Pre GE2025 Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Pre GE2025 Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wezi wanataka kuiba tu. Eti umeme unatoka Ethiopia . Ni bwawa sasa umeme wetu wa bwawa vipi? Yaani umeme wa Ethiopia unapita nchi ngapi? Wanasingizia umbali. Kusini ni mbali kuliko Ethiopia!
Naomba kujua climate ya Ethiopia na tz wap kuna mvua ya kutosha?.
Hivi humu kama kuna wataalamu wa haya mambo wanaweza kutupa abc's angalau tupate mwanga.
Au kama ndo hvihiv,nafikiri kati ya viongoz/serikali na wananch kuna kundi mojawapo linatatzo rohoni, moyon au ubongo wa mbele juu ya maamuzi kama hayo.
Au tuseme tumevurugwa tugavuriguka sio bure.
 
Kwa stlye hii kila mtu mtamuona Hana akili na sio chadema Tu

Shida yenu huwa mnaongea Kwa mihemuko Sana mpaka mnajisahau

Mara zote mnasema umeme ni mwingi mpaka mnataka kuuza nje

Hamna siku mmewahi kusema umeme ni mwingi yes but not Kwa zone ya kaskazini

Au mnaposema inchi mzima shida ya umeme imeisha, kule kaskazini sio Tanzania?

That's why watu wanahisi mnawaibia
Mkuu acha waendelee kuisema chadema tuu maana hawajui kama wapinzani hatari kuliko chadema wako ccm na serikalini humohumo.
 
Sema kama kuna kitu nawakubali ni timing za kutoa hizi taarifa, kupiga matukio. Hiki kipindi story kubwa itakuwa ni game ya Simba na Yanga, na unaweza kutwa ilihailishwa kitaalamu tu.

Waache kuchezea hela kwenye mambo yayo ya muhimu, wapeleke sehemu husika mambo yatakaa sawa tu. Hakuna nchi imewahi kujengwa kwa uchawa.
Yaani mkuu kwa zama hiz wangeacha hiyo michezo ya miaka 1710s ya ufusad au dalili zake.

Wanatakiwa kujua jobless ni wengi mtaa na hasa wasomi. Wengi wanapitia situation ya kutaka kujiua kwa ugumu wa maisha.
Na serikali inasema haiwez ajiri kisa haina hela.

Sasa wanapoona viongoz wanacheza na pesa kizembe ignation point yao inashuka sana. Hivyo at low temperature and pressure can cause fire outbreak.
 
Niliwaabia kuwa 99% ya viongozi wa ccm ni wajinga, hili ni zap la mfumo mbovu wa elimu yetu, tuna zalisha vichwa maji kila siku. Hakuna wanachoweza , wamejenga bwana kubwa la kuzalisha umeme wa kutosha lakini kila siku kulalamika.
 
Fuatilia mada mwanzo mwisho. Bila kuhemuka.

Halafu elewa kuwa kuna hoja za kidhahania zaidi.

Swali langu hujajibu.

Wewe unaona ni Sawa kununua umeme nje?

Why hawakusema wakati wote?

Maana ya tuna umeme mwingi mpaka tunataka kuuza nje ni nini?
 
Naomba kujua climate ya Ethiopia na tz wap kuna mvua ya kutosha?.
Hivi humu kama kuna wataalamu wa haya mambo wanaweza kutupa abc's angalau tupate mwanga.
Au kama ndo hvihiv,nafikiri kati ya viongoz/serikali na wananch kuna kundi mojawapo linatatzo rohoni, moyon au ubongo wa mbele juu ya maamuzi kama hayo.
Au tuseme tumevurugwa tugavuriguka sio bure.

Nani kasema tatizo ni mvua. Tumesha sema hapa ni biashara za watu.
 
Nani kasema tatizo ni mvua. Tumesha sema hapa ni biashara za watu.
Mkuu nmeuliza hilo baada ya kusoma maon ya mdau aliyesema kwamba kwamba nivema kununua huo umeme mkushi, kwamb ikiwa umeme wa JNHEP ukizngua tutakuwa na mbadala.

Pia kwa waliokuwa wakionesha umeme wetu sio wa uhakika kama huo wa mkushi.
 
Wewe unaona ni Sawa kununua umeme nje?

Why hawakusema wakati wote?

Maana ya tuna umeme mwingi mpaka tunataka kuuza nje ni nini?

Kununua umeme kutoka nje in itself hakuna tatizo, tatizo lipo katika detail, na serikali yetu ina tatizo la kutoa detail.

Maswali yako yanaonesha hujasoma hata pale niliposema serikali ya Tanzania ina tatizo la usiri na mtu hawezi kuitetea hata pale inapofanya sawa, kwa sababu ina usiri sana hata kwenye mambo yanayotakiwa kuwa wazi. Na usiri huu unaleta imani kwamba kuna mabaya yanafichwa, ikiwa kuna mabaya yanafichwa kweli au la. Na watu wana haki ya kufikiri hivyo. Usiri ni chaka la rushwa.

Ungesoma nilipoandika hivyo, usingeuliza "why hawakusema wakati wote?".

From a purely abstract point of view, kwa hoja ya kidhahania tu, siitetei serikali, inawezekana upande wa kati na kusini wa Tanzania ukawa na umeme mwingi sana mpaka wa kuuza nje, lakini, miundombinu ya kuupeleka umeme huo sehemu za kaskazini ikawa na matatizo sana mpaka ikawa rahisi kununua umeme wa nje kwa sehemu hizo za kaskazini, halafu gharama zake zikaliliwa na umeme unaouzwa nje, na kama tunauza zaidi ya tunavyonunua, hapo tutabaki na net positive.

Tatizo I cannot make this case for Tanzania kwa sababu hawajaweka wazi fine details za kuonesha hii ndiyo hali halisi.
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ipo kwenye hatua za mwisho za kusaini mikataba ya kununua umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini ili Mikoa hiyo ipate umeme wa uhakika na iondokane na adha ya umeme kukatikakatika.

Rais Samia amesema hayo baada ya kufungua mradi wa Maji wa Same-Mwanga-Korogwe kwenye hafla iliyofanyika Mwanga Mkoani Kilimanjaro leo March 09, 2025.

Soma: Rais Samia: Tanzania inayo nafasi ya kuuza umeme nje

Rais Samia amesema "Umeme unakatikatika maeneo ya Kaskazini huku lakini Serikali yenu inachukua hatua ya kununua umeme nje maalum kwa Mikoa hii ya Kaskazini ili umeme upatikane masaa 24 muda wote bila kukatikakatika"

"Tuko kwenye hatua za mwisho kusaini mikataba ili tuweze kununua umeme ule uungwe Kanda ya Kaskazini na Wananchi wafaidi na umeme, kwahiyo tutakuwa na umeme wa uhakika, maji ya uhakika kila pahali, Vijiji vyote vina umeme tunakwenda Vitongojo na umeme wa kutosha tunaununua unaingia ili kazi za maendeleo ziendelee"


Mara watauza umeme. Mara watajitosheleza baada ya Bwawa la Mwalimu Nyerere kukamilika. Sijui kama hawa wanajua wanachofanya.
 
Tenda za kuchapisha vitabu ni ufisadi mbaya sana unaoliangamiza taifa la Tanganyika .
Tanganyika ni shamba la bibi kuja kuchota kodi za wananchi na kwenda kula maisha ughaibuni.

Wakati vitabu vilipokuwa vinachapishwa na serikali hapakuwa na huu utituri wa kubadili mitaala na vitabu kila kukicha .

Shule za private badala ya kuwa na Library ya vitabu kazi zake ni kubebesha watoto mabegi ya kila kumi ya vitabu mgongoni . No one cares .

Taifa lenye watawala waovu linawakilisha matakwa ya mafisadi kuneemesha matumbo ya wachache kwa kuliangamiza taifa la kuishi kielimu na hata kimaendeleo.
Kuna soko kubwa la kuuza vitabu kila siku na suala hilo limewafanya wamiliki wa shule binafsi kuwa mawakala wa kuuza vitabu visivyo na kikomo cha kubadilishwa mitaala yake na ubora wake kitaaluma .

Nani aseme kama sio mkuu wa nchi ?
Mitano tena italeta Majanga na ufisadi tena
Ila hili la kutokuwepo kwa mwendelezo wa mikakati ya kimaendeleo litatufanya tuendelee kubaki pale pale,maana kila utawala unakuja na yake

Mfano kwenye elimu hakuna miendelezo,kila utawala unakuja na utaratibu wake
 
Hivi political calculation zimepigwa kweli kabla kutoa misimamo huu!?Hapa sijagusia economic and technological calculations
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ipo kwenye hatua za mwisho za kusaini mikataba ya kununua umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini ili Mikoa hiyo ipate umeme wa uhakika na iondokane na adha ya umeme kukatikakatika.

Rais Samia amesema hayo baada ya kufungua mradi wa Maji wa Same-Mwanga-Korogwe kwenye hafla iliyofanyika Mwanga Mkoani Kilimanjaro leo March 09, 2025.

Soma: Rais Samia: Tanzania inayo nafasi ya kuuza umeme nje

Rais Samia amesema "Umeme unakatikatika maeneo ya Kaskazini huku lakini Serikali yenu inachukua hatua ya kununua umeme nje maalum kwa Mikoa hii ya Kaskazini ili umeme upatikane masaa 24 muda wote bila kukatikakatika"

"Tuko kwenye hatua za mwisho kusaini mikataba ili tuweze kununua umeme ule uungwe Kanda ya Kaskazini na Wananchi wafaidi na umeme, kwahiyo tutakuwa na umeme wa uhakika, maji ya uhakika kila pahali, Vijiji vyote vina umeme tunakwenda Vitongojo na umeme wa kutosha tunaununua unaingia ili kazi za maendeleo ziendelee"



Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ipo kwenye hatua za mwisho za kusaini mikataba ya kununua umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini ili Mikoa hiyo ipate umeme wa uhakika na iondokane na adha ya umeme kukatikakatika.

Rais Samia amesema hayo baada ya kufungua mradi wa Maji wa Same-Mwanga-Korogwe kwenye hafla iliyofanyika Mwanga Mkoani Kilimanjaro leo March 09, 2025.

Soma: Rais Samia: Tanzania inayo nafasi ya kuuza umeme nje

Rais Samia amesema "Umeme unakatikatika maeneo ya Kaskazini huku lakini Serikali yenu inachukua hatua ya kununua umeme nje maalum kwa Mikoa hii ya Kaskazini ili umeme upatikane masaa 24 muda wote bila kukatikakatika"

"Tuko kwenye hatua za mwisho kusaini mikataba ili tuweze kununua umeme ule uungwe Kanda ya Kaskazini na Wananchi wafaidi na umeme, kwahiyo tutakuwa na umeme wa uhakika, maji ya uhakika kila pahali, Vijiji vyote vina umeme tunakwenda Vitongojo na umeme wa kutosha tunaununua unaingia ili kazi za maendeleo ziendelee"


Uoongoooo na kambaa za kampeni. Mara mgao wa umeme utakuwa historia kumbe wanamaanisha utaweka historia ya kutoisha na mazwazwa wataendelea kupigwa changa la mato.
 
Tunapelekwa mzobemzobe tu.

Tulipojenga Bwawa la Nyerere mahesabu yetu yalikuwa ni kuzalisha umeme tusiutumie ili tununue wa nje?
 
Tunapelekwa mzobemzobe tu.

Tulipojenga Bwawa la Nyerere mahesabu yetu yalikuwa ni kuzalisha umeme tusiutumie ili tununue wa nje?
Bado unawaamini wezi hawa?! Mradi wenyewe hata ukikamilika ujue ni bomu. Umehujumiwa na hawa wahujumu wasio na maana wala akili
 
Ilikuwa tuuze umeme nje, leo tunataka kununua umeme nje..
🤣 🤣 🤣

Nchi ya kijinga sana hii 😂🤣
 
Wakuu Mama ni kama amepewa taarifa Sio wame mislead Sijapenda kabisa, Kwasasa Total Capacity ya Uzalishaji wa Umeme Countywide ni 3040MW against matumizi ambayo hayafiki ata 2500MW kitu ambacho tunaweza Kusema kwa Sasa tuna Surplus

Issue ya Kukatika Kwa umeme sidhani kama Ni scarcity isipokuwa Miundo Mbinu ya Usambazaji na Usafirishaji ndio sio rafiki Ministry of Energy ime take ilo onboard na Kuna Miradi ya Usafirishaji Inafanyika Kuongeza Expansion ya Grid mfano wanajenga Mradi Wa 400KV kutoka Chalinze mpaka dodoma Ili umeme unaotoka Bwawa la Mwalimu Nyerere uwe distributed Vyema.

Mwezi uliopita walifanikiwa Kuunganisha Line za Msongo wa 400KV kutoka isenye Kenya Mpaka Singida Via Arusha Na Kujenga Kituo Kikubwa cha Kupooza umeme Substation Arusha Namuguru (400KV) Kiasi kwamba Muunganiko Huo utasaidia Cross-border trading ya Umeme kati yetu sisi Kenya kupitia (Ketraco) na Ethiopia ambaye Ethiopia ndio giant kwenye Ukanda Huu Muunganiko huo Uko guided na Kitu kinaitwa Eastern African power pool Power(EAPP) chenye wanachama Mataifa 13 to date

Ivo issue ya Kusema sisi tununue umeme hakuna sababu kabisa ya msingi ya Kufanya Ivo unless tupate scarcity kitu ambacho kwa sasa hatuna ujenzi wa Line ya msongo 400Kv chalinze dodoma utasaidia Vituo Vinne Kuwa interconnected vya 400Kv ambacho ni Chalinze, Zuzu pamoja Kituo kikubwa cha Singida na Namguru Arusha Ivo izo infrastructure zikishakuwa Constructed tutakuwa na Usafirishaji mzuri na Kaskazini itaenda Kuwa Stable upande wa Nishati

Mheshimiwa Naibu waziri Mkuu ni zaidi ya Mara Moja Tumesikia Ukisema Kuwa Kwa sasa nchi ina Kiwango cha Ziada(Surplus) upande wa uzalishaji ila tu Changamoto Ni Miundo Mbinu ya Usafirishaji na Usambazaji ambalo ni swala wote tunaelewa kuwa Linarekebishwa kwa Muda na ni swala Progressive hii Policy ya kusema tununue Umeme Kenya au Ethiopia sana sana Ethiopia ila Tupitishie kenya Naona Haijakaa Vizuri kabisa
Wakenya kwa sasa tumewapita Upande wa Capacity ya Grid zetu.
Umefafanua vizuri sana, japo bado inafikirisha mno!
Kwamba tunajenga maradi mkubwa wa uzalishaji wa umeme, mpaka mradi unakamilika, lakini hatujajenga transmission ways? Mradi umegharimu trillions of money, lakini hatukufikiria namna ya kufikisha kwa Wateja?
Okay tu-assume kwamba tulisahau! He, kuusafirisha umeme kutoka Ethiopia hakutahitaji hizo najua za kuusafirisha? Njoo hizo zitajengwa na nani? Kwa gharama gani? Tutazitumia kwa muda gani? Na je, ni rahisi kujenga njia za mkataba wa muda kuliko za kwetu?
Je, ni rahisi kujenga kutoka Ethiopia mpaka Arusha kuliko kutoka Rufiji?

Kuna mambo yanafanyika unabaki kujiuliza maswali magumu mno, hivi wafanya maamuzi ni watu wa aina gani?
 
Nimeshangaa sana na huu mpango wa kununua umeme kutoka Ethiopia.

Mnannua umeme wakati mnazalisha zaidi ya mahitaji ya ndani maradufu.

Kwa nini umeme usishuke bei? Maana tulitegemea Bwawa la JNHPP likikamilika baai bei ya uameme itashuka na maisha ya watanzania yatapata nafuu.

CCM hii haina huruma na wananchi.
 
Back
Top Bottom