Rais Samia: Milioni 960 za sherehe ya Uhuru zikajenge mabweni shule nane za wanafunzi wenye mahitaji maalum

Rais Samia: Milioni 960 za sherehe ya Uhuru zikajenge mabweni shule nane za wanafunzi wenye mahitaji maalum

Mheshimiwa Rais Dr. Samia S.Hassan zile milioni 500 ulizotoa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa Nje (OPD) Hospitali ya wilaya ya Nyamagana zimepigwa zote, jengo halijaisha watumishi wapo wanarushiana mpira! Mh. Rais pengine una nia nzuri ila tunajua huku chini wanasubiria huo mgao wa madaraja wazitafune kama mchwa!
Unauhakika kuwa zilifika zote?
 
Mheshimiwa Rais Dr. Samia S.Hassan zile milioni 500 ulizotoa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa Nje (OPD) Hospitali ya wilaya ya Nyamagana zimepigwa zote, jengo halijaisha watumishi wapo wanarushiana mpira! Mh. Rais pengine una nia nzuri ila tunajua huku chini wanasubiria huo mgao wa madaraja wazitafune kama mchwa!
Nilivyoona hiyo 500 nikadhani zile milioni 500 kila kijiji.
 
Uhuru wa taifa letu ndiyo msingi wa taifa husika. Kama tunaweza kufanya sherehe za kuzindua matundu ya vyoo, miradi ya maji nk kwa gharama kubwa tunashindwaje kuona umuhimu wa sherehe ya kumbukumbu ya siku ya uhuru ambayo inabeba alama na historia ya taifa letu?. Kwa viongozi mliopo madarakani kunahaja ya kuweka vipaumbele vya taifa hili vizuri kwani vinginevyo taifa litaangamia.
Labda kama kuna nadharia nyingine kwamba uhuru waliopigania wakati huo umeshaporwa hivyo hakuna haja ya kufanya sherehe hizi kwa maana kwamba walichopigania kutoka kwa utawala wa mkoloni hakipo tena.
Uhuru gani huo unaouzungumzia kama bado kuna watu wanasafiri kilometers kadhaa kufuata huduma za afya? Maji tatizo,Umeme shida,Barabara kikwazo.....ungejua maana ya neno Uhuru kwanza
 
Sio kila kitu ni Cha kuiga kwamba Hakuna haja ya sherehe si ndio?
Mimi sioni tatizo kuadhimisha miaka ya uhuru wa Tanganyika kwa kufanya kazi za ujenzi wa taifa.

Yani badala ya kukaa uwanjani na kuangalia gwaride, watu wafanye kazi za ujenzi wa taifa, wasafishe nchi etc.

Nyerere aliandika falsafa ya "Uhuru ni Kazi".

Na katika kuadhimisha uhuru, tunaweza kufanya kazi.

Hili si jambo geni, wala halitakuwa la kwetu tu.

Wamarekani hufanya kazi kuadhimisha siku ya mpigania haki Martin Luther King Jr.

Ila, pia, nina tatizo ninapoona pesa ndiyo inafanywa kuwa kigezo na kipimo. Kwamba habari nzima inazunguka kwenye pesa zimeondolewa huku zikapelekwa huku.

Wakati kwanza hiyo pesa ukiilinganisha na nguvukazi ya Watanzania, ni pesa ndogo sana.

Kwa nini serikali inashindwa ku mobilize watu kwamba mwaka huu tutaadhimisha uhuru kwa kufanya kazi fulani za kujitolea?

Serikali imejikita kuongeza kodi na tozo, kwa hela ambazo wananchi hawana, lakini imeshindwa kujua kutumia muda wa wananchi na nguvu zao, vitu ambavyo wanavyo zaidi.

Poor planning.
 
Asimamishe semina zote za wafanyakazi wa serikali zinazotafuta hela baadala yake wafanye online, ile michezo ya mashirika shimuta ni kupoteza hela tu apige marufuku.

Apige marufuku ziara zote za mawaziri mpaka atoe yeye ruhusa, safari zisizo na kichwa wala miguu azipige marufuku, apunguze msafara wake na safari za nje zisizo na issue baadala yake atume mabalozi tu. Apige marufuku matumizi ya migari inayobwia mafuta kama V8 na kuweka usimamizi mkali kwenye matumizi yake.

Atambue tu, wizi, uzembe, ubabaishaji na ujinga mwingi kwenye taasisi za umma umerudi kwa kasi na watu wanahomola tu, APIGE JICHO HUKO KUNA HELA NYINGI ZINAPOTEA.

Afanye reform ya uhakika TISS na JESHI LA POLISI kwa maslahi mapana ya nchi na kuajili watu wa kada mbalimbali based na mahitaji na sio KAMLETE na MAKADA.
TISS kuwe na kitengo maalum chenye engineers wabobezi wa kila idara waliofanya sana kazi nje na ndani ya nchi kwenye private sector hasa hizi international business na hawa watamsaidia kwa uangalizi kwenye mamiradi haya, maujenzi, mamikataba na kunusu issue ambazo ni very technically ambazo Taifa linapigwa kila uchwao..

HII NCHI SIO MASIKINI BALI INA SHIDA YA WATU COMPETENT, WAAMINIFU, COMMITED NK, MATUMIZI YA HOVYO YA HELA ZA UMMA NA WIZI....HIVI VILIFANYWA IN A YEAR UTAONA TAIFA LINAVYOKIMBIA KWENYE MAMBO MBALIMBALI..
 
Kuna mawaziri wanazururazurura tu kama manyapara ilihali kuna structure na chain ya kazi ambayo inataka proper supervision tu huko huko mikoani.
Haya maziara na misafara ya hovyohovyo kila siku yanafanya operation cost zinakuwa juu.

Usimamizi thabiti wa mali za umma kupitia TISS na Jeshi la polisi wakiwa kama joint force in special department itakayoundwa na watalaam kila kada kuanzia Accountants, Lawyers, doctors wa binadamu, engineers nk hawa kazi yao kuangalia facilities za nchi kuanzia viti, magari, meza, Energy management nk. hawa moja kwa moja wanakuwa wanareport ikulu.

Huwa nashangaa sana tunavyohangaila eti makusanyo au kutafuta hela kwa wafadhili wakati kuna loops kibao tunachezea hela buree kabisa.
 
Asali Ya Kulamba Imemwagika/Imemwagwa......
 
Milioni 960 ziko kwenye karatasi ( Bajeti) kama figure .

Hadi zitumwe eneo husika ni March 2023.
Kwahiyo Sherehe za Uhuru mwaka huu zingefanyika March 2023!? Na mbona Simbachawene anasema wameshazituma maeneo husika...au katuma makaratasi tuu.
 
View attachment 2436580

NB: Ya Magufuli ni yake Samia.
====


Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekeza TZS milioni 960 ambazo zilitengwa katika bajeti kwa ajili ya maadhimisho ya sherehe za Uhuru inayoadhimishwa kila Desemba 9, zipelekwe Ofisi ya Rais TAMISEMI na zitumike kujenga mabweni katika shule nane za msingi zenye wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 5, 2022 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera na Uratibu, George Simbachawene amezitaja shule hizo kuwa ni Buhangija (Shinyanga), Goeko (Tabora), Darajani (Singida), Mtanga (Lindi), Songambele (Manyara), Msanzi (Rukwa), Idofi (Njombe), na Longido (Arusha).

Amesema shule hizo zimekwisha ratibiwa na TAMISEMI na tayari zimekwisha gawiwa fedha hizo kwa ajili ya kuwajengea mazingira rafiki wanafunzi wenye mahitaji maalumu.

“Ikiwa ni dhamira ya dhati ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwajali na kuwajengea mazingira rafiki watu wenye mahitaji maalum hapa nchini, hili ni jambo kubwa na la kishujaa na la kupongezwa sana,” amesema.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kushiriki kwa wingi katika midahalo na makongamano katika wilaya zote na kujadili kwa kina kuhusu maendeleo endelevu katika siku ya maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania.

View attachment 2436676
Zile mlizowapa simbion si zingetosha kabisa
 
sijawahi kuzielewa hizi sherehe za Uhuru, Za wafanyakzi, Muungano wakati nchi mpaka leo Maji tabu, Bara bara za mchongo, Shule majanga, Hospitali majanga.
 
Back
Top Bottom