Rais Samia: Mimi ni Mzanzibari

Rais Samia: Mimi ni Mzanzibari

Huyu bibi ni mbaguzi balaa
Wewe jamaa una nongwa sana.....

Kwako hakujawahi kutokea kiongozi wa CCM akawa mwema....

Endelea kuufukuza upepo...labda iko siku CDM mtaipata dola kwa staili hiyo ya kupinga ,kuzusha na chuki.... 🤣🤣
 
Mtu aliyezaliwa Zanzibar mwaka 1960 ni Mzanzibari. Tanzania haikuwepo huo mwaka 1960.
Kama hivyo ndivyo basi Nyerere aliyezaliwa 1922 enzi za ukoloni asingejiita Mtanzania na kudumu katika hilo hadi kifo chake!!! Mtu aongee ni Mzanzibari akiwa ndani ya eneo la Zanzibar pekee sio nje ya hapo. La sivyo watu wa jamii zingine wanapotoka kwenda mataifa mengine wasijitambulishe wao wanatokea Tanzania bali kwa mfano Mbena wa Njombe, Mruri wa Mara, Mmanyema wa Kigoma, Mkaguru wa Gairo nk

Inawezekana hata huko UNGA utambulisho ulikuwa ............
 
Kilichoharibika ni kwa kuwa yeye amejitaja Mzanzibari ?!!!

Mbona hayati JPM(Rip)alikuwa anajitaja kuwa msukuma na anakiongea akiwa kanda ya ziwa?!!!

Tensions zote hizi zisizo na maana ,mantiki na faida ni za kumtengenezea mh.Rais apate tabu kuongoza.....
Amesema hana kabla. Kwa hiyo alitakiwa kusema kuwa yeye ni Mtanzania..... Period. Kujiconnect nakule aliko toka ni sawa na kusema mimi ni kabila fulani.

JF humu kuna watu wengi tu ambao hawajui lugha nyingine yeyote nchini zaidi ya kiswahili. Ila pale watakapotumia makabila ya wazazi wao kujitambulidha tayari wanakuwa wamechanja upande.
 
Tunataka Rais mtanzania siyo mtanganyika wala mzanzibari. Tunataka Rais asiyebagua nchi kikanda, Tunataka Rais anaejivunia Utanzania wake siyo utanganyika wala UZANZIBARI wake.
Kama JPM vile alivyokuwa hana ubaguzi kikanda
 
Inamaana hujui kua hao Wazanzibari asili yao si bara, ambako watumwa walikua wanachukuliwa na kusafirishwa kupitia Soko la watumwa huko Zanzibar kwenda ughaibuni!?

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Tukianza hivyo .wabara wenyewe watabaki wachache.kiasili watanzania wengi ni wahamiaji.
 
Wewe jamaa una nongwa sana.....

Kwako hakujawahi kutokea kiongozi wa CCM akawa mwema....

Endelea kuufukuza upepo...labda iko siku CDM mtaipata dola kwa staili hiyo ya kupinga ,kuzusha na chuki.... [emoji1787][emoji1787]
Kuna kiongozi gani mwema kutoka CCM? Mtaje hata mmoja
 
Mi sijaona kosa lake kwa kauli hiyo. Infact, alikuwa anawapiga dongo watanganyika. Tanzania ni Muungano wa nchi mbili. Tanganyika na Zanzibar. Bara ndio kuna huo ujinga wa Kabila ila kule ZANZIBAR haupo. Hivyo anawaambia nanyi achaneni na ujinga wa makabila. Yeye amesema wazi kwamba KABILA lake ni Mzanzibari. Hajasema utaifa wake. Kwanini kuna watu mna nongwa kwa kila jambo. Mna lengo gani kwani?
 
Alitakiwa aseme mimi ni MTANZANIA! Lakini kinywa cha mtu husema yaliyojaa moyoni!! Uzanzibari umejitokeza kuwa umejaa moyoni kuliko Utanzania!! Very unfortunate!! Imeshatoka hiyo live!!

Mkuu umeandika sahihi kabisa kabisa.

Rais kama alitaka kukosoa ukabila, angejinasibisha na u Tanzania na si uzanzibari.

Alikosea, aliharibu badala ya kutengeneza.

Watu wanarefer Magufuli kuwa aliongea kisukuma, hata yeye tulimkosoa hapa kama tunavyomkosoa Samia. Kosa la aliyepita halijustify kosa la aliyepo.
 
Tunataka Rais mtanzania siyo mtanganyika wala mzanzibari. Tunataka Rais asiyebagua nchi kikanda, Tunataka Rais anaejivunia Utanzania wake siyo utanganyika wala UZANZIBARI wake.
Sahihi kabisa and well stated
 
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mapema leo amesema yeye hapendi Ukanda ila yeye ni "Mzanzibar!"

Kiukweli Rais kakosea sana kukemea ukabila huku yeye akitamka bayana ni wa mahali fulani.

Samia umekosea sana!

====


Samia Suluhu ninapotoka hatuna makabila. Kwetu kule Zanzibar tunajuana kwa maeneo...

Kwenye system ya makuzi – shule na siasa – tunamshukuru sana Baba wa Taifa Mwl. Nyerere. Kwahiyo, tunapofanya kazi hapa, na mimi binafsi, ninafanya kazi bila kuangalia kabila fulani.

Sasa watu wakifanya makosa, “nimewajibishwa kwakuwa ni kabila Fulani”. Sina kabila. Mimi hapa ukiniuliza kabila lako nani nitakwambia ni Mzanzibari.
Wafuasi wa mwendazake ndio wanalialia mara tunaonewa, mara, tunatumbuliwa,....
 
Ulitaka aseme ni ngosha au mangi wa kibosho
Sijui kama umeelewa hoja hapa
Yeye ni Mzanzibari kwa kuwa Zanzibar hakuna makabila kama yangekuwepo angejitaja kwa kabila lake
Kwetu Bara makabila yapo kwanini nisiseme mi mchaga au msukuma?

Angekuwa mfano kwa kusema mimi ni mtanzania na siyo kujitaja kwa eneo analotoka tungemuelewa

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Angejitambulisha kwamba yeye ni Mkojani au Mnungwi isingekuwa na tatizo lolote. Ni sawa na ilivyokuwa haina tatizo kwa JPM alivyokuwa akijitambulisha kwamba alikuwa Msukuma. Pamoja na kwamba tulikuwa tunafahamu kwamba JPM alikuwa Mtanganyika, lakini ingeleta kero sana kama kwa siku yoyote angejitambulisha kwamba alikuwa Mtanganyika. Hata Samia kwa kujitambulisha kwamba yeye ni Mzanzibar kakosea na nadhani haina afya kwa taifa. Kujitambulisha kwa kutumia utaifa wetu wa zamani ambao kimsingi ulishakufa siyo vyema sana.
Mimi binafsi sioni tatizo. Inaonekana wewe ndio wale wale wa lile kundi. Mnatumia kila kisingizio ili kumuharibia sifa rais wetu.
 
Dah Hilo jina Mkuu ni la kipekee kweli kweli [emoji38]
 
Tusikuze mambo hapa hana tofauti na Magu kusema yeye ni msukuma. Zanzibar hawana makabila ni wahamiaji hivyo wanatumia neno mzanzibari sio kitaifa lakini kijamii kama wachagga, wapare, wasambaa, wahehe, wasukuma. Magu alikuwa akisema yeye ni msukuma hakuna aliyesema chochote sasa Samia ni kabila gani? Wote kule wanatumia neno mzanzibari kwa maana ya jamii na sio utaifa
 
Back
Top Bottom