Rais Samia: Nani atazikwa na hela?

Rais Samia: Nani atazikwa na hela?

Hii sio kauli ya amiri jeshi mkuu hata kidogo. Mwizi wa hela, hela ilivyo tamu, hela ni madaraka, hela kwa sasa ndio kipimo cha utu/ubinadamu, hela ni pesa...then unakuja na simple statement, unadhani mtu anashtuka?
 
Samia badala asimame kama Rais, anasimama kama mchungaji ama mtume.

Watu wanakula hela yeye anawahibiria.

Mifumo ni mibovu ndio maana mnataka rais achunge hela. Kwenye mifumo yenye nguvu, CAG angejiridhisha na wezi amgewapeleka mahakamani kwa kesi. Sio mambo ya kusubiri rais wakati hakuna uhakika kama rais ni muadilifu. Kuna mwingine hivi majuzi alikuwa anajifanya mzalendo, matokeo yake imekutwa account huko China.
 
Rais Samia S
Ni kauli fupi sana lakini nzito kwelikweli. Akionyesha kukerwa na majizi Rais Samia aliitoa kauli hii. Majizi yote hakuna linalolala kwenye vitanda viwili, vyumba viwili wala kula sahani mbili za ugali kwa wakati mmoja, wanaiba na kurundika pesa ambazo wataziacha wakati wakifa.

Pesa hizo mara nyingi ndio zinageuka chanzo cha vifo vyao kwanjia ya kisukari, shinikizo kubwa la damu, uzito mkubwa, ugonjwa wa ini na figo, kansa, ajali za magari, ukimwi na msongo wa mawazo. Na mara nyingi fedha hizo huwa ama zinapotea au kugeuka pia kuwa chanzo cha laana na vifo kwa watoto, ndugu na wajukuu atakaowaacha. Ni heri ya mtu aliacha mti mmoja wa kivuli kwenye uwanja wake wa nyumba kuliko yule aliyeacha mabilioni ya fedha kwenye vihenge na bank.

Nimuombe tu mama yetu atengeneze katiba nzuri yenye meno kabla hajaondoka madarakani. katiba "nzuri" kwangu ni katiba ambayo:
1. Inaondoa kinga ya kushitakiwa kwa wezi wote wa mali ya umma
2. Unatoa njia rahisi ya kumuondoa kiongozi wa ngazi yoyote ambae ni mwizi au mbadhilifu.
3. Inatoa adhabu kubwa sana ya kunyonga au inayokaribia na kunyonga
4. Inatoa dira na mwelekeo wa taifa kwenye uchumi, afya, elimu, chakula na ulinzi.

Mali za Nchi haziwezi kulindwa kwa ukali wa mtu mmoja, bali kwa katiba na taasisi zenye nguvu na meno ya kuzilinda.
Rais Samia Suluhu alionyesha kukerwa sana na wezi wa pesa za umma kwaiyowasijidanyanye kuwa kuongea vile ndio imeishia hapo hapo Hapana Mama hawezi kuruhusu ubadhilifu wa fedha za umma na akakaa kimya lazima awachanie mkeka siku zinahesabika
 
Yaan hizi kauli haziwez mfanya mwizi aache kuiba .

Mama kama anataka kua Mtume, aanzishe Msikiti awe Mtume huko !!.

Mwanadamu ameumbwa kupewa Adhabu ili abadilike..

Hivi kama Yesu mwenyewe alipigwa misumali na wanazengo licha ya kwamba aliponya viwete, alifufua, na waliona kabisa Kwa macho, ila bado wakamuua,

Sembuse Hela ?? Hela ??? .
Lazima wawajibike mkuu we subiri tu mkeka mpya
 
Hiyo kauli ni kama ile ya yule shoga aliemumwagia mwizi shombo ya samaki kwamba akaliwe na mijipaka.
 
Yaan hizi kauli haziwez mfanya mwizi aache kuiba .

Mama kama anataka kua Mtume, aanzishe Msikiti awe Mtume huko !!.

Mwanadamu ameumbwa kupewa Adhabu ili abadilike..

Hivi kama Yesu mwenyewe alipigwa misumali na wanazengo licha ya kwamba aliponya viwete, alifufua, na waliona kabisa Kwa macho, ila bado wakamuua,

Sembuse Hela ?? Hela ??? .
Exactly: Reward & Punishment
mwizi lazima aadhibiwe
hodari apewe motisha
 
Yaan hizi kauli haziwez mfanya mwizi aache kuiba .

Mama kama anataka kua Mtume, aanzishe Msikiti awe Mtume huko !!.

Mwanadamu ameumbwa kupewa Adhabu ili abadilike..

Hivi kama Yesu mwenyewe alipigwa misumali na wanazengo licha ya kwamba aliponya viwete, alifufua, na waliona kabisa Kwa macho, ila bado wakamuua,

Sembuse Hela ?? Hela ??? .
Misikitini hakuna mitume,acha ujinga,uwe unajielimisha kabla ya kuzungumzia Jambo hadharani
 
Mhusika au wahusika mpaka sasa walipaswa kuwa wameshazikwa, mali zao zote mufilisi.... short and clear, kuendelea kupoteza muda na wajingawajinga matokeo yake ndio haya.

Wajinga wakiwa wengi wanachagua Rais na kuiweka serikali madarakani, wajinga wakiwa wengi wanatunga katiba yao yakuwalinda, Wajinga wakiwa wengi hata uwe na katiba bora kiasi gani watateka kila njia ili wawe salama.

Dawa ya mpumbavu na mjinga ni risasi au jela na mateso makali.
 
Mifumo ni mibovu ndio maana mnataka rais achunge hela. Kwenye mifumo yenye nguvu, CAG angejiridhisha na wezi amgewapeleka mahakamani kwa kesi. Sio mambo ya kusubiri rais wakati hakuna uhakika kama rais ni muadilifu. Kuna mwingine hivi majuzi alikuwa anajifanya mzalendo, matokeo yake imekutwa account huko China.
Huyu mama ni dhaifu hilo halina ubishi.

Hilo la china ni propaganda tu.

Rais anahubiria wala rushwa na waiba mali za umma, amekua mtume mwamposa?

Kwa nchi yenye watu wanaojielewa Samia hana sifa ya kua hata balozi wa nyumba kumi.

Ajabu ndio rais, ndio maana haya yanatokea, sasa acha ahubirie wezi kwa miaka 7 ijayo kama hii nchi itakuwepo.
 
Kwa kauli hiyo ni kama Rais amesha surrender kwa wezi, sasa ameamua kuwapa maneno ya upole ili waingiwe na huruma waache kuiba.

Hataki kutumia sheria zilizopo kuagiza vyombo vya usalama viwakamate wahusika wahojiwe, na hatua kali zichukuliwe dhidi yao.

Kwa kauli hiyo, sasa ni rasmi Rais anawalinda au kuwaogopa wezi.
Rais anaetegea watu kama Makamba ndio wamshauri unategemea atakua na sauti tena juu ya wizi.

Eti Rais anawaomba wezi waachie nafasi ama wezi warudishe pesa ama wasiibe eti hataenda nazo mbinguni, yeye mbinguni nani alimwambia ipo?

Rais sasa anategemea huruma za mafisadi na wezi wa mali za umma ili waache kuiba, huruma iwaingie waache kuiba, isipowaingia basi anawaambia hawataenda nazo mbinguni.

Hii nchi, tumioiga hatua mbili mbele za maendeleo, kidogo tunarudi nyuma hatua 9. Imekua ni mzunguko wa umasikini na ujinga usio isha.

Ngoja tuone kama wezi watatuhurumia waache kuiba.
 
Huyu mama ni dhaifu hilo halina ubishi.

Hilo la china ni propaganda tu.

Rais anahubiria wala rushwa na waiba mali za umma, amekua mtume mwamposa?

Kwa nchi yenye watu wanaojielewa Samia hana sifa ya kua hata balozi wa nyumba kumi.

Ajabu ndio rais, ndio maana haya yanatokea, sasa acha ahubirie wezi kwa miaka 7 ijayo kama hii nchi itakuwepo.
Wanaona aibu kusema huu ukweli, wanamtetea kwa visababu vyepesi tu.
 
Back
Top Bottom