bodaboda kwako ndiyo kipaumbele chenye tija au sikuelewi vizuri?
 
Hii ziara inaweza kuwa ya kimkakati na ya muhimu pengine kuliko ziara zote zilizofanyika toka mama aingie ikulu. Ni jambo la wazi kuwa katika nchi zote za maziwa makuu, DRC imejaaliwa kuwa na idadi kubwa ya watu takriban watu 120,000,000.

Itakumbukwa kuwa Tanzania tumejaaliwa kuwa na bandari, ambapo miongoni mwa nchi zinazotumia bandari yetu ni DRC.

Tanzania imekuwa ujenzi mkubwa wa reli ya mwendokasi ambayo inategemewa kuwa msaada mkubwa wa usafirishaji wa watu na mizigo kuelekea nchi za Rwanda, Burundi na DRC. Kimkakati, kama ujenzi huo utakamilika, Tanzania itakuwa imalamba dume kwa sababu tutaweza kujiinua kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji pamoja na kufaidika na masoko ya bidhaa zetu kupitia wato miliuoni miamoja waliopo mashariki mwa Kongo.

Mnyonge mnyongeni lakini haki haki yake apewe. Ziara ya Rais wetu huko DRC haipaswi kubezwa kwa sababu kiuchumi inalipa tofauti na nchi kama Rwanda, Burundi na Uganda ambazo zinapitisha mizigo yao katika bandari yetu ya Dar Es Salaam lakini, mizigo yao kidogo kuliko ile DRC kutokana na idadi ya watu katika nchi hizo ni ndogo.

Hongera Mh. Raisi wetu kwa kupanga ziara ya kimkakati ya DRC ambayo ni muhimu sana kwa musakabali wa uchumi wa nchi yetu.
Hizi tantarira tu
 
Mkuu hebu niambie unaelewaje hiyo kauli ya kipaumbele chenye tija?
Kila Taifa duniani lina nchi ambazo ni muhimu sana kwake kiuchumi,kisiasa na kijamii na pia lina nchi ambazo siyo muhimu sana kwake kiuchumi,kisiasa na kijamii.Ninavyosema kuwa Rais wa nchi anapaswa aanze kutembelea kwanza nchi ambazo ni kipaumbele namaanisha zile nchi ambazo ni muhimu sana kwa Taifa lake kiuchumi,kisiasa na kijamii.
Yaani kwenda kuwabembeleza majirani waendelee kutumia bandari yako na kufanya biashara na wewe sio kipaumbele chenye tija kwa definition yako?
Umetumia data gani au statistics gani au credible source gani kujua kuwa Burundi,Congo,Kenya na Rwanda zina tija kuliko nchi zingine kama vile Marekani,Uengreza,Japan,China na kadhalika kwa mfano?
Ila kwenda china kuwaomba wafungue kiwanda cha bajaji na bodaboda kwako ndiyo kipaumbele chenye tija au sikuelewi vizuri?
Halafu unaanza kuniboa.Wapi nimesema kuwa China ni kipaumbele chenye tija kwa Tanzania?Tokea nimeanza kucomment kwenye huu uzi hakuna sehemu yoyote ambayo nimetaja kuwa nchi fulani ni kipaumbele chenye tija kwa Tanzania.

Msingi wa mazungumzo yote haya ni swali ambalo nimeuliza mwanzoni kabisa mwa huu uzi kuwa Rais anapotoa kipaumbele katika kuanza kuitembelea Congo,Rwanda na Burundi hizi ndiyo nchi duniani ambazo ni kipaumbele chenye tija kwetu?Hili ni swali ambalo niliuliza watu kama wewe ili mnipe majibu ila mpaka sasa hivi hakuna mtu alienipa jibu.
 
Hilo wasema wewe, mimi nilijibu swali lako la awali. Sijui unalikukmbuka!? Hili la sasa ni swali jingine jipya na linahitaji majibu mengine mapya.
Swali nililouliza awali ndiyo hilihili labda uwe hukunielewa na ndiyo maana sasa hivi nikatumia lugha inayoeleweka zaidi ili unielewe.
 
Wakuu Kazi Iendeleee.

Taarifa zilizopo ni kwamba Rais Samia ana ziara ya kikazi nchini Congo.

Ataanza ziara hiyo wakati atakapotoka Zambia kwenye inauguration ya Hakainde Hichilema.

Akifika Congo atapokekewa na Mwenyeji Wake Rais Felix Tshisekedi.

Hakika Ziara zimeanza na Zimetaradadi
Huyu bibi kwa umri wake mkubwa hivi hachoki kusafiri?
 
Hii ziara inaweza kuwa ya kimkakati na ya muhimu pengine kuliko ziara zote zilizofanyika toka mama aingie ikulu. Ni jambo la wazi kuwa katika nchi zote za maziwa makuu, DRC imejaaliwa kuwa na idadi kubwa ya watu takriban watu 120,000,000.

Itakumbukwa kuwa Tanzania tumejaaliwa kuwa na bandari, ambapo miongoni mwa nchi zinazotumia bandari yetu ni DRC.

Tanzania imekuwa ujenzi mkubwa wa reli ya mwendokasi ambayo inategemewa kuwa msaada mkubwa wa usafirishaji wa watu na mizigo kuelekea nchi za Rwanda, Burundi na DRC. Kimkakati, kama ujenzi huo utakamilika, Tanzania itakuwa imalamba dume kwa sababu tutaweza kujiinua kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji pamoja na kufaidika na masoko ya bidhaa zetu kupitia wato miliuoni miamoja waliopo mashariki mwa Kongo.

Mnyonge mnyongeni lakini haki haki yake apewe. Ziara ya Rais wetu huko DRC haipaswi kubezwa kwa sababu kiuchumi inalipa tofauti na nchi kama Rwanda, Burundi na Uganda ambazo zinapitisha mizigo yao katika bandari yetu ya Dar Es Salaam lakini, mizigo yao kidogo kuliko ile DRC kutokana na idadi ya watu katika nchi hizo ni ndogo.

Hongera Mh. Raisi wetu kwa kupanga ziara ya kimkakati ya DRC ambayo ni muhimu sana kwa musakabali wa uchumi wa nchi yetu.
Hakuna lolote ni matumizi mabaya ya fedha za umma, toka ameshika madaraka hajawahi hata kufika Mbeya lakini tayari Rwanda na Uganda keshaenda mara 2
 
Bora afanye haya, kuliko kuuwa watu, kubambija kesi watu. In short kuonea watu kama mtangulizi wake.
 
Kama mshauri wake ni vasco da gama unategemea nini?

Halafu nchi anazosafiri kwenda zina mchango mdogo kwenye uchumi wetu.

Asafiri kutafta wawekezaji wa maana huko Ulaya walete mitaji kutusaidia ku exploit hizi natural resources tulizonazo.

Sio muda utasikia ana ziara Somalia.

Yaani hapa tumeingia cha kike kweli.
yaani watanzania tumejisahau sana nafikiri ni kutokana na hii amani tuliyo nayo ndiyo maana kila rais anayeingia madarakani sasa hivi munamuona ana kasoro yaani sijui mnataka rais wa namna gani ? aliingia magufuli hataki safari za nje mkaanza kusema rais gani hasafiri ? amejitahidi kufanya kazi kizarendo kwa muda mchache amefanya makubwa lakini bado mnamsema vibaya mzee wa watu mpaka akaamua kurudi kwa baba yaani siku itafika nchi itakapo kua kama somalia au hata kama kenya tu kila siku tuwe tunasikia sehemu alshababu wamelipua sehemu wamekaba nafikiri ndiyo akili zitawakaa sawasasahivi bado mnaona kila kitu ni rahisi sana
 
Back
Top Bottom