Rais Samia kuingia na mlinzi wa kiume msikitini, ni jambo la kawaida. Tuache Mihemko isiyo na Tija

Unasema yote hayo kwa manufaa ya nani?
Kama kulikua na tishio la kiusalama kwanini aende?
Hakuna haja ya kutafuta maelezo lukuki. Hata hao walioratibu wamemkosea maana kama ukimvisha mwanaume nguo za kike na watu wakajua sio mwanamke huo mpango umekua butu.
Wamefanya makosa makubwa. Wafanye toba ya kweli kabla ya hasira ya Mungu. Wametenda jambo la tofauti hadharani. WATUBU
 
Sijielewi Kivipi mkuu...

Huo mskiti una umuhimu gani mbele ya kiongozi wa nchi??


Rais anatakiwa alindwe kwa kutumia mbinu zozote zile.
Kwani yeye ndie imamu wa huo msikiti? Kama Kuna tishio la usalama siangeacha kwenda?
Mbona mnaleta siasa kwenye dini? Mbona polis wanawakataza viongozi wengine kufanya mikutano kwa kigezo cha usalama?
 
Naamini walinzi wa kike wapo ambao ingefaa kuingia nao hapo au labda kama wanataka kusema wale walinzi wake wa kike hawana uwezo wa kumlinda raisi wetu.
Kwanini wanahangaika na walinzi misikitini? Tena wanawake? Siaswalie nyumbani kisha mambo yamajukwaani ndio aende na hao walinzi?
 
Kwani yeye ndie imamu wa huo msikiti? Kama Kuna tishio la usalama siangeacha kwenda?
Mbona mnaleta siasa kwenye dini? Mbona polis wanawakataza viongozi wengine kufanya mikutano kwa kigezo cha usalama?
. Tishio la usalama kwa kiongozi wa juu lipo mda wowote, siyo siku moja tu.

. Kazi ya police ni kulinda raia wao.,
 
😀😀, MUNGU yupi huyo??..

Ebu niambie niwapi mungu alisema binadamu akifanya hivyo, ataadhibiwa vikali..??
 
Ni wakati sasa ikulu zetu ziwe na nyumba za kuabudia. La sivyo haya mambo yataendelea kujirudia
Siasa ni dini, na dini siyo siasa.... Kwa Rais kwa namna yeyote ile atashiriki tu kwenye nyumba za ibada..
 
Jasusi la kitanzania la gundulika likimlinda mh rais msikitini kwa kamera za tecno. Wakati majasusi wa kule duniani wao hata scaner zinapatashida kuwagundua. Teh teh ten .
😬😬😬😬😬
 
Unaposema kawaida inalinganisha na wapi au nan

Pia watu hawashangai mwanaume kuingia msikitini ishi kwanini wamkikishe ? Ilihari wadada tunao wazur kiulinzi
. Ni kawaida kwa sehem tulipo kwa sasa..

. Hao wa Dada wazuri siku ya jana hawakufaa kulingana na eneo.. Ndo maana wakaamua kuweka njemba..
 
Kwahiyo sio nyumba ya Mungu tena? Mpaka ajenge Mungu physical ndio inakuwa ya Mungu?
Ndio, ule unaitwa mskiti watu wanakusanyika kuomba/kuabudu mungu asiye onekana ( nadharia)
 
Naamini walinzi wa kike wapo ambao ingefaa kuingia nao hapo au labda kama wanataka kusema wale walinzi wake wa kike hawana uwezo wa kumlinda raisi wetu.
Inawezekana nayo pia au isiwezekane... Maana masuala ya usalama hayasimamiwi na mtu mmoja.. Hivyo waliona kuna umuhimu wa kuingia na mlinzi wa kiume mskitini.
 
Huyo mlinzi naye alizingua. Angejifunika completely akaacha macho tu nje nani angemtambua? Mlinzi wa Rais anashindwa kujiongeza? Mara marehemu kateuliwa, mara fukuzafukuza ikulu, mara mlinzi kwa wanawake yaani ni fujo tu.
 
Hizi comments kuna swali na jibu hap.. 😐😐
 
Reactions: Tsh
Huyo mlinzi naye alizingua. Angejifunika completely akaacha macho tu nje nani angemtambua? Mlinzi wa Rais anashindwa kujiongeza? Mara marehemu kateuliwa, mara fukuzafukuza ikulu, mara mlinzi kwa wanawake yaani ni fujo tu.
Sidhani kama walikuwa hawalijui hili... Hiyo ilikuwa ni attention tu hapo kwa mskiti..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…