Rais Samia, mfute kazi Waziri wa Maliasili na Utalii, mzungu naye akamatwe na kushtakiwa kwa uhujumu uchumi

Rais Samia, mfute kazi Waziri wa Maliasili na Utalii, mzungu naye akamatwe na kushtakiwa kwa uhujumu uchumi

Mzungu huyu ameonekana akiwa na maafisa wa wanyama pori akifurahia kumuua mamba mkubwa mwenye urefu zaidi ya mita 4 ndani ya hifadhi moja wapo ya Taifa.

Huu ni uhujumu wa makusudi ambae umefadhiliwa na vyombo vya dola (maafisa wa hifadhi kwani kazi ya kumuwinda mamba mkubwa kama huyo na hatimae kumuua na kuanza kumburuta na kumfunga abebwe sio jambo la siri na clips zimeenea mitandaoni na dunia nzima.

Mzungu husika akamatwe kama ndugu zetu na jamaa wanavuokamatwa hata kwa kukutwa na vipande vya nyama tu ya kitoweo cha familia.

Waziri husika nae aachie ngazi, ikiwa watu wanafikia hadi kufanya ujangiri wa kuhujumu uchumi huku wanalindwa na vyombo vya dola na wakijitajgaza wazi wazi, je vungapi hatuoni ambavyo ni zaidi ya hivi?


Mzungu huyu ameonekana akiwa na maafisa wa wanyama pori akifurahia kumuua mamba mkubwa mwenye urefu zaidi ya mita 4 ndani ya hifadhi moja wapo ya Taifa.

Huu ni uhujumu wa makusudi ambae umefadhiliwa na vyombo vya dola (maafisa wa hifadhi kwani kazi ya kumuwinda mamba mkubwa kama huyo na hatimae kumuua na kuanza kumburuta na kumfunga abebwe sio jambo la siri na clips zimeenea mitandaoni na dunia nzima.

Mzungu husika akamatwe kama ndugu zetu na jamaa wanavuokamatwa hata kwa kukutwa na vipande vya nyama tu ya kitoweo cha familia.

Waziri husika nae aachie ngazi, ikiwa watu wanafikia hadi kufanya ujangiri wa kuhujumu uchumi huku wanalindwa na vyombo vya dola na wakijitajgaza wazi wazi, je vungapi hatuoni ambavyo ni zaidi ya hivi?



===

Raia mmoja wa Kizungu anayejiita Bowmarbow hunting ameonekana mitandaoni akitrend kwa kujisifu kuua Mamba mkubwa zaidi kutoka Tanzania.

Kupitia Instagram yake ameandika kuwa ameingia kwenye rekodi ya kuua Mamba mkubwa zaidi.

Ameandika haya;

“PENDING NEW WORLD RECORD CROC with a bow. This monstrous crocodile measured in at an astounding 16’ 3”! Making him the largest croc in history to ever be harvest with a bow and arrow. The best part is, he’s a 100% wild & 100% free ranging croc in the wilds of Tanzania, which is not how most of the WRs are shot in Africa.

This hunt was beyond incredible to say the least, I can’t wait to share it with you all! The footage we captured was some of our best and this is by far the biggest animal ever shot with a beast_broadheads at 25 yards with an 84lb bow and only a 530 gr arrow it buried through his armor and went all the way up to the fletching.

Just a crazy testament to the lethality of the head.

PSA: As for the Broadheads, next week we’ll be opening them back up for you everyone again A thank you all for your patience with being sold out”

Je, ni sahihi kwa Wanyama kama hawa kuuawa kiholela kwa ajili ya kuweka Rekodi?

Bongo 5
"Je, ni sahihi kwa Wanyama kama hawa kuuawa kiholela kwa ajili ya kuweka Rekodi?
Hajauawa kiholela - Vigezo na masharti vimezingatiwa.
Lakini kama huridhiki kwa mujibu wa kichwa cha Mada milango iko wazi ya kuchukua hatua dhidi ya huyo Mzungu wala hili halimhitaji Rais aingilie kati.
 
Ndio
Lile jina mods walinibadilishia bila ridhaa yangu
Kiukweli mimi binafsi nililipenda lile zaidi. Kuna watu wanajiita shetani na majina mengine ya ajabu kabisa sijui shida ilikuwa wapi kwenye hiyo user name?

Je ulijaribu kuwauliza ni kwanini? Au je walikwambia sababu ya kulibadili?

Maana nafahamu na hata founder wetu Maxence Melo , huwa anahakikisha hata ukifungiwa na sababu ya kufanya hivyo unajulishwa pia nafasi ya kujitetea.
 
... sema mama mjane maskini alambwa miaka 20 jela kwa kukutwa na ndoo yenye vipande vya mzoga wa swala huko Iringa.

Mzungu tajiri milionea apongezwa duniani kote kwa kuua mamba mkubwa zaidi duniani kutoka Tanzania. Umaskini kitu kibaya sana!
Hakika, inasikitisha sana.
 
Unajua madhara ya mamba mkubwa hivyo kuroam freely?

Bora nchi imepata mapato na mamba kauwawa, siku zake zilikua zinahesabika na angeuwawa bure kabisa. BTW hunting is legal in TZ.
Ana madhara gani mkuu, tuache mambo ya kufikilika.
 
Sijaelewa theme ya hii story, kwamba ni ruhusa kuwinda maonesho ya kuvunja rekodi mamba mkubwa au ni kwa ajili ya matumizi ya binadamu...??
Jamhuri imuonee huruma yule Mama Mjane aliyekutwa na vipande vya nyama Poli kwa ajili ya watoto wake.
 
Da
Mkuu hao wanyama wote wana bei zao,kalipa huyo.
Mamba si chini ya dola 25000.
tembo 40000 zamani hiyo.
Simba 45000Usd zamani hiyo.
Nyati 20000
Swala,ndege,fisi,nyoka,kanga hao ni nyongeza.
So hao wanawinda kihalali kabisa.
na hachukui huyo mnyama ataondoka na ngozi tu na meno.
Mtaachiwa nyama hapo mle kama mnakula mamba.
Dah, yule Dada aliefungwa miaka 20 kwa kukutwa na mapande tisa, ya nyama poli, ni bora wange mlipisha tu, kuliko kifungo cha miaka yote ile.
 
Umesahau!

Pia iwaachie wote walofungwa Jela kwa kukutwa na Nyama za Swala, sijui Nyati...

Bila kusahau wale walofungwa kwa kugonga Twiga n.k

Wote waachiwe Huru.
 
Duh...!.
Naomba tusubirie taarifa ya MNT, kujua kama crocodiles ni endangered species ambao hawaruhusiwi kuvunwa, maana Tanzania tuna hunting blocks za uwindaji wa kitalii ila muwindaji, anaandamana na game rangers ambao ndio huwa wanaelekeza ni mnyama yupi wa kuwindwa kuepuka kuwinda mnyama mja mzito, au anayenyonyesha.
P
Maonesho ya hiyo nyara yanatupa picha gani kwa yule Mama aliyekutwa na tuvipande twa minofu ya nyama poli kwa ajili ya watoto wake.??
Tupe Elimu kidogo Mkuu.
 
Mkuu hao wanyama wote wana bei zao,kalipa huyo.
Mamba si chini ya dola 25000.
tembo 40000 zamani hiyo.
Simba 45000Usd zamani hiyo.
Nyati 20000
Swala,ndege,fisi,nyoka,kanga hao ni nyongeza.
So hao wanawinda kihalali kabisa.
na hachukui huyo mnyama ataondoka na ngozi tu na meno.
Mtaachiwa nyama hapo mle kama mnakula mamba
Da

Dah, yule Dada aliefungwa miaka 20 kwa kukutwa na mapande tisa, ya nyama poli, ni bora wange mlipisha tu, kuliko kifungo cha miaka yote ile.
Huyo hakuwa hata na haja ya kulipishwa chochote.
Hizo nyama inawezekana ni hizo za wanyama hawa hunter wanaacha porini,wanakijiji wanachukua wanapeleka kuuza.
Hunter huwa wanachukua ngozi tu au meno au mapembe.
Ila viswalaswala hivi,kanga sijui mnyama gani mnatafuna tu havina deal.
Sasa fikiria Nyati mzima ni kilo 700-1000 nani atamaliza?
Tembo sio wengi wanauliwa


bei yao kali.
 
Kwa akili yako ya kawaida,kumuua mamba kama huyo kwenye hifadhi ni sawa?!! Unaweza kukadiria imechukua miaka mingapi mpaka akawa na ukubwa huo?!!

Kama angebaki na akajengewa eneo maalumu kwa ajili ya watu kwenda kumuona ingekua ni hasara kwa Taifa ama faida zaidi?!! Baada ya huyo kuuliwa,kuna wengine wenye ukubwa huo?!! Kama wapo,nao hawatauliwa?!! Aliemuua anaenda mfanyia nini?!!!! Hicho anachoenda kukifanyia- Taifa linanufaikaje?!!

Tuache kutetea upuuzi na uharibifu wa Mali asili
Anzia kwa watunza ifadhi kabla ya kumlaumu muuaji.
 
Usikurupuke kuandika vitu usivyovijua, kuna hifadhi za taifa na mbuga za wanyama. Kati ya hizo mbili, moja wapo, watu wanapewa vibali na wanawinda wanyama kwa lengo la ku-balance idadi. Jiongeze wewe boya
Mpuuzi kweli vitu vingine ni Bora kufatilia ukweli kwanza ndo uje kuandika hapa kwenye mitandao, utaratibu uko wazi na umefatwa halafu anatoka boya mmoja anataka waziri ajiuzulu!
 
Back
Top Bottom