DOKEZO Rais Samia, Mwanao Abdulhalim Amer adaiwa kuwapa tabu sana maofisa wa TRA kutekeleza majukumu yao Kariakoo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Status
Not open for further replies.
Acha chuki binafsi, zingatia kupata faida kiasi kwenye biashara yako, Huyu kijana hana tamaa ya kuuza bei ghali ya kupata faida za kufuru, hapendi makuu, yeye huridhika na kiduchu apatacho, chuki zako haziwezi kukufikisha popote mtoa mada.
Sijaandika kwa chuki kama udhaniavyo.sio mara moja huyu mtu ameingia matatani na kila akibanwa basi itapigwa simu kutoka juu,kuna siku tena pale science akakamatwa na police wakiwa na tra mzigo wake ukiwa kwenye canter flani hivi nyeupe ulikua umetoka kwa hao hao wachina wanaojiita hiview international akiwa hana documents zozote,mchezo ukawa huo huo wa simu kutoka juu.
 
Daah Wabongo bhana mtu anajiuzia matairi yake mnaandika andika humu njoo Johannesburg uone watu wananunua makontena na makontena ya matairi ishu ya invoice unakutana nayo mpakani huko na SARS sio ndani huko ndani ni polisi kujua labda huu mzigo ni wizi au laa hivyo vikaratasi mnavyofatilia kwa box moja au mbili ni Umasikini tuu huo...ndio maana vitu vingi vipo bei juu na bandari tunayo hao wanaoweza kushusha hapo kwa usumbufu huo wanajiuzia bei yeyote..
Makampuni ya TV na mashine za kuoshea nguo kila mwezi wanashindana kutoa brand mpya ila bongo hivyo vitu bado ni hatari kwa sababu ya Ujinga huo au Microwave...
Wasiokua na bandari ndio wananufaika na bandari yetu ninyi kutwa na TRA yenu kudumaza matumizi ya vitu bora kwa Wananchi hakuna asietaka kulipa kodi punguzeni usumbufu ili hata wageni waache kwenda kununua bidhaa Nairobi Nchi iwe na mzunguko kama huko kwa wenzetu..
 
Unazungumzia nchi ipi huko nje??

Ikiwa Trump ana kesi nyingi za kukwepa kodi unataka kutuambia nini??
 
Niliwahi kufanya biashara na hao wachina wa mikocheni wanaojiita hiview international, hao jamaa hiyo kutokutoa risiti ndiyo michezo yao na sijui kwa nini TRA Tanzania hawawachukulii hatua.hapo kariakoo wafanyabiashara wengi wanawaita shamba la bibi kwa sababu ya hiyo michezo yao.
Huenda huyo mtoto wa Rais nae kaamua kutumia hiyo fursa kwani wenzake nao wanaitumia.
 
Unazungumzia nchi ipi huko nje??

Ikiwa Trump ana kesi nyingi za kukwepa kodi unataka kutuambia nini??
Sasa kumbe ana kesi tayari iko mahakamani?means vyombo vyao vya usalama viko imara na independent kumshughulikia yeyote anaevunja sheria zao walizojiwekea.
Ushaskia tanzania mtoto wa kiongozi au kiongozi kafikishwa mahakamani kwa kesi kama hizo?
 
Unadhani yeye ni mpuuzi kiasi hicho mpaka akauze matairi? Achaneni na mambo ya Abdul hamtayaweza. Ingawaje simfahamu.

Na huo muda hata wa kurecord hayo unautoa wapi? Nyie mnaoshauri arekodiwe. Kwa taarifa yako Huyu Rais Hata ungejitoa kafara wewe na ukoo wako na kabila lako lote. Huwez kumchafua maana influence yake imefika mpaka kwa Mungu achilia mbali kimataifa.

Ndio mana ikatabiriwa na IMF licha ya uchumi kuyumba duniani ila wa Tanzania utakua zaidi kwa ajili yake.
 
Shida ipo wap? Usilallie bahat ya mwenzako mlango waz. Assume anaishi na mzaz wake.obvius atafanyiw gharam zote.wewe mwanao unamuachaga ukisafir?
 
Africa,tanzania ndiyo ilivyo

Watu fulani kusumbua kisa

Baba zao ,wazazi wao wako kwenye uongozi ni kawaida hiyo

Ova
 
uzuri mie namfahamu samia kwa zaidi ya miaka 25 hii kitu kama ni kweli huyo mwanae anafanya,hakijui na hakiungi mkono,lakini huyo kijana pia namfahamu vizuri mno ni mtu asiye na makuu na wala sio mjivuni,sidhani kama anafanya na nitampigia simu nimwambie kuwa kaandikwa jf in case atakuwa hana taarifa
 
Sasa mkuu MBNA Inaonekana Kama Wew imekuuma Sana shida nn, Fanya kazi zako acha maisha ya watu utaishi vzuri mambo ya umbea umbea Achana nazo unadhan wahusika hawajui?
Wapuuzi wote huwa na mawazo kama yako
 
Inaonyesha jinsi gani unafuatilia nyendo za binadamu mwenzako hatua kwa hatua, kama binadamu tunalakujifunza kutoka kwako, "kumbe wapo binadamu kazi yao kuu ni kuhangaika na maisha ya wengine"
 
bw abdul anaweza hata kumkoromea mpango na akanyamaza sembuse hao tra!

mpaka hapo lazima mkuu wa usalama amelazimika kumuongezea ulinzi na kumpa namba maalumu ya kuwasiliana nae, igp na kamisha wa tra nao wametoa namba maalumu inayotumiwa na watu maalumu.

shem wake mchengelwa na aweso wameshamtuliza kiakili.
wasaka fursa akina dr kilaza msukuma na gachuma wanawaza kuingza pesa kwenye matairi.

doto biteko anawaza amkabidh mgodi wa dhahabu.

pindi anawaza amkabdh mikumi na serengeti.

maafisa wa benki wanamuomba akope kwao ili wapate koneksheni na ten pa!

MLITAKA AJE AFANANE NA AKINA JOSE WALIVOPAUKA AU AKINA MADARAKA WANAZEKEANA KIMASIKINI?
 
Hamjui mlisemalo, mama Samia hana tofauti na Nyerere (kimitazamo),kwa jinsi Nijuavyo, hadekezi, anamsimamo wa kunyoosha, na haki, so ni ngumu hata kwa mtoto kumwambia mamaye jambo la hovyo! (hana tabia ya kutodekeza mtoto)
 
Mbona kama umeandika kwa unyonge sana?! Watu na nyadhifa zao, anatumia mgongo wa mama kufanya uharamu wake. Kwani yeye hatumii jf, najua ujumbe ataupata tu.
 

Si bora ni tairi ingekuwa drugs si ungeenda CNN kabisa wewe? Acha husda.

Kwahiyo wewe kila hatua unamfuatilia yeye tuu eti? Kwanza nashangaa kwanini hakuna wasaidizi wa kumfanyia cover huyo kijana kweli Mzazi wake hana makuu.
 
Hivi unapata wapi jeuri wewe afisa wa TRA kumkamata mtoto wa Rais, hivi unajua nguvu ya Rais achenj jitafutia matatizo
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…