Rais Samia, nani kakushauri kununua Treni zenye muundo mbovu namna hii?

Rais Samia, nani kakushauri kununua Treni zenye muundo mbovu namna hii?

Ni ukosefu wa fedha tu,pesa ingekuwepo angeshusha kitu cha muitaliano " PENDOLINO" ,mtu kula miguu na vichwa vya kuku si kupenda ni kukosa pesa ya kununua mapaja
 
Naona design nyingi kutoka kwa hawa jamaa, either picha/toleo lililotumika imekuwa special product kwa Afrika.
Screenshot_20210711_113132.jpg
 
hapa jamaa hata sielewi tatizo liko wapi, unacho lalamika ni uzuri wa treni au? Maana hizo mbona zinatuika nchi nyingi tu na hazina tatizo lolote. Kumbuka kuna treni za abiria pekee na kuna za abiria na mizigo.
 
Hapo ng'ombe akijichanganya sijui itakuwaje.....
Ngoma inakata kama kisu maana inakimbia kwa speed ya 350km/h mpaka 600km/h yani hapo kwa kweli hamtoona kitu zaidi ya masalia ya ng’ombe tu! Labda wawekee wavu pembeni mdudu asikatize
 
Ngoma inakata kama kisu maana inakimbia kwa speed ya 350km/h mpaka 600km/h yani hapo kwa kweli hamtoona kitu zaidi ya masalia ya ng’ombe tu! Labda wawekee wavu pembeni mdudu asikatize
Hiyo tuachane nayo kwanza tunusuru hawa ng'ombe wetu.....
 
Tatizo watu wanajifanya kujua kila kitu. Hii treni ya Hyundai ina viwango bora tofauti na Mtoa mada anavyosema na propaganda zake . Hyundai ni kampuni kubwa duniani . wangekuwa wanatengeneza India au Indonesia au Vietnam au Malaysia tungekuwa na Shaka .
Hio treni hapo chini ya ujerumani inafanana na hio ya Hyundai

1FFA4CB1-243E-42E3-AEE5-4B9DECA2AC0D.jpeg
 
Humu ndani watu wanavyongea utadhani wao wana drive ma ferrari na ma Bugatti...kumbe vi baby walker second hand...bora ht serikali inanunua brand new...[emoji1787][emoji1787]

kifupi ni kua serikali imenunua hizo treni kulingana uwezo wake ki fedha na uwezo wa reli yenyewe...huwezi kununua bullet train ya 350km/h ukaileta kwenye rail yetu ya 160km/h hio ni under utilization na matumizi mabaya ya fedha za umma.
But still train zetu zitakua bora kuliko za Majirani zetu.
 
Tuliahidiwa hivyo kuwa tutapata High speed trains. Hayati Magufuli na Mh Kadogosa wakati ule walikuwa wakiimba hivyo.
Hata mabasi ya mwendo kasi siyo ya mwendo kasi kweli. Watu mnataka bullet trains wakati hata reli yenyewe haikidhi vigezo vya bullet trains achilia mbali kuwa ni nchi chache zenye bullet trains.
 
Mkuu utamudu kununua treni toleo la kisasa inayoenda kwa supersonic speed iliyotengenezwa na majapan au mkorea? Je, kwa namna miundombinu yetu ya SGR ilivyojengwa inamudu kweli ku operate toleo la kisasa la hizi treni ambazo zinakwenda kasi ya ajabu. Nafikiri pamoja na ubora na kasi lazima wazingatie gharama au bei ya hizo treni, ili angalau kukidhi mahitaji. Huko mbeleni baada ya kukusanya pesa ya kutosha ndo unaweza kuingiza mdogo mdogo matoleo ya kisasa zaidi.......mwanzo mgumu.
Mkuu yani watu wanashangaza sasa, wanataka train ya bullet iwekwe kwenye kireli chetu, pia zile train technolojia yake ni ghali sana na ziko sehemu chache duniani. Hiyo train mimi naona nzuri sana na zinatumiaka sehemu kibao
 
Jikune pale mkono unaweza kufika! Sio unakimbilia kununua treni za bei kubwa wakati sehemu nyingi bado watoto wanakaa chini mashuleni, huduma ya maji na umeme bado shida. Kisha watu waseme Tanzania ina treni za kisasa Kupita nchi nyingi za Africa!!
 
Mkuu.zina nyuma.sasa unaposema hakuna nyuma ni kwamba dereva yuko mbele na nyuma ?.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ulaya hasa Ujerumani kuna baadhi ya Railway Station kama ya Munich au Frankfurt wanaziita Sackbahnhof, wakimaanisha kuwa Railway stations ambazo treni hazipiti moja kwa moja. Kwenye Stations kama hizi treni inaingia kwa mbele na kutokea kwa nyuma na kuendelea na safari. Mbele na nyuma kwote ni sawa.

Angalia hii clip utaelewa nini namaanisha. Usijali lugha. Wewe angalia mandhali yake tu.

 

Kusema kweli leo nimesikitika sana kuona aina ya muundo wa treni ambayo serikali yetu imeweka mkataba na kampuni ya Hyundai-Rotem ni treni zenye mwonekano wa ki-Hitler!

Mimi nilifikiri tunaondokana na treni zenye muundo wa kutisha za enzi za George and Robert Stephenson na kuingia kwenye era ya treni za umeme zenye kuburudisha macho kwa design kama za wenzetu wajerumani.

Mama samia Suluhu Hassan Rais wetu nani kakupa ushauri wa kutua saini ya makubaliano ya kununua treni za aina hiyo? Mimi sitaki kuamini na sikutegema kama aina ya treni ambazo zitatereza kwenye reli yetu zingekuwa na mwonekano huo kwenye hiyo picha ya taarifa tuliyoipata kwenye Website ya hiyo kampuni iliyo shinda zabuni ya Hyndai-Rotem. Mbona inatisha?

Nitashangaa sana kama upande mmoja tumejitahidi kutengeneza Stations nzuri, za kisasa na zenye mwonekano mzuri na wa kupendeza na kupata system yenye technology mpya, alafu leo tunaambiwa kuwa tunapata treni zenye vichwa na mabehewa ya enzi za Hitler? Ama kweli Tanzania tunawatu ambao kweli hawajui kwenda na na wakati. Watu wasiokuwa na test ya biashara. Mnategemea nani mtampata kwenye kwenye hayo ma-wreck yenu?

Mkurugenzi Kadogosa hii sio treni ambazo models zake mtangazaji wako Beni Mwanantala amekuwa akituonyesha kwenye maonyesho uwanja wa sabasaba kurasini.

That's awful! Are you really serious with this mkurugenzi?

Sasa naomba niambie kuna tofauti gani na SGR ya kenya kimwonekano? Inamaana mnatufanya sisi ni masokwe mpaka mnatuletea matakataka kama haya ambayo hakuna mtu anaye yataka?

Waziri wa Ujenzi na uchukuzi hivi ni sahihi kweli sisi watanzania mtusweke kwenye ma-wagon yanayo onekana kama treni za kusafirisha mizigo na wanyama kama haya ambayo hata hayavutii? Mmepewa bure nini? Ama ndiyo tuseme mmedhamiria nini kutuletea? Tuambieni?

Nilipokuwa kwenye jengo lenu la maonyesho ya sabasaba mwaka jana na kujionea mwenyewe models za treni na mabehewa ambayo Mr. Mwanantala alitupa maelezo yake, aisee, nilifarijika sana sana moyoni na niliwaombea baraka nyingi kwa muumba wetu za kuwaongoza vizuri katika shughuli zenu za kuwatumikia Watanzania.

Sikutegemea kabisa kuwa leo ingekuwa siku ya majonzi makubwa kwa kuona au kusikia mashine zitakazo tereza kwenye reli yetu ya kisasa ya SGR kumbe ni madudu ambayo yamepitwa na wakati na yasiyo na mvuto hata lidogo. ES IST SCHRECKLICH!


Unamlaumu mama bure mzigo umechaguliwa Msoga
 
Back
Top Bottom