samia akifeli ni taifa zima limefeli,sawa kijana!!!
usione watu wanapiga kelele ukafungwa na hisia zako za chuki tu kwa jpm wakati wote.
kule kwenye ule uzi nimekuuliza sababu ya mahindi kuzuiwa ilikuwa nini,hujajibu mpaka sasa.kwanini mmeamua kiwa wazembe tu kufikiri???
Akifeli au mnaombea afeli?!
Nimekuuliza kuna ubaya upi kwa Samia kama Rais kutaka kuongea na business community, na kufungua milango ya biashara?
Sina kawaida ya kutojibu post, na wala sijaona hiyo post yako kuhusu mahindi... weka hapa!!!
Post zako 3 za mwisho ni:-
najua ni maumivu tu yanakuhangaisha mkuu,wala sio wewe huyu.
jpm anapofanya mnayohisi ni mazuri mtasema kwamba ni utekelezaje wa yale waliyoyaasisi watangulizi wake.ila mabaya yote kwa muono wenu ni ya kwake mwenyewe.
kama ametekeleza ilani ya chama chake,ambacho ndio mipango ya watanguulizi wake,ubays wa jpm kwa makada wa chama ni nini??
Sasa unaniuliza habari za makada wa chama wakati post yangu haikuhusiana na habari za makada?
Na kama anatekeleza ya wenzake, sasa hizi legacy mnazoimba zinatokana na nini?! Kwanini mnadhani yeye ndie anastahili hizo legacies wakati kuna miradi kaikuta imetafutiwa hadi pesa, na yeye katekeleza tu lakini bado mnaimba legcy ya JPM!!
Post yako nyingine ni hii:-
nimekwambia mimi ni mhehe wa iringa,najua utabisha ili ku suit hisia zako.nahusiana nini na ukanda wa magufuli???
kwa misimamo,matamko,na hata maamuzi ya jpm,unadhani ni msukuma gani atasimama mbele za watu asijivunie usukuma wake!!!au hukuwepo enzi za hayari sokoine na wamasai???
Mara ya kwanza nilikuambia wewe ndo wale wanaodhani urais wa JPM ni wa Wasukuma wote kwa sababu ulionekana unawafahamu sana Wasukuma kuliko Wakwere?!
Lakini uliposema wewe Mhehe, wala sikuendelea kusema wewe ni Msukuma... sasa ulikuwa na sababu ipi ya kusisitiza kwamba "...nimekuambia mimi ni mhehe" wakati post yangu ilikuwa inasema:-
Sizungumzii kupata shavu, nazungumzia Wasukuma walivyojipanga kutetea ya JPM hadi Askofu Rashid kufikia kuhamasiaha Wasukuma wautetee urais wake!!!
Na asilimia kubwa ya wapiga mapambio hapa wala sio wafuasi wa CCM ambao nawaheshimu kwa sababu wana wajibu wa kutetea kiongozi anayetokana na chama chao lakini wengi wao wanatetea kwa sababu tu ya ukabila na ukanda!!!
Hiyo post unaona inakulenga wewe?
Lakini sitaki kuwa mnafiki... WEWE HUONGOZWI NA ITIKADI BALI NI MFUASI WA MTU!! Anayeongozwa na itikadi hawezi kupinga kila kinachofanywa na rais aliyetoka chama kile kile!!! Na wengi wa aina hii ni watu wa kanda maalumu ingawaje wapo wanaojitambua miongoni mwao!!
Wana-CCM wa kweli wanamuunga mkono Mama kwa sababu kwao, JPM na Mama ni kitu kimoja!!
Aidha, post yako nyingine miongoni mwa zile 3 za mwisho inasema:-
mbona hujiamini ndugu yangu,nafsi inakusuta eh???
nasemajee jpm hakuna akichofanya,vyote ni bure.
Sasa hiyo post ya mahindi ni ipi?!
Btw, kwanini nishindwe kujibu hoja nyepesi kama ya mahindi?!
Anyway, jibu maswali niliyokuuliza kuhusu ubaya wa Samia kutaka kufungua milango! Au unaona anam-challenge Malaika Mtukufu Mungu ambae bila aibu mnafikia kumlinganisha hadi na Nyerere!