Rais Samia mabadiliko haya ni ya kawaida tujitahidi tuwatumikie wananchi

Rais Samia mabadiliko haya ni ya kawaida tujitahidi tuwatumikie wananchi

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewaapisha viongozi mbalimbali aliowateua jana huku akisisitiza kuwa mabadiliko hayo ni ya kawaida kwa ajili ya kuongeza ufanisi katika maeneo husika.

Rais Samia ameyasema hayo leo Alhamisi Agosti 15,2024 wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua jana, Ikulu jijini Dar es Salaam huku akiwataka kujiongeza ili kutumikia wananchi.

“Kwanza ni shukurani kwa Mungu kutujalia kukutana hapa, lakini la pili niwapongeze mlioapa hapa leo mlioaminiwa, la tatu niseme tu mabadiliko haya ni ya kawaida ni kuongezea ufanisi katika maeneo yetu na Makamu wa Rais (Dk Philip Mpango) amesema vizuri tunachotarajia ni kwenda kuongeza ufanisi kwenye maeneo yenu na la nne kiapo.”

‘Mmeapa viapo viwili hapa pale nyuma kimoja cha maadili lakini mbele mliapa maadili na kiapo kwa miungu yenu mnayoiamini au kwa dini zenu mnazoziamini muende mkaishi na viapo hivyo, lakini pia mfuate maadili ya kazi inavyotakiwa​
 
huyu mama ni makini sana wallah

ukitizama utendajikazi wake ni kama mujiza flani kwa kweli
 
Hakuna muadilifu hapo wala nini wote ni walewale tu,asichokijua mteuzi ni kwamba wenzake wameshajua mtu akiteuliwa wakati wowote atapigwa chini hivyo anahakikisha akiingia tu anaanza upigaji wa kishindo hata akikaa kwa mwezi mmoja tu unamtosha kujichumia utajiri wa maana pia wamemdharau sana.
Uwa namuangaliaga sana anapokaa pale kwenye kiti wakati akiwaapisha wateule uwa anavimba na kujaribu kutaka kuonesha ni mtu anayejiamini na kujaribu kama kutuma ujumbe kwa watu kwamba wamuogope lakini wenzake wanamchukulia tofauti na anavyotamani na anavyofikiria yeye.
Watanganyika tumepatikana😅😅
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewaapisha viongozi mbalimbali aliowateua jana huku akisisitiza kuwa mabadiliko hayo ni ya kawaida kwa ajili ya kuongeza ufanisi katika maeneo husika.

Rais Samia ameyasema hayo leo Alhamisi Agosti 15,2024 wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua jana, Ikulu jijini Dar es Salaam huku akiwataka kujiongeza ili kutumikia wananchi.

“Kwanza ni shukurani kwa Mungu kutujalia kukutana hapa, lakini la pili niwapongeze mlioapa hapa leo mlioaminiwa, la tatu niseme tu mabadiliko haya ni ya kawaida ni kuongezea ufanisi katika maeneo yetu na Makamu wa Rais (Dk Philip Mpango) amesema vizuri tunachotarajia ni kwenda kuongeza ufanisi kwenye maeneo yenu na la nne kiapo.”

‘Mmeapa viapo viwili hapa pale nyuma kimoja cha maadili lakini mbele mliapa maadili na kiapo kwa miungu yenu mnayoiamini au kwa dini zenu mnazoziamini muende mkaishi na viapo hivyo, lakini pia mfuate maadili ya kazi inavyotakiwa​

Hakuna tija yoyote ile kwenye teuzi kama hizi.
Hakuna faida yoyote ile ambayo nchi hii itapata kutokana na suala hili la Kuteua na Kutengua Mara kwa mara zaidi ya kuliangamiza Taifa kwa kufuja fedha za Kodi za Wananchi ili kugharamia teuzi hizi.

Aidha, kitendo cha Rais kufanya Uteuzi na Utenguzi wa Viongozi wa Serikali mara kwa mara kinaonyesha na kuthibitisha kwamba Rais huyo ni Dhaifu kupindukia hususani kwenye suala la kufanya Maamuzi sahihi na kwa wakati sahihi.

Hivi inawezekana vipi uwateue Watu kwenye nafasi za Uongozi halafu ndani ya kipindi kifupi kabisa Mfano ktk kipindi Cha miezi mitatu tu unatengua teuzi zao zote kabisa na kisha unawateua tena Watu wengine ambao nao pia uteuzi wao ulitengua siku chache zilizopita????? Hii inawezekanaje?????

Ina maana kabla ya kuwateua Watu hao alikuwa hajawachunguza kwa umakini ili kuona Kama wanafaa au la ????? Je, ina maana kwamba Rais amekuwa akifanya uteuzi wa Watu kwa kukurupuka bila ya kuwafanyia kwanza Vetting ya kutosha Watu hao????

Pia inaonyesha kwamba ndani ya Tiss kuna tatizo kubwa sana, hususani kwenye Kitengo Cha Kufanya Vetting za hawa Wateuliwa. Kuwepo kwa Teuzi za hovyo hovyo kama hizi ni reflection ya kuwepo kwa Watu wa hovyo hovyo ndani ya Mamlaka za Uteuzi hususani wale wanaofanya Mchakato wa Vetting za hawa Wateuliwa.
 
Kaogopa kuzungumzia madudu ya rafiki yake ummy
 
Back
Top Bottom