Rais Samia: Mahabusu wengi kesi zao ni za kubambikwa, wenye hatia wanaachwa uraiani

Rais Samia: Mahabusu wengi kesi zao ni za kubambikwa, wenye hatia wanaachwa uraiani

Hayo yote mnayajua ila mnajizima data yaani kuna Watu mpaka sasa hivi wanaamini Mahakamani ni sehemu ya kupata haki ila ukweli ni kwamba katika Watu watakaongoza gwaride la kwenda jehannam baada ya Polisi ni Mahakimu wajinga hawa...
Tatizo ni kukithiri kwa rushwa kwenye hiyo idara
 
Pale serikali inapolalamika.
Hata Mimi hapo huwa nashindwa kuelewa. Serikali imeshaona tatizo, na kulielewa - tunategemea ije na solution; sio kulalamika. Ni sawasawa na yule PM mwingine, alikuwa analia akisikia Albino ameuawa au kukatwa kiungo - wakati ana vyombo vya ulinzi viko chini yake - unaona kabisa hapa kuna tatizo kwa huyu Bwana Mkubwa, Badala ya kuwashughulikia wahalifu, Yeye analia.
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema “Tulikuwa tunaangalia magereza yetu tukabaini waliofungwa na walio mahabusu idadi yao ni kama ilikuwa sawa, wengi wao ni kesi za kubambikwa ndio maana unakuta mtu yupo ndani miaka mitatu, haendi mahakamani, haulizwi na hakuna kesi ya maana.

“Tulichofanya ni kuwatoa magereza yakapata kupumua, msipofanya haki, mnapochukua rushwa kumtia mtu hatiani ambaye hana hatia na mwenye hatia mkamuacha nje anaendeleza ubabe akiamini pesa yake itambeba, ambaye hana hela anaishia jela.

“Usiangalie Duniani, umechukua fedha sawa, imekufanya umekuwa nani, imekufikisha wapi, matatizo yako ya Dunia yameisha, ni ushawishi tu wa akili, itendeeni haki sheria.”

Amesema hayo Novemba 24, 2022 alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wanasheria wa 27 Afrika Mashariki unaofanyika Jijini Arusha.
Huyu Mama ana anza kujichanganya sasa.

Kingai alimbambikia kesi Mbowe na walinzi wake. Leo Kingai kapandishwa cheo na huhyu huyu Mama.
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, UKIZOWEA KULA NYAMA YA MTU HUTAACHA.

Hivi Mh Rais kwa mawazo yake, ana amini Kingai ata acha tabia ya kubambikia watu kesi kweli?
Unapo hitaji kumpa mtu nafasi ya kukusaidia nadhani una takiwa uwe na taarifa za utendaji wake.
Je inaweza kuwa hukujua ni Kingai gani una mpa cheo cha DPP?

Msitufanye Watanzania ni mazwazwa hatuna kimbukumbu.. Kama kuna adhabu baada ya haya maisha nyie viongozi wanafiki mtachelewa sana kufika mbinguni.
 
Huyu Mama kwa hili atabarikiwa sana!.
P
Yeye ndie Baba mwenye nyumba, baraka ana zipata wapi kama hawachukulii hatua alio wateua na wana fanya uonevu wa wazi?
Je? Kuwanyima upinzani kufanya shughuli za kisiasa ni sawa? Haoni kwamba nae hatendi haki? Katiba gani anayo tumia?
Mungu hatoi baraka kwa vile umesema, Mungu hubariki matendo mema yanayo mpendeza!!!! Period!!!
 
Tulikuwa tunaangalia magereza yetu tukabaini waliofungwa na walio mahabusu idadi yao ni kama ilikuwa sawa, wengi wao ni kesi za kubambikwa ndio maana unakuta mtu yupo ndani miaka mitatu, haendi mahakamani, haulizwi na hakuna kesi ya maana.

“Tulichofanya ni kuwatoa magereza yakapata kupumua, msipofanya haki, mnapochukua rushwa kumtia mtu hatiani ambaye hana hatia na mwenye hatia mkamuacha nje anaendeleza ubabe akiamini pesa yake itambeba, ambaye hana hela anaishia jela.[emoji2827]
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema “Tulikuwa tunaangalia magereza yetu tukabaini waliofungwa na walio mahabusu idadi yao ni kama ilikuwa sawa, wengi wao ni kesi za kubambikwa ndio maana unakuta mtu yupo ndani miaka mitatu, haendi mahakamani, haulizwi na hakuna kesi ya maana.

“Tulichofanya ni kuwatoa magereza yakapata kupumua, msipofanya haki, mnapochukua rushwa kumtia mtu hatiani ambaye hana hatia na mwenye hatia mkamuacha nje anaendeleza ubabe akiamini pesa yake itambeba, ambaye hana hela anaishia jela.

“Usiangalie Duniani, umechukua fedha sawa, imekufanya umekuwa nani, imekufikisha wapi, matatizo yako ya Dunia yameisha, ni ushawishi tu wa akili, itendeeni haki sheria.”

Amesema hayo Novemba 24, 2022 alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wanasheria wa 27 Afrika Mashariki unaofanyika Jijini Arusha.
Nchi ngumu sana hii
 
Kama hivyo ndivyo basi mifumo wa utoaji haki nchini kwetu imekufa kifo kibaya sana, sasa wewe kama Rais wetu unachukua hatua zipi za dharura kunusuru hali hii?
 
Nini maana ya kuwa kiongozi kama unakaa kuongea tu utafkiri uko kijiweni! We all know all these problems so what are you going to do about them?? Au we kazi yako ni kutukumbusha matatizo tuliyonayo kila siku! Too much talk no action! This woman should step down!
 
Baada ya kugundua huo upuuzi wa watendaji wake ni hatua gani ame wachukulia, kama hajafanya chochote basi hizo ni hadithi za shule ya msingi msingeni "mfalme ana maskio kama ya punda"
 
Maneno aliyoongea yamenyooka sana,shida ni wasimamizi,na wa kuwasimamia hao wasimamizi wa hizo sheria ndio shida kubwa...
 
Ni vigumu sana kudhania, mie kuna mda nashindwa kutofautisha kati ya yeye na rais was TAWLA. Kumbe anaongoza nchi
 
Rais Samia Suluhu Hassan amesema “Tulikuwa tunaangalia magereza yetu tukabaini waliofungwa na walio mahabusu idadi yao ni kama ilikuwa sawa, wengi wao ni kesi za kubambikwa ndio maana unakuta mtu yupo ndani miaka mitatu, haendi mahakamani, haulizwi na hakuna kesi ya maana.

“Tulichofanya ni kuwatoa magereza yakapata kupumua, msipofanya haki, mnapochukua rushwa kumtia mtu hatiani ambaye hana hatia na mwenye hatia mkamuacha nje anaendeleza ubabe akiamini pesa yake itambeba, ambaye hana hela anaishia jela.

“Usiangalie Duniani, umechukua fedha sawa, imekufanya umekuwa nani, imekufikisha wapi, matatizo yako ya Dunia yameisha, ni ushawishi tu wa akili, itendeeni haki sheria.”

Amesema hayo Novemba 24, 2022 alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wanasheria wa 27 Afrika Mashariki unaofanyika Jijini Arusha.
Huyu maza huwa kazi kubwa ni kulalamika tu hakuna hatua zozote
 
Back
Top Bottom