Rais Samia kupokea Gawio na Michango kutoka Mashirika na Taasisi za Umma, Matukio kurushwa live kupitia vyombo vyote vya habari

Hujaziona Reforms?

Unamfahamu Kitila Mkumbo? Hivi yupo wizara ipi vile?
Anaelewa vyema ila anajifanya ni kipofu wa akili na macho. Kila mtanzania mwenye akili Timamu anafahamu Mageuzi makubwa yaliyofanyika katika kuleta ufanisi wa utendaji kazi wa mashirika na taasisi mbalimbali za Umma,hususani usimamizi na sera bora.
 
Kwa busara mashirika yangekaguliwa kwanza na CAG ndipo idhini ya gawio itoke ili kujiridhisha kwamba mashirika hayajakopa ili kumridhisha rais kwa kumpa gawio feki nayeye kuchekelea na kusifu WAHUNI hao!!
Hii nchi wengi tukiwa timamu tukaacha upambe wakipumbafu tutasogea LAKINI kwa uzwazwa wakusifu hovyo WAHUNI watalitafuna taifa na watoto wetu tutawarithisha misiba tuu kwasababu ya wajinga wasifio tuuu kilakukicha!!!
 
Mkono na jicho la serikali lipo kila eneo ikiwepo hapo ulipo wewe.
 
Mkono na jicho la serikali lipo kila eneo ikiwepo hapo ulipo wewe.
Ficha ujinga wako wewe,kunawatu wamefilisi NHIF,PSSF Kwa kuiba kizeembe mpaka mifuko hiyo kufikia kufeli kizembe,huko tanapa zinachotwa mpaka aibu,tanesco inapigwa michezo hata wabibi vijijini wanajua lkn serikali na takukuru haijui,halmashauri ndiyo usiseme mpaka aibu!!
Acha kutetea upuuzi kijana watu tumechoshwa na huu uvundo ila hatuwezi kuzuia kwasababu ya system za hovyo tulizonazo
 
Bado anaiga propaganda za dhalimu magu?!
 
Wananchi wabubujikwa na machozi!
 
RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ATAPOKEA GAWIO NA MICHANGO KUTOKA MASHIRIKA NA TAASISI ZA UMMA


 
Hakuna anayebakia salama wala kuonewa huruma pale atakapobainika kufuja pesa za Umma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…