Rais Samia kuwa kama Hayati Magufuli, achana na maridhiano na wasiotaka, watakupotezea muda

Rais Samia kuwa kama Hayati Magufuli, achana na maridhiano na wasiotaka, watakupotezea muda

Mimi ni katika MODERATES....

Ninaamini katika siasa za kiasi....kukosoa na KUKOSOANA kwa STAHA......

Kinyume na siasa za staha siamini kutumia njia za STAHA kuwaendea wasiotaka STAHA.....

Post hii ina MADINI ADHIMU kabisa[emoji120][emoji120]

Kudos mtoa hoja[emoji106]

#SiempreJMT[emoji120]

#Punda Afe JMT Ibaki Tulivu Na Salama amen[emoji120]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Nikikumbuka tulikotoka, Samia alivyorekebisha mambo mengi halafu sasa hivi mijitu inatukana familia yake, inamdhalilisha kijinsia, inambagua asili yake, hata dini yake,. Naona hawa watu haina haja ya kuwa muungwana kwao, usiwape uhuru, hawapo responsible katika kutumia huko uhuru
 
Nadhani tunahitaji kujadili siasa za nchi yetu kwa uhalisia zaidi kuliko kwa kujipa moyo au kwa wishful thinking

Uhalisia upo hivi, Rais Samia Suluhu ndio Rais ambaye amejaribu kuwa fair zaidi kwa Chadema kuliko Rais yeyote, na sidhani kama atatokea Rais mwingine akawa fair kwao kama Samia.

Chadema kwa miaka zaidi ya 5 walikuwa treated kama 'kikundi cha waasi ama wahalifu, na haki zao nyingi kuporwa na hakuna walichoweza kufanya zaidi ya kukimbia nchi na kuomba msaada kwa wazungu.

Walimtishia sana Rais Magufuli kwa maandamano na migomo, Magufuli akawatilia ngumu mwanzo mpaka mwisho, walipoona huyu mtu hatishiki wakaona waombe kukutana naye, hata hivyo Magufuli akawapuuza na kuwaweka ndani, na kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na Uchaguzi mkuu wote mnajua kilichofanyika.

Chadema pamoja na vitisho vyote hawakuweza kufanya kitu zaidi ya kukimbilia nje ya nchi, Rais Samia alipoingia kitu cha kwanza kufanya ni waliomba wakutane naye, Rais Samia kwa ubinadamu wake akawakubalia kwa sababu ni watanzania wenzetu, waliokimbilia nje akawaruhusu warudi nyumbani na kuwahakikishia usalama.

Pia akawaruhusu kufanya mikutano waliyokuwa wamezuiwa kuifanya kwa miaka mitano, sasa katika CCM, kama vyama vingi duniani, kuna makundi mawili, kuna kundi la hardliners na kundi lingine la moderates

Hili kundi la moderates, ni lile kundi linaloamini kuwa CCM ni chama ambacho kinafaa kukosolewa na vyama vya upinzani, na vyama vya upinzani vinatakiwa kupewa nafasi ya kuikosoa CCM na kupewa nafasi katika uwanja wa kisiasa

Hili kundi la Hardliners ni lile kundi linaloamini CCM ni chama kinachotakiwa kutumia nguvu zozote kukandamiza upinzani, na upinzani hawapaswi kupewa upenyo kabisa wa kuitikisa CCM.

Hili kundi ndio kubwa ndani ya CCM na ndio lililokuwa linashika hatamu katika awamu ya 5

Samia alipokutana na Wapinzani na hata kuwapa nafasi ya kufanya mikutano, alikutana na upinzani mwingi kutoka katika kundi hili, lakini kwa kuwa anaamini wapinzani wana mchango pia katika siasa za nchi hii, alienda against nao na kuwapa upinzani haki nyingi ambazo walikuwa hawana kabla ya Samia kuingia.

Sasa wanachokifanya Chadema, kutumia lugha ambazo ni very provocative kwenye mikutano yao, kususia vikao vyenye kujenga utaifa, nao wanakua ni hardliners, au misimamo mikali, na wanawa prove right au kuwa 'vindicate' lile kundi la hardliners ndani ya CCM ambalo lilikuwa linamtahadharisha Samia kuwa asiwape upenyo wapinzani maana atakuja kujutia.

Sasa kitakachoweza kutokea ni either Samia ataendelea kuwa mvumilivu au atawasikiliza hardliners wa CCM

Akiwasikiliza hardiliners ni kuwa tunarudi kwenye Magufulism 2.0

Je, Chadema wataweza kukabiliana na wahafidhina wa CCM?


Kwa akili yako anayafanya sababu kaamua kufanya maridhiano na hayana faida kwake!!!!!! Za kuvuka barabara hizi.
 
Nyie matapeli kama mlishindwa kuitoa CCM pamoja na kumchukua yule fisadi 2015, hamtakaa muitoe tena, maana watanzania ndio waliona sura zenu halisi
Kwa taarifa yako kwa mazingira haya ya uchaguzi, ccm itaendelea kutangazwa washindi na sio kushinda. Lakini mazingira yakibadilika aidha kwa machafuko ama mapinduzi ya kijeshi uje utoe mrejesho. Hakuna wananchi wanaoamua nani awe rais nchi hii, bali kigenge kinachojiita system ndio huamua nani awe rais, bila kujali box la kura linasemaje. Sasa sijui ni wananchi gani unawaongelea.
 
Kwa taarifa yako kwa mazingira haya ya uchaguzi, ccm itaendelea kutangazwa washindi na sio kushinda. Lakini mazingira yakibadilika aidha kwa machafuko ama mapinduzi ya kijeshi uje utoe mrejesho. Hakuna wananchi wanaoamua nani awe rais nchi hii, bali kigenge kinachojiita system ndio huamua nani awe rais, bila kujali box la kura linasemaje. Sasa sijui ni wananchi gani unawaongelea.
Vyovyote vile, ni afadhali kutawaliwa na CCM, shetani ninayemjua kuliko Chadema, ambayo hata sasa kabla ya kuwa na madaraka wanaonyesha ni wabaya mara 100 kuliko CCM, wakiwa na madaraka sijui itakuwaje
 
Vyovyote vile, ni afadhali kutawaliwa na CCM, shetani ninayemjua kuliko Chadema, ambayo hata sasa kabla ya kuwa na madaraka wanaonyesha ni wabaya mara 100 kuliko CCM, wakiwa na madaraka sijui itakuwaje
Mabadiliko hayakwepeki boss, ndio maana unaona wizi WA kura umebaki kuwa ngao ya CCM kubaki madarakani kwa shuruti. CCM sio chama cha kizazi hiki. Ni sawa na kutaka kizazi hiki kisikilize miziki ya Sikinde na Ottu jazz, badala ya miziki ya kina Ali Kiba na Diamond.
 
Si kweli kwamba Rais Samia amekuwa fair kwa CHADEMA, bali Katiba yetu ndo inayowapa uhuru CHADEMA kufanya mikutano.
 
Tanzania ni nchi huru, hakuna cha beberu wala nani atakayetutishia kwenye maamuzi yetu...Kama mikutano imejaa matusi na uchochezi inafungiwa tu, tunachapa kazi... Hatutaki kuwa kama DRC nyingine
...[emoji848] Hamuamini Mahakama mlizochagua Nyinyi Wenyewe ?? Anayeona ametukanwa SI aende Mahakamani ?? Mnaogopa ??
 
1.Maridhiano maana yake ni nini??

2. Ni kitu/jambo gani linaloridhiwa??
 
Si kweli kwamba Rais Samia amekuwa fair kwa CHADEMA, bali Katiba yetu ndo inayowapa uhuru CHADEMA kufanya mikutano.
Katiba yetu ilikuwa ni hiii hii awamu ya 5 ila walikuwa hawafanyi hiyo mikutano
 
Nadhani tunahitaji kujadili siasa za nchi yetu kwa uhalisia zaidi kuliko kwa kujipa moyo au kwa wishful thinking

Uhalisia upo hivi, Rais Samia Suluhu ndio Rais ambaye amejaribu kuwa fair zaidi kwa Chadema kuliko Rais yeyote, na sidhani kama atatokea Rais mwingine akawa fair kwao kama Samia.

Chadema kwa miaka zaidi ya 5 walikuwa treated kama 'kikundi cha waasi ama wahalifu, na haki zao nyingi kuporwa na hakuna walichoweza kufanya zaidi ya kukimbia nchi na kuomba msaada kwa wazungu.

Walimtishia sana Rais Magufuli kwa maandamano na migomo, Magufuli akawatilia ngumu mwanzo mpaka mwisho, walipoona huyu mtu hatishiki wakaona waombe kukutana naye, hata hivyo Magufuli akawapuuza na kuwaweka ndani, na kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na Uchaguzi mkuu wote mnajua kilichofanyika.

Chadema pamoja na vitisho vyote hawakuweza kufanya kitu zaidi ya kukimbilia nje ya nchi, Rais Samia alipoingia kitu cha kwanza kufanya ni waliomba wakutane naye, Rais Samia kwa ubinadamu wake akawakubalia kwa sababu ni watanzania wenzetu, waliokimbilia nje akawaruhusu warudi nyumbani na kuwahakikishia usalama.

Pia akawaruhusu kufanya mikutano waliyokuwa wamezuiwa kuifanya kwa miaka mitano, sasa katika CCM, kama vyama vingi duniani, kuna makundi mawili, kuna kundi la hardliners na kundi lingine la moderates

Hili kundi la moderates, ni lile kundi linaloamini kuwa CCM ni chama ambacho kinafaa kukosolewa na vyama vya upinzani, na vyama vya upinzani vinatakiwa kupewa nafasi ya kuikosoa CCM na kupewa nafasi katika uwanja wa kisiasa

Hili kundi la Hardliners ni lile kundi linaloamini CCM ni chama kinachotakiwa kutumia nguvu zozote kukandamiza upinzani, na upinzani hawapaswi kupewa upenyo kabisa wa kuitikisa CCM.

Hili kundi ndio kubwa ndani ya CCM na ndio lililokuwa linashika hatamu katika awamu ya 5

Samia alipokutana na Wapinzani na hata kuwapa nafasi ya kufanya mikutano, alikutana na upinzani mwingi kutoka katika kundi hili, lakini kwa kuwa anaamini wapinzani wana mchango pia katika siasa za nchi hii, alienda against nao na kuwapa upinzani haki nyingi ambazo walikuwa hawana kabla ya Samia kuingia.

Sasa wanachokifanya Chadema, kutumia lugha ambazo ni very provocative kwenye mikutano yao, kususia vikao vyenye kujenga utaifa, nao wanakua ni hardliners, au misimamo mikali, na wanawa prove right au kuwa 'vindicate' lile kundi la hardliners ndani ya CCM ambalo lilikuwa linamtahadharisha Samia kuwa asiwape upenyo wapinzani maana atakuja kujutia.

Sasa kitakachoweza kutokea ni either Samia ataendelea kuwa mvumilivu au atawasikiliza hardliners wa CCM

Akiwasikiliza hardiliners ni kuwa tunarudi kwenye Magufulism 2.0

Je, Chadema wataweza kukabiliana na wahafidhina wa CCM?
Kwa taarifa yako hata huyo Magufuli kama angeendelea mpaka leo, hayo maridhiano angeyatafuta tu.
Tanzania ni maskini sana kujitutumua eti hujali.
Ilikuwa ni suala la muda tu, mdororo wa uchumi ungemlazimisha na angesalimu amri tu.
Hakuna aliyekuwa na kiburi kama Mwalimu Nyerere, aliyethubutu kutaifisha hata makampuni ya wazungu na waliojaribu kumuingilia kwenye maamuzi aliwatimua nchini kama alivyowatimua raia wote wa iliyokuwa ujerumani ya magharibi enzi hizo miaka ya 70.
Lakini ilifika mahala aliona hawezi kuendelea na aina hiyo ya misimamo na ili asionekane amesalimu amri ilimbidi astaafu na kumuachia Mwinyi ndio akubali yale aliyoyakataa.
Kwa hiyo hakuna ubabe wa kudumu, zaidi utakaribisha kuondolewa kwa nguvu.
 
Back
Top Bottom