Rais Samia: Nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?

Rais Samia: Nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?

Jinsia yake haihusiki. Dini yake haihusiki. Sehemu ya Kijiografia anayotokea nayo haihusiki.

Kinachohusika hapa ni uwezo wake mdogo alionao.

Uwezo mdogo wa kiuongozi. Uwezo mdogo wa kuchanganua mambo. Na uwezo mdogo wa kujenga hoja.

Mara kadhaa sasa nimeona ona humu baadhi ya watu wakisema kwamba Rais Samia kaonyesha na kuthibitisha kuwa wanawake hawafai katika nafasi kiuongozi.

Mimi hilo nalikataa. Mtu mmoja mwenye uwezo mdogo si mwakilishi wa wanawake wote nchini wala duniani, kwa ujumla.

Uwezo wake mdogo alionao ni wa kwake yeye tu, Rais Samia.

Kilichonisukuma kuileta hii mada hapa ni yale maoni yake aliyoyatoa hapo jana.


View: https://youtu.be/O8SVrOeYtck?si=zAtsS1VP_q_B5Hmo

Rais anahoji kuwa kwani katiba ndo inaleta maendeleo?

Hivi huyu Rais hajui kuwa katiba ya nchi ndo framework ya uongozi na utawala ulio bora?

Bila uongozi na utawala ulio bora, kuna maendeleo gani yaliyo ya maana yanayoweza kupatikana?

Huo ni uwezo mdogo sana wa kufikiri ambao siutegemei utoke kwa kiongozi aliye wa juu kabisa nchini.

Au labda yeye anadhani maendeleo yanatoka wapi au yanakujaje?

Jingine la ajabu alilolizungumzia ni suala la elimu. Kwamba eti watu walio wengi hawajui hata katiba ni kitu gani. Hivyo ni lazima kwanza watu wapewe elimu kabla ya kuiandika hiyo katiba mpya.

Nilichoking’amua hapo ni ‘projection’ yake yeye kuhusu katiba.

Kulingana na kauli zake kuhusu katiba, nadhani yeye ndo hajui katiba ni kitu gani na hivyo anadhani hata wengine nao hawajui katiba ni nini!

Kenya waliandika katiba mpya mwaka 2010 [kama sijakosea].

Afrika Kusini waliandika katiba mpya baada ya kuachana na sheria za ubaguzi wa rangi kwenye miaka ya 90.

Marekani waliandika katiba yao miaka zaidi ya 200 iliyopita na ambayo wameifanyia marekebisho mara 27.

Sehemu nyingi tu duniani zimeandika katiba mpya na zingine kuzifanyia marekebisho katiba zilizopo.

Ni wapi ambako waliielimisha jamii kwanza kabla ya kuandika mpya?

Afrika Kusini walifanya elimu gani kwa wananchi kabla ya kuandika katiba yao mpya?

Waliwakalisha watu madarasani na kuanza kuwafundisha somo la katiba?

Katiba iliyopo sasa hivi wakati inaandikwa elimu ya katiba ilitolewa na nani? Lini? Wapi?

Naona sasa suala la kwamba wananchi hawana elimu ya katiba ndo litakuwa ‘narrative’ ya CCM kukwepa kujadili hoja za katiba mpya.

Kwa nilichokisikia jana, ni dhahiri shahiri kwamba anayehitaji elimu ya kujua katiba ni nini, ni Rais Samia.

Samia hafai kuwa Rais. Alichaguliwa kuwa mgombea mwenza kwa sababu zingine na si kwa sababu alikuwa ni mtu mwenye uwezo unaofaa.

Tuna Rais bomu ambaye hafai kuwepo madarakani hata kwa sekunde moja.

Nadiriki kusema kuwa Samia ndo Rais bomu kushinda marais wote tuliowahi kuwa nao Tanzania.

Najuta sana watz wanisamehe sana niliwahi kumshauri kitu kuhusu kuandika katiba na yeye anatekeleza ushauri ule Aiseh!

"Mheshimiwa Rais kuliko kusitisha mchakato wa katiba mpya,bora uendeleze pole pole Ili usikosane nao"

Sikumbuki vizuri ile tittle lakini ilisomeka hivyo,nikimwambia apige siasa pole pole HADI 2025 aseme muda hautoshi hivyo tufanye uchaguzi KWA hii iliyopo kwa marekebisho FULANI halafu mbeleni tutaendeleza!

SASA naona anafanyia KAZI ushauri ule!SASA sijui wale jamaa wenye mamlaka watamvumilia!!?

Maana walisema kabisa kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 usubiri HADI katiba mpya !!

Hao hao wamesema operation inaanza ile iliyositishwa yaani "original plan is on" yaani ile ya FDR!

Ngoja tuone!
 
Kwa hiyo Rais Samia alitaka kusema nini?
Hakuna haja ya kuwa na vitabu vitakatifu au katiba?
Hata tukiwa na hivyo vitabu bado hatupaswi kuvifuata?

Kuna vitu mtu mwenye heshima au mamlaka hupaswi kuvisema mbele za watu, maana ukivisema watu watagundua ujinga ulionao.
Huyu maza Kizimkazi hana akili
 
Rais Samia amesema "Viongozi wa Kisiasa tunadhani tuna Haki ya kuburuza watu tunawageuza watu Makasuku, nenda kamuulize kifungu gani cha Katiba kinakuudhi, hajui sasa Katiba mpya ilete nini anakujibu Maendeleo tu, nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Kama kuheshimu Vitabu tungeheshimu Vitabu Vitakatifu, mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?"

Source: East Africa TV

Nimependa huu Ujumbe na utakuwa ndio Ujumbe bora wa mwezi September!
Kunwakati anajitoa ufahamu kama c katiba angekwepo alipo
 
Rais yuko sahihi kbs, amesema kinachohitajika si karatasi but the political will za viongozi. Kwamba pamoja na CDM kuwa na katiba nzuri lkn mbowe kabakia kuwa kiongozi wa milele yote.
 
Rais Samia amesema "Viongozi wa Kisiasa tunadhani tuna Haki ya kuburuza watu tunawageuza watu Makasuku, nenda kamuulize kifungu gani cha Katiba kinakuudhi, hajui sasa Katiba mpya ilete nini anakujibu Maendeleo tu, nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Kama kuheshimu Vitabu tungeheshimu Vitabu Vitakatifu, mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?"

Source: East Africa TV

Nimependa huu Ujumbe na utakuwa ndio Ujumbe bora wa mwezi September!
Kama hakina umhimu basi na hiki tuachane nacho! Mbona teuzi mnatumia kanuni za kitabu mnachoona hakina maana sana ktk shughuli za kitafa?
 
Rais Samia amesema "Viongozi wa Kisiasa tunadhani tuna Haki ya kuburuza watu tunawageuza watu Makasuku, nenda kamuulize kifungu gani cha Katiba kinakuudhi, hajui sasa Katiba mpya ilete nini anakujibu Maendeleo tu, nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Kama kuheshimu Vitabu tungeheshimu Vitabu Vitakatifu, mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?"

Source: East Africa TV

Nimependa huu Ujumbe na utakuwa ndio Ujumbe bora wa mwezi September!
Hapo samia yuko sawa kwani inaelekea wapinzani wanapewa agenda na nchi za magharibi kuyumbisha nchi zetu tu kwa faida yao.
 
Rais Samia amesema "Viongozi wa Kisiasa tunadhani tuna Haki ya kuburuza watu tunawageuza watu Makasuku, nenda kamuulize kifungu gani cha Katiba kinakuudhi, hajui sasa Katiba mpya ilete nini anakujibu Maendeleo tu, nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Kama kuheshimu Vitabu tungeheshimu Vitabu Vitakatifu, mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?"

Source: East Africa TV

Nimependa huu Ujumbe na utakuwa ndio Ujumbe bora wa mwezi September!
Hana jipya huyo. WADANGANYIKA tumeibiwa bandari, wanyama kwenda zenji, hela za misaada kugawana pasu Kwa pasu wakati zenji na pemba ni kama ka wilaya tu, wabunge wao kulipwa mara 2, ardhi yao kwetu NO NO. Yaani kunyonywa, kuibiwa, kuburuzwa mtindo mmoja! Bila kusahau wakina Masai kunyang'anywa ardhi na kupewa waarabu!
Wacha niamie Burundi aisee..
🤬😤😡😠👺
 
Najuta sana watz wanisamehe sana niliwahi kumshauri kitu kuhusu kuandika katiba na yeye anatekeleza ushauri ule Aiseh!

"Mheshimiwa Rais kuliko kusitisha mchakato wa katiba mpya,bora uendeleze pole pole Ili usikosane nao"

Sikumbuki vizuri ile tittle lakini ilisomeka hivyo,nikimwambia apige siasa pole pole HADI 2025 aseme muda hautoshi hivyo tufanye uchaguzi KWA hii iliyopo kwa marekebisho FULANI halafu mbeleni tutaendeleza!

SASA naona anafanyia KAZI ushauri ule!SASA sijui wale jamaa wenye mamlaka watamvumilia!!?

Maana walisema kabisa kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 usubiri HADI katiba mpya !!

Hao hao wamesema operation inaanza ile iliyositishwa yaani "original plan is on" yaani ile ya FDR!

Ngoja tuone!
Anasema kitabu hakina maana ila waliotaka asipewe uraisi kioindi kile alilia kilio hadi nje kilisikika kuwa kitabu kinakiukwa. Mpaka akamtaja pm kwa jina lake kuwa walitaka awe raisi wa mpito wakati katiba haisemi hivyo. Leo kaingi pale juu mara kawa mjuaji na machino!! Kweli madaraka ni ulevi kuliko bangi.
 
Huwa nasema siku zote maendeleo yanaletwa na kiongozi mwenye maono na mwenye kujua nini anafanya. JPM alikuja kuumbua sana watu, kwa katiba hii hii tunayosema mbovu alifanya mambo mazito yaliyowashinda wengine tena ndani ya muda mfupi. Alikomesha ujambazi, wezi na mafisadi. Alianzisha miradi mikubwa na kuitekeleza kwa kasi ya 4G. Wananchi wa kawaida wao hawana shida na katiba mpya watu wanataka kiongozi bora atayowatumikia wao na sio kuitumikia katiba. Hivyo vyama vihakikishe vinatuchagulia viongozi wenye sifa na uchungu na nchi wenye kusimamia ukweli kama alivyokuwa JPM.
 
Back
Top Bottom