Rais Samia ni kiongozi pekee mpaka sasa aliyefanikiwa kupata uungwaji mkono na kukubalika na makundi yote na vyama vyote

Rais Samia ni kiongozi pekee mpaka sasa aliyefanikiwa kupata uungwaji mkono na kukubalika na makundi yote na vyama vyote

Ndugu zangu Ni historia ambayo Rais Samia amejiandikia na kujiwekea kwa kufanikiwa kupata uungwaji na kukubalika na makundi yote na vyama vyote, hii Ni kutokana na Imani kubwa ambayo watu wamejenga na kuwa Nayo juu ya Rais Samia,

Hakuna mtu au kundi ambalo Ni tishio katika uongozi wa Rais Samia, kwa kuwa watu wote na makundi yote Yana matumaini na Imani na Rais Samia kuhusu madai yao, vyama vya siasa vina matumaini na Imani na Rais Samia Ndio sababu unaona vikiwa tayari kukaa Naye katika meza ya mazungumzo na hata kupanda jukwaa moja na Rais Samia Kama tulivyoona katika ziara yake ambayo wapinzani wamejitokeza kumuunga mkono mh Rais na kuhubiri habari za maendeleo na umoja wa kitaifa na kutanguliza mbele maslahi ya kitaifa

Hali hii imeleta umoja wa kitaifa na kuleta mshikamano na Sasa tunabishana na kupambana kwa hoja tu ya namna ya kuijenga nchi yetu na njia za kupita kupata maendeleo, hii Ni kutokana na kuwa nais Samia Ni mama mwenye dhamira njema na mwaminifu Sana katika kauli zake, Ni mama na kiongozi anayezungumza kilicho katika moyo na kifua chake.

Rais Samia ameonyesha kuwa na dhamira njema katika kulitumikia Taifa hili, Ni kiongozi ambaye ameonyesha kuumizwa Sana na matatizo ya watu, Ni kiongozi anayetamani kila Siku Taifa letu linakuwa kiuchumi na watanzania tunaondokana na Hali ya umaskini na kwamba kila Siku watanzania tunafanikiwa kupata Milo mitatu mezani petu,

Kila mtanzania anamatumaini kuwa kesho yake itakuwa njema na kila mtu anajiona kuwa anaweza pata fursa ya kiuchumi bila kujarisha Hali yake.

Serikali ya Rais Samia imejikita katika kusaidia watu na siyo kuwaumiza watu, serikali ya mama Samia imejikita katika kumtafutia mtanzania fursa za kiuchumi na siyo kuwa kizuizi katika fursa za kiuchumi, Rais Samia amejikita katika kuona kila siku watanzania tunaaamka na kupata Tabasamu jipya na siyo kuishi kwa kukosa matumaini.

Rais Samia anataka kuona kuwa kila mtu anafaidika na jasho lake na juhudi zake katika kujitafutia na kujikwamua kiuchumi, ndio sababu anajitahidi kuweka mazingira mazuri ya kumuwezesha kila mtu mahali anapojishughulisha na kazi anafaidika na kuinuka kiuchumi kupitia mikono yake na ubunifu wake

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
Malizia kusifu then usiku utarudi kwenye nyumba ya babako ya tembe kulala
 
Wanaosimamia ni wajibu wao maana wanalipwa mshahara kutokana na malipo tuyafanyayo sisi watumiaji. Inapaswa wao ndio watupongeze sisi maana wao hata kodi hawalipi, na wanatumia huduma zote za serikali bure.
UNafikiri walioanzisha hata tuzo walikuwa wajinga?
Maisha yalivyo magumu mtaani,Yan ww unaweza kupata ujasiri wa kusifia?
Nampongeza kwa kuwa juhudi za mh Rais Samia zinaonekana kabisa katika kuimarisha uchumi wetu, kwani nchi gani wanakoishi maisha ya starehe Kama wapo paradiso?
 
Inawezakuwa kweli sababu nilimuona zito Jana wenzake wametulia wanaskiliza kwa makini yeye anatingisha kichwa kama vile anaitikia mudawote kuashiria anaelewa haswaaaaa kilaneno.
 
Inawezakuwa kweli sababu nilimuona zito Jana wenzake wametulia wanaskiliza kwa makini yeye anatingisha kichwa kama vile anaitikia mudawote kuashiria anaelewa haswaaaaa kilaneno.
Ni sahihi kabisa maana Rais Samia anaeleweka vizuri maneno ayatoayo yaliyojaa uzalendo na upendo mkubwa Sana kwa Tanzania na watanzania
 
Naona siasa zile zile za Magu zimerudi kwa nguvu Chawa bana mmekosa kazi, Mwacheni Rais achape kazi mkitaka kujua anakubalika fanyeni fare election akipita kweli hicho kitakuwa kigezo mahususi cha kupima kukubalika kwake. Do not just give sweeping statements.
 
Kumbe ulianza zamani kusifia upumbavu na bado mpaka leo hujala shavu la uteuzi hata la kuwa mtendaji wa kata!!!! Laana ya kusifia ujinga itaendelea kukuandama hadi kwa vizazi vyako,hujui hii serikali inavyowaumiza watanzania.watu wamefunga biashara zinazotegemea umeme kwa sababu ya kuleta undugu kwenye serikali mmemkabidhi wizara mwizi anatuhenyesha raia
 
Kumbe ulianza zamani kusifia upumbavu na bado mpaka leo hujala shavu la uteuzi hata la kuwa mtendaji wa kata!!!! Laana ya kusifia ujinga itaendelea kukuandama hadi kwa vizazi vyako,hujui hii serikali inavyowaumiza watanzania.watu wamefunga biashara zinazotegemea umeme kwa sababu ya kuleta undugu kwenye serikali mmemkabidhi wizara mwizi anatuhenyesha raia
Kwani wapi nimeandika uteuzi
 
Back
Top Bottom