Rais Samia kuhudhuria Uapisho wa Ruto ni kuendelea kudumisha Diplomasia

Rais Samia kuhudhuria Uapisho wa Ruto ni kuendelea kudumisha Diplomasia

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
FchkrWDXEAAYCPp.jpg


Rais Samia Suluhu Hassan anaendelea kudumisha diplomasiano na mahusiano mazuri kati ya Tanzania na Kenya pia Rais Samia Suluhu amezungumza na Rais Mteule wa Kenya, William Ruto na wameafiki kukuza ushirikiano katika biashara, kilimo na usalama kwa manufaa ya nchi zote. Uuzaji wa bidhaa za Tanzania nchini Kenya ulikua kufikia 6.2% mwaka 2021 kutoka 3.8% mwaka 2020.

Baada ya mazungumzo Rais Mteule Ruto amesema, "Tutapanua ushirikiano wetu na Tanzania katika masuala ya biashara, kilimo, usalama miongoni mwa maeneo mengine yenye maslahi, kando na kufanya kazi pamoja katika moyo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa manufaa yetu sisi sote", William Ruto.

Mwaka 2021 Tanzania na Kenya zilitatua vikwazo 56 vya kibiashara, hivyo biashara ikakua kufikia zaidi ya TZS trilioni 2.3.

Hivyo Rais Samia Suluhu Hassan anaendelea kuimarisha Diplomasia ya Uchumi. Tuendelee kumuombea Rais wetu maana kazi anayoifaya ya kuleta maendeleo ni kubwa sana.
 
Hajaalikwa, hajaalikwa, Tanzania Haijaalikwa..... Ujumbe toka kwa Thread moja hapa JF iliandika.

Sijui kwanini mtu anapenda sana/ anafurahia sana mabaya mpaka kiasi cha kusambaza uongo. Tuache tabia hii haitufikishi popote pale.

Kama ni wakereketwa/wanachama wa chama fulani, nawaambia chama hicho kamwa hakitafanikiwa kushika utawala wa nchi hii. Tabia hii ilaaniwe na pande zote.

Rais Tanzania- Samia Suluhu Hasan muda huu yupo mjengoni Kasarani katika sherehe za kumuapisha Rais wa Kenya S ruto.

Amani juu yenu.
 
Mke wa DP Rigathi Gachagua ni Mchungaji, anaitwa mchungaji Dorcas Rigathi.
Pia First Lady Rachel Ruto pia yuko vizuri.
 
Hajaalikwa, hajaalikwa, Tanzania Haijaalikwa..... Ujumbe toka kwa Thread moja hapa JF iliandika.

Sijui kwanini mtu anapenda sana/ anafurahia sana mabaya mpaka kiasi cha kusambaza uongo. Tuache tabia hii haitufikishi popote pale.

Kama ni wakereketwa/wanachama wa chama fulani, nawaambia chama hicho kamwa hakitafanikiwa kushika utawala wa nchi hii. Tabia hii ilaaniwe na pande zote.

Rais Tanzania- Samia Suluhu Hasan muda huu yupo mjengoni Kasarani katika sherehe za kumuapisha Rais wa Kenya S ruto.

Amani juu yenu.

Kwani kushika madaraka nchi hii kunahitaji sifa yoyote zaidi ya mbeleko ya vyombo vya dola, na Backup ya tume ya uchaguzi?
 
Daah kwenye utambulisho sisi ni wa mwisho na katutambulisha kwa kiswahili.
 
Daah kwenye utambulisho sisi ni wa mwisho na katutambulisha kwa kiswahili.
Labda hukuona vizuri kwenye protocol ya viongozi mkubwa huja mwishoni na kutambulishwa mwishoni ni heshima kubwa unaweka lasting memory kwa watu BTW ukijiona sisimizi ndivyo itakavyokuwa kwako
 
Labda hukuona vizuri kwenye protocol ya viongozi mkubwa huja mwishoni na kutambulishwa mwishoni ni heshima kubwa unaweka lasting memory kwa watu BTW ukijiona sisimizi ndivyo itakavyokuwa kwako
Hali ni Tofauti pale alianza na Museveni.
 
Hajaalikwa, hajaalikwa, Tanzania Haijaalikwa..... Ujumbe toka kwa Thread moja hapa JF iliandika.

Sijui kwanini mtu anapenda sana/ anafurahia sana mabaya mpaka kiasi cha kusambaza uongo. Tuache tabia hii haitufikishi popote pale.

Kama ni wakereketwa/wanachama wa chama fulani, nawaambia chama hicho kamwa hakitafanikiwa kushika utawala wa nchi hii. Tabia hii ilaaniwe na pande zote.

Rais Tanzania- Samia Suluhu Hasan muda huu yupo mjengoni Kasarani katika sherehe za kumuapisha Rais wa Kenya S ruto.

Amani juu yenu.

..aliyeandika hayo unayosema ni mkereketwa wa CCM aliyekuwa anataka kujenga picha kwamba mahusiano yetu na Kenya ni mabaya baada ya Ruto kuchaguliwa.
 
Hajaalikwa, hajaalikwa, Tanzania Haijaalikwa..... Ujumbe toka kwa Thread moja hapa JF iliandika.

Sijui kwanini mtu anapenda sana/ anafurahia sana mabaya mpaka kiasi cha kusambaza uongo. Tuache tabia hii haitufikishi popote pale.

Kama ni wakereketwa/wanachama wa chama fulani, nawaambia chama hicho kamwa hakitafanikiwa kushika utawala wa nchi hii. Tabia hii ilaaniwe na pande zote.

Rais Tanzania- Samia Suluhu Hasan muda huu yupo mjengoni Kasarani katika sherehe za kumuapisha Rais wa Kenya S ruto.

Amani juu yenu.
Watu wengine wanajua ujanja ni kupinga kila kitu lakini lakini Rais Samia Suluhu anawaprove wrong kila siku kwa kuendelea kudumisha diplomasia na uhusiano
 
Mh DR William Samoi Ruto na Wakenya wengi wamemtukuza za Mungu wa Mbinguni na Bwana Yesu Kristo kwenye hii sherehe ya uapisho. Injili na nyimbo za Gospeli za kutosha .
Mungu atamuongoza Inshallah, atakua kiongozi mzuri kama Rais wetu mpendwaa Samia Suluhu Hassan
 
Kwani kushika madaraka nchi hii kunahitaji sifa yoyote zaidi ya mbeleko ya vyombo vya dola, na Backup ya tume ya uchaguzi?
Acheni maneno maneo Rais Samia Suluhu yuko vizuri na 2025 atapita bila kupingwa maana asilimia kubwa ya watanzania tunamkubali sana
 
Daah kwenye utambulisho sisi ni wa mwisho na katutambulisha kwa kiswahili.
Daah! ila wabongo bana sasa issue si ni kutambulishwa tu na tumetambulishwa bado mnataka kuleta maneno
 
Labda hukuona vizuri kwenye protocol ya viongozi mkubwa huja mwishoni na kutambulishwa mwishoni ni heshima kubwa unaweka lasting memory kwa watu BTW ukijiona sisimizi ndivyo itakavyokuwa kwako
Tatizo la wabongo kila kitu wanataka watoe kasoro issue ni kutambulishwa alietambulishwa wa kwanza wa katikati na wa mwisho wote wametambulishwa tena kamtambulisha Rais Samia Suluhu kwa heshima ya juu
 
Mungu atamuongoza Inshallah, atakua kiongozi mzuri kama Rais wetu mpendwaa Samia Suluhu Hassan

Haswa na leo Mh Rais Mama SSH kashuhudia mwenzake anavyo ongelea kwa kumanisha nini maana halisi ya kupunguza gharama za makali ya maisha kwa .wananchi. Ndio mgeni kwenye kiti cha Ursis lakini hakusubiri kupewa muongozo na muungano wa Kenya kwanza aka wanasiasa nini cha kufanya..
 
..aliyeandika hayo unayosema ni mkereketwa wa CCM aliyekuwa anataka kujenga picha kwamba mahusiano yetu na Kenya ni mabaya baada ya Ruto kuchaguliwa.
Rais Samia Suluhu anaendelea kuboresha mahusiano na majirani yetu kila siku wanaosema maneno hayo ni wapotoshaji na Rais Samia Suluhu amepewa nafasi ya pekee kabisa ametambulishwa kwa heshima kubwa
 
Haswa na leo Mh Rais Mama SSH kashuhudia mwenzake anavyo ongelea kwa kumanisha nini masna halisi ya kupunguza gharama za maisha kwa .wananchi. Ndio mgeni kwenyekiti lakini hakusubiri kupewa muongo'o na muungano wa Kenya kwanza aka wsnasiasa.
Rais Samia Suluhu kama ulifatilia jana alisema atapunguza kodi na Tozo ili wafanyabiashara wafanye biashara zao vizuri zaidi lengo ni kuinua watanzania na sio kuwadidimiza
 
Back
Top Bottom