Rais Samia: Nimebuni na kubeba Mradi wa matumizi ya Nishati Safi Afrika, aweka Lengo la asilimia 80% ya Watanzania watumie Nishati Safi Kufikia 2030

Rais Samia: Nimebuni na kubeba Mradi wa matumizi ya Nishati Safi Afrika, aweka Lengo la asilimia 80% ya Watanzania watumie Nishati Safi Kufikia 2030

Ngoja nikupe mfano kidogo ili twende sawa... Hiki kinachofanyika sasa, tumepewa mikopo na pesa lukuki ili tuhakikishe tunaingia kwenye Nishati safi... Ni sawasawa wewe unapewa pesa za urithi na nyingine unaende kukopa ili uweze kujitosheleza na vitumbua...., Sasa wewe unachofanya ni kutumia pesa hizo na kununua vitumbua kwa jirani.., wakati ungeweza kutumia pesa hizo kununua kikaango chako mwenyewe na kuhakikisha kuanzia leo na mpaka wajukuu zako mtakuwa mnajitosheleza kwa vitumbua bila kutegemea jirani kama amepika au hajapika

Sio kwa sasa tu LPG tutaendelea kuagiza sababu hatuzalishi Liquid Petroleum Gas..., ila sio lazima tuagize sababu tungeweza kutumia vyanzo vyetu kuongeza capacity ya UMEME na kuhakikisha watu wanatumia vifaa vya umeme ambavyo ni efficient na vinazidi kuwa energy efficient kila kukicha bora hio ruzuku iwekwe kwenye vifaa vya umeme mara baada ya kushusha umeme (after all BWAWA tu la Nyerere capacity itakuwa double yailiopo sasa)
Kafanye cost analysis ya matumizi ya umeme katika kupikia vs LPG utapata jibu. Hata huko kwa wakubwa wenu kule ambako per unit cost ya umeme ni ndogo wanakozalisha umeme mwingi na cheap wa Nuclear still wan opt to imported LPG as the cheapest clean cooking solution available to market. Umeme unaouongela wa hapa kwenu Bongo kuja kuwa cheap enough for use in cooking it will not be feasible technically and financially. So LPG an the likes will remain our most feasible option for the Tanzania market environment.
 
Mambo mengine serikali huwa inaongea as if haina watu wa kutizama mambo haya kwa kina..aliyebuni modal ya kufunga mita kwenye mitungi ya gas na kutumia kwa kununua kidogo kidogo ni mtanzania, alizungushwa zungushwa hapa nchi wanaofahamu thamani ya kuwa na watu wa aina hii wakachukua wazo lake likafanyiwa utafiti likakubalika na zipo nchi zinatumia gas ya kupikia kwa mfumo wa kununu kulingana na hela yako kama ilivyo kwa umeme..
Hii ajenda ya nishati safi ni wazo zuri, sielewi kitu gani kinakwamisha serikali au huyo anayetangaza kila siku kufanya pilot project kwenye baadhi ya wilaya na kata zenye changamoto kubwa ya mazingira ili kupima adoption rate na affordability..ni hela kidogo sana! ili hata huko anakoenda kuwahamasisha awaambie tayari kuna pilot project zinafanyika kwenye maeneo kadhaa waone hiyo seriousness kwa jambo hili kwanza kwake mwenyewe! unakwendaje kumwambia mtu akusupport huna hata cha kumuonyesha ulichofanya??? hivi lini tutajifunza kufanya wajibu wetu kabla ya kualika wengine tusaidiane nao??? kaenda cop 2023 na maneno tu, kaenda ufaransa na maneno tena..r ou serious???
Halafu nini kinakwamisha serikali isianze mradi kuweka bomba ya gas kuja dodoma?? hao TPDC hela za kutafiti mafuta ambayo wala hawana uhakika kama yapo wanazo, ila za kuanza mradi kuweka bomba ya gas kuja dodoma hawana, r these people serious??TPDC kuendelea kutafiti wa mafuta Bonde la Eyasi Wembere | Nipashe unatafiti mafuta ya nini wakati gas tayari unayo??? unataka kukimbiza ndege wawili kwa gharama ya kumwachia huyu mmoja uliyemkamata, ni akili au matope???
Hii ajenda ni ubabaishaji tu kuombea hela watu wale, hakuna lolote!
Wewe kasome chimbuko la PAYGAS model and its technology, haijavumbuliwa hapa Tanzania wala haijaanzia hapa kwetu kutumika. Hapa TZ tumeifanyia Piloting test kwa kuanzia hapo Dar kwa mradi mdogo wa wateja wasiozidi 800 na kuoneysha it can work, na still kuna initiatives zinaendelea za scaling up of the same kwa baadhi ya maeneo mapya kwa kushirikisha wadau wengine. Hii PAYGAS imekuwepo before huko nchi nyingtine kama South Africa, Ghana , Kenya na kwingineko, na imeprove to be one of the options for the low income households who can not afford purchase of full unit Cylinders available in the market but can afford the pay as you use model and we many partners are working to scale it up.
 
Na mikataba imesainiwa,Rudi kusoma maelezo Juu Yana majibu ya haya unayouliza
Kutolewa mahari ndio umeoa/umeolewa? sijui akili yenu ina shida gani..tabia ya kusifia mambo hata kabla ya kuanza wakati mwingine ni dalili ya kuwa mjinga pasipo kujua ujinga ulio nao..shida ni ya watu wako, lakini mbio kualika watu wengine wafanye pasipo hata wewe mwenyewe kuanza kwanza! mentality km hii ni kutoelewa wajibu wako kwenye jambo husika, hata hicho unachotaka kufanya hakina future..sababu unadhani majibu ya shida zako wanayo wengine si wewe!
 
Wewe kasome chimbuko la PAYGAS model and its technology, haijavumbuliwa hapa Tanzania wala haijaanzia hapa kwetu kutumika. Hapa TZ tumeifanyia Piloting test kwa kuanzia hapo Dar kwa mradi mdogo wa wateja wasiozidi 800 na kuoneysha it can work, na still kuna initiatives zinaendelea za scaling up of the same kwa baadhi ya maeneo mapya kwa kushirikisha wadau wengine. Hii PAYGAS imekuwepo before huko nchi nyingtine kama South Africa, Ghana , Kenya na kwingineko, na imeprove to be one of the options for the low income households who can not afford purchase of full unit Cylinders available in the market but can afford the pay as you use model and we many partners are working to scale it up.
Scale it up..! this is business, toka mwaka jana wimbo ni ule ule, shida ni nini ya kuzunguka zunguka km vitu vyote vipo? lakini tunasoma bajeti ya serikali 2024/25 huoni haya mnasema..lini serikali inatekeleza miradi pasipo kutengea fedha zikapitishwa bungeni?
 
Kafanye cost analysis ya matumizi ya umeme katika kupikia vs LPG utapata jibu.
Sio tu kwamba nifanye analysis bali hili jambo nilishalidadavua...
Matumizi ya Umeme ni makubwa sababu mwananchi anauziwa unit kwa bei kubwa, jambo ambalo ukipunguza hio bei per unit itashuka..., juzi tu hapa walifungulia maji Kwenye Bwawa ili yasitumike (waste of energy) Tanzania ni a Tropic Country kuna Nishati ya Jua ya Kumwaga..., Kwahio kwa kutumia energy mix ya vyanzo vilivyopo ndani vitatosha wala bila kuhitaji kuagiza LPG kutoka nje pili kumbuka vyanzo vingine ni vya ndani hivyo pesa inazunguka LPG tunampa mwingine..., Na bado bei ya LPG ni kubwa ndio maana Serikali inataka kuchukua Kodi zetu tena ili kulipia hio LPG (kuwapa watu biashara) eti ili bei ipungue
Hata huko kwa wakubwa wenu kule ambako per unit cost ya umeme ni ndogo wanakozalisha umeme mwingi na cheap wa Nuclear still wan opt to imported LPG as the cheapest clean cooking solution available to market.
Hizo nchi unazoongelea zinatumia huko wanazi import kutoka wapi na kwa bei gani ? Kumbuka Europe sehemu nyingi wanatumia Piped Gas ambayo ni gesi asilia na kama ikiwa piped this is very cheap (ila huku hatuna miundombinu ya kufanya hivyo...) Unapoonglea cheapest cleaning cooking solution available to market unasema nini ? Yaani unaweza kuliganisha Electricity from Hydro na LPG from Petroleum na ambayo wala hauna unaagiza na unatoa ruzuku ili ionekane cheaper (ingawa bado watu wanashindwa kumudu ndio cheapest available to market). Yaani tukimaliza Bwawa la Nyerere ambapo capacity itakuwa double iliyopo sasa bado unasema uzalishaji utakuwa ni mdogo na wala tusifanye hivi tuagize LPG na kutumia kodi zetu kupunguzia mwananchi bei hio ndio Cheapest ?
Umeme unaouongela wa hapa kwenu Bongo kuja kuwa cheap enough for use in cooking it will not be feasible technically and financially.
Why ? Tena wewe nadhani umezaliwa Juzi ulizia wazee wako enzi zile taa ni 100watts (achana na hizi za sasa) watu walikuwa na taa mpaka nje na zinawaka usiku mzima. watu walikuwa na majiko ya umeme tena plate na coils achana na haya majiko ya sasa ambayo ni energy efficient kuliko hata gesi, watu walikuwa na ma oven na wanapikia kila siku..., watu shule walikuwa mpaka wana heaters za kujitengenezea za wembe (zinakula umeme balaa) ila waliweza kumudu (WHY) sababu per unit cost ilikuwa ndogo sio sasa hivi imekuwa kubwa kutokana na kwamba Tanesco wananunua kwa watu (madalali) hivyo kufanya biashara kichaa (kunufaisha wachache)
So LPG an the likes will remain our most feasible option for the Tanzania market environment.
Narudia tena unaongelea kitu hata ambacho huna (hauzalishi) kwamba ndio feasible wakati una vyanzo vyote vya kuzalisha nishati kuliko hata nchi nyingi duniani (alafu unaona ndio ujanja kutumia kila ambacho hauna)? Ukitaka kufanikiwa play according to your strength
 
Kafanye cost analysis ya matumizi ya umeme katika kupikia vs LPG utapata jibu.
Kuepuka kujirudia rudia kama santuri mbovu hii kitu nimeshaizungumzia kwenye uzi mwingine...


Kwa mahesabu ya haraka haraka kilo moja ya LPG ni kama 13.6 Kwh (yaani units 13.6) ule mtungi wa kwenye elfu 60 average tuseme una kilo 15 (ingawa sio 15 kuna uzito wa cylinder) kwahio mtungi huu una kama 13.6 x 15 = 204 Units

Kwahio tuseme kwa bei ya sasa ya mtungi inabidi unit moja iwe kwenye 294/= (60,000/= gawia 204)

Tukija kwenye ufanisi kama mtu atatumia induction cooker ambayo ni most efficient kulikio hata gesi.... (Kuna vyanzo vinasema zaidi ya mara tatu) utaona kwamba umeme unaweza ukawa Nishati Safi Kabisa ya kupikia na gharama ndogo kabisa...

Kwahio unaona hata tukishusha bei ya units mpaka 200/= ingawa mimi nasema inaweza kushuka hata mpata 20/ au hata kwa wengine bure by getting credit

 
Awareness ya nini km unajua watu hawana uwezo?
Halafu Awareness unafanyia Ufaransa wao wamekuambia wanataka awareness kwa tatizo lako?
Huo uwezo unaosema hawana nani anawalisha mwaka mzima? au unatamka tu kwa vile ni rahisi kutamka..una uhakika tatizo ni uwezo au uvivu na uzembe wa watu na viongozi kufikiri, kupanga na kutenda juu ya maisha yao wao wenyewe..aliyesimamia nchi ikaingia uchumi wa kati, chakula kikawepo kikatosha na kusaidia Malawi na Zimbabwe alileta watu wake kulimia watu mashamba yao?
Akili ya mtu anayewaza namna hii ni ya mtu masikini, omba omba, hana analojua juu ya leo na kesho anawaza km kifaranga cha kuku!
Mfano, una hakika miti ya mkaa wanaotumia dodoma leo baada ya miaka 10 ijayo bado itakuwepo? au kwako dunia inakwisha unapokufa wewe..
Umejibu kwa jazba sana, kwanza lengo la awareness ni kwa wale walio na uwezo lakini wanapuuzia matumizi ya nishati Safi sababu ya mazoea. Wasio na uwezo hawana namna hata ukiwapa awareness

Wasio na uwezo Nani anawalisha mwaka mzima? Hili swali ni la kipuuzi ambalo hukupaswa kuuliza. Unaposikia population kubwa ni masikini isiyoweza kumudu Milo mitatu unaelewa nini? Unaamini watu ni maskini na wasio na uwezo sababu ni uzembe? Alafu sio mm niliofanya population yetu kubwa kuwa masikini, so punguza jazba

Kuingia uchumi wa Kati kunahusiana vipi na Hilo kundi kubwa la masikini? Kaangalie percent ya watanzania wanaoshindwa kumudu Milo mitatu alafu uje ulete hayo mambo ya uchumi wa Kati. Tulisaidia chakula Malawi na Zimbabwe? How?

Miti ya mkaa kuwepo miaka 10 ijayo au kutokuwepo hiyo haihusiani na uwezo wa population kubwa kuweza kumudu kununua gesi. Nimekuambia nusu ya population ya Tanzania haina uhakika wa milo mitatu, mtu ambae hawezi kumudu Milo mitatu unamueleza suala la kutumia gesi? Umewahi kupita mazingira ya vijijini ukaona yalivyo? Nyumba tu kuweka bati miaka nenda rudi population kubwa umeshindwa, leo ndio kila mwezi aweze kununua mtungi wa 60k? Unaota?
 
Umejibu kwa jazba sana, kwanza lengo la awareness ni kwa wale walio na uwezo lakini wanapuuzia matumizi ya nishati Safi sababu ya mazoea. Wasio na uwezo hawana namna hata ukiwapa awareness

Wasio na uwezo Nani anawalisha mwaka mzima? Hili swali ni la kipuuzi ambalo hukupaswa kuuliza. Unaposikia population kubwa ni masikini isiyoweza kumudu Milo mitatu unaelewa nini? Unaamini watu ni maskini na wasio na uwezo sababu ni uzembe? Alafu sio mm niliofanya population yetu kubwa kuwa masikini, so punguza jazba

Kuingia uchumi wa Kati kunahusiana vipi na Hilo kundi kubwa la masikini? Kaangalie percent ya watanzania wanaoshindwa kumudu Milo mitatu alafu uje ulete hayo mambo ya uchumi wa Kati. Tulisaidia chakula Malawi na Zimbabwe? How?

Miti ya mkaa kuwepo miaka 10 ijayo au kutokuwepo hiyo haihusiani na uwezo wa population kubwa kuweza kumudu kununua gesi. Nimekuambia nusu ya population ya Tanzania haina uhakika wa milo mitatu, mtu ambae hawezi kumudu Milo mitatu unamueleza suala la kutumia gesi? Umewahi kupita mazingira ya vijijini ukaona yalivyo? Nyumba tu kuweka bati miaka nenda rudi population kubwa umeshindwa, leo ndio kila mwezi aweze kununua mtungi wa 60k? Unaota?
Kujibu kwa jazba hakuondoi sense au facts hicho ndio main concern!
1. Kwanza huhitaji kutoa awareness kwa jambo ambalo serikali ndio anapaswa kuanzisha hatua za upatikanaji wa hiyo nishati safi hasa kwa kuondoa kodi ili watu wengi zaidi watumie, hasa watu wa kipato cha kati na cha chini ambao ndio waathirika wakubwa wa matokeo ya matumizi ya nishati km mkaa na kuni na si hao unasema wenye uwezo, wao hawana cha kupoteza na huwezi walazimisha watumie hicho unachotaka!
2. Swali la nani anawalisha kwa mwaka mzima, hili ni la kukufanya ufikiri..hao unaowataja wanakula mlo mmoja kwa siku ni watu gani? watanzania wengi wako vijijini ambako ziko fursa nyingi kuwafanya waishi zaidi ya kiwango cha kujikimu..taarifa za TASAF zinasema nini? kundi hilo unalotaja si wengi, wajane, wazee wasio na watoto wa kuwatunza, walemavu nk ambao sababu za kuwa hivyo ni za kijamii.. kijijini hakuna mtu anakula mlo mmoja km anajishughulisha na kilimo, ufundi au kazi yoyote ya kumuingizia kipato, ndio maana ya mfano wa yule alihamasisha kilimo na kuondoa usumbufu wa kirasimu kusafirisha mazao ili watu wapate stahiki ya jasho lao..alifaulu kutokuwepo kelele za kukosa chakula, hata ziada ilipatikana kusaidia jirani waliopatwa na majanga wakakosa chakula..malawi na zimbabwe, maana hasa ya mfano huu ni kukuonyesha tatizo si UWEZO na wewe ubadilishe mtizamo ulio nao kushabikia matokeo ya tatizo, kukosa uwezo ni matokeo ya tatizo la msingi UVIVU na KUTOWAJIBIKA kwa watu wenyewe na wale wana jukumu la kusimamia watu wasile mlo mmoja unaoushabikia!
3. matumizi ya nishati safi hata tu ukianza na kundi la watu waajiriwa wote wakamudu kutumia nishati hiyo matokeo ya badiliko ni makubwa, kimapato na kimazingira..miti haitakatwa kwa kiwango kikubwa vile wanunuzi wa kuni na mkaa wamepungua, kwa hivyo si lazima kwa mara moja wote tutumie nishati safi la, pako pa kuanzia ili kunusuru misitu na uharibifu wa mazingira..walimu, matabibu, polisi, wanajeshi, wafanyabiashara ni kundi kubwa kwa kuanzia kabla ya hao unawaita wasio na uwezo..
4. sijui ni mazingira gani ya kijijini unayoeleza ambako nyumba za mabati hakuna wakati takwimu za sensa ya 2022 zinasema asilimia 77 ya watanzania wana nyumba bora za kuishi, ni za matofali hata km ni udongo na zimeezekwa kwa bati https://www.nbs.go.tz/uploads/stati...55-04. Building_Census2022_English08April.pdf
km mtu ana nyumba ya bati atashindwa kununua mtungi japo ule mdogo au ule mkubwa ambao umeboreshwa kiteknolojia ili anunue kulingana na matumizi yake..? na hivyo ndio serikali inapaswa kufanya! mbona kuleta Luku za tanesco serikali waliweza?
Tusiwe mashabiki kushabikia matokeo ya matatizo yetu wenyewe, tutafute majibu..serikali ifanye wajibu wake, huwezi kila siku unaimba awareness..!tenda kwanza wewe kwa kiwango cha uwezo wako kabla ya kuita wengine kukusaidia!
 

Attachments

  • Screenshot 2024-09-30 at 11-43-29 sw-1719124055-04. Building_Census2022_English08April.pdf.png
    Screenshot 2024-09-30 at 11-43-29 sw-1719124055-04. Building_Census2022_English08April.pdf.png
    13 KB · Views: 4
Kama mnataka watu watumie gesi punguzeni bei.mfano mtungi mkubwa wa kilo 15 uuzwe elfishirini na ule mdogo kabisa elfu Tano.Nyinyi mumeweka Kodi lukuki halafu mnataka watu watumie gesi halafu wakati huohuo ninyi mmejiunganishia mfumo ya gesi asilia na wanaolipia gharama ni sisi wakamuliwe Kodi mlizojiwekea pasipo kutushirikisha.
 
Sio tu kwamba nifanye analysis bali hili jambo nilishalidadavua...
Matumizi ya Umeme ni makubwa sababu mwananchi anauziwa unit kwa bei kubwa, jambo ambalo ukipunguza hio bei per unit itashuka..., juzi tu hapa walifungulia maji Kwenye Bwawa ili yasitumike (waste of energy) Tanzania ni a Tropic Country kuna Nishati ya Jua ya Kumwaga..., Kwahio kwa kutumia energy mix ya vyanzo vilivyopo ndani vitatosha wala bila kuhitaji kuagiza LPG kutoka nje pili kumbuka vyanzo vingine ni vya ndani hivyo pesa inazunguka LPG tunampa mwingine..., Na bado bei ya LPG ni kubwa ndio maana Serikali inataka kuchukua Kodi zetu tena ili kulipia hio LPG (kuwapa watu biashara) eti ili bei ipungue

Hizo nchi unazoongelea zinatumia huko wanazi import kutoka wapi na kwa bei gani ? Kumbuka Europe sehemu nyingi wanatumia Piped Gas ambayo ni gesi asilia na kama ikiwa piped this is very cheap (ila huku hatuna miundombinu ya kufanya hivyo...) Unapoonglea cheapest cleaning cooking solution available to market unasema nini ? Yaani unaweza kuliganisha Electricity from Hydro na LPG from Petroleum na ambayo wala hauna unaagiza na unatoa ruzuku ili ionekane cheaper (ingawa bado watu wanashindwa kumudu ndio cheapest available to market). Yaani tukimaliza Bwawa la Nyerere ambapo capacity itakuwa double iliyopo sasa bado unasema uzalishaji utakuwa ni mdogo na wala tusifanye hivi tuagize LPG na kutumia kodi zetu kupunguzia mwananchi bei hio ndio Cheapest ?

Why ? Tena wewe nadhani umezaliwa Juzi ulizia wazee wako enzi zile taa ni 100watts (achana na hizi za sasa) watu walikuwa na taa mpaka nje na zinawaka usiku mzima. watu walikuwa na majiko ya umeme tena plate na coils achana na haya majiko ya sasa ambayo ni energy efficient kuliko hata gesi, watu walikuwa na ma oven na wanapikia kila siku..., watu shule walikuwa mpaka wana heaters za kujitengenezea za wembe (zinakula umeme balaa) ila waliweza kumudu (WHY) sababu per unit cost ilikuwa ndogo sio sasa hivi imekuwa kubwa kutokana na kwamba Tanesco wananunua kwa watu (madalali) hivyo kufanya biashara kichaa (kunufaisha wachache)

Narudia tena unaongelea kitu hata ambacho huna (hauzalishi) kwamba ndio feasible wakati una vyanzo vyote vya kuzalisha nishati kuliko hata nchi nyingi duniani (alafu unaona ndio ujanja kutumia kila ambacho hauna)? Ukitaka kufanikiwa play according to your strength
LOGIKOS,

Upendo,

Mawazo/maono yako ni mazuri kabisa! na tena yako mbele kisuluhu juu ya masuala yanayoanika aibu ya mabovu ya 'siasa-uchumi' za kileo...

Unalijua hili fika -- kwa kuwa unayajua ya 'lobbying' na mambo mengine, hauko pekee yako...

Kuwa na AMANI YAKO!

Tafadhali Usichoke kushiriki Mawazo/maono mazuri hata kama unadhani 'hakuna tumaini'... LIPO!

Mambo ya kiufundi ya 'Nishati' na 'Sera' ni 'MUZIKI' kote duniani--hili, alhamdulillah, unaonesha unalifahamu fika!

SASA, haijalishi eti kwa kuwa 'Nishati' na 'Sera' na 'Mipango' daima hugubikwa na 'figisu' basi wadau wasizungumze, hapana, yazungumzwe!

Tukiacha yote, UMEME NDIYO JIBU -- anayebisha ni 'mhuni'--fundi wa upotoshaji kwa ghiriba za 'Usomi Mashudu'; tena yako mengi hata humu siyo jukwaa lililotayari kwa mashauri.​

BARAKA
 
Kujibu kwa jazba hakuondoi sense au facts hicho ndio main concern!
1. Kwanza huhitaji kutoa awareness kwa jambo ambalo serikali ndio anapaswa kuanzisha hatua za upatikanaji wa hiyo nishati safi hasa kwa kuondoa kodi ili watu wengi zaidi watumie, hasa watu wa kipato cha kati na cha chini ambao ndio waathirika wakubwa wa matokeo ya matumizi ya nishati km mkaa na kuni na si hao unasema wenye uwezo, wao hawana cha kupoteza na huwezi walazimisha watumie hicho unachotaka!
2. Swali la nani anawalisha kwa mwaka mzima, hili ni la kukufanya ufikiri..hao unaowataja wanakula mlo mmoja kwa siku ni watu gani? watanzania wengi wako vijijini ambako ziko fursa nyingi kuwafanya waishi zaidi ya kiwango cha kujikimu..taarifa za TASAF zinasema nini? kundi hilo unalotaja si wengi, wajane, wazee wasio na watoto wa kuwatunza, walemavu nk ambao sababu za kuwa hivyo ni za kijamii.. kijijini hakuna mtu anakula mlo mmoja km anajishughulisha na kilimo, ufundi au kazi yoyote ya kumuingizia kipato, ndio maana ya mfano wa yule alihamasisha kilimo na kuondoa usumbufu wa kirasimu kusafirisha mazao ili watu wapate stahiki ya jasho lao..alifaulu kutokuwepo kelele za kukosa chakula, hata ziada ilipatikana kusaidia jirani waliopatwa na majanga wakakosa chakula..malawi na zimbabwe, maana hasa ya mfano huu ni kukuonyesha tatizo si UWEZO na wewe ubadilishe mtizamo ulio nao kushabikia matokeo ya tatizo, kukosa uwezo ni matokeo ya tatizo la msingi UVIVU na KUTOWAJIBIKA kwa watu wenyewe na wale wana jukumu la kusimamia watu wasile mlo mmoja unaoushabikia!
3. matumizi ya nishati safi hata tu ukianza na kundi la watu waajiriwa wote wakamudu kutumia nishati hiyo matokeo ya badiliko ni makubwa, kimapato na kimazingira..miti haitakatwa kwa kiwango kikubwa vile wanunuzi wa kuni na mkaa wamepungua, kwa hivyo si lazima kwa mara moja wote tutumie nishati safi la, pako pa kuanzia ili kunusuru misitu na uharibifu wa mazingira..walimu, matabibu, polisi, wanajeshi, wafanyabiashara ni kundi kubwa kwa kuanzia kabla ya hao unawaita wasio na uwezo..
4. sijui ni mazingira gani ya kijijini unayoeleza ambako nyumba za mabati hakuna wakati takwimu za sensa ya 2022 zinasema asilimia 77 ya watanzania wana nyumba bora za kuishi, ni za matofali hata km ni udongo na zimeezekwa kwa bati https://www.nbs.go.tz/uploads/statistics/documents/sw-1719124055-04. Building_Census2022_English08April.pdf
km mtu ana nyumba ya bati atashindwa kununua mtungi japo ule mdogo au ule mkubwa ambao umeboreshwa kiteknolojia ili anunue kulingana na matumizi yake..? na hivyo ndio serikali inapaswa kufanya! mbona kuleta Luku za tanesco serikali waliweza?
Tusiwe mashabiki kushabikia matokeo ya matatizo yetu wenyewe, tutafute majibu..serikali ifanye wajibu wake, huwezi kila siku unaimba awareness..!tenda kwanza wewe kwa kiwango cha uwezo wako kabla ya kuita wengine kukusaidia!
Umeandika upuuzi. Ni Kama unaishi kwenye sayari yako
Unashangaa watu kula mlo mmoja? Unajua hata idadi ya maskini waliopo nchi zetu hizi hasa Tanzania

Unasema Kama ana nyumba ya bati anashindwa vipi kununua jiko la gesi dogo? Unajua gharama ya kununua gesi kila inapoisha au unafikiri ukinunua ndio umemaliza? Pia hiyo mitungi yenye teknolojia kununua kadri unavyotumia hata dar upatikanaji wake sio reliable, ndio iwe mtu aliye namtumbo ambae hata umeme tu haujafika.

Wewe huenda haujui unachoandika, nakupa kazi ndogo tembelea ndugu, marafiki, hapo mjini yu ulipo alafu kangalie ni wangapi wanamudu kutumia gesi
 
Tatizo bei za nishati ziko juu mno, hivyo utekelezekaji wa mpango huo kwa mwananchi asiyejua kesho anakula nini ni mgumu.

Mfano ingekuwa umeme ukinunua wa shilingi 1000/= unapata units 20 na mtungi mdogo wa gas unajazwa kwa Tsh 5,000/=, hapo malengo yangetimia.
Naam, ajenda ya mama ni NZURI ,sasa asimamie kupunguza Bei ya umeme na gesi ili utekelezaji uwezekane kwa VITENDO.
 
Back
Top Bottom