Rais Samia, kuna Fursa ipo kwetu kwenye Uchumi wa Gesi, ichangamkie haraka

Rais Samia, kuna Fursa ipo kwetu kwenye Uchumi wa Gesi, ichangamkie haraka

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Nakusalimu tena kwa Jina la Jamhuri ya Muungano Tanzania Mama yangu!

Ni nadra sana Mimi Lord Denning kuandika nyuzi mbili humu ndani Ila leo imebidi nikuandikie humu maana nimegundua kuwa wewe ni mwanachama na mpenzi wa hili jukwaa! Nimeandika ushauri wangu kwako juu ya reformation ninayopendekeza Uifanye hasa kwenye ukusanyaji wa kodi (TRA) na sasa naandika hili kuhusu jambo ninaloliona linakuja hivi punde kuwa kama fursa kubwa ya kiuchumi kwa Tanzania.

Leo vyombo vya Habari vya kimataifa, vimetangaza kuhusu Kampuni kubwa ya ufaransa, Total , kusitisha shughuli zake msumbiji kutokana na sababu za kiusalama.

Kwanza kabisa napenda kukiri kuwa hali ya kiusalama msumbiji sio ya kufurahia hata kidogo, Nawapa polee ndugu zetu wale.
Kilichonilazimu kukuandikia humu huu ushauri ni fursa niliyoiona kuwa inakuja Tanzania kutokana na hali ya usalama kule msumbiji.

Ni ukweli usio na shaka kuwa Tanzania na Msumbiji ndo future ya Africa Kwa miaka mingi ijayo kutokana na hazina kubwa ya gesi. Uchumi wa gesi, pamoja na changamoto zote ni uchumi unaotegemewa sana na dunia kwa sababu gesi ni bidhaa adhimu kwa Tanzania, Hivyo kwa yanayoendelea Msumbiji hasa changamoto za kiusalama, ni dhahili kuwa makampuni makubwa ya mafuta, sasa yanaenda kuhamisha interest zao za uwekezaji kuja Tanzania.

kutokana na fursa Hii niliyoiona, napendekeza haya yafanyike kwa haraka ili Tanzania tuikamate hii fursa vizuri na kuitumia vizuri kiuchumi kwa faida ya Taifa letu.

1. Ingawa kiulinzi na kiusalama tuko vizuri na ushahidi wake ni kuwa wale wanaosumbua Msumbiji ni watu ambao vikosi vyetu vya ulinzi na Usalama vilifanikiwa kuwaondoa Tanzania napendekeza ili kuzidi kuimarisha confidence ya hawa wawekezaji kuja kuwekeza kwetu na kuimarisha uchumi na maendeleo ya Taifa letu, Boresha zaidi jeshi letu la wananchi (JWTZ) hasa kizana, kimafunzo na kiteknolojia ili liweze kujiimarisha kiulinzi na kukabiliana vizuri na tishio katika ukanda ule na kuleta confidence kwa hawa wawekezaji walete mitaji yao na pesa zao hapa nchini. Kwenye hili naomba boresha zaidi Navy Kwa kununua meli na boti kubwa za kivita huku ukiimarisha vikosi vingine kama jeshi la anga na la ardhini pia. Nimesema naamini majeshi yetu yako vizuri ila kwa mustakabali wa kukamata huu uchumi wa gesi kwa Africa hii, naomba viimarishe vikosi vyetu kwenye kila nyanja ili tuwe vizuri zaidi na kuondokana na matishio yote.

2. Naomba Kupitia timu zenu za mazungumzo ya mikataba mbalimbali, muweke nguvu kwenye kuweka sawa mikataba ya LNG na uwekezaji mwingine wa Gesi katika ukanda wa LINDI na Mtwara. Nina uhakika wawekezaji waliowekeza msumbiji watakuwa comfortable zaidi kuja kuwekeza Tanzania Kwa sababu haitawagharimu sana kuhamisha mitambo yao na teknolojia yao kutoka pwani ya msumbiji kuja Pwani ya Tanzania kutokana na ukaribu, Hivyo naomba kuanzia sasa serikali yako ianze lobbying kuyaita haya makampuni kuja mezani na kuzungumza kuhusu kuhamishia mitaji yao na uwekezaji wao Tanzania katika terms ambazo zitatufavor sisi na kutengeneza mapato makubwa kwa Taifa letu na ajira.

Naomba kuwasilisha!

SOMA PIA: Mashambulizi yapelekea Total kusitisha shughuli Msumbiji
 
Nitajie ni nchi gani Afrika ilishanufaika na ikapata maendeleo kwa sababu ina raslimali! Sana sana naona raslimali zinaleta janga la vita! Unajua Total wamewekeza nini Nigeria? Je wanaigeria unaona wananufaika sana?
 
Nitajie ni nchi gani Afrika ilishanufaika na ikapata maendeleo kwa sababu ina raslimali! Sana sana naona raslimali zinaleta janga la vita! Unajua Total wamewekeza nini Nigeria? Je wanaigeria unaona wananufaika sana?
Shida ni aina ya viongozi wa Kiafrica ambao wanachukulia kama maliasili ni sehemu ya wao kunufaika binafsi na familia zao. Makampuni ya kigeni hawana shida wao wanachotaka ni uwekezaji mzuri ulio salama na kupata faida.

Kama Tanzania tukitumia hii fursa vizuri kwa sasa, tunaweza kuwa casestudy Nzuri kwa nchi zingine za Africa.
 
Nitajie ni nchi gani Afrika ilishanufaika na ikapata maendeleo kwa sababu ina raslimali! Sana sana naona raslimali zinaleta janga la vita! Unajua Total wamewekeza nini Nigeria? Je wanaigeria unaona wananufaika sana?
Ngojea na Uganda huyo Mzee akishakata Roho Vita vitakavyolipuka hapo sio vya mchezo.

Kila mmoja atataka anyonye Mazutu ya Hoima.
 
Ngojea na Uganda huyo Mzee akishakata Roho Vita vitakavyolipuka hapo sio vya mchezo

Kila mmoja atataka anyonye Mazutu ya Hoima
Amani, Ulinzi na Usalama vilivyopo Tanzania ni kete muhimu sana katika kuleta uwekezaji mkubwa hapa Tanzania utakaolinufaisha taifa katika sehemu kubwa sana kiuchumi na kimaendeleo. Kikubwa tusisite kufanya maamuzi hasa katika kutumia fursa zilizo mbele yetu!
 
Shida ni aina ya viongozi wa Kiafrica ambao wanachukulia kama maliasili ni sehemu ya wao kunufaika binafsi na familia zao. Makampuni ya kigeni hawana shida wao wanachotaka ni uwekezaji mzuri ulio salama na kupata faida.

Kama Tanzania tukitumia hii fursa vizuri kwa sasa, tunaweza kuwa casestudy Nzuri kwa nchi zingine za Africa.
Na nina uhakika hatuwezi. Vidogo vimetushinda ni hayo makubwa? Kama tumeshindwa kunufaika na dhahabu ambayo usimamizi wake ni rahisi itakuja kuwa hivyo vimiminika?
 
Ushauri mzuri, muhimu kwenye mikataba ndio tuwekwe wazi isifichwe, hao jamaa wa TOTAL kama watakuja watafanya mengi kwa serikali yetu ikiwemo kulipa kodi lakini hata kwa watanzania naamini watatoa ajira na kuongeza mzunguko wa pesa.

Lakini tatizo la viongozi wetu waliopita ni kutokuwa waaminifu wanaposaini hiyo mikataba, wamekuwa wanafanya hivyo kwa kuangalia maslahi yao binafsi zaidi ya watanzania kwa ujumla kitu ambacho sio sahihi.

Hapa ningeshauri tu kwasababu nia ya kurudisha imani ya wawekezaji tunayo, basi tuanze safari mpya sasa, serikali ya Samia itengeneze njia ambayo itakuwa somo kwa viongozi wengine wajao kwa kuweka siri terms za kwenye hiyo mikataba wananchi waione, kwasababu hizo resources ni mali ya watanzania, sio viongozi wa serikalini.
 
Mie napendekeza tuichukue pia sehemu ya msumbiji iwe kwetu.
Duh! Ushauri wako mgumu. Ingawa naona kama nao msumbiji wamepashindwa pale. In the future hali ikiendelea kuwa vile tutawaomba watuuzie kama US alivyonunua Alaska kutoka Kwa Alaska
 
Ushauri mzuri, muhimu kwenye mikataba ndio tuwekwe wazi isifichwe, hao jamaa wa TOTAL kama watakuja watafanya mengi kwa serikali yetu ikiwemo kulipa kodi lakini hata kwa watanzania naamini watatoa ajira na kuongeza mzunguko wa pesa.

Lakini tatizo la viongozi wetu waliopita ni kutokuwa waaminifu wanaposaini hiyo mikataba, wamekuwa wanafanya hivyo kwa kuangalia maslahi yao binafsi zaidi ya watanzania kwa ujumla kitu ambacho sio sahihi.

Hapa ningeshauri tu kwasababu nia ya kurudisha imani ya wawekezaji tunayo, basi tuanze safari mpya sasa, serikali ya Samia itengeneze njia ambayo itakuwa somo kwa viongozi wengine wajao kwa kuweka siri terms za kwenye hiyo mikataba wananchi waione, kwasababu hizo resources ni mali ya watanzania, sio viongozi wa serikalini.
Nakubaliana na wewe hasa kwenye hiyo sehemu ya mwisho. Samia ana nafasi ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kipekee sana , kimaendeleo na kimfumo.

Afanye tu maamuzi!
 
Nitajie ni nchi gani Afrika ilishanufaika na ikapata maendeleo kwa sababu ina raslimali! Sana sana naona raslimali zinaleta janga la vita! Unajua Total wamewekeza nini Nigeria? Je wanaigeria unaona wananufaika sana?
Sasa matatizo na ubinafsi wetu sisi ndio tuwalaumu wao?mbona BOTSWANA, waliweza kufaidika na madini?tatizo kubwa ni viongozi wetu , mbona GADAFI, alifanikiwa ?kwahiyo unadhania hizo rasilimali zikiendelea kuwa huko zilipo ndio utafaidika?hata haya maendeleo tuliyofikia asilimia 90, ni kutokana na hizo rasilimali licha ya kuibiwa!!tuna nini zaidi ya kutuingizia pesa tofauti na hizo?
Chanzo cha migogoro ya Afrika, kiasi kikubwa ni waafrika wenyewe,
 
Nakusalimu tena kwa Jina la Jamhuri ya Muungano Tanzania Mama yangu!

Ni nadra sana Mimi Lord Denning kuandika nyuzi mbili humu ndani Ila leo imebidi nikuandikie humu maana nimegundua kuwa wewe ni mwanachama na mpenzi wa hili jukwaa! Nimeandika ushauri wangu kwako juu ya reformation ninayopendekeza Uifanye hasa kwenye ukusanyaji wa kodi (TRA) na sasa naandika hili kuhusu jambo ninaloliona linakuja hivi punde kuwa kama fursa kubwa ya kiuchumi kwa Tanzania.

Leo vyombo vya Habari vya kimataifa, vimetangaza kuhusu Kampuni kubwa ya ufaransa, Total , kusitisha shughuli zake msumbiji kutokana na sababu za kiusalama.

Kwanza kabisa napenda kukiri kuwa hali ya kiusalama msumbiji sio ya kufurahia hata kidogo, Nawapa polee ndugu zetu wale.
Kilichonilazimu kukuandikia humu huu ushauri ni fursa niliyoiona kuwa inakuja Tanzania kutokana na hali ya usalama kule msumbiji.

Ni ukweli usio na shaka kuwa Tanzania na Msumbiji ndo future ya Africa Kwa miaka mingi ijayo kutokana na hazina kubwa ya gesi. Uchumi wa gesi, pamoja na changamoto zote ni uchumi unaotegemewa sana na dunia kwa sababu gesi ni bidhaa adhimu kwa Tanzania, Hivyo kwa yanayoendelea Msumbiji hasa changamoto za kiusalama, ni dhahili kuwa makampuni makubwa ya mafuta, sasa yanaenda kuhamisha interest zao za uwekezaji kuja Tanzania.

kutokana na fursa Hii niliyoiona, napendekeza haya yafanyike kwa haraka ili Tanzania tuikamate hii fursa vizuri na kuitumia vizuri kiuchumi kwa faida ya Taifa letu.

1. Ingawa kiulinzi na kiusalama tuko vizuri na ushahidi wake ni kuwa wale wanaoaumbua Msumbiji ni watu ambao vikosi vyetu vya ulinzi na Usalama vilifanikiwa kuwaondoa Tanzania napendekeza ili kuzidi kuimarisha confidence ya hawa wawekezaji kuja kuwekeza kwetu na kuimarisha uchumi na maendeleo ya Taifa letu, Boresha zaidi jeshi letu la wananchi (JWTZ) hasa kizana, kimafunzo na kiteknolojia ili liweze kujiimarisha kiulinzi na kukabiliana vizuri na tishio katika ukanda ule na kuleta confidence kwa hawa wawekezaji walete mitaji yao na pesa zao hapa nchini. Kwenye hili naomba boresha zaidi Navy Kwa kununua meli na boti kubwa za kivita huku ukiimarisha vikosi vingine kama jeshi la anga na la ardhini pia. Nimesema naamini majeshi yetu yako vizuri ila kwa mustakabali wa kukamata huu uchumi wa gesi kwa Africa hii, naomba viimarishe vikosi vyetu kwenye kila nyanja ili tuwe vizuri zaidi na kuondokana na matishio yote.

2. Naomba Kupitia timu zenu za mazungumzo ya mikataba mbalimbali, muweke nguvu kwenye kuweka sawa mikataba ya LNG na uwekezaji mwingine wa Gesi katika ukanda wa LINDI na Mtwara. Nina uhakika wawekezaji waliowekeza msumbiji watakuwa comfortable zaidi kuja kuwekeza Tanzania Kwa sababu haitawagharimu sana kuhamisha mitambo yao na teknolojia yao kutoka pwani ya msumbiji kuja Pwani ya Tanzania kutokana na ukaribu, Hivyo naomba kuanzia sasa serikali yako ianze lobbying kuyaita haya makampuni kuja mezani na kuzungumza kuhusu kuhamishia mitaji yao na uwekezaji wao Tanzania katika terms ambazo zitatufavor sisi na kutengeneza mapato makubwa kwa Taifa letu na ajira.

Naomba kuwasilisha!

SOMA PIA: Mashambulizi yapelekea Total kusitisha shughuli Msumbiji

Wewe unadhani vitalu vya Gesi huko kusini bado havijauzwa? Kikwete alisaini mikataba na WACHINA under certificate of urgency siku za mwisho wa utawala wake. Hujui Mwendazake ndio maana akakasilika kuona walimaliza vitalu akaona na yeye aanzishe mradi wake wa Stiegler's !!
 
Kwa Tanzania tuna nafasi ya kuweka mifumo imara badala ya watu imara. Tuko sehemu nzuri kuelekea kunufaika . Kikubwa tutumie hii fursa na kufanya maamuzi bila kusita
Tena hao TOTAL, kabla ya kwenda Msumbiji walianzia hapa, vikwazo vikawa vingi mno kama kawaida yetu!!ndio maana juzi mama Samia alitoa maagizo huo mchakato wa LNG, inabidi serikali ifikie uamuzi liishe!!!na tatizo letu wanasiasa ndio huwa wanajifanya kuwa mbele zaidi kuliko wataalam, kutokana na wataalam wengi kutoaminika!!
 
Sasa matatizo na ubinafsi wetu sisi ndio tuwalaumu wao?mbona BOTSWANA, waliweza kufaidika na madini?tatizo kubwa ni viongozi wetu , mbona GADAFI, alifanikiwa ?kwahiyo unadhania hizo rasilimali zikiendelea kuwa huko zilipo ndio utafaidika?hata haya maendeleo tuliyofikia asilimia 90, ni kutokana na hizo rasilimali licha ya kuibiwa!!tuna nini zaidi ya kutuingizia pesa tofauti na hizo?
Chanzo cha migogoro ya Afrika, kiasi kikubwa ni waafrika wenyewe,
Sijakuelewa maana sijasema tumlamu mtu yoyote. Nimejaribu kuonyesha uzembe ni wetu.
 
Nakusalimu tena kwa Jina la Jamhuri ya Muungano Tanzania Mama yangu!

Ni nadra sana Mimi Lord Denning kuandika nyuzi mbili humu ndani Ila leo imebidi nikuandikie humu maana nimegundua kuwa wewe ni mwanachama na mpenzi wa hili jukwaa! Nimeandika ushauri wangu kwako juu ya reformation ninayopendekeza Uifanye hasa kwenye ukusanyaji wa kodi (TRA) na sasa naandika hili kuhusu jambo ninaloliona linakuja hivi punde kuwa kama fursa kubwa ya kiuchumi kwa Tanzania.

Leo vyombo vya Habari vya kimataifa, vimetangaza kuhusu Kampuni kubwa ya ufaransa, Total , kusitisha shughuli zake msumbiji kutokana na sababu za kiusalama.

Kwanza kabisa napenda kukiri kuwa hali ya kiusalama msumbiji sio ya kufurahia hata kidogo, Nawapa polee ndugu zetu wale.
Kilichonilazimu kukuandikia humu huu ushauri ni fursa niliyoiona kuwa inakuja Tanzania kutokana na hali ya usalama kule msumbiji.

Ni ukweli usio na shaka kuwa Tanzania na Msumbiji ndo future ya Africa Kwa miaka mingi ijayo kutokana na hazina kubwa ya gesi. Uchumi wa gesi, pamoja na changamoto zote ni uchumi unaotegemewa sana na dunia kwa sababu gesi ni bidhaa adhimu kwa Tanzania, Hivyo kwa yanayoendelea Msumbiji hasa changamoto za kiusalama, ni dhahili kuwa makampuni makubwa ya mafuta, sasa yanaenda kuhamisha interest zao za uwekezaji kuja Tanzania.

kutokana na fursa Hii niliyoiona, napendekeza haya yafanyike kwa haraka ili Tanzania tuikamate hii fursa vizuri na kuitumia vizuri kiuchumi kwa faida ya Taifa letu.

1. Ingawa kiulinzi na kiusalama tuko vizuri na ushahidi wake ni kuwa wale wanaoaumbua Msumbiji ni watu ambao vikosi vyetu vya ulinzi na Usalama vilifanikiwa kuwaondoa Tanzania napendekeza ili kuzidi kuimarisha confidence ya hawa wawekezaji kuja kuwekeza kwetu na kuimarisha uchumi na maendeleo ya Taifa letu, Boresha zaidi jeshi letu la wananchi (JWTZ) hasa kizana, kimafunzo na kiteknolojia ili liweze kujiimarisha kiulinzi na kukabiliana vizuri na tishio katika ukanda ule na kuleta confidence kwa hawa wawekezaji walete mitaji yao na pesa zao hapa nchini. Kwenye hili naomba boresha zaidi Navy Kwa kununua meli na boti kubwa za kivita huku ukiimarisha vikosi vingine kama jeshi la anga na la ardhini pia. Nimesema naamini majeshi yetu yako vizuri ila kwa mustakabali wa kukamata huu uchumi wa gesi kwa Africa hii, naomba viimarishe vikosi vyetu kwenye kila nyanja ili tuwe vizuri zaidi na kuondokana na matishio yote.

2. Naomba Kupitia timu zenu za mazungumzo ya mikataba mbalimbali, muweke nguvu kwenye kuweka sawa mikataba ya LNG na uwekezaji mwingine wa Gesi katika ukanda wa LINDI na Mtwara. Nina uhakika wawekezaji waliowekeza msumbiji watakuwa comfortable zaidi kuja kuwekeza Tanzania Kwa sababu haitawagharimu sana kuhamisha mitambo yao na teknolojia yao kutoka pwani ya msumbiji kuja Pwani ya Tanzania kutokana na ukaribu, Hivyo naomba kuanzia sasa serikali yako ianze lobbying kuyaita haya makampuni kuja mezani na kuzungumza kuhusu kuhamishia mitaji yao na uwekezaji wao Tanzania katika terms ambazo zitatufavor sisi na kutengeneza mapato makubwa kwa Taifa letu na ajira.

Naomba kuwasilisha!

SOMA PIA: Mashambulizi yapelekea Total kusitisha shughuli Msumbiji
Hayo yote mpaka sasa yanaendelea kufanyika, lakini ama kwa nia njema au ovu umeamua kukimbilia hapa ili uonekane umeibua jambo la maana kumbe lilishaanza kufanyika tangu Januari 2021
 
Tena hao TOTAL, kabla ya kwenda Msumbiji walianzia hapa, vikwazo vikawa vingi mno kama kawaida yetu!!ndio maana juzi mama Samia alitoa maagizo huo mchakato wa LNG, inabidi serikali ifikie uamuzi liishe!!!na tatizo letu wanasiasa ndio huwa wanajifanya kuwa mbele zaidi kuliko wataalam, kutokana na wataalam wengi kutoaminika!!
Kwakweli katika kipindi cha Magu sikuwa na shakha nae kwenye suala la usimamizi wa rasilimali, naamini total hakushindwa kisa aliwekewa vikwazo lakini kuhusu taifa linanufaika vipi...!!! Hapa ulikuwa ukitaka kugombana na Magu usicheze karata yako vizuri.

Habari za kumwaminisha Magu eti tukioata faida baada ya miaka 30 ndo tutatoa ilo kwake lilikuwa hapana.
 
Hayo yote mpaka sasa yanaendelea kufanyika, lakini ama kwa nia njema au ovu umeamua kukimbilia hapa ili uonekane umeibua jambo la maana kumbe lilishaanza kufanyika tangu Januari 2021
Kwa iyo kumbe una shida na mie na sio hoja zangu??? Utasubiri sana mzee. Hatushindani, kikubwa ni kulisaidia Taifa na huu ndo uzalendo. Sio nyie kumuabudu na kumsifia magufuli ndo mlijua uzalendo
 
Kwakweli katika kipindi cha Magu sikuwa na shakha nae kwenye suala la usimamizi wa rasilimali, naamini total hakushindwa kisa aliwekewa vikwazo lakini kuhusu taifa linanufaika vipi...!!! Hapa ulikuwa ukitaka kugombana na Magu usicheze karata yako vizuri.

Habari za kumwaminisha Magu eti tukioata faida baada ya miaka 30 ndo tutatoa ilo kwake lilikuwa hapana.
Hoja sio Magufuli. Hoja ni kutumia fursa iliyopo kuleta uwekezaji mkubwa Tanzania
 
Back
Top Bottom