Rais Samia: Nimebuni na kubeba Mradi wa matumizi ya Nishati Safi Afrika, aweka Lengo la asilimia 80% ya Watanzania watumie Nishati Safi Kufikia 2030

Rais Samia: Nimebuni na kubeba Mradi wa matumizi ya Nishati Safi Afrika, aweka Lengo la asilimia 80% ya Watanzania watumie Nishati Safi Kufikia 2030

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Rais Samia amefurahishwa na kuendelea kuhimiza jamii ya Watanzania Kuunga mkono juhudi alizozianzisha za Matumizi ya Nishati Safi.

Akizungumza huko Namtumbo wakati wa uzinduzi wa Shule ya Sekondari ya Samia,amesema alibuni mradi huo baada ya kuona wanawake wanapata upofu na vifo kutokana na matumizi ya Kuni na mkaa.

Aidha anasema Mpango huo inalenga Kuokoa amazingira. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais Samia amesema malengo ya serikali ni kuona asilimia 80 ya wananchi wawe wakitumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2030, miaka takribani sita ijayo.

Ili kufikia malengo hayo, Rais Samia amesema wameanza na taasisi za elimu pamoja na taasisi nyingine kubwa kubwa (kama magereza) kutumia nishati safi ya kupikia na baadaye itaenea kwingine.

Swali.
Hivi Kuna Rais mwingine yeyote waTanzania Baada ya Nyerere ambae amewahi buni programu ikawa ajenda ya Afrika.?

Snapinsta.app_461434830_527817299853036_968695043382168581_n_1080.jpg

Hongera Rais Samia Kwa Maono Yako mema.Mnaweza kusoma hapa pia Rais Samia afanikisha kupatikana Kwa TSHS.Trilioni 6 za Nishati ya Kupikia. Rais wa Benki ya AfDB Asema ni Kiongozi wa Mfano

Soma zaidi hapa Rais Samia kuwa Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano wa Kimataifa Kujadili Nishati Safi utakaofanyika Ufaransa

---
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.Dkt. Doto Biteko amesema Serikali inafanya kila jitihada kuhakikisha kunakuwa na unafuu katika upatikanaji wa bidhaa za Nishati Safi ya kupikia ili kumwezesha kila mwananchi kutumia nishati iliyo safi na salama.

Dkt. Biteko amesema hayo tarehe 13 Septemba 2024 Jijini Dodoma wakati wa hafla ya Kusaini mikataba ya ushirikiano ya utekelezaji wa Nishati Safi ya Kupikia yenye thamani ya shilingi bilioni 50.98 kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Jeshi la Magereza, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Wasambazaji wa Gesi ya kupikia, hafla ambayo ilienda sambamba na uzinduzi wa jengo la REA.

“Namshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake yanayowezesha Sekta ya Nishati kuendeshwa kwa mafanikio ambayo yamepelekea leo hii tushuhudie hatua ikizidi kupigwa katika kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia unaolenga kuokoa maisha ya watanzania na pia kuiwezesha Wizara ya Nishati kutatua changamoto zinazojitokeza lengo likiwa ni kutoa huduma iliyo bora kwa wananchi," amesema Dkt. Biteko

Akizungumzia usambazaji wa nishati vijijini ikiwemo umeme, Dkt. Biteko ameipongeza Bodi na Menejimenti ya REA kwa kusimamia ipasavyo miradi na kwa kuwahimiza wakandarasi kukamilisha kazi kwa wakati.

"Nawapongeza sana Bodi ya REA; mnafanya kazi nzuri, nimekuwa nikiwaona mara kwa mara mkiwa vijijini mnahimiza Wakandarasi," alipongeza.

Akizungumzia jengo la REA alilolizindua, Dkt.Biteko amesema litawawezesha watumishi kutoa huduma kwa wananchi na kuwapongeza REA kwa kujenga jengo hilo la kisasa lenye ghorofa tano kwa gharama ya shilingi bilioni 9.8 kwa miezi 18 badala ya shilingi bilioni 13 zilizopangwa awali.

View: https://www.instagram.com/p/DAbgS54NtFi/?igsh=MTJxcTJic2lhOGRzbQ==
 
Tatizo bei za nishati ziko juu mno, hivyo utekelezekaji wa mpango huo kwa mwananchi asiyejua kesho anakula nini ni mgumu.

Mfano ingekuwa umeme ukinunua wa shilingi 1000/= unapata units 20 na mtungi mdogo wa gas unajazwa kwa Tsh 5,000/=, hapo malengo yangetimia.
 
Aisee Kwamba Clean Energy ni Brain Child yake ? Okay hilo ni moja...

Mbili tunapoelekea kwa taarifa yako sipo kabisa Tunatumia Pesa za kutosha na kupiga propaganda kwenye Nishati ambayo inajumlisha LPG kwangu mimi hii athari yake ni kubwa kwa kutumia pesa zetu kuagiza wakati Nishati safi kuliko zote tunayo Tanzania na kulingana na vyanzo vyetu itakuwa gharama nafuu....


Lakini matokeo yake tunawekeza huku pengine kwa kutumia matrilioni ya pesa eti kwenye uhamishaji
 
Tatizo bei za nishati ziko juu mno, hivyo utekelezekaji wa mpango huo kwa mwananchi asiyejua kesho anakula nini ni mgumu.

Mfano ingekuwa umeme ukinunua wa shilingi 1000/= unapata units 20 na mtungi mdogo wa gas unajazwa kwa Tsh 5,000/=, hapo malengo yangetimia.
Ruzuku imewekwa Kwa Sasa mitungi itapatikana Kwa nusu ya bei
 
Aisee Kwamba Clean Energy ni Brain Child yake ? Okay hilo ni moja...

Mbili tunapoelekea kwa taarifa yako sipo kabisa Tunatumia Pesa za kutosha na kupiga propaganda kwenye Nishati ambayo inajumlisha LPG kwangu mimi hii athari yake ni kubwa kwa kutumia pesa zetu kuagiza wakati Nishati safi kuliko zote tunayo Tanzania na kulingana na vyanzo vyetu itakuwa gharama nafuu....


Lakini matokeo yake tunawekeza huku pengine kwa kutumia matrilioni ya pesa eti kwenye uhamishaji
Weka input kwenye sera sio kupinga Kila kitu
 
Weka input kwenye sera sio kupinga Kila kitu







 
Ruzuku imewekwa Kwa Sasa mitungi itapatikana Kwa nusu ya bei
Kwahio unaona ni akili kutumia pesa zetu (kodi) ili kuwalipa pesa wachuuzi (pesa ambayo mwisho wa siku inakwenda nje ya nchi) kuliko kutumia pesa hio kuimarisha na kuhakikisha miundombinu ya nchini inakuwa up to standard na kuweza kupunguza operating costs ambayo inaweza kabisa kuhakikisha hata unit moja inakuwa Tshs 20/=
 
Kwahio unaona ni akili kutumia pesa zetu (kodi) ili kuwalipa pesa wachuuzi (pesa ambayo mwisho wa siku inakwenda nje ya nchi) kuliko kutumia pesa hio kuimarisha na kuhakikisha miundombinu ya nchini inakuwa up to standard na kuweza kupunguza operating costs ambayo inaweza kabisa kuhakikisha hata unit moja inakuwa Tshs 20/=
Ndio ni sawa kabisa kwani hiyo ruzuku inawekwa Ili nani anufaike? Wakati bei za Mafuta zimepaa Serikali ikiweka ruzuku mbona hukuongea hizi pumba?

Wakulima wanapata ruzuku za pembejeo mbona hupingi?
 
Rais Samia amefurahishwa na kuendelea kuhimiza jamii ya Watanzania Kuunga mkono juhudi alizozianzisha za Matumizi ya Nishati Safi.

Akizungumza huko Namtumbo wakati wa uzinduzi wa Shule ya Sekondari ya Samia,amesema alibuni mradi huo baada ya kuona wanawake wanapata upofu na vifo kutokana na matumizi ya Kuni na mkaa.

Aidha anasema Mpango huo inalenga Kuokoa amazingira. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais Samia amesema malengo ya serikali ni kuona asilimia 80 ya wananchi wawe wakitumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2030, miaka takribani sita ijayo.

Ili kufikia malengo hayo, Rais Samia amesema wameanza na taasisi za elimu pamoja na taasisi nyingine kubwa kubwa (kama magereza) kutumia nishati safi ya kupikia na baadaye itaenea kwingine.

Swali.
Hivi Kuna Rais mwingine yeyote waTanzania Baada ya Nyerere ambae amewahi buni programu ikawa ajenda ya Afrika.?


Hongera Rais Samia Kwa Maono Yako mema.👇👇

View: https://www.instagram.com/p/C_3Fcartw6K/?igsh=dTlqeDRvaTdxOHhq

Total crap, anabuni mradi, ye ye ni engineer,? Ni mtaalamu wa nishati? What a small mind this prezzoo has!
 
Weka input kwenye sera sio kupinga Kila kitu
Kwa hili la Kusukuma Nishati Safi ya Kupikia kama Agenda Yake ya Kitaifa na kimataifa, tumpe Maua yake. Amedhamiria kwa Moyo wake wote labda kama ataangushwa na watendaji wake. Kwa hili tumuunge mkono afanikishe agenda yake hii. It could be one her few Legacy to be remembered with . Keep it up !
 
Ndio ni sawa kabisa kwani hiyo ruzuku inawekwa Ili nani anufaike?
Aisee naomba uvute pumzi kidogo alafu uangalie mambo kwa umoja wake na sio kwa mafungu..., Swali hivi unajua pesa ya ruzuku inatoka wapi ? Kwa taarifa yako Pesa inatoka kwa mwananchi huyo huyo either through kodi directly au kwa mikopo ambayo mwananchi huyu itabidi alipe..., kwahio ruzuku inabidi iwekwe sehemu ili kuchochea mambo au kusaidia kitu ambacho faida yake ni kubwa kuliko hata pesa (HUDUMA) Kwahio ukichukua Kodi nyingi kwa watu ili baadae uwape ruzuku ni kama unachukua mfuko wa surualia ili uweke mfuko wa shati wakati pesa ni zako...; Ingawa kwenye hili unachukua mfuko wa suruali alafu unampa jirani yako ili akupe kitu ambacho wewe unacho
Wakati bei za Mafuta zimepaa Serikali ikiweka ruzuku mbona hukuongea hizi pumba?
Wewe una Petroli nchini ? By the way kwenye Petroli wakitoa matozo yao na makodi bei itakuwa sio hii iliyopo sasa, na mimi nakwambia tuna alternative nchini ya kuweza hata kuuza nishati kwanini tununue LPG kutoka nje kwa kodi zetu ?
Wakulima wanapata ruzuku za pembejeo mbona hupingi?
Kwahio wasipewe ruzuku ya pembejeo ili washindwe kulima na chakula tuagize nje kama tunavyofanya LPG ambayo ikija tunatumia kodi zetu kama ruzuku eti ili ionekane bei ni ndogo ?
 
Kwa hili la Kusukuma Nishati Safi ya Kupikia kama Agenda Yake ya Kitaifa na kimataifa, tumpe Mau yake. Amedhamiria kwa Moyo wake wote labda kama ataangushwa na watendaji wake. Kwa hili tumuunge mkono afanikishe agenda yake hii. It could be one her few Legacy to be remembered with . Keep it up !
Hivi nimepinga kwamba Nishati safi ni Mbaya (dunia nzima kutokana na tabia nchi hii ndio ajenda ndio maana hata sisi tumepata pesa nyingi sana za msaada ili kufanikisha hili) Sasa swali langu lipo kwenye kufanikisha...

Je tunatumia pesa zetu na za mikopo ili kuendelea kunufaisha madalali na nchi za nje katika LPG au tutumie vyanzo vyetu ambavyo tunavyo na watu wanaweza kutumia kupikia kwa bei ndogo ambayo haiwezi kwamwe kupunguzwa kwenye LPG (Umeme tunazalisha na LPG tunanunua)
 
Hivi nimepinga kwamba Nishati safi ni Mbaya (dunia nzima kutokana na tabia nchi hii ndio ajenda ndio maana hata sisi tumepata pesa nyingi sana za msaada ili kufanikisha hili) Sasa swali langu lipo kwenye kufanikisha...

Je tunatumia pesa zetu na za mikopo ili kuendelea kunufaisha madalali na nchi za nje katika LPG au tutumie vyanzo vyetu ambavyo tunavyo na watu wanaweza kutumia kupikia kwa bei ndogo ambayo haiwezi kwamwe kupunguzwa kwenye LPG (Umeme tunazalisha na LPG tunanunua)
Nadhani nenda kafanye hesabu gharama za umeme bado ziko juu sana kama nishati ya kupikia kulinganisha na LPG ambayo hata kama tunainunua kutoka nje. Pia kumbuka umeme haujafika sehemu nyingine za nhci hii na hata ulikofika bado gharama zake nu kubwa katika kupikia compared to LPG. LNG or even other forms of Clean cooking solutions such as Fuel briquettes etc. Hakuna nchi duniani inajitosheleza 100% kwa bidhaa zinazotumika ndani mwake. Ulisomea uchumu kidogo ujikumbushe kuhusu the Comparative Advantage principle? So usiumie roho kuona tunafanya trade na nchi nyingine kwa bidhaa ambazo hatuzalishi, na sisi kuna bidhaa tunazalisha lakini hatuzitu,mii sisi, bali tunawapelekea wengine. Uwe na amani .
 
Aisee naomba uvute pumzi kidogo alafu uangalie mambo kwa umoja wake na sio kwa mafungu..., Swali hivi unajua pesa ya ruzuku inatoka wapi ? Kwa taarifa yako Pesa inatoka kwa mwananchi huyo huyo either through kodi directly au kwa mikopo ambayo mwananchi huyu itabidi alipe..., kwahio ruzuku inabidi iwekwe sehemu ili kuchochea mambo au kusaidia kitu ambacho faida yake ni kubwa kuliko hata pesa (HUDUMA) Kwahio ukichukua Kodi nyingi kwa watu ili baadae uwape ruzuku ni kama unachukua mfuko wa surualia ili uweke mfuko wa shati wakati pesa ni zako...; Ingawa kwenye hili unachukua mfuko wa suruali alafu unampa jirani yako ili akupe kitu ambacho wewe unacho

Wewe una Petroli nchini ? By the way kwenye Petroli wakitoa matozo yao na makodi bei itakuwa sio hii iliyopo sasa, na mimi nakwambia tuna alternative nchini ya kuweza hata kuuza nishati kwanini tununue LPG kutoka nje kwa kodi zetu ?

Kwahio wasipewe ruzuku ya pembejeo ili washindwe kulipa na chakula tuagize nje kama tunavyofanya LPG ambayo ikija tunatumia kodi zetu kama ruzuku eti ili ionekane bei ni ndogo ?
Kwani ruzuku kwenye Nishati safi Haina faida kubwa Kwa jamii na mazingira? Kwani faida ni za kimazingira tuu?

LPG Kwa Sasa tunaagiza Nje so ruzuku lazima
 
Hivi nimepinga kwamba Nishati safi ni Mbaya (dunia nzima kutokana na tabia nchi hii ndio ajenda ndio maana hata sisi tumepata pesa nyingi sana za msaada ili kufanikisha hili) Sasa swali langu lipo kwenye kufanikisha...

Je tunatumia pesa zetu na za mikopo ili kuendelea kunufaisha madalali na nchi za nje katika LPG au tutumie vyanzo vyetu ambavyo tunavyo na watu wanaweza kutumia kupikia kwa bei ndogo ambayo haiwezi kwamwe kupunguzwa kwenye LPG (Umeme tunazalisha na LPG tunanunua)
Pesa ipi ya mikopo inayonufaisha madalali? Kwa nini usiseme inatunugaisha sisi Wananchi tutakaokuwa tunanunua Kwa bei chee?
 
Back
Top Bottom